MAFUNZO YA SWALAH - KIKAO BAINA YA SIJDA
Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh
Naam,Mswaliji anyanyue kichwa chake na huku akisema "Allaahu Akbar" na auinamishe mguu wake wa kushoto na auikalie na wakati huo huo asimamishe mguu wa kulia na aweke mikono yake juu ya mapaja na magoti yake na aseme:
"Rabb Ighfir liy, wahdiniy, warhamniy, warzuqniy, wa ´aafiniy na wajburniy."
"Ee Mola! Nisamehe, uniongoze, unihurumie, uniruzuku, nipe afya na uniunge."at-Tirmidhiy (284), Abu Daawuud (850) na Ibn Maajah (898).
Mswaliji anatakiwa awe na utulivu katika kikao hichi.
Asujudu Sijda ya pili na huku akisema "Allaahu Akbar" kisha afanye yale yale aliyofanya katika Sajdah ya kwanza.
Ainue kichwa chake na huku akisema "Allaahu Akbar" na akae kikao khafifu kama mfano wa kikao baina ya Sajdah mbili. Hiki huitwa kuwa ni "kikao cha kustarehe" ambacho kimependekezwa kwa mujibu wa maoni sahihi ya wanachuoni. Endapo atakiacha hakuna neno.
Katika kikao hichi hakuna Dhikr wala du´aa. Kisha asimame/apande kwenda katika Rakaa´ ya pili hali ya kujisaidiza kwa kushika mapaja - ikiwa kuna urahisi wa kufanya hivo - la sivyo ajisaidize kwa ardhi. Halafu asome "al-Faatihah" na kilicho chepesi kwake katika Qur-aan baada ya al-Faatihah.
Ataendelea kufanya kama alivyofanya katika Rakaa´ ya kwanza.
Na Allaah anajua zaidi
from fisabilillaah.com http://bit.ly/2TgbRKd
via IFTTT
Translate
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah
إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! 20 - Isti’aadhah (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah ...
-
Dalili 18 zinazoashiria una ujauzito wa mtoto wa kiume Awali ya yote nitoe pongezi kwa mama K na Baba K wote popote walipo kwa kazi nzuri ...
-
SWALI: Assalaam alaykum Naomba maana ya majina yeyote tuwapao watoto wetu AU mnielekeze wapi naweza kupata labda katika kitabu cha fas...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni