Translate

Jumamosi, 26 Septemba 2020

Faida 10 za mayai kiafya

FAIDA 10 ZA MAYAI KIAFYA

Mayai ni moja ya vyakula vichache ambavyo naweza kuviweka katika kundi la vyakula ‘bora zaidi’ kuliko vyote.

Mayai yamejaa viinilishe mhimu na vingi kati ya hivyo viinilishe havipatikani kirahisi katika vyakula vingi vya kisasa.

Zifuatazo ni faida 10 za kiafya zitokanazo na kula mayai kama zilivyothibitishwa katika tafiti nyingi duniani:

1. Mayai yana virutubisho vya kushangaza

Mayai ni moja ya vyakula vyenye virutubisho vizuri zaidi katika sayari dunia.
Yai moja zima lina viinilishe vyote vinavyohitajika kuibadili seli moja kuwa kifaranga cha kuku.

Yai moja kubwa lililochemshwa lina:
Vitamin A: 6%
Folate: 5%
Vitamin B5: 7%
Vitamin B12: 9%
Vitamin B2: 15%
Phosphorus: 9%
Selenium: 22% o

Mayai pia yana kiasi cha kutosha cha Vitamini D, Vitamini E, Vitamini K, Vitamini B6, kalsiamu na Zinki.

Yai moja pia linakuja na kalori au nishati 77, gramu 6 za protini na gramu 5 za mafuta yenye afya au mafuta safi kwa ajili ya mwili (healthy fats).

Mayai pia yana viinilishe vingine vidogo vidogo (trace nutrients) ambavyo ni mhimu kwa afya bora.

Hakika… mayai ni chakula ambacho ni karibu kimejikamilisha, mayai yana karibu kila aina ya kiinilishe mhimu tunachokihitaji kila siku.

2. Mayai huwa na kolesto nyingi lakini hayaathiri kolesto katika damu

Ni kweli kwamba mayai yana kolesto nyingi.

Ukweli ni kuwa, yai moja tu huwa na kolesto mg 212, ambayo ni zaidi ya nusu ya kiasi cha kolesto ambacho imependekezwa ule kwa siku ambacho ni mg 300.

Hata hivyo…ni mhimu kuelewa kuwa kolesto katika mlo huwa si lazima ipandishe kolesto ya kwenye damu.

Kwa kawaida Ini peke yake huzalisha kiasi kingi cha kolesto kila siku. Wakati tunapokuwa tumekula mayai zaidi, Ini lenyewe huzalisha kiasi kidogo zaidi cha kolesto ili kusawazisha hiyo tofauti.

Matokeo ya ulaji wa mayai hutofautiana toka kwa mtu mmoja hadi mwingine:

. Asilimia 70 ya walaji wa mayai hawapati kabisa kuongezeka kwa kolesto .
. Asilimia 30 ya walaji wanaripotiwa kuwa wanatokewa kuongezeka kwa kolesto

3. Mayai huuongeza Msongamano wa juu wa lipoprotini kolesteroli (Kolesto nzuri)

Mayai huuongeza Msongamano wa juu wa lipoprotini kolesto ijulikanayo kwa kiingereza kama ‘High Density Lipoprotein’ (HDL). Ambayo hujulikana kama ni kolesto nzuri, maana kuna kolesto nzuri na kolesto mbaya.

Watu wenye msongamano wa juu wa lipoprotini kolesto kwa kawaida huwa na uwezekano mdogo wa kupatwa na maradhi kama ugonjwa wa moyo, kiharusi (stroke) na matatizo mengine mengi ya kiafya.

Kula mayai ni njia nzuri ya kuongeza msongamano wa juu wa lipoprotini kolesto.

Katika moja ya majaribio; kula mayai 2 kwa siku kwa wiki 6 kuliwezesha kuongezeka asilimia 10 ya msongamano wa juu wa lipoprotini kolesto.

4. Mayai yana kiinilishe mhimu sana kiitwacho ‘Choline’

Choline ndicho kiinilishe mhimu kabisa ambacho watu wanakikosa na watu wengine hawana habari kabisa juu ya uwepo wake.

Ndiyo, ni kiinilishe mhimu zaidi na mara nyingi hupangwa pamoja na vitamini za kundi B.

Hiki ni kiinilishe kinachopatikana katika mayai ambacho kazi yake kuu mwilini ni kutengeneza ukuta wa seli na kinacho kazi pia ya kutengeneza molekuli za hisia katika ubongo na kazi zingine nyingi.

Tafiti zinaonyesha zaidi ya asilimia 90 ya watu wanapata kiasi kidogo cha choline kati ya kile ambacho kimependekezwa kila mmoja ale kwa siku.
Yai zima, lote, ni chanzo kizuri cha choline.

Yai moja huwa na zaidi ya mg 100 za kiinilishe hiki mhimu ambacho watu wengi hawakijuwi.

5. Mayai hubadili msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto

Msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto au kwa kiingereza ‘Low Density Lipoprotine’ (LDL) ndio ambao hujulikana kama ni kolesto mbaya.

Inajulikana wazi, kuwa na msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto huleta uwezekano wa hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo.

Lakini kile watu wengi hawakifahamu ni kuwa huu msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto umegawanyika tena katika matawi madogo ambayo yanafanya jumla ya chembe chembe za msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto.

Kuna msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto mdogo, kuna msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto wa kati na kuna msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto mkubwa zaidi katika hizo chembe chembe zinazounda msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto.

Tafiti nyingi zimeonyesha kuwa watu wenye msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto mdogo kwa muda mrefu, na msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto wa kati ndio ambao huwa na hatari kubwa zaidi ya kupatwa na ugonjwa wa moyo kuliko watu wenye chembe chembe nyingi za msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto mkubwa zaidi.

Hata kama mayai huwa na uwezo kidogo wa kuongeza kiasi cha msongamano wa chini wa lipoprotini kolesto katika baadhi ya watu, tafiti zinaonyesha kwamba chembe chembe hizo hubadilika toka katika usawa mdogo hadi katika usawa wa kati hadi kuja kuwa katika usawa mkubwa ambao ni jambo zuri.

mayai kwa afya

6. Mayai huondoa sumu na kusaidia kuongeza nuru ya macho

Moja ya matokeo ya kuzeeka ni macho kupoteza uwezo wake wa kuona vizuri.
Kuna viinilishe kadhaa ambavyo vinaweza kusaidia macho yetu kubaki na nuru na uwezo mzuri zaidi kwa miaka mingi hata uzeeni.

Moja ya viinilishe viwili mhimu zaidi katika kufanya kazi hiyo ni hivi vijulikanavyo kama Lutein na Zeaxanthin vipatikanavyo katika mayai, ambavyo ni viuaji sumu vyenye nguvu au vyenye kazi ya kuondoa sumu ambavyo hujijenga katika retina ya jicho.

Tafiti zinasema matumizi ya kutosha ya viinilishe hivi viwili yanaweza kupunguza kwa kiasi kikubwa hatari ya kupatwa na ugonjwa wa mtoto wa jicho (cataract).
Kwa ujumla kiini cha yai kina kiasi kingi kabisa cha Lutein na Zeaxanthin.

Katika moja ya jaribio, ulaji wa 1.3 wa kiini cha mayai kwa siku kwa wiki 4 ulionyesha kuongezeka kwa kiasi cha usawa wa Lutein kwa asilimia 28 hadi 50 na Zeaxanthin kwa asilimia 114 hadi 142.

Mayai pia yana kiasi kingi cha vitamin A. Upungufu wa vitamin A ndicho chanzo kikuu cha upofu katika sehemu nyingi duniani.

7. Mayai yenye kiasi kingi cha Omega-3 husaidia kupunguza mafuta yapatikanayo katika damu (triglycerides);

Kwa hakika, haijalishi ni chakula gani tunakula … tunaangalia pia ni vyakula gani ambavyo tunakula na tumekula.

Katika hili, ni kuwa siyo mayai yote ya kuku yapo sawa na ni mazuri. Viinilishe vilivyomo kwenye yai vinategemea ni kwa namna gani kuku waliotaga hayo mayai walikuwa wakilishwa nini na wamekua katika mazingira gani.

Mayai toka kwa kuku ambao wanafugwa vizuri na wanapewa vyakula vyenye Omega-3 hutokea kuwa na asidi mafuta mhimu zijulikanazo kama ‘Omega-3 fatty acids’.

Asidi mafuta Omega-3 zinajulikana katika kupunguza usawa wa mafuta yapatikanayo katika damu (triglycerides), ambayo yanahusika sana na ugonjwa wa moyo.

Tafiti zinaonyesha kwamba ulaji wa mayai yenye asidi mafuta Omega-3 ni njia nzuri zaidi katika kupunguza mafuta yapatikanayo katika damu.

Katika moja ya majaribio, ulaji wa mayai matano tu yenye asidi mafuta Omega-3 kwa wiki kwa muda wa wiki tatu kulipunguza mafuta yapatikanayo katika damu (triglycerides) kwa asilimia 16 hadi 18.

8. Mayai yana protini yenye ubora wa hali ya juu na amino asidi mhimu kwa uwiano mzuri

Protini ndiyo matofali mhimu zaidi katika ujenzi wa mwili wa binadamu.
Protini hutumika kutengeneza aina zote za tishu na molekuli ambazo ni mhimu katika ujenzi na ufanyaji kazi wa mwili.

Kupata kiasi cha kutosha cha protini katika mlo wako ni mhimu sana na tafiti zinaonyesha kiasi cha protini ambacho kimependekezwa kuwa ndicho unachopaswa kula kila siku chaweza kuwa ni kidogo sana.

Ndiyo… mayai ni chanzo kizuri kabisa cha protini, huku yai moja likiwa na gramu 6 za protini.

Mayai yana amino asidi zote mhimu zaidi kwa usawa mzuri na hivyo mwili wetu unakuwa umehakikishiwa utumikaji wa protini hiyo ipatikanayo katika mayai.

Kula kiasi cha kutosha cha protini kunaweza kuwa msaada katika kupunguza uzito, kuongeza uwingi wa mishipa, kupunguza shinikizo la juu la damu na kuimarisha afya ya mifupa, kwa kuyataja machache kati ya mengi ya faida ya ulaji wa kutosha wa protini.

9. Mayai hayaleti ugonjwa wa moyo na yanaweza kupunguza hatari ya kupatwa na kiharusi (Stroke)

Kwa karne nyingi au kwa miaka mingi sasa mayai yamekuwa yakisemwa vibaya sana bila sababu yoyote yenye ukweli.

Imekuwa ikiaminiwa kwamba kwa sababu mayai yana kiasi fulani cha kolesto ndani yake basi lazima yatakuwa ni mabaya kwa afya ya moyo!

Tafiti nyingi zilizofanywa katika miaka ya karibuni zimejaribu kuangalia uhusiano uliopo kati ya ulaji wa mayai na hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo.

Katika uchunguzi mmoja ukihusisha tafiti 17 katika jumla ya watu 263,938, hakuna uhusiano wowote ulioonekana kuwepo baina ya ulaji wa mayai na ugonjwa wa moyo.

Tafiti nyingi zaidi na zaidi zimeendelea kutoa hitimisho hili moja linalofanana.

Ingawa… baadhi ya tafiti zimeweza kuonyesha kuwa watu wenye kisukari hasa wenye kisukari cha aina ya pili wanaokula zaidi mayai wanakuwa na hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo.

Iwe ni kweli kwamba mayai yanasababisha kuongezeka kwa hatari ya kupatwa na ugonjwa wa moyo bado hili halijulikani, sababu tafiti za namna hii huwa zinaonyesha tu uhusiano wa kitakwimu, tafiti hizo huwa haziwezi kuthibitisha kwamba ni mayai ndiyo yamesababisha chochote.

Inawezekana kwamba baadhi ya wagonjwa wa kisuakri wana uelewa mdogo juu ya mambo mhimu kuhusu afya zao.

Katika mlo ambao inahimizwa kuepuka vyakula vya wanga, mlo ambao ndiyo watu wenye kisukari hushauriwa kuishi hivyo, ulaji wa mayai ungeweza kuwa ni msaada katika kuepuka hatari za kupatwa na ugonjwa wa moyo.

10. Mayai humtosheleza mlaji kwa haraka na hivyo kusaidia kupunguza uzito

Kwa hakika mayai ni matamu sana!

Ni chakula chenye protini ya kutosha… na kwa hakika protini ndiyo sehemu mhimu zaidi katika lishe.

Mayai yanashikilia alama ya juu kabisa katika kipimo kijulikanacho kama ‘Satiety Index’, ambacho kinapima uwezo wa chakula katika kumtosheleza na kumlidhisha mlaji huku yakiepusha ulaji wa kuzidi wa kalori.

Katika utafiti mmoja uliohusisha wanawake 30 wenye uzito uliozidi, kitendo cha kula mayai asubuhi badala ya mkate kiliwaongezea hisia za kujisikia kutosheka na hivyo moja kwa moja (automatically) wakafanikiwa kuwa wanakula chakula kiasi kwa masaa 36 yaliyofuata.

Katika jaribio lingine, kitendo cha kubadili kula mayai badala ya mkate katika mlo wa asubuhi kilisababisha kupungua uzito kwa haraka ndani ya kipindi cha majuma 8 tu.

NAMNA YA KUJUWA IWAPO MAYAI NI FRESHI AU LA

Utajuwaje kama haya mayai ni freshi au ni mapya kwamba yatakuwa hayajaharibika ndani yake?

Fanya hivi; weka maji ndani ya kindoo kidogo au hata katika bakuli kubwa, tumbukiza yai, ikiwa yai litakwenda moja kwa moja chini hilo ni yai zuri, ikiwa linaelea katikati ya maji hilo ni zuri lakini linatakiwa litumike haraka na ikiwa linaelea tu hapo juu ya maji hilo ni la kutupwa tu tayari limeshakuwa bovu.

UJUMBE MHIMU KUHUSU ULAJI MAYAI

Tafiti zinaonyesha ulaji wa mayai hadi matatu kwa siku ni salama kabisa kwa afya.

Hakuna ushahidi kwamba kula kwa kiasi hicho ni vibaya. Mimi binafsi ninakula wastani wa mayai 3 hadi 6 kwa siku na afya yangu ipo safi kabisa.

Ndiyo … mayai ni chakula cha asili ambacho ni safi kabisa.

Zaidi ya yote, mayai pia yanauzwa bei rahisi, ni rahisi kuyapika na yanaweza kulika karibu na kila chakula na yana ladha ya kipekee yawapo mdomoni.

Mayai mazuri, safi na salama kwa afya yataendelea kuwa ni mayai ya kuku wa kienyeji, yaani hawa kuku wetu wa kitanzania, wa asili.

Kama unauza mayai ya kienyeji niambie unauza bei gani na upo wapi.

Faida 10 za mayai kiafya Click To Tweet

Tafadhari SHARE post hii kwa ajili ya wengine

Fadhili Paulo
Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
Imesomwa mara 28

Let's block ads! (Why?)

Alhamisi, 24 Septemba 2020

15-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kuapa Kwa Asiyekuwa Allaah

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

15- Kuapa Kwa Asiyekuwa Allaah

Alhidaaya.com

 

 

 

Haijuzu Muislamu kuapa isipokuwa kwa Jina la Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa sababu kuapia kwa yeyote au chochote ni kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Inavyopasa kuapa ni ima kusema: “Wa-Allaahi”, au “BiLLaahi” au “Ta-Allaahi” kama ilivyothibiti katika Qur-aan. Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kuapia chochote isipokuwa kwa Jina la Allaah akasema:

 

 مَنْ حَلَفَ بِغَيْرِ اللَّهِ فَقَدْ كَفَرَ أَوْ أَشْرَكَ

((Atakayeapa pasi na Allaah, atakuwa amekufuru na amemshirikisha Allaah) [Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Ibn Hibbaan, Al-Haakim na wengineo na ameipa daraja ya Swahiyh Al-Albaaniy]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Pekee Ndiye Mwenye haki kuapia Atakacho kwani Yeye ni Muumba wa kila kitu. Ndio maana Anaapia katika Qur-aan vitu vingi; Wa-Tiyni waz-Zaytuni, Wal-‘Aswr, Wadh-Dhwuhaa, Wash-Shamsi, Wal-Layli, Wal-Fajr, Wal-‘Aadiyaat n.k.

