Translate

Jumamosi, 20 Aprili 2019

Haijuzu Kuswali Kwa Kumfuata Imaam Kupitia Redio Au Televisheni


Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu-Allaah) :

Haijuzu mtu kumfuata Imaam kupitia redio au televisheni kwa sababu Swalaah ya Jamaa'ah inakusudiwa mkusanyiko, basi hakuna budi iwe katika sehemu moja au kuunganisha safu moja baada ya nyingine.

Wala Swalaah haijuzu kupitia viwili hivyo (redio na televisheni) kwa sababu ya kutopatikana malengo yake. 

Na tungelijuzisha hilo, basi kila mmoja angeliswali nyumbani kwake Swalaah zote tano pamoja na Swalaah ya Ijumaa pia. Na hili linakwenda kinyume na shariy’ah inayohusu Swalaah ya Ijumaa na ya jamaa'ah. 


[Majmuw’ Al-Fataawaa (15/213)]


http://bit.ly/2Iv22Hb i live islam

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...