Translate

Alhamisi, 21 Machi 2019

Maana ya Masiku Meupe

MAANA YA MASIKU MEUPE

Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh

Yameitwa ‘Biydhw’ (meupe) sababu usiku wa siku hizo hung'aa kutokana na mwanga wa mwezi. Ayyaam Al-Biydhw (Masiku Meupe) tarehe zake ni 13, 14 na 15 katika kila mwezi wa kalenda ya Kiislamu.

عَنْ جريرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَن النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيهِ وَسَلَّمَ قَالَ  : ((صِيَامُ ثَلاثَةِ أَيَّامٍ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ صِيَامُ الدَّهْرِ ، أَيَّامُ الْبِيضِ صَبِيحَةَ ثَلاثَ عَشَرَةَ وَأَرْبَعَ عَشَرَةَ وَخَمْسَ عشَرَةَ)) 

Imepokelewa kutoka kwa Jariyr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabii (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

((Swiyaam (kufunga) siku tatu kila mwezi ni sawa na swiyaam ya dahari (milele!) Na masiku meupe ni tarehe kumi na tatu, kumi na nne na kumi na tano [13, 14, 15])) 

[An-Nasaaiy (2420) na ameisahihisha Al-Abaaniy katika Swahiyh At-Targhiyb (1040) ]

عن أبي ذر رضي الله عنه: قال لي رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((يَا أَبَا ذَرٍّ ، إِذَا صُمْتَ مِنَ الشَّهْرِ ثَلاثَةَ أَيَّامٍ فَصُمْ ثَلاثَةَ عَشَرَ وَأَرْبَعَةَ عَشَرَ وَخَمْسَةَ))

Imepokelewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia:

((Ee Abu Dharr! Endapo utafunga (swiyaam) siku tatu za kila mwezi, basi funga siku ya 13, ya 14, na ya 15))

[Imepokewa na At-Tirmidhiy na kasema Shaykh Al-Albaaniy kuwa ni Swahiyh ]

قال صلى الله عليه وسلم: ((أَلا أُخْبِرُكُمْ بِمَا يُذْهِبُ وَحَرَ الصَّدْرِ صَوْمُ ثَلاثَةِ أَيَّامٍ مِنْ كُلِّ شَهْر))

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

((Je, nikujulisheni jambo litakaloondosha uovu wa moyo? Ni swiyaam (kufunga) siku tatu kila mwezi))

[An-Nasaaiy 2/2386 na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh An-Nasaaiy (2249)]

Asw-Swuyuutwiy (Rahimahu Allaah) amesema katika An-Nihaayah: "Uovu wa moyo ni; udanganyifu, wasiwasi, na imesemwa pia ni uhasidi, chuki, na imesemwa pia uadui na imesemwa ghadhabu".

Na Allaah anajua zaidi



https://ift.tt/2uhSFRY i live islam

Maoni 2 :

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...