Swali
Je, ni lazima kuelekea Qiblah wakati wa kuchinja...?
Jibu
Kuelekea Qiblah wakati wa kuchinja sio wajibu.
Mtu anaweza kuchinja kichinjwa chake ijapokuwa hakuelekea Qiblah. Lakini wanachuoni (Rahimahumu Allaah) wamesema kuwa bora zaidi ni mtu aelekee Qiblah. Kwa sababu ni ´ibaadah.
Lakini hata hivyo hawakusema kuwa ni sharti. Iwapo mtu atachinja kwa kuelekea upande usiokuwa Qiblah ni halali. Sio jambo limechukizwa. Hapana neno.
Tofauti na wanavosema watu wasiokuwa na elimu. Baadhi yao wanasema kwamba ni lazima kuelekea Qiblah, jambo ambalo si sahihi.
Rejea : Al-Liqaa' ash-Shahriy (42)
from fisabilillaah.com http://bit.ly/2SvU024
via IFTTT
Translate
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah
إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! 20 - Isti’aadhah (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah ...
-
Dalili 18 zinazoashiria una ujauzito wa mtoto wa kiume Awali ya yote nitoe pongezi kwa mama K na Baba K wote popote walipo kwa kazi nzuri ...
-
Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh YAFUATAYO NI MAJINA YA MASWAHABA WANAWAKE (RADHI ZA ALLAAH...
-
SWALI: Assalaam alaykum Naomba maana ya majina yeyote tuwapao watoto wetu AU mnielekeze wapi naweza kupata labda katika kitabu cha fas...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni