Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh
Allaah Ameumba viumbe Wake ili wamwabudu Yeye Mmoja asiyekuwa na mshirika.
Amesema katika Kitabu Chake Titukufu:
ُونِ د ُ ب ْ ع َ ي ِ َّل ل َِّ إ َ نس اْْلِ َ ن و َّ ُت ا ْْلِ ْ لَق َ ا خ َ م َ و
“Na Sikuumba majini na wanadamu wa isipokuwa waniabudu.”51:56
Ametuma Mitume Wake watukufu ili wawaoneshe waja njia ya ´ibaadah:
َ و َ ه َّ ُوا الل د ُ ب ْ اع واَّل أَنِ ُ رس َّ ٍ َّمة ا ِِف ُك ِّل أُ َ ن ْ ث َ ع َ َ ْد ب لَق َ َت و اغُو َّ وا الط ُ ب ِ ن َ ت ْ اج
“Na kwa yakini Tulituma katika kila ummah Rasuli (awaamrishe watu wake) kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na twaaghuwt (miungu ya uongo).”16:36
Amefanya maisha ya dunia kuwa ni sehemu ya majaribio yao na mtihani ili waoneshe ni nani katika wao alie na matendo mazuri:
ال َ َم ع ُ ن َ ْس أَح ْ ُّ ُكم أَي ْ ُكم َ لُو ْ ب َ ي ِ ل َ اة َ ي َ ا ْْل َ ْ َت و و َ الْم َ لَق َ ي خ ذِ َّ ال
“Ambaye Ameumba mauti na uhai ili Akujaribuni ni nani kati yenu mwenye ‘amali nzuri zaidi.”67:02
Kisha Akasema:
ُو َف الْغ ُ ِزيز َ الْع َ و ُ ه َ و ُ ر
“Naye ni Al- ‘Aziyzul-Ghafuwr (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika daima - Mwingi wa kusamehe).”67:02
Amesema hivi ili kuonesha kuwa Anawalipa hawa wanaopewa mtihani wanaotenda matendo mema. Malipo haya yametokamana na Jina Lake alGhafuur (Mwingi wa kusamehe).
Upande mwingine Ameonesha pia kuwa wale wasiotenda matendo mazuri wanastahiki kuadhibiwa kutokana na Jina Lake al-´Aziyz (Mwenye enzi ya nguvu asiyeshindika daima). Hili linaenda sambamba na Kauli Yake:
ُ يم ِ ُب اْْلَل َذا َ الْع َ و ُ َذاِِب ه َ ن ع أَ َّ َ و
“Na kwamba Adhabu Yangu, ndiyo adhabu iumizayo.”15:50
Kwahiyo Ndugu zangu katika Imaani, Tumche Allaah na Tufanye Mema
from fisabilillaah.com http://bit.ly/2SzcPla
via IFTTT
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni