Translate

Jumatatu, 18 Februari 2019

Hukmu ya mswaliji kuinuka kabla ya Tasliym ya pili ya imamu

Swali

Mtu Alambaye alikuja amechelewa kuingia katika swalah akiinuka katika swalah baada ya Tasliym ya imamu ya kwanza na kabla ya Tasliym ya pili swalah yake inabatilika?

Jibu

Swalah yake sio batili. Lakini kuna baadhi ya wanachuoni wamesema katika hali hii swalah yake inageuka kuwa swalah ya sunnah na haizingatiwi kwake kuwa ni ya faradhi.

Hivyo ni kwa sababu amejitenga na imamu kabla ya kutimia swalah ya imamu.

Kwa sababu swalah ya imamu haimaliziki isipokuwa baada ya Tasliym ya pili.

Pindi ataposimama kukidhi yaliyompita basi amejitenga kabla ya swalah ya imamu wake. Wamesema kuwa inageuka kuwa ya sunnah. Kwa sababu swalah ya sunnah kwa mtazamo wa wengi katika watu hawa wanaonelea kuwa mtu anaweza kutoka kwa Tasliym moja.

Rejea Kitab Al-Liqaa' ash-Shahriy (37) 



http://bit.ly/2SXZsy5 i live islam

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...