Swali
Ni Eneo gani ya Ardhi ambayo Jua lilipigwa kwa Siku moja na halitopigwa tena Mpaka siku ya Qiyamah...?
Jibu
BismilLaahir Rahmaniir Rahiim
Naam ama Sehemu iliyopigwa jua siku moja na haitopigwa tena jua mpaka siku ya Qiyamah ni Eneo katika Bahari ya sham ambapo Nabii Mussa (Aleiyhi Sallaam) Alipokuwa akifuatwa na jeshi la fir-'aun.
Ndipo Allaah (Subhaana wa Taala) Akamuamrisha Nabii Mussa (Aleyhi Sallaam) kwamba⤵
فَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنِ اضْرِبْ بِعَصَاكَ الْبَحْرَ ۖ فَانْفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَالطَّوْدِ الْعَظِيمِ
Mara tulimletea Wahyi Musa (Tukamwambia): ''Piga bahari kwa fimbo yako''. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama jabali (mlima) kubwa.
↪Surat Ash-Shu'ara Aya ya 63
Kwahiyo ndugu zangu katika Imaani, Baada ya Nabii Musaa (Aleyhi Sallaam) kuipiga ile Bahari kwa Fimbo yake kama alivyoamrishwa na Allaah (Subhaana wa Taala) ile Bahari hii ilipasuka sehemu mbili, ikafanyika njia katikati yake kwa maana ya Kwamba Allaah (Subhaana wa Taala) alilileta Jua na pakakausha sehemu ile ya katikati ili Nabii Mussa (Aleyhi Sallaam) apite na Wati wake.
Kwahiyo Nabii Mussa (Aleyhi Sallaam) akapita na watu wake, Firaun kuona vile akajitia na yeye na jeshi lake, Lakini Ilipomalizika tu kuvuka Nabii Mussa(Aleyhi Sallaam) na watu wake, bahari ilijifunga palepale, ikamfunga Firaun na watu wake.
Kwahiyo Allaah (Subhanahu wa Ta'ala) Aliliamlisha jua kupiga kwa Nguvu sehemu ile ili pakauke Watu waliombatana na Nabii Mussa (Aleyhi Sallaam) wapite bila shida.
Na baada ya Watu wa Mussa kuvuka katika Bahari ile Watu wa Fir-'aun pamoja na Fir-'aun Mwenyewe walipoingia Bahari kupitia njia ile ile Aliyopitia Nabii Mussa (Aleyhi Sallaam) kama nilivyosema hapo juu na watu wake, basi Allaah (Subhanahu wa Ta'aala) Akaifunika Bahari ile na watu wa Fir-'aun wakaangamia.
Kwaiyo tangia siku hiyo Eneo lile halikuwai tena kupigwa na jua mpaka siku ya Qiyamah.
Na Allaah anajua zaidi
http://bit.ly/2N9WrFx i live islam
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni