Translate

Jumamosi, 20 Aprili 2019

Hukmu ya Kisimamo Cha Usiku wa Niswf Sha’baan

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu-Allaah) amejibu kuhusu Swali la maudhui ya kisimamo cha usiku wa Niswf Sha’baan:

“Kisimamo cha usiku wa Niswf Sha’baan kiko katika hali au hukmu tatu:

1-Iwe ni ada (desturi) ya mtu kuwa anafanya hivyo (kuamka kwa ajili ya ‘ibaadah) kwa hiyo hufanya hata siku hiyo ya usiku wa Niswf Sha’baan kama anavyofanya nyusiku nyenginezo  bila ya kuufanya usiku huo kuwa ni makhsusi kwa kuzidisha ‘ibaadah. Jambo hili hakuna ubaya.

2- Kuswali  usiku wa Niswf Sha’baan juu ya kuwa hakuwa mtu akifanya hivyo katika nyusiko nyenginezo.  Hii ni bid’ah.


3-Kuswali usiku huo Swalaah zenye idadi maalumu, ambazo anakariri kila mwaka kuziswali.  Hii ni bid’ah shadidi (ya nguvu) zaidi kuliko ya hali ya pili na iko mbali zaidi na Sunnah.”

[Majmuw’ Al-Fataawaa (20/28-30)]


http://bit.ly/2XuPFhI i live islam

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...