 

Hata Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) haikumpasa kuapia chochote, na ndio maana tunaona anapotaka kuapa, mara nyingi husema:

 

وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ

Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake… [Akimkusudia Allaah]

 

 

Na akakataza katika Hadiyth mbali mbali zifuatazo kuapia kwa yeyote au kwa chochote isipokuwa kuapia kwa Allaah pekee:

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عُمَرَ رَضِي اللَّه عَنْهمَا أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَدْرَكَ عُمَرَ بْنَ الْخَطَّابِ وَهُوَ يَسِيرُ فِي رَكْبٍ يَحْلِفُ بِأَبِيهِ فَقَالَ : أَلَا إِنَّ اللَّهَ يَنْهَاكُمْ أَنْ تَحْلِفُوا بِآبَائِكُمْ مَنْ كَانَ حَالِفًا فَلْيَحْلِفْ بِاللَّهِ أَوْ لِيَصْمُتْ

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaahi bin ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikutana na ‘Umar bin Al-Khattwaab akiwa katika msafara wa ngamia akawa ameapia kwa baba yake. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Tanabahi Allaah Anawakatezeni kuapia kwa baba zenu. Anayetaka kuapa basi aapie kwa Allaah au anyamaze kimya)) [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

Pia:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ - رضي الله عنه: لَا تَحْلِفُوا بِآبَائِكُمْ, وَلَا بِأُمَّهَاتِكُمْ, وَلَا بِالْأَنْدَادِ, وَلَا تَحْلِفُوا إِلَّا بِاللَّهِ, وَلَا تَحْلِفُوا بِاللَّهِ إِلَّا وَأَنْتُمْ صَادِقُونَ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Msiapie kwa baba zenu wala mama zenu, wala kwa mnaowalinganisha na Allaah. Na wala msiape isipokuwa kwa Allaah, wala msiape kwa Allaah isipokuwa mnapokuwa mnasema ukweli)) [Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy]

 

Amekataza pia kuapia kwa uaminifu akasema Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam:

 

 عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ بُرَيْدَةَ عَنْ أَبِيهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: (لَيْسَ مِنَّا مَنْ حَلَفَ بِالأَمَانَةِ

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Buraydah kutoka kwa baba yake kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Si miongoni mwetu anayeapia kwa amana)) [Ahmad (5/325) na ameisahihisha Al-Albaaniy katika As-Silsilah Al-Hadiyth Asw-Swahiyhah (1/325)]

 

 

Na Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

مَن حلَف فقال في حَلِفه: باللات والعُزَّى، فليقل: لا إله إلا الله

((Yeyote atakayeapa akasema katika kiapo chake: “Naapa kwa Al-Laata, na Al-’Uzzaa” basi aseme: “Laa ilaaha illa-Allaah”)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Na Ibn Mas-‘uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema:

 

لأَنْ أَحْلِفَ بِاللَّهِ كَاذِبًا أَحَبُّ إِلَيَّ مِنْ أَنْ أَحْلِفَ بِغَيْرِهِ صَادِقًا

“Ni bora kwangu kuapa kwa Jina la Allaah wakati naongopa kuliko kuapa kwa asiyekuwa Allaah kwa jambo la kweli.” [Majm’a Az-Zawaaid (4/180), na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh At-Targhiyb (2953)]

 

 

 

Aina za viapo ni vitatu: 

 

 

1- Al-Yamiyn Al-Ghamuws (Kiapo cha uongo):

 

Ni kula kiapo huku kukusudia kuongopa, kama vile kusema: “Wa-Allaahi nimenunua kitu kadhaa kwa gharama ya fedha kadhaa”, na hali si kweli kuwa umenunua bei hiyo. Au kusema: “Wa-Allaahi nimefanya kadhaa”, na hali hakufanya. Kuapa hivi ni miongoni mwa madhambi makubwa kama alivyosema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو بْن الْعاص (رضي الله عنهما) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ َقَالَ: ((الْكَبَائِرُ الإِشْرَاكُ بِاللَّهِ وَعُقُوقُ الْوَالِدَيْنِ وَقَتْلُ النَّفْسِ وَالْيَمِينُ الْغَمُوسُ)) البخاري

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amri bin Al-‘Aasw (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa)  ambaye amesema: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Al-Kabaair [Madhambi makubwa] ni kumshirikisha Allaah,  kuwaasi wazazi wawili, kuua nafsi na yamini [kiapo] ya uongo)) [Al-Bukhaariy]

 

Na katika riwaya nyingine:

 

أنَّ أَعْرَابِياً جَاءَ إِلَى النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللَّه,ِ مَا الْكَبَائِر؟ ُ قَالَ: ((الإشْرَاكُ بِاللَّهِ)) قَالَ: ثُمَّ مَاذَا؟ قَالَ: ((الْيَمِينُ الْغَمُوسُ)) قُلْتُ: وَمَا الْيَمِينُ الْغَمُوسُ؟  قَالَ: ((الَّذِي يَقْتَطِعُ مَالَ امْرِئٍ مُسْلِمٍ!)) يَعْنِ: بِيَمِينٍ هُوَ فِيهَا كَاذِبٌ

Alikuja Bedui mmoja kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza: Ee Rasuli wa Allaah! Ni yepi Al-Kabaair [madhambi makubwa]?” Akasema: ((Kumshirikisha Allaah)) Akasema: Kisha yepi? Akasema: ((Yamini ya uongo)). Nikauliza: Ni ipi yamini ya uongo? Akasema: ((Ni ambayo mtu hujichukulia mali ya Muislamu!)) yaani akaapa kwa uongo. [Al-Bukhaariy]

 

Imeitwa Yamiyn Al-Ghamuws (kiapo cha uongo) kwa sababu yamzamisha mwenye yamini hiyo ndani ya dhambi na yamini hii ndiyo iliyokusudiwa katika kauli ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

 

مَنْ حَلَفَ يَمينٍ صَبْرٍ لِيَقْتَطِعَ بِها مَالَ امْرِىءٍ مُسْلِمٍ، لَقِيَ اللهَ وَهُوَ عَلَيْهِ غَضْبانُ

((Atakayekula yamini hali yeye katika yamini hiyo anaongopa ili apate kwa yamini hiyo kumega mali ya mtu mwengine Muislamu basi mtu huyo atakutana na Allaah hali Amemghadhibikia)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Hukmu yake:  Kuna kauli mbili,

 

i) Yamiyn Al-Ghamuws haina kafara bali mtu atubie tawbah ya kwelikweli. Ni rai ya Imaam Abiy Haniyfah, Imaam Maalik na Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahumu-Allaah). Pia Fatwa ya Al-Lajnatud-Daaimah (23/133) wamefutu: ”Al-Yamiyn Al-Ghamuws ni katika madhambi makubwa na haihitaji kafara kwa sababu ya ukubwa wa dhambi yake, bali inahitaji tawbah na kuomba maghfirah na ndio ilivyo sahihi kutokana na kauli za ‘Ulamaa.”

 

Na Shaykh Al-Islaamiy Ibn Taymiyyah amesema katika Majmuw’ Al-Fataawaa (34/139) baada ya kutaja ikhtilafu kuhusu kiapo cha Ghamuws….

“Wameafikiana kwamba dhambi haianguki kwa ajili ya kufanya kafara”. 

Amesema pia:

Ikiwa amemdhulumu mja mwenziwe basi amrudishie haki yake pamoja na kumuomba msamaha.

 

ii) Ama Imaam Ash-Shaafi’iy ameona inapasa kafara.  

 

 

2-Al-Yamiyn Al-Laghw (Kiapo cha upuuzi):

 

Hiki ni kile kiapo kipitacho katika ulimi wa Muislamu bila kukusudia, kama yule ambaye katika mazungumzo yake hujitokeza kwa wingi mno wa neno: “Wa-Allaahi hapana”. Hii ni kufuatia kauli ya Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa):

لغو اليمين كقول الرجل لا والله وبلى والله،

 “Upuuzi katika yamini ni maneno anayozungumza mtu, “Hapana Wa-Allaahi, Ndio Wa-Allaahi.” [Al-Bukhaariy]

 

Hukumu ya yamini aina hii ni kuwa haina dhambi wala kafara kwa mhusika, kwa kauli yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) katika Suwrah Al-Maaidah (5: 89):

 

لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّـهُ بِاللَّغْوِ فِي أَيْمَانِكُمْ

Allaah Hatokuchukulieni kwa viapo vyenu vya upuuzi, [Al-Maaidah: 89]

 

 

 

3-Al-Yamiyn Al-Mun’aqidah (Kiapo cha kufungika):

 

Ni kukusudia jambo la baadae. Kama vile Muislamu kusema: “Wa-Allaahi nitalifanya jambo kadhaa” Au “Wa-Allaahi sitolifanya…” kisha akafanya kinyume chake.

 

Hukmu yake ni katika Suwrat Al-Maaidah (5: 89):

 

وَلَـٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا عَقَّدتُّمُ الْأَيْمَانَ

lakini Atakuchukulieni kwa (kuvunja) viapo mlivyoapa kwa niyyah mlioifunga thabiti. [Al-Maaidah: 89]

 

ambayo inampasa afanye kafara:

 

فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚوَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿٨٩﴾

Basi kafara yake ni kulisha maskini kumi chakula cha wastani mnachowalisha ahli zenu, au kuwavisha nguo, au kuacha huru mtumwa. Lakini asiyeweza kupata (katika hayo), basi afunge Swiyaam siku tatu. Hiyo ndio kafara ya viapo vyenu mnapoapa. Na hifadhini yamini zenu. Hivyo ndivyo Allaah Anavokubainishieni Aayaat (na hukmu) Zake ili mpate kushukuru.  [Al-Maaidah: 89]

 

 

Vinavyoapiwa kimakosa:

 

1- Kuapia vitu kadhaa:

 

Unapoapa kimakosa kwa kutumia vitu kuapia huhitaji kafara bali inakupasa urudi kutubia kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). ‘Ulamaa wamekubaliana hivyo kama alivyosema Shaykh Al-Islaam Ibn Taymiyyah katika Al-Fataawa Al-Kubraa (3/222): 

“Kuapia vitu viliyvoumbwa kama Al-Ka’bah, Malaika, mashekhe, wafalme, wazazi, makaburi ya wazazi n.k haihitajiki kafara kama ilivyokuwa ni rai ya Wanavyuoni. Bali imeharamishwa na Wanavyuoni na haramisho hili ni haraam kutokana na rai iliyo na nguvu kabisa”.

 

 

2- Kuapia kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

Baadhi ya watu huapa kwa tamshi la: “Wan-Nabiy!”, “Haki ya Mtume!” n.k.

 

 

3- Kuapia kwa Msahafu:

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) aliulizwa kuhusu hukmu ya kuapia Msahafu alijibu:

"Hairuhusiwi kuweka nadhiri au kuapa isipokuwa kwa Allaah au moja ya Sifa Zake. Ikiwa mtu ataapa kwa jina la Allaah, basi hakuna haja tena kuleta Msahafu kwa ajili ya kuapa kwa sababu kuapa kwa Msahafu haikufanyika zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba. Hata baada ya Qur-aan kukusanywa katika Kitabu kimoja hawakuwa wakiapia Msahafu bali mtu alikuwa akiapa kwa Allaah bila ya kushika Msahafu."

[Fataawaa Nuwr 'Alaa Ad-Darb]

 

 

4- Kuapia kwa Al-Ka’bah:

 

Baadhi ya Waislamu hufikishana Makkah kuapizana kwa Al-Ka’bah jambo ambalo halijuzu bali ni kuvuka mipaka ya ‘Ibaadah, na kupoteza muda na mali ya kuwapeleka huko.

 

 

5- Kuapia wazazi, watoto:

 

Makatazo katika Hadiyth zilotanguliwa kutajwa juu.

 

 

6- Kuapia ‘amali njema kama Swiyaam (funga), Swadaqah n.k.

 

 

 



53-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Amepewa Ummah Bora Kabisa

 Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

53-Amepewa Ummah Bora Kabisa  

 

www.alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):   

 

كُنتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ تَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَتُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ ۗ وَلَوْ آمَنَ أَهْلُ الْكِتَابِ لَكَانَ خَيْرًا لَّهُم ۚ مِّنْهُمُ الْمُؤْمِنُونَ وَأَكْثَرُهُمُ الْفَاسِقُونَ ﴿١١٠﴾

Mmekuwa Ummah bora kabisa uliotolewa (mfano) kwa watu; mnaamrisha mema na mnakataza munkari na mnamwamini Allaah. Na lau wangeliamini Ahlul-Kitaabi ingelikuwa ni bora kwao, miongoni mwao wanaoamini na wengi wao ni mafasiki [Aal-‘Imraan: 110]

 

 

Na Hadiyth zinathibitisha na kufafanua zaidi:  

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَة َ رضى الله عنه ((‏كُنْتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ‏)) قَالَ خَيْرَ النَّاسِ لِلنَّاسِ، تَأْتُونَ بِهِمْ فِي السَّلاَسِلِ فِي أَعْنَاقِهِمْ حَتَّى يَدْخُلُوا فِي الإِسْلاَمِ‏.‏

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kuhusu:    

 ‏كُنْتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ‏

"Mmekuwa Ummah bora kabisa uliotolewa (mfano) kwa watu"

 

Kasema:  “Watu bora kabisa kati ya watu, mtawajia kwa minyororo katika shingo zao mpaka waingie Uislamu.” [Al-Bukhaariy]

 

تَأْتُونَ بِهِمْ فِي السَّلاَسِلِ فِي أَعْنَاقِهِمْ حَتَّى يَدْخُلُوا فِي الإِسْلاَمِ‏

Maana ya: “Mtawajia kwa minyororo katika shingo zao mpaka waingie Uislamu.”

 

“Ni matekwa waliokamatwa na Waislamu, basi Allaah huwaongoza na kuingia katika Uislaam kwa hivyo wanafaidika na kuingia Peponi. Hii ni katika neema adhimu na fadhila za Allaah  juu ya matekwa kisha wakaingia Uislamu na hawakuuawa na makafiri.” [Imaam Ibn Baaz – Sharh Riyaadhw Asw-Swaalihiyn]

 

 

Na pia:

 

عَنْ بَهْزِ بْنِ حَكِيمٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ، أَنَّهُ سَمِعَ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ فِي قَوْلِهِ كُنْتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ ‏ قَالَ ‏"‏ إِنَّكُمْ تُتِمُّونَ سَبْعِينَ أُمَّةً أَنْتُمْ خَيْرُهَا وَأَكْرَمُهَا عَلَى اللَّهِ ‏"‏

Kutoka kwa Bahz bin Haakim, kutoka baba yake, kutoka kwa babu yake kwamba kamsikia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema kuhusu kauli ya Allaah:

‏كُنْتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ‏

Mmekuwa Ummah bora kabisa uliotolewa (mfano) kwa watu

Nyinyi ni  umaliziaji wa mataifa sabini, nyie ndiye bora zaidi, na ndiyo (Ummah) mtukufu bora mbele ya Allaah. [Hadiyth Hasan At-Tirmidhiy]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):   

 

وَكَذَٰلِكَ جَعَلْنَاكُمْ أُمَّةً وَسَطًا لِّتَكُونُوا شُهَدَاءَ عَلَى النَّاسِ وَيَكُونَ الرَّسُولُ عَلَيْكُمْ شَهِيدًا ۗ

Na ndivyo hivyo Tumekufanyeni ummah bora na adilifu ili muwe mashahidi juu ya watu na awe Rasuli shahidi juu yenu. [Al-Baqrah: 143]

 

 



09-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Zuhd Yake: Amefariki Hali Ya Kuwa Hapakuwa Na Chakula Nyumbani Mwake Isipokuwa Chakula Duni

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

09-Zuhd Yake:

Amefariki Hali Ya Kuwa Hapakuwa Na Chakula Nyumbani Mwake  Isipokuwa Chakula Duni

 

 

www.alhidaaya.com

 

 

عَنْ عَائِشَةَ، قَالَتْ تُوُفِّيَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَمَا فِي بَيْتِي مِنْ شَىْءٍ يَأْكُلُهُ ذُو كَبِدٍ، إِلاَّ شَطْرُ شَعِيرٍ فِي رَفٍّ لِي، فَأَكَلْتُ مِنْهُ حَتَّى طَالَ عَلَىَّ، فَكِلْتُهُ فَفَنِيَ‏.‏

‘Aaishah (رضي الله عنها) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alifariki ilhali  hakuna kitu ndani ya nyumba yangu ambacho mtu aliye hai angeweza kula, isipokuwa shayiri  iliyokuweko katika rafu. Kwa hivyo, nilikula hiyo kwa muda mrefu kwa kuipimia, na (baada ya kipindi kifupi) ikamalizika. [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

Na pia,

 

عَنْ عَائِشَةَ، زَوْجِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَتْ لَقَدْ مَاتَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَمَا شَبِعَ مِنْ خُبْزٍ وَزَيْتٍ فِي يَوْمٍ وَاحِدٍ مَرَّتَيْنِ ‏.‏

‘Aaishah mke wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alifariki hali yakuwa hakuwahi kushiba mkate na mafuta ya zaytuni mara mbili kwa siku.” [Muslim]

 

 

Na pia,

عَنْ عَائِشَةَ، أَنَّهَا قَالَتْ مَا شَبِعَ آلُ مُحَمَّدٍ صلى الله عليه وسلم مِنْ خُبْزِ شَعِيرٍ يَوْمَيْنِ مُتَتَابِعَيْنِ حَتَّى قُبِضَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏.‏

‘Aaishah (رضي الله عنها) amesema: Familia ya Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) haikushiba mkate wa shayiri siku mbili kufuatana mpaka kufariki kwake.” [Al-Bukhaariy, Muslim]  

 

 



017-Aayah Na Mafunzo: Kukimbilia Kuomba Tawbah Kabla Ya Mauti

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa Aayah 17-18

Kukimbilia Kuomba Tawbah Kabla Ya Mauti

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّمَا التَّوْبَةُ عَلَى اللَّـهِ لِلَّذِينَ يَعْمَلُونَ السُّوءَ بِجَهَالَةٍ ثُمَّ يَتُوبُونَ مِن قَرِيبٍ فَأُولَـٰئِكَ يَتُوبُ اللَّـهُ عَلَيْهِمْ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴿١٧﴾

Hakika tawbah inayokubaliwa na Allaah ni ya wale wanaofanya uovu kwa ujahili kisha wakatubia haraka, basi hao Allaah Anapokea tawbah yao. Na Allaah ni Mjuzi wa yote, Mwenye hikmah wa yote.

 

وَلَيْسَتِ التَّوْبَةُ لِلَّذِينَ يَعْمَلُونَ السَّيِّئَاتِ حَتَّىٰ إِذَا حَضَرَ أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ إِنِّي تُبْتُ الْآنَ وَلَا الَّذِينَ يَمُوتُونَ وَهُمْ كُفَّارٌ ۚ أُولَـٰئِكَ أَعْتَدْنَا لَهُمْ عَذَابًا أَلِيمًا ﴿١٨﴾ 

Lakini tawbah si kwa wale wanaofanya maovu mpaka mauti yanapohudhuria kwa mmoja wao husema: “Hakika mimi sasa nimetubu.” Na wala wale wanaokufa na hali wao ni makafiri. Hao Tumewaandalia adhabu iumizayo. [An-Nisaa: 17-18]

 

Mafunzo:

 

Umuhimu wa kuomba tawbah kabla ya kufika wakati wa kutokupokelewa: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hakika Allaah Huikubali tawbah ya mja Wake kabla ya roho kufika kwenye mkoromo wa mauti.” [At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na wengineo; Swahiyh At-Tirmidhiy (3537), Swahiyh Ibn Maajah (3449)].

 

Na pia. “Atakayetubu kabla ya kuchomoza jua upande wa Magharibi, Allaah Atamkubalia tawbah yake.” [Muslim].

 

Bonyeza kiungo kifuatacho upate faida ziyada:

 

Tawbah: Hukmu Na Fadhila Zake

 

 

 

 



126-Asbaab Nuzuwl: An-Nahl: Na Mkilipiza, Basi Lipizeni Kulingana Na Vile Mlivyoadhibiwa

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

016-Asbaab Nuzuwl An-Nahl  Aayah : 126

 

 

Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى)

 

وَإِنْ عَاقَبْتُمْ فَعَاقِبُوا بِمِثْلِ مَا عُوقِبْتُم بِهِ ۖ وَلَئِن صَبَرْتُمْ لَهُوَ خَيْرٌ لِّلصَّابِرِينَ﴿١٢٦﴾

Na mkilipiza, basi lipizeni kulingana na vile mlivyoadhibiwa. Na mkisubiri, basi bila shaka hivyo ni bora kwa wenye kusubiri. [An-Nahl: 126]

 

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

حَدَّثَنَا أَبُو عَمَّارٍ الْحُسَيْنُ بْنُ حُرَيْثٍ، حَدَّثَنَا الْفَضْلُ بْنُ مُوسَى، عَنْ عِيسَى بْنِ عُبَيْدٍ، عَنِ الرَّبِيعِ بْنِ أَنَسٍ، عَنْ أَبِي الْعَالِيَةِ، قَالَ حَدَّثَنِي أُبَىُّ بْنُ كَعْبٍ، قَالَ لَمَّا كَانَ يَوْمُ أُحُدٍ أُصِيبَ مِنَ الأَنْصَارِ أَرْبَعَةٌ وَسِتُّونَ رَجُلاً وَمِنَ الْمُهَاجِرِينَ سِتَّةٌ فِيهِمْ حَمْزَةُ فَمَثَّلُوا بِهِمْ فَقَالَتِ الأَنْصَارُ لَئِنْ أَصَبْنَا مِنْهُمْ يَوْمًا مِثْلَ هَذَا لَنُرْبِيَنَّ عَلَيْهِمْ قَالَ فَلَمَّا كَانَ يَوْمُ فَتْحِ مَكَّةَ فَأَنْزَلَ اللَّهُ ‏ ((وَإِنْ عَاقَبْتُمْ فَعَاقِبُوا بِمِثْلِ مَا عُوقِبْتُمْ بِهِ وَلَئِنْ صَبَرْتُمْ لَهُوَ خَيْرٌ لِلصَّابِرِينَ))‏ فَقَالَ رَجُلٌ: لاَ قُرَيْشَ بَعْدَ الْيَوْمِ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم :‏"‏ كُفُّوا عَنِ الْقَوْمِ إِلاَّ أَرْبَعَةً ‏"‏ ‏.‏ قَالَ هَذَا حَدِيثٌ حَسَنٌ غَرِيبٌ مِنْ حَدِيثِ أُبَىِّ بْنِ كَعْبٍ ‏

Ametuhadithia Abuu ‘Ammaar Al-Husayn bin Hurayth, ametuhadithia Al-Fadhwl bin Muwsa kutoka kwa ‘Iysaa bin ‘Ubayd, kutoka kwa Ar-Rabi’y bin Anas, kutoka kwa Abuu Al-‘Aaliyah amesema: amenihadithia Ubayy bin Ka’b ambaye amesema: Siku ya vita vya Uhud, watu sitini na nne katika Answaariy waliuawa, na sita kutoka kwa Muhaajiriyn. Mmoja wao alikuwa ni Hamzah, wakamtumbua basi Answaariy wakasema: “Ikiwa (siku za mbele) tukijaaliwa kupigana nao (tukawaua) siku kama hii, nasi tutawatumbua baadhi yao mara mbili yake (kama walivyowatumbua baadhi yetu).” Akasema:  Basi siku ya Fat-h Makkah Allaah Akateremsha:

 

وَإِنْ عَاقَبْتُمْ فَعَاقِبُوا بِمِثْلِ مَا عُوقِبْتُم بِهِ ۖ وَلَئِن صَبَرْتُمْ لَهُوَ خَيْرٌ لِّلصَّابِرِينَ﴿١٢٦﴾

Na mkilipiza, basi lipizeni kulingana na vile mlivyoadhibiwa. Na mkisubiri, basi bila shaka hivyo ni bora kwa wenye kusubiri. [An-Nahl: 126]

 

Mtu mmoja akasema: “Hakutakuwa na Quryash tena baada ya leo.”  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Waacheni watu isipokuwa wanne tu.” [At-Tirmidhiy, amesema Hii Hadiyth Hasan Ghariyb katika Hadiyth za Ubayy bin Ka’ab]

 

 



053-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Anayelia Kwa Kumkhofu Allaah Hatoingia Motoni

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 53

Anayelia Kwa Kumkhofu Allaah Hatoingia Motoni

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((لاَ يَلِجُ النَّارَ رَجُلٌ بَكَى مِنْ خَشْيَةِ اللَّهِ حَتَّى يَعُودَ اللَّبَنُ فِي الضَّرْعِ. ولاَ يَجْتَمِعُ غُبَارٌ فِي سَبِيلِ اللَّهِ وَدُخَانُ جَهَنَّمَ)) رواه الترمذي وقال: حديث حسن صحيح

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hatoingia motoni mtu anayelia kwa sababu ya kumkhofu Allaah mpaka maziwa yarudi katika chuchu. Wala haliwezi kujumuika vumbi katika Njia ya Allaah na moshi wa Jahannam)). [At-Tirmdihiy na amesema: Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Chozi la kumkhofu Allaah (سبحانه وتعالى) lina fadhila kubwa ya kuepushwa na moto.

 

 

2. Mifano anayopiga Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم ) ni ya aina ya pekee yenye mazingatio makubwa, sawa na mifano Anayopiga Allaah (سبحانه وتعالى) katika Qur-aan kama Anavyosema:

 

وَلَقَدْ ضَرَبْنَا لِلنَّاسِ فِي هَـٰذَا الْقُرْآنِ مِن كُلِّ مَثَلٍ لَّعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ ﴿٢٧﴾

Na kwa yakini Tumewapigia watu mifano ya kila aina katika hii Qur-aan ili wapate kukumbuka.

 

قُرْآنًا عَرَبِيًّا غَيْرَ ذِي عِوَجٍ لَّعَلَّهُمْ يَتَّقُونَ ﴿٢٨﴾

Qur-aan ya Kiarabu isiyokuwa kombo ili wapate kuwa na taqwa. [Az-Zumar (39: 27-28)]

 

Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَقَدْ صَرَّفْنَا لِلنَّاسِ فِي هَـٰذَا الْقُرْآنِ مِن كُلِّ مَثَلٍ فَأَبَىٰ أَكْثَرُ النَّاسِ إِلَّا كُفُورًا ﴿٨٩﴾

Na kwa yakini Tumesarifu namna kwa namna hii Qur-aan kwa watu, kwa kila mfano, lakini watu wengi wamekataa kabisa (haki; hawakukubali) isipokuwa kukufuru tu. [Al-Israa (17: 89)]

 

Na pia Anasema (سبحانه وتعالى):

 

وَلَقَدْ صَرَّفْنَا فِي هَـٰذَا الْقُرْآنِ لِلنَّاسِ مِن كُلِّ مَثَلٍ ۚ وَكَانَ الْإِنسَانُ أَكْثَرَ شَيْءٍ جَدَلًا ﴿٥٤﴾

Na kwa yakini Tumesarifu namna kwa namna katika hii Qur-aan kwa watu, kwa kila mifano. Lakini binaadamu amezidi kuliko kila kitu kwa ubishi. [ Al-Kahf: 54]

 

Baadhi ya mifano hiyo Aliyoipiga Allaah (سبحانه وتعالى) katika Qur-aan: Al-Baqarah (2: 261-266) Al-A’raaf (7: 40), (175-177), Yuwnus (10: 24), Ibraahiym (14: 24-27), An-Nahl (16: 75-76), Al-Hajj (22: 73), An-Nuwr (24: 35), (39-40), Az-Zumar (39: 29), Al-Hadiyd (57: 20), Al-‘Ankabuwt (29: 41), Huwd (11: 24), Al-Jumu’ah (62: 5)].

 

 

3. Umuhimu wa Muislamu kufahamu kauli za Allaah (سبحانه وتعالى) katika Qur-aan, na anapoisoma awe anazingatia na kupata mafunzo pamoja na mawaidha, na imzidishie iymaan hata atokwe na machozi khasa pale anapopitia adhabu Zake aingiwe na khofu kwazo.

 

 

4. Fadhila za mtu kutoka ili kupigana katika Njia ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 



20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...