Swali
Je, ni lazima kwa mwanamke kufunika miguu anaposwali?
Jibu
Ndio ni Wajiib kwa Mwanamke kufunika Miguu yake wakati wa Swalah.
Umm Salamah alimuuliza Mtume Muhammad (Swalla Allahu ´alayhi wa sallam):
“Mwanamke anaweza kuswali na kanzu pasi na sketi?” Akasema: “Ndio, ikiwa kanzu hiyo inafunika miguu.”
↪Imepokelewa na Imaam Abu Daawuud (1/149).
Ibn Qudaamah amesema: ”Wanachuoni wengi wanasema haya ni maneno ya Umm Salamah, ilihali ´Abdur-Rahmaan bin ´Abdillaah bin Diynaar anaonelea kuwa ni maneno ya Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”
↪Rejea Al-Mughniy (2/329))
Rejea Kitab Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (35)
Na Allaah anajua zaidi
http://bit.ly/2tqb6n7 i live islam
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni