Translate

Jumamosi, 18 Mei 2019

Zipi Nguzo Za I’tikaaf Na Sharti Zake? Na Je, Inasihi Bila Ya Swawm?

Zipi Nguzo Za I’tikaaf Na Sharti Zake? Na Je, Inasihi Bila Ya Swawm?

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema:

a. Nguzo ya I’tikaaf ni kulazimika (kufanyika I’tikaaf) katika Msikiti kwa ajili ya utiifu kwa Allaah (‘Azza wa Jalla) katika kumwabudu Yeye, na kujikurubisha Kwake na kujipwekesha katika kumwabudu.

b. Ama sharti zake, basi ni kama zilivyo sharti za ‘ibaadah zote miongoni mwazo ni: Uislamu, akili, na inasihi kwa asiyebaleghe, na inasihi kwa mwanaume na mwanamke.

c. Na inasihi bila ya Swawm, na inasihi katika Misikiti yote.

[Majmuw’ Al-Fataawaa (20/162)]


http://bit.ly/2Q92c8d i live islam

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...