Translate

Jumatano, 24 Aprili 2019

29. Kushuka kwa ´Iysaa

Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) amesema:

“Inatakiwa kuamini kuwa ´Iysaa bin Maryam (´alayhis-Salaam) atashuka na kumuua karibu na mlango wa Ludd.”

MAELEZO

Imepokelewa kwamba ´Iysaa bin Maryam (´alayhis-Salaam) atateremka wakati ambapo waislamu wanasubiri Fajr. Atakuwa amevaa shuka mbili za juu za manjano na atakuwa ameweka mikono yake miwili juu ya mbawa za Malaika wawili. Wakati kutapokimiwa swalah al-Mahdiy atamwambia:

“Tangulia mbele, ee roho ya Allaah.” Aseme: “Maimamu wenu ni kutokamana na nyinyi.”

Kisha atoke kwenda kumtafuta ad-Dajjaal, mikononi mwake atakuwa na mkuki. Atamkuta karibu na mlango wa Ludd na atamuua hapo. Halafu atawaendea waumini awapongeze na awaeleze ngazi zao Peponi. Imepokelewa vilevile kwamba atamuuoa msichana wa al-Mahdiy ambaye atamfungulia njia.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2IFoMnJ
via IFTTT

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...