Faida ya pili: Muheshimiwa msomaji ameona matamshi mbalimbali yote ndani yake kuna kuwasifu jamaa zake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), wakeze na kizazi chake pamoja naye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa ajili hiyo sio Sunnah wala kuafikiana na maamrisho yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mtu peke yake kusema:
اللهم صل على محمد
“Ee Allaah! Msifu Muhammad.”
Ni lazima kwa mtu kusoma sentesi/jumla yote kamilifu kama ilivyopokelewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Katika suala hili hakuna kutofautisha kati ya Tashahhud ya kwanza na Tashahhud ya pili. Haya yamesemwa na Imaam ash-Shaafi´iy:
“Tamko katika ile Tashahhud ya kwanza na Tashahhud ya pili ni moja. Hakuna tofauti. Tashahhud maana yake ni kushuhudia na kumsifu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Haisihi moja pasi na nyingine.”[1]
Kuhusu Hadiyth inayosema:
“Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) baada ya Rak´ah mbili hasomi zaidi ya kushuhudia.”
Ni dhaifu sana, kama nilivyothibitisha katika “adh-Dhwa´iyfah”[2].
[1] al-Umm (1/102).
[2] 5816.
from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2F1sy9v
via IFTTT
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni