Translate

Ijumaa, 28 Desemba 2018

Swalaah ya Ijumaa ni Fardhi kwa kila Mwanamume

                            SWALAH  YA  IJUMAA NI  FARDHI  KWA  KILA  MWANAUME



Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh


Swalaah ya Ijumaa ni Fardhw ‘Ayn (Fardhi kwa kila mtu mwanamme) wala haijuzu kuiacha kwa sababu ya kazi au masomo  na sababu kama hizo.

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

“Na yeyote anayemcha Allaah; Atamjaalia njia ya kutoka (shidani).”


[Rejea Kitab Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/184)]


Ndugu zangu katika Imaani, Swalaah ya Ijumaa ni fardhi kwa kila mwanamme mwenye kukafilika katika ‘Ibaadah, mkazi, wala haikupasi kuikhalifu kwa sababu ya kazi hata kama mwajiri wako atakukataza.

[Rejea Kitab Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/185)]


Kwahiyo ndugu zangu katika Imaani ni wajibu kwa wanaume kuswali Ijumaa pamoja na ndugu zao Waislamu katika nyumba za Allaah (Misikitini). Ama wanawake wao hawana Ijumaa na ni wajibu kwao kuswali Adhuhuri.


[Rejea Kitab Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/196)]


Na  Allaah  anajua  zaidi


from fisabilillaah.com http://bit.ly/2CDjMvY
via IFTTT

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...