Translate

Jumamosi, 16 Februari 2019

”al-Albaaniy ni Murjiy”

Swali: Wako ambao wanasema kwamba maoni ya Shaykh al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) katika imani ni yaleyale kama ya Murji-ah. Unasemaje juu ya hilo?

Jibu: al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) ni mwanachuoni, Muhaddith na Faqiyh, hata kama alikuwa mwenye nguvu zaidi katika Hadiyth kuliko Fiqh.

Sijui kuwa ana maoni yenye kufahamisha juu ya Irjaa´. Lakini wanaotaka kuwakufurisha watu husema juu yake na kwa watu mfano wake kwamba ni Murji-ah. Inahusiana na kupeana majina bandia. Mimi nashuhudia juu ya Shaykh al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) juu ya kuwa na msimamo, ´Aqiydah salama na makusudio mazuri.

Lakini pamoja na hivyo sisemi kuwa hakosei. Kwa sababu hakuna yeyote, baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amekingwa na kukosea.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2V8ynpF
via IFTTT

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...