Translate

Jumatano, 23 Januari 2019

Mamrisho ya kumswalia Mtume kwa kiwango maalum

Swali: Nimesoma Hadiyth yenye kusema:

“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Atakayeniswalia kwa siku mara elfumoja, basi hatokufa mpaka abashiriwe Pepo.” Ameipokea Abush-Shaykh kutoka kwa Anas (Radhiya Allaah ´anh)

Je, Hadiyth hii ni Swahiyh, nzuri au dhaifu? Inafaa kuitumia kama hoja? Ikiwa ni Hadiyth Swahiyh ni yepi malengo ya kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?

Jibu: Hadiyth hii haijasihi kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kila Hadiyth ambayo ndani yake kuna kumuwekea kiwango cha kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni dhaifu. Kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni jambo limewekwa kwa njia ya kuachwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameamrisha kukithirisha kumswalia sana na khaswa siku ya Ijumaa. Ameeleza kuwa swalah zetu anafikishiwa (´alayhi-Swalaatu was-Salaam).

Hivyo, kithirisha kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) nyakati zote na bila ya kuweka idadi maalum. Atayemswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)  mara moja, basi Allaah atamswalia kwa swalah hiyo mara kumi.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2FUn9QU
via IFTTT

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...