Translate

Jumatano, 20 Februari 2019

Kuchukua mkopo bank kwa ajili ya kulipa Deni

*Swali*

Assalam  alaykum warahmatullah
Ndugu  yangu  nisaidie  hapa  yupo  mtu  mie  namdai  pesa  zangu   sasa  juzi  nnamkumbusha   asema   wacha  nifanye  process   nichukue  mkopo  bank  kisha  nikupe  pesa  zako  sasa  akichukua  huko   bank  kisha  akanipa  itakuwa  sahih  mm  kutumia  hizo  pesa?

*Jibu*

Wa Aleykum Sallaam WarahmatulLaah Wabarakatuh

✅Naam, Inajuzu Muislamu kuchukua Mkopo Bank kwa ajili ya Kulipa (Kufidia) Deni analodaiwa kwa Sharti tu Mkopo huo anaochukua Bank usiwe na *Riba*.

➡Ama ikiwa kuna Riba ndani yake basi Haijuzu na ni Haraam.

➡Hakika ni kuwa Allaah Aliyetukuka Ameharamisha kuchukua na kutoa ribaa katika njia zake zote.

➡Allaah (Subhaana wa Taala) Anasema: “Allaah Amehalalisha biashara na kuiharamisha ribaa”
↪Surat Al-Baqarah Aya ya  275.

➡Na amesema tena Allaah(Subhaana wa Taala); “Enyi Mlioamini! Mcheni Allaah, na acheni yaliyobakia katika ribaa, ikiwa mmeamini. Na kama hamtafanya hivyo, basi fahamuni mtakuwa mmetanganza vita na Allaah na Mtume Wake”
↪Surat Al-Baqarah Aya ya  278 – 279.3

➡Na Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametuambia kuwa: “Allaah Amemlaani mwenye kula ribaa, mwenye kuitoa na mashahidi wake na mwandishi wake”
↪Imepokelewa na Imaam Ahmad, Abu Daawuud, at-Tirmidhiy, an-Nasaa’iy na Ibn Maajah.

➡Na amesema tena Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu uovu wa ribaa: “Dirhamu ya ribaa anayokula mtu na huku anajua ni mbaya zaidi kuliko kuzini mara thelathini na sita”
↪Imepokelewa na Imaam Ahmad.

➡Amesema tena: “ribaa ina milango 73 iliyo nyepesi na sahali ni mtu kumuoa (kumuingilia) mamake”
↪Imepokelewa na Imaam Al-Haakim.

Na Allaah anajua zaidi

Imeandaliwa na *Imaam Masjid Tawbah*



https://ift.tt/2V83wct i live islam

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...