Translate

Jumamosi, 19 Januari 2019

Watoto kujifanyia ´Aqiyqah wao wenyewe ikiwa baba hakufanya

Swali: Kuna mtu ana watoto sita na hakumfanyia ´Aqiyqah isipokuwa mmoja tu katika wao. Ni ipi hukumu? Ni lipi la wajibu kwake? Je, ni wajibu kwa watoto kujifanyia wao wenyewe ´Aqiyqah pamoja na kuzingatia ya kwamba watatu katika wao wana uwezo juu ya hilo?

Jibu: Ikiwa baba huyu ambaye hakuwafanyia ´Aqiyqah watoto wake wote hawa ni fakiri hakuna kinachomlazimu. Kwa sababu ´Aqiyqah ni kama mfano wa zakaah. Kama ambavo fakiri halazimiki zakaah kadhalika fakiri halazimiki vilevile ´Aqiyqah.

Lakini kama alikuwa ni tajiri lakini kila siku anasema kwamba atafanya kesho kesho, katika hali hii tunamwambia kwamba awafanyie ´Aqiyqah watoto wake ambao hakuwafanyia. Wakitaka baadhi yao kujifanyia wao wenyewe, basi wapate kwanza idhini kutoka kwa baba yao na wamweleze kwamba wanataka kujifanyia wao wenyewe. Kwa sababu jukumu la ´Aqiyqah ni la baba.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2Cvba9b
via IFTTT

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...