Swali: Katika Sunnah kumethibiti Takbiyr iliyofungamanishwa (Muqayyad)?
Jibu: Takbiyr iliyofungamanishwa kwa mujibu wa wanachuoni inakuwa baada ya zile swalah tano. Kuanzia siku ya ´Arafah mpaka ile siku ya mwisho ya Tashriyq. Mtu anatakiwa kuleta Takbiyr siku ya ´Arafah, siku ya ´Iyd na yale masiku matatu ya Tashriyq. Kwa mwenye kuhiji ni pindi atapohudhuria ile siku ya kuchinja atakaporusha mawe kwenye nguzo ya ´Aqabah. Hii ndio Takbiyr iliyofungamanishwa. Imechukuliwa katika maneno Yake (Ta´ala):
وَاذْكُرُوا اللَّـهَ فِي أَيَّامٍ مَّعْدُودَاتٍ
”Mtajeni Allaah katika siku za kuhesabika.”[1]
[1] 02:203
from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2HmUvKQ
via IFTTT
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni