Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) amesema:
“Inatakiwa kuamini kuwa ´Iysaa bin Maryam (´alayhis-Salaam) atashuka na kumuua karibu na mlango wa Ludd.”
MAELEZO
Imepokelewa kwamba ´Iysaa bin Maryam (´alayhis-Salaam) atateremka wakati ambapo waislamu wanasubiri Fajr. Atakuwa amevaa shuka mbili za juu za manjano na atakuwa ameweka mikono yake miwili juu ya mbawa za Malaika wawili. Wakati kutapokimiwa swalah al-Mahdiy atamwambia:
“Tangulia mbele, ee roho ya Allaah.” Aseme: “Maimamu wenu ni kutokamana na nyinyi.”
Kisha atoke kwenda kumtafuta ad-Dajjaal, mikononi mwake atakuwa na mkuki. Atamkuta karibu na mlango wa Ludd na atamuua hapo. Halafu atawaendea waumini awapongeze na awaeleze ngazi zao Peponi. Imepokelewa vilevile kwamba atamuuoa msichana wa al-Mahdiy ambaye atamfungulia njia.
from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2IFoMnJ
via IFTTT
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni