Swali: Je, imethibiti kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alizaliwa tarehe 12 Rabiy´ al-Awwaal? Ni ipi hukumu ya kusherehekea siku ya kuzaliwa kwake?
Jibu: Haijuzu kusherehekea siku ya kuzaliwa kwake. Alizaliwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) Rabiy´ al-Awwaal. Lakini haifai kusherehekea siku ya kuzaliwa kwake. Hii ni Bid´ah. Kila Bid´ah ni upotevu. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Tahadharini na mambo yaliyozuliwa. Kwani hakika kilichozuliwa ni Bid´ah, kila Bid´ah ni upotevu na kila Bid´ah ni Motoni.”
Haijuzu kusherekea kuzaliwa kwa Mtume wala kuzaliwa kwa mwengine yeyote.
Usile chakula kilichotengenezwa kwa ajili ya maulidi. Chakula kilichotengenezwa kwa mnasaba wa maulidi usikile.
http://bit.ly/2W79jTT
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni