Swali: Wako ambao wanasema kwamba maoni ya Shaykh al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) katika imani ni yaleyale kama ya Murji-ah. Unasemaje juu ya hilo?
Jibu: al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) ni mwanachuoni, Muhaddith na Faqiyh, hata kama alikuwa mwenye nguvu zaidi katika Hadiyth kuliko Fiqh.
Sijui kuwa ana maoni yenye kufahamisha juu ya Irjaa´. Lakini wanaotaka kuwakufurisha watu husema juu yake na kwa watu mfano wake kwamba ni Murji-ah. Inahusiana na kupeana majina bandia. Mimi nashuhudia juu ya Shaykh al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) juu ya kuwa na msimamo, ´Aqiydah salama na makusudio mazuri.
Lakini pamoja na hivyo sisemi kuwa hakosei. Kwa sababu hakuna yeyote, baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye amekingwa na kukosea.
from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2V8ynpF
via IFTTT
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni