Translate

Jumatatu, 28 Januari 2019

Mume afanye nini ikiwa mkewe hataki kuswali?

*Swali*

Mume achukue hatua gani ikiwa mke hataki kuswali?

*Jibu*

✅Mara nyingi kama vile wanawake wanashindwa kufuata maagizo ya kuchagua mume wa sawa Kidini ndivyo wanaume wanavyofanya makosa hayo hayo.

➡Mume wa Kiislamu anatakiwa amchague mke mwenye Dini na Imani, maadili na tabia nzuri.

✅Kukosa kufuata maagizo hayo ya Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ndio kunatokea matatizo kama hayo.

➡Hata hivyo, kosa lishatokea na inabidi tupate suluhisho kwa suala hilo nyeti.

➡Kulingana na maelezo yako ni kuwa mkeo inaonyesha bado ana Uislamu na Imani, hivyo anataka msukumo wa kuweza kutekeleza wajibu huo bila ya tatizo.

➡Jambo ambalo unatakiwa mwanzo kabisa kufanya ni kumnasihi mkeo kwa njia nzuri, kwani Allaah (Subhaana wa Taala) Anatuambia⤵

“Waite waelekee kwenye Njia ya Mola wako Mlezi kwa hikima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora”
↪Rejea Qur'an 16: 125.

➡Inatakiwa utumie mbinu tofauti za kuweza kumvutia katika kuswali bila ya yeye kuwa na kinyongo juu ya suala hilo.

➡Mpatie vipeperushi kuhusu umuhimu wa Swalah na madhara ya kuacha, vitabu, kanda, kaseti na njia nyingine.

✅Ikiwa imeshindikana hilo, itabidi sasa uingize mkono wa wazazi wenu kama inavyotaka sheria.

➡Allaah (Subhaana wa Taala) Anasema kwamba⤵

“Na ambao mnachelea kutoka katika utiifu wanasihini, muwahame katika malazi na wapigeni. Wakikutiini msiwatafutie njia ya kuwaudhi bure. Hakika Allaah ndiye Aliye juu na Mkuu. Na mkichelea kutakuwapo mfarakano baina ya mke na mume basi pelekeni muamuzi kutokana na jamaa za mume, na muamuzi kutokana na jamaa za mke. Wakitaka mapatano Allaah Atawawezesha. Hakika Allaah ni Mjuzi Mwenye khabari”
↪Rejea Qur'an 34 – 35.

➡Hivyo Mume inatakiwa ufuate mfumo ufuatao⤵

1⃣Kuwanasihi katika ya haki na ukweli.

2⃣Mhame(Jitenge naye katika Kitanda) katika malazi.

3⃣Mpige mkeo kipigo ambacho hakitamuumiza bali cha kumtisha wala usimpige uso.

4⃣Kuwe na suluhisho kwa kutumia waamuzi kutoka upande wa mke na mume ili waamue hilo.

✅Ikiwa hakukupatikana suluhisho lolote na wala mkeo hakubadilika basi itabidi umuache.

➡Na ikiwa itatokea hilo itabidi usirudie kosa tena unapotaka kuoa mwingine. Hata hivyo, tunaamini kuwa haitofikia hapo, In Shaa Allaah

Na Allaah Anajua zaidi

Imeandaliwa na *Imaam Masjid Tawbah*



from fisabilillaah.com http://bit.ly/2CL0y68
via IFTTT

Hukmu ya Mke Asiyeswali

SWALI

 

Ni ipi hukmu ya mke asiyeswali, kwa kutambua kuwa nimeshambainishia adhabu anayopata mwenye kuacha kuswali, kuna baadhi ya nyakati anaswali na wakati mwengine anaacha. Kwa mfano anaswali Adhuhuri na anaacha (Swalaah) zote za Faradhi zilizobaki?

 

 

JIBU

 

Hukmu yake ni Kafiri.

Na haijuzu kuendelea kubaki naye katika hifadhi yako. Inapasa kuwa naye mbali, isipokuwa kama atatubu tawbah ya kweli, la sivyo, ni waajib kuwa naye mbali (kuachana naye).

Kwa sababu kuacha Swalaah ni ukafiri mkubwa.

 

Anasema Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

“Baina ya mtu na baina ya ushirikina na ukafiri ni kuacha Swalaah.” [Muslim]

 

Na anasema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

“Agano (Kinachotutofautisha) baina yetu (Waumini) na baina yao (Washirikina, Makafiri na Wanafiki) ni Swalaah, anayeiacha (Swalaah) amekufuru.” [At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na An-Nasaaiy]

 

Hii ndio kauli sahihi katika kauli za Wanachuoni; kwamba kuiacha (Swalaah) ni ukafiri mkubwa.

 

Na Allaah anajua zaidi



from fisabilillaah.com http://bit.ly/2WqkhkE
via IFTTT

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake.

Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika Swahiyh yake wenye kichwa cha habari, “Elimu Kabla Ya ‘Amali”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.

 

Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo.

Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi, kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema:

Wakikutiini, basi msiwatafutie njia” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii inamaanisha kuwa lau wake zenu watakutiini kwa mnayowaamrisha basi msiwatafutieni njia za kuwadhuru.

 

Na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

Mbora wa wanawake wote ni yule ambaye unapomuangalia hukufurahisha, na unapomuamrisha hukutii na unapokuwa haupo naye, hukulindia nafsi yake na mali yako” (Abu Daawuud).

 

Hivyo, mke wako anafaa kishari’ah awe ni mwenye kukutii na asiwe ni mwenye kutoka bila ya ruhusa yako.

Na Allaah Anajua zaidi



from fisabilillaah.com http://bit.ly/2RlWxKT
via IFTTT

Hukmu ya mke kutoroka kwa Mumewe sababu ya mume kuongeza mke wa pili

Naam

➡Hakika ni kuwa ni vigumu kutoa hukumu ya moja kwa moja kwani tumesikia kesi au kujitetea kwa upande mmoja. Hatujasikia yaliyomfanya mke atoroke. Hata hivyo, katika hali yoyote ile mke kisheria hafai kutoka kwa mumewe kwa sababu yoyote ila iwe kwa ajili ya kisheria ambayo amemnasihi mumewe mpaka akachoka.

➡Suala la mke kutoka mara moja ni ikiwa mume ameritadi kutoka katika Uislamu au maasiya makubwa dhahiri shahiri.

➡Mara nyingi wake kwa wivu ulio nje ya sheria hupandwa na hasira wakafanya mambo kama hayo kisha wakajuta baadaye. Wakati huo huenda majuto kama hayo yakawa hayana faida yoyote ile.

➡Kwa kuwa suala hilo lishatendeka wewe usiwe na hasira bali fuata njia za kisheria kumpata na kumrudisha mkeo. Njia ya rahisi ni kwako kwenda kwa wazazi wake na kutoa taarifa hiyo.

➡Mbali na kuwa wazazi wake huenda wakawa pamoja na binti yao. Hiyo ni kwa kuwa mke wa mtu akaja kwa wazazi na wazazi nao wakamuacha bila kumshurutisha kurudi.

➡Hata hivyo, tukichukulia dhana nzuri ni kuwa huenda wazazi walimwambia arudi kwako naye akatoka lakini asifike kwako. Kwa hiyo, nenda kwa wazazi wake na uzungumze nao kwa upole, ulaini na kwa heshima kuhusu hilo.

➡Kwa mke kumtoroka mumewe kwa sababu yoyote ile au bila ya sababu ni makosa ambayo mwanamke wa Kiislamu hafai kufanya kabisa. Ikiwa mume amemkosea mke zipo njia ambazo zinaweza kufuatwa ili kutatua tatizo ambalo limetokea. Inatakiwa tuelewe kuwa kosa halitatuliwa na kosa.

➡Uislamu umeweka nidhamu ya kila jambo na kutoa suluhisho kwa matatizo yetu yote hata katika mas-ala ya ndoa, talaka na mengineyo. Kutoroka kutoka nyumba ya mume huwa bado hujatatua tatizo ambalo lipo. Ikiwa mume amemkosea mke inatakiwa mke amueke chini na kumueleza anavyofikiri kwa lile jambo.

➡Ikiwa hakuweza kutatua, anaweza kuwatumia wazazi wake na wale wa mumewe au masheikh wazoefu katika mas-ala ya suluhu za kindoa. Mke kafanya vizuri kujirudi kwa makosa yakutoroka kwani makosa hayasamehewi na Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) mpaka mtu aombe msamaha kwa aliyemkosea akiwa ni mwanadamu mbali na kujuta, kuwa na azma ya kutorudia kosa na pia kutolifanya kosa hilo. Sasa mke hajaomba msamaha kwani huu unakuwa ni kama mfano wa gazeti la Denmark, Jyllands-Posten, pale meneja aliposema tunaomba msamaha kuwaudhi Waislamu lakini sio kuchapisha vikaragosi vya Mtume Muhammad(Swalla Allahu  'alayhi wa aalihi wa sallam). Na hapa tunaona hivyo hivyo kuwa mke amejirudi kwa kumuomba mumewe msamaha lakini hataki kubaki naye na mas-ala makubwa ya mtu anapofanya kosa na kusamehewa ni ajiondoe katika lile kosa na kurudi kama awali.

➡Ili kosa hilo kuondoka ni mke arudi baada ya kusamehewa katika nyumba yake ili waweze kuishi pamoja na mumewe na wawalee watoto wao ikiwa wanao. Na lau amekimbia kwa sababu ya tatizo baina yake na mumewe wanaweza kukaa chini na wakaangalia ni njia gani wanaweza kutumia ili kusuluhisha tatizo hilo.

➡Allaah (Subhaana wa Taala) Anasema kwamba⤵

“Na mkichelea kutakuwapo mfarakano baina ya mke na mume basi pelekeni muamuzi kutokana na jamaa za mume, na muamuzi kutokana na jamaa za mke. Wakitaka mapatano Allaah Atawawezesha. Hakika Allaah ni Mjuzi Mwenye khabari”
↪Rejea Qur'an 4: 35.

✅Mwanamke kama huyu hatima yake ni mbaya hapa ulimwenguni na Kesho Akhera, kwani Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Ikiwa mwanamke yeyote atamuomba mumewe talaka bila ya kuwa na sababu nzito (yenye nguvu), harufu ya Pepo itakuwa ni haramu kwake”
↪Imepokelewa na Imaam Abu Dawuud kutoka kwa Thawbaan [Radhiya Allahu 'anhu] )

✅Hii itakuwa ni hasara ambayo mke atapata Kesho Akhera.

✅Tufahamu kuwa hapa duniani pia atapigwa muhuri wa unafiki. Mtume (Swalla Allahu  'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Wanawake ambao watajiachisha kutoka kwa waume zao na wanawake wenye kuwashawishi waume zao wawapatie talaka kwa malipo ni wanafiki”
↪Imepokelewa na Imaam At-Tirmidhiy na an-Nasa’iy kutoka kwa Abu Hurayrah [Radhiya Allahu 'Anhu] 

➡Na hakika ni kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Amewazungumzia wanawake ambao wana sifa ya kubaki na waume zao hata kama waume wanataka kuwaacha kwa kuwa na maagano na ahadi kati yao.

➡Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema kwamba⤵

“Na mwanamke akichelea kutupwa au kutojaliwa na mumewe, basi si vibaya kwao wakisikizana kwa suluhu. Na suluhu ni bora. Na nafsi zimewekewa machoni mwake tamaa na choyo. Na mkifanya wema na mkamchamngu basi hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari za yote mnayoyatenda”
↪Rejea Qur'an 4: 128.

➡Aishah (Radhiya Allahu 'anha) amesema yafuatayo kuhusu aya hii kuwa⤵

“Ikiwa mwanamke akichelea kutupwa au kutojaliwa na mumewe” (yaani mume ameona kitu asichopenda kwa mkewe, kama uzee au mfano wake, na akataka kumpatia talaka, lakini mke akamtaka mume akae na ampatie anachopenda mwenyewe. Ndio Allah Akasema: ‘basi si vibaya kwao wakisikizana kwa suluhu’”
↪Imepokelewa na Imaam Al-Bukhaariy. 

➡Ikiwa hakutakuwa na natija yoyote na mke akakataa kukaa kwako kwa ajili ya kuoa mke wa pili basi ni afadhali umuache na ubakie na huyo wa pili kwani ukitofanya hivyo utasumbuka pasi na kuwa na haja hiyo.

Na Allaah Anajua zaidi

Imeandaliwa na *Imaam Masjid Tawbah*



from fisabilillaah.com http://bit.ly/2Wrs1mo
via IFTTT

He, Uislamu umegawanyika makundi?

*Swali*

Jee
Uislam umegawanyikaaa?
Una makundii?

*Majibu*

✅Naam ni kweli kwamba Uislamu umegawanyika katika Makundi tofauti tofauti.

➡Kwa kifupi tu kwa kukupa mwangaza kidogo, utayajua yale makundi yaliyo potofu kwa kuona na kujua itikadi zao.

➡Mfano mzuri leo utaona wanaodai kuna mtume baada ya Mtume wa haki na wa mwisho Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), utawaona pia wale wanaowakufurisha Maswahaba (Radhiya Allaahu ‘anhum) na kuwatukana wake za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), pia utawaona wengine wanaokufurisha Waislam na kuwatoa katika Dini kwa sababu wanaamini kuonekana Allaah Qiyaamah, na wanakufurisha Waislamu kwa sababu ya kufanya baadhi ya maasi, na pia utawaona wengine wanakataa Hadiyth za Mtume na kudai kuwa wao wanafuata Qur-aan pekee, na pia utawakuta wengine wanakwenda kuwaomba watu waliokufa makaburini ili wawasaidie haja zao, na wengi wengine wasio na idadi.

➡Tutalijua kundi lililookoka na ambalo halipo katika hayo makundi 72, kwa kuitazama ile Hadiyth ya bwana Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) isemayo⤵

((Wamegawanyika Mayahudi katika mapote 71, wakagawanyika Wakristo katika mapote 72 na Ummah wangu utagawanyika mapote 73. Yote hayo yataingia motoni ila moja tu)) Maswahaba waliuliza: Ni lipi hilo, ewe Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wa Allaah! Akasema: ((Ni lile nililokuwemo mimi na Swahaba zangu))
↪Imepokelewa na Imaam Ahmad, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na Ad-Daarimiy.

✅Kundi hilo litakuwa ni lenye kufuata maagizo ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala), Sunnah za Mtume Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Makhalifa waongofu (Radhiya Allaahu ‘anhum) na Maswahaba wengine (Radhiya Allaahu ‘anhum) na wema wote waliotangulia (Salafus-Swaalih). Muislam atakayejikita na kuwa imara katika hayo basi atakuwa katika njia nyoofu. Dalili ni nyingi katika Qur-aan na Sunnah.

➡Miongoni mwayo ni kauli ya Allaah (Subhaana wa Taala)⤵

((Na anayemtii Allaah na Mtume Wake, bila ya shaka amefanikiwa mafanikio makubwa))
↪Rejea Qur'an 33: 71. 

➡Pia Amesema Allaah (Subhaana wa Taala)⤵

((Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Allaah basi nifuateni mimi, Allaah Atakupendeni na Atakufutieni madhambi yenu. Na Allaah ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu))
↪Rejea Qur'an 3: 31.

➡Mtume Muhammad(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) naye anatueleza yafutayo katika khutbah yake ya Hijjatul Wadaa: ((Hakika nimewaachia kitu ambacho hamtapotea baada yangu lau mtashikana nacho, Kitabu cha Allaah))
↪Imepokelewa na Imaam Muslim

Sehemu nyengine kasema: ((Kitabu cha Allaah na Sunnah zangu))
↪Imepokelewa na Imaam Al-Bukhaariy na Muslim.

➡Na katika masimulizi ya Abu Najiih al- 'Irbaadh bin Saariyah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba⤵

"Alituwaidhia Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) yaliyozifanya nyoyo kuingia hofu na macho yakatokwa na machozi. Tukamwambia: "Ewe Mtume wa Allaah! Yaonyesha kama haya ni mawaidha ya kuaga, basi tuusie". Akasema: ((Nawausia kumcha Allaah, Kwani hakika atakayeishi katika nyinyi ataona khitilafu nyingi, basi jilazimisheni kufuata Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa walioongoka, yashikeni kwa magego mambo yao))
↪Imepokelewa na Imaam Abu Daawuwd, Ahmad, At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na Ad-Daarimiy

✅Mambo muhimu ambayo tunayapata katika dondoo za hapo juu ni kuwa, kuwepo kwetu katika kundi litakaloongoka ni kufuata mwendo aliokuwa nao Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Makhalifa wake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na kushikamana nao kivitendo barabara.

Tunamuomba Allaah Aliyetukuka Atufanye ni wenye kuyashikilia hayo vilivyo ili tuwe ni wenye kuingia katika Rehma Yake na kuwa ni kundi lililosalimika na moto, kundi lililonusurika na ni kundi liliokoka. Tunamuomba Allaah Aliyetukuka Atusahilishie hatua zetu katika kuelekea katika mwendo wa sawa na wa haki.

Na Allaah Anajua zaidi 

Imeandaliwa na *Imaam Masjid Tawbah*



from fisabilillaah.com http://bit.ly/2RlWwqj
via IFTTT

07. Kulenga kusikika katika mambo ya ki-´Ibaadah ni shirki ndogo

Vivyo hivyo mtu kutaka kusikika. Ni kama kujionyesha. Kutaka kusikika ni kule mtu kupenda asikike na watu. Kwa mfano wasikie du´aa zake, kauli zake ambazo uinje wake ni nzuri na anaonekana anamdhukuru Allaah ilihali anachokusudia watu wamsifu na watu waseme kwa kweli fulani anamdhukuru Allaah sana, fulani anatafuta elimu, anafundisha elimu, fulani anafanya hivi na vile. Anaboresha sauti yake katika kisomo cha Qur-aan kwa ajili ya kutaka kusifiwa na watu. Yote haya ni katika aina za mtu kutaka kusikika. Mwenye kutaka kuonekana, basi Allaah atamfanya kweli aonekane. Kwa sababu malipo yanategemea na vile mtu alivyotenda. Mwenye kutaka kusikika, basi Allaah atamfanya kweli asikike.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2CMSvG8
via IFTTT

06. Kulenga kujionyesha katika mambo ya ki-´Ibaadah ni shirki ndogo

Miongoni mwa hayo ni yale yanayokuwa ndani ya moyo katika kujionyesha. Bi maana mtu akajionyesha kwa matendo. Mtu akafanya ´ibaadah uinje wake zikaonekana ni kwa ajili ya Allaah pamoja na kwamba anawaonyesha watu. Lengo anataka watu wamsifu, wamtape n.k. Huku ndio kujionyeasha. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Je, nisikwambieni kile ninachokukhofieni kuliko hata huyo al-Masiyh ad-Dajjaal?” Wakasema: “Ndio, ee Mtume wa Allaah!” Akasema: “Ni shirki iliyojificha.”

Shirki iliyojificha ni kujionyesha. Kwa sababu inakuwa ndani ya moyo na hakuna aijuaye isipokuwa Allaah pekee.

“Anasimama mtu kuswali na akaipamba swalah yake kwa kuwa anaona watu wanamwangalia.”[1]

Amesema (Ta´ala):

فَوَيْلٌ لِّلْمُصَلِّينَ الَّذِينَ هُمْ عَن صَلَاتِهِمْ سَاهُونَ الَّذِينَ هُمْ يُرَاءُونَ

“Basi adhabu kwa wanaoswali, ambao kuhusu swalah zao wanapuuza, ambao wanajionyesha.” (107:04-07)

Kujionyesha ni khatari. Ni jambo ambalo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kalikhofia juu ya Maswahabah zake. Kwa sababu kila mtu anapenda sifa, matapo, kuonekana kwa sura nzuri n.k., huenda hayo yakampelekea akaanza kujionyesha katika mambo ya ´ibaadah. Kujipamba mwili wake kwa mavazi na nguo nzuri, hili ni jambo linalotakikana kujipamba na kuvaa vizuri. Ama kuyapamba matendo yake mbele za watu ilihali hakusudii uso wa Allaah, bali kinyume chake anawakusudia watu, huu ndio msimba mkubwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Kikubwa ninachokikhofia juu yenu ni shirki iliyojificha.” Wakasema: “Ni ipi hiyo, ee Mtume wa Allaah?” Akasema: “Ni kujionyesha.”

Imeitwa ´kujionyesha` (Riyaa`) kwa sababu malengo yake anataka watu wamuone.

[1] Ahmad (11270) na Ibn Maajah (4203). Nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Sunan Ibn Maajah” (3389).



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2RUi82h
via IFTTT

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...