Swali: Nimesoma Hadiyth yenye kusema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayeniswalia kwa siku mara elfumoja, basi hatokufa mpaka abashiriwe Pepo.” Ameipokea Abush-Shaykh kutoka kwa Anas (Radhiya Allaah ´anh)
Je, Hadiyth hii ni Swahiyh, nzuri au dhaifu? Inafaa kuitumia kama hoja? Ikiwa ni Hadiyth Swahiyh ni yepi malengo ya kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?
Jibu: Hadiyth hii haijasihi kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kila Hadiyth ambayo ndani yake kuna kumuwekea kiwango cha kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni dhaifu. Kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni jambo limewekwa kwa njia ya kuachwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameamrisha kukithirisha kumswalia sana na khaswa siku ya Ijumaa. Ameeleza kuwa swalah zetu anafikishiwa (´alayhi-Swalaatu was-Salaam).
Hivyo, kithirisha kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) nyakati zote na bila ya kuweka idadi maalum. Atayemswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mara moja, basi Allaah atamswalia kwa swalah hiyo mara kumi.
from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2FUn9QU
via IFTTT
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni