Translate

Jumatatu, 21 Septemba 2020

Sababu 9 zinazosababisha ukose au uchelewe kuona siku zako

Sababu 9 zinazosababisha ukose au uchelewe kuona siku zako

Kwa mwanamke kuchelewa kupata hedhi huwa hakushitui iwapo mwanamke anajua ni nini tatizo au sababu iliyopelekea yeye kukosa hedhi.

Na majibu ya kuchelewa kwa hedhi hupatikana pindi hedhi hiyo inapochelewa.

Mfano kama ulikua unategemea kupata mimba, ikichelewa inakua ni dalili ya kwanza ya wewe kuanza kufikiria jambo ulilolitaka linaelekea kutimia na hata ukatabasamu na kuwaza hatua nyingine ya kujipima nyumbani au kuenda hospitali.

Na kama hukuwa umetarajia ndio hivyo tena mawazo ya kila aina yatakuja kichwa kutaka kujua kwanini hedhi yako imechelewa na pengine usipate majibu kabisa.

Naitwa Tabibu Fadhili Paulo, mawasiliano yangu ni WhatsApp +255714800175

Sababu 9 zinazosababisha ukose au uchelewe kuona siku zako 1

Sababu 9 zinazosababisha ukose au uchelewe kuona siku zako

1. Umeacha kutumia dawa za uzazi wa mpango

Kama umekuwa ukitumia aina yoyote ya dawa ya uzazi wa mpango za kizungu iwe ni vidonge, sindano, kijiti na kadharika mara tu utakaposimama kuzitumia dawa hizi linaweza kukutokea tatizo la kutoona siku zako.

Dawa hizi za uzazi wa mpango za kizungu kwa sehemu kubwa wakati unazitumia zinaweza kurekebisha mzunguko wako wa hedhi na hivyo unapoacha kuzitumia mwili wako unaweza kupatwa na mshituko.

Hakuna maelezo zaidi ya kwanini mwili wako unapatwa na mshituko huu baada ya wewe kuacha kuzitumia dawa hizi lakini kinachojulikana ni kuwa mwili wako utahitaji muda fulani au miezi kadhaa mpaka urudi kwenye hali yako ya kawaida kama zamani kabla hujaanza kutumia dawa za uzazi wa mpango.

Jambo moja la kuwa nalo makini hapa ni kwamba bado unaweza kupata ujauzito wakati huu hata kama huoni siku zako kama matokeo ya kuvurugika kwa siku zako yaliyotokana na kuacha kutumia dawa za uzazi wa mpango.

Kwa hiyo ikiwa hutaki kupata ujauzito unahitaji kuwa makini sana wakati huu kwani unaweza kupata ujauzito wakati wowote ikiwa utashiriki tendo la ndoa bila kinga.

2. Inawezekana umepata ujauzito

Hata kama umekuwa ukitumia dawa za uzazi wa mpango na umekuwa makini sana katika hilo bado kama unaona hupati siku zako ghafa kuna uwezekano umepata ujauzito.

Hili ndiyo linapaswa kuwa wazo lako la kwanza ikitokea siku zako zimeacha au unaona zinachelewa sana.

Hii inatokana na ukweli kuwa wakati mwingine dalili za mwanzo za ujauzito zinaweza kufanana sana na dalili za kutaka kuona siku zako na inaweza kuwa shida kutofautisha dalili za mimba na dalili za kutaka kuona siku zako.

Kwahiyo kama umekuwa ukishiriki tendo la ndoa mara kwa mara na ghafla unaona huoni tena siku zako ni vizuri kufanya kipimo kuona ikiwa ni mjamzito au la. Fanya kipimo kila baada ya wiki mbili.

3. Umepata ugonjwa fulani

Wakati mwingine ukitokewa ukaona hupati siku zako inaweza kuwa ni matokeo ya wewe kuumwa au kupatwa na ugonjwa fulani mkubwa.

Homa, mafua, aleji au ugonjwa wowote mkubwa unaoweza kuklazimisha kwenda hospitali vinaweza kuwa sababu ya wewe kukosa siku zako kama kawaida.

Magonjwa yanaweza kuwa chanzo cha kuleta mfadhaiko au msongo wa mawazo katika sehemu ya ubongo inayohusika na kuweka sawa homoni na hivyo kuvuruga mzunguko wako wa kawaida.

4. Inawezekana una uvimbe

Je chuchu zako zinatoa maji maji ya maziwa?

Wanawake wengi ukikutana nao wenye matatizo ya uzazi watakuambia wameacha kuona siku zao na wanatokewa na maji maji katika chuchu zao za maziwa na wanapata maumivu ya kichwa ya mara kwa mara.

Ikiwa umepata uvimbe hasa katika tezi ya pituitari (prolactinoma au benign tumor) uvimbe huu unaweza kusababisha kuzalishwa kwa wingi kwa homoni iitwayo prolactin.

Homoni ya prolactin inapozalishwa kwa wingi kuliko inavyohitajika na mwili inaweza kukuletea tatizo la kukosa siku zako sababu inaingiliana kimajukumu na kuzuia homoni ya estrogen kuzalishwa.

Wakati wowote homoni ya estrogen inapokuwa ndogo au chache mwili wako unapata wakati mgumu kuleta hedhi yako na kukufanya usione siku zako.

5. Unafanya SANA mazoezi ya viungo kupita kiasi

Unaenda gym au kufanya mazoezi hata kama unahisi umechoka sana na kazi za kutwa nzima? Au kwa kifupi unaishi kwenye mazoezi?

Kufanya sana mazoezi na huku unakula chakula kidogo na huku unatokewa na kupungua uzito kwa haraka vyote hivi vinaweza kuwa sababu yaw ewe kukosa siku zako hasa kama BMI yako inashuka chini ya 19 au 18.

Unachohitaji hapa ni kupunguza mazoezi na kuongeza uzito kidogo kama ulishuka sana kama matokeo ya mazoezi.

Kumbuka kama inakutokea unakosa kuona siku zako kwa muda mrefu pengine zaidi hata ya mwaka basi ni hatari kwa afya yako hasa afya ya mifupa kama inavyowatokea wamama wengi baada ya siku zako kukoma baada ya miaka 45.

6. Una mfadhaiko wa akili (stress)

Labda unakabiliwa na mzigo mkubwa wa kazi kazini kwako au una shida nyingine tu za kila siku zinazokufanya uwe na mawazo mawazo kila mara inaweza kuwa sababu kwanini huoni siku zako.

Mfadhaiko, msongo wa mawazo, mvurugiko wa akili au stress kwa kiingereza ni kitu ambacho kinaweza kuufanya mwili wako uamuwe sasa siyo wakati wa wewe kupata ujauzito na hivyo kukataa kukupa siku zako.

Mfadhaiko wa akili unaweza kukuletea tatizo la mayai yako kushindwa kupevuka vizuri.

Hii njia ya asili ya mwili ili kukulinda wewe.

Wakati wowote utakapoamua kuachana na stress mwili wako utakurudishia hedhi yako na mzunguko wako utarudi na kutulia kama mwanzo.

Kwanini mwili unapunguza kasi ya upevushaji wa mayai wakati wa msongo wa mawazo?

Mwili unatambua kwamba upo kwenye kipindi cha hatari na unatakiwa upambane ili uishi kutokana na hatari inayokuwa mbele kwa hivo maisha ni kitu cha kwanza ndipo swala na hedhi lifuate.

Mwili utatengeneza homoni za kudhibiti stress kwa wingi kama cotisoli na adrenalini ili kukuandaa kupambana, ama kukimbia hatari iliyopo mbele yako.

Fikiria pale unapotembea usiku na ukaona kitu kisicho cha kawaida mbele yako, tazama mwili unavyobadilika, sasa mabadiliko ya homoni pale unapokutana na kitu cha hatari ni sawa na vile unapopata msongo wa mawazo.

Kadiri mawazo yanavyokuathiri ndivyo uvyonaharibu mpangilio wako wa mwili na kukupelekea ukose hedhi.

Soma hii pia > Kama una stress ni vigumu kupata ujauzito

7. Homoni zako zimevurugika

Hii ndiyo sababu namba moja ya hedhi yako kuacha kutoka au kuvurugika.

Tezi ya thairodi ni kiungo chenye umbo la kipepeo.

Kiungo hiki kipo kwenye shingo chini ya koromeo la sauti.

Kazi kuu ya Tezi hii ni kuzalisha homoni za (T3) na (T4), ambazo kwa pamoja hufanya kazi ya kurekebisha mzunguko wa damu na kazi mbalimbali za mwili.

Matatizo kwenye tezi ya Thairodi kama kushuka kwa uzalishaji wa homoni ama tezi kufanya kazi kupita kiasi huweza kuleta mabadiliko pia kwenye kiwango cha homoni za estrogeni na cotisoli.

Kiwango cha cotisoli kwenye damu kinapokuwa kingi hupunguza uwezo wa tezi ya thairoidi ambapo matokeo yake ni kushuka kwa kazi za mwili kama upevushaji wa mayai na uzalishaji wa homoni za kike

Vile vile lishe mbaya yenye upungufu wa virutubisho ikiwemo vitamini na madini na yenye sukari na viambata vya kuongeza ladha kwa wingi hupelekea tezi za Adrenali na Thairodi kufaya kazi kupita kiasi.

Kitendo hiki hupelekea uzalishaji wa kichocheo cha cotisoli ambacho kinapunguza uzalishaji wa homoni za uzazi.

Cotisoli inapokuwa nyingi zaidi pia inaweza kuleta madhara mwilini kama udhaifu wa mifupa, ngozi kuharibika, tishu za ubongo  na misuli kudhoofika na kukupa wewe tatizo la kuvurugika au kukosa hedhi.

8. Umeongezeka uzito

Kama vile ukiwa na uzito pungufu kunaleta tatizo la kukosa siku zako kadharika uzito uliozidi au unene uliozidi pia unaweza kukusababishia ukapoteza kuona siku zako.

Wanawake wenye uzito wa juu au unene uliopitiliza wana uwezekano wa mara mbili zaidi wa kuwa na mzunguko wa hedhi usioeleweka tofauti na wenye uzito mzuri wa kawaida.

Mwanamke kuwa na uzito uliozidi unaweza kuwa sababu ya matatizo ya homoni zake na uzito kupita kiasi una uhusiano na tatizo linguine la uzazi kwa wanwake lijuliknalo kwa kitaalamu kama Polycystic Ovarian Sydrome (PCOS).

Kama unataka kupungua uzito wako kwa njia salama bonyeza hapa.

9. Umepata watu wengine wa kulala nao chumba kimoja

Hili linaweza lisiwe na uthibitisho wa kisayansi lakini tafiti mbalimbali zinasema ikiwa ulikuwa unalala peke yako kwa kipindi kirefu na mara ukapata wasichana wengine wa kulala na wewe chumba kimoja hili linaweza kusababisha kuanza kupata hedhi isiyoeleweka.

Hili ni rahisi kutokea hasa kama umetoka nyumbani na umehamia shule ya bweni au hosteli kitendo hiki cha kuanza kuwa pamoja na wengine na kuzoeana nao kinaweza kukuletea kuvurugika kwa siku zako kama sehemu ya kuzoeana na makundi ya watu wengine.

Wasichana wengi wa chuo wanaweza kukuambia hili limewahi kuwatokea kwenye maisha yao.

Vipimo vifuatavyo vinaweza kufanywa kuchunguza sababu za kukosa hedhi kwa mwanamke:

  • Kupima damu kwa ajili ya kuchunguza kiwango cha homoni za FSH, LH, TSH na prolactin ambazo uzalishwaji wake unachochewa na tezi ya pituitary, na pia kupima kiwango cha homoni ya estrogen inayozalishwa na ovary.
  • Kipimo cha ultrasound ya nyonga kwa ajili ya kuchunguza uwepo wa matatizo katika njia ya uzazi na pia kuchunguza hali ya ovary.
  • CT scan au MRI ya kichwa kwa ajili ya kuchunguza uwepo wa matatizo kwenye tezi ya pituitary au hypothalamus.
  • Vipimo vya kufahamu ufanyaji kazi wa tezi ya thyroid
  • Kupima damu ili kufahamu kiwango cha homoni ya prolactin katika damu
  • Kuchunguza uterus kwa kutumia aina ya X-ray inayoitwa Hysterosalpingogram na kipimo kingine kiitwacho Hysteroscopy ambacho huchunguza chumba cha uterus.
Kama unatafuta dawa nzuri ya asili ili upate ujauzito niachie tu ujumbe WhatsApp +255714800175
SHARE POST HII NA WENGINE UWAPENDAO
Fadhili Paulo
Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
Imesomwa mara 4

Let's block ads! (Why?)

Alhamisi, 17 Septemba 2020

14-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kuvaa Kitu Kwa Ajili Ya Kinga

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

14 -Kuvaa Kitu Kwa Ajili Ya Kinga

Alhidaaya.com

 

 

Itikadi za watu kuvaa vitu au kujifunga navyo mwilini kwa kuepusha au kujikinga na kijicho, husda na madhara mengineyo. Jambo hili halijuzu kwa sababu hivyo vitu havina uwezo wa hayo wala hakuna atakayeweza kumuondoshea mtu madhara isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Anasema:

 

وَإِن يَمْسَسْكَ اللَّـهُ بِضُرٍّ فَلَا كَاشِفَ لَهُ إِلَّا هُوَ ۖ وَإِن يَمْسَسْكَ بِخَيْرٍ فَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١٧﴾

Na Allaah Akikugusisha kwa dhara, basi hakuna yeyote wa kukuondolea hiyo isipokuwa Yeye; na Akikugusisha khayr, basi Yeye juu ya kila kitu ni Muweza. [Al-An’aam:  17]

 

 

Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameharamisha hayo  katika Hadiyth mbali mbali:

 

 عَنْ قَيْسِ بْنِ السَّكَنِ الأَسَدِيِّ قَالَ: دَخَلَ عَبْدُ اللهِ بْنُ مَسْعُودٍ رضي الله عنه عَلَى امْرَأَةٍ، فَرَأَى عَلَيْهَا خَرَزًا مِنَ الحُمْرَةِ، فَقَطَعَهُ قَطْعًا عَنِيفًا، ثُمَّ قَالَ: إِنَّ آلَ عَبْدِ اللهِ عَنِ الشِّرْكِ أَغْنِيَاءُ، كَانَ مِمَّا حَفِظْنَا عَنِ النَّبِيِّ صلّى الله عليه وسلّم: ((إِنَّ الرُّقَى وَالتَّمَائِمَ وَالتِّوَلَةَ شِرْكٌ)) رواه الحاكم وقال: " صحيح الإسناد "، ووافقه الذّهبي والألبانيّ في "الصّحيحة" (برقم 331).

Imepokelewa kutoka kwa Qays bin As-Sakan Al-Asadiyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Abdullaah bin Mas‘uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) aliingia kwa mwanamke ambaye alivaa shanga nyekundu, akazikatilia mbali kisha akasema: “Hakika ahli ya ‘Abdullaah hawahitaji shirki!”. Akasema pia: “Katika ambayo amehifadhi kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni: ((Hakika Ar-Ruqaa (zisizothibiti), At-Tamaaim, At-Tiwaalah ni shirki).)) [Al-Haakim amesema Isnaad Swahiyh na ameikubali Adh-Dhahabiy na Al-Albaaniy katika Asw-Swahiyhah (331)]

 

At-Tamaaim:  Wanachofungwa watoto (kama kitambaa cheusi au nyuzi n.k.) shingoni (au mkononi) kukinga jicho baya.

 

 

Ar-Ruqaa au Al-‘Azaaim: Ni tabano au azima inayosomwa. Imeruhusiwa tu inapokuwa haina shirki. Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameiruhusu inapokuwa hali ya kudonelewa na mdudu sumu au anapopatwa mtu na jicho baya (au husda) au homa.

 

 

At-Tiwaalah (mvuto wa ndere): Kinachodaiwa kuwa kinasababisha mwanamke apendwe zaidi na mumeme au mume apendwe zaidi na mkewe.

 

 

Hadiyth nyenginezo zinazoharamisha kuvaa vitu kwa ajili ya kinga ni zifuatazo:

 

عَنْ أَبِي بَشِيرٍ الأَنْصَارِيِّ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) أَنَّهُ كَانَ مَعَ رَسُولِ اللهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فِي بَعْضِ أَسْفَارِهِ، فَأَرْسَلَ رَسُولاً, أَنْ ((لاَ يَبْقَيَنَّ فِي رَقَبَةِ بَعِيرٍ قِلادَةٌ مِنْ وَتَرٍ أَوْ قِلادَةٌ إِلاَّ قُطِعَتْ)).

Imepokewa kutoka kwa Abu Bashiyr Al-Answaariyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba alikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika safari mojawapo. Akamtuma mjumbe kuamrisha kwamba: ((Kusiachwe kidani cha uzi au kidani chochote katika shingo za ngamia isipokuwa kikatwe)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Pia:

 

 رَوَى أَحْمَدُ عَنْ رُوَيْفِعٍ قَالَ؛ قَالَ لِي رَسُولُ اللهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((يَا رُوَيْفِعُ، لَعَلَّ الْحَيَاةَ سَتَطُولُ بِكَ؛ فَأَخْبِرِ النَّاسَ أَنَّ مَنْ عَقَدَ لِحْيَتَهُ، أَوْ تَقَلَّدَ وَتَرًا، أَوِ اسْتَنْجَى بِرَجِيعِ دَابَّةٍ أَوْ عَظْمٍ؛ فَإِنَّ مُحَمَّدًا بَرِيءٌ مِنْهُ))

Ahmad amepokea kutoka kwa Ruwayfi’ ambaye amesema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameniambia: ((Ee Ruwayfi’! Huenda ukaishi zaidi baada yangu. Kwa hiyo wajulishe watu kwamba: Yeyote atakayefunga fundo ndevu zake, au akaweka nyuzi au mshipi shingoni mwake [kuwa ni talasimu] au akastanji na mkojo wa mnyama au mfupa, basi Muhammad amejitenga naye)). [Ahmad, Abuu Daawuwd]

 

 

Vitu ambavyo aghlabu hutumiwa na watu kuvivaa au kujifunga wakiamini vinawakinga:

 

 

a) Hirizi za vitambaa vyenye maandishi ndani ikiwa ya Quraan au mengineyo.

 

 

                   

 

   

 

 

 

 

 

b) Mtoto mchanga kupakwa masinzi au wanja usoni au kuandikwa Jina la Allaah!

 

 

c) Kuwapaka watoto wachanga wanja usoni na nakshi za nyota na mwezi, kwa kuamini ule wanja unazuia 'ayn (kijicho).  

 

 

d) Anapolazwa mtoto mchanga kukiwa chini ya mto wake vitu kama kisu, ndimu n.k.

 

 

e) Kuvalishwa vyuma mkononi.

 

f) Kuvalishwa mtoto mchanga au hata wakubwa, kidani chenye lakti ya Aayatul-Kursiy au Jina la Allaah! Ni jambo linalotendwa na wengi! Hakika ni kosa kubwa kwani ni kudhihirisha kutokumadhimisha Allaah kwa sababu kidani hicho anaingia nacho mtu chooni. Juu ya hivyo ni kuitakidi kuwa kinamkinga mtu na shari, uhasidi, jicho n.k. Imeshatangulia Hadiyth mbali mbali na Fataawa za ‘Ulamaa kukataza haya, na rejea mlango wa “Kutundika vitu”. 

 

g) Kuvalishwa kitambaa cheusi mkononi wengine wanatia mvuje ndani yake yenye harufu mbaya kuepusha majini.

 

h) Mapambo yenye kuandikwa Aayah za Qur-aan:

 

 

 

 

i) Mapambo ya vijiwe vya rangi ya buluu, vinginevyo vina jicho.

 

   

             

    

 

   

            

 

 

 

           

 

 

           

 

 

 

 

j) Kuvaa pete au mapambo yenye vito rangi kadhaa kwa kuitakidi rangi hizo zina maana ya wanachoita ‘bahati nzuri’ au kuleta hali fulani njema kutokana na tarehe au miezi ya kuzaliwa:

 

           

 

 

 

 



52-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Ametumwa Kubashiria Na Kuonya Walimwengu

 

Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

52-Ametumwa Kubashiria Na Kuonya Walimwengu

 

www.alhidaaya.com

 

 

Kama ilivyotangulia fadhila ya kuwa Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) ametumwa kwa Walimwengu wote, basi kubashiria na kuonya kwake hali kadhalika ni kwa ajili ya ulimwengu mzima na si kaumu yake tu kama ilivyokuwa desturi ya Manabii wengineo kabla yake:

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):   

 

تَبَارَكَ الَّذِي نَزَّلَ الْفُرْقَانَ عَلَىٰ عَبْدِهِ لِيَكُونَ لِلْعَالَمِينَ نَذِيرًا ﴿١﴾

Amebarikika Ambaye Ameteremsha kwa mja Wake pambanuo (la haki na batili) ili awe muonyaji kwa walimwengu. [Al-Furqaan: 1]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَكَانَ لِلنَّاسِ عَجَبًا أَنْ أَوْحَيْنَا إِلَىٰ رَجُلٍ مِّنْهُمْ أَنْ أَنذِرِ النَّاسَ وَبَشِّرِ الَّذِينَ آمَنُوا أَنَّ لَهُمْ قَدَمَ صِدْقٍ عِندَ رَبِّهِمْ ۗ قَالَ الْكَافِرُونَ إِنَّ هَـٰذَا لَسَاحِرٌ مُّبِينٌ﴿٢﴾

Je, imekuwa ni ajabu kwa watu kwamba Tumemfunulia Wahy mtu miongoni mwao kwamba: Waonye watu na wabashirie wale walioamini kwamba watapata cheo kitukufu mbele ya Rabb wao. Makafiri wakasema: Hakika huyu bila shaka ni mchawi bayana. [Yuwnus: 2]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَأَرْسَلْنَاكَ لِلنَّاسِ رَسُولًا ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ شَهِيدًا ﴿٧٩﴾

Na Tumekutuma (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kwa watu uwe Rasuli na inatosheleza Allaah kuwa ni Mwenye kushuhudia yote. [An-Nisaa: 79]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَأُوحِيَ إِلَيَّ هَـٰذَا الْقُرْآنُ لِأُنذِرَكُم بِهِ وَمَن بَلَغَ ۚ

Na nimefunuliwa Wahy hii Qur-aan ili nikuonyeni kwayo na kila itakayomfikia.[Al-An’aam: 19]

 

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ إِنَّا أَرْسَلْنَاكَ شَاهِدًا وَمُبَشِّرًا وَنَذِيرًا ﴿٤٥﴾

Ee Nabiy! Hakika Sisi Tumekutuma uwe shahidi, na mbashiriaji na mwonyaji.

 

وَدَاعِيًا إِلَى اللَّـهِ بِإِذْنِهِ وَسِرَاجًا مُّنِيرًا ﴿٤٦﴾

Na mlinganiaji kwa Allaah kwa idhini Yake; na siraji kali yenye nuru.

 

وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ بِأَنَّ لَهُم مِّنَ اللَّـهِ فَضْلًا كَبِيرًا ﴿٤٧﴾

Na wabashirie Waumini kwamba watapata kutoka kwa Allaah fadhila kubwa.

 

وَلَا تُطِعِ الْكَافِرِينَ وَالْمُنَافِقِينَ وَدَعْ أَذَاهُمْ وَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ ۚ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ وَكِيلًا ﴿٤٨﴾

Na wala usiwatii makafiri na wanafiki, na achilia mbali maudhi yao, na tawakali kwa Allaah. Na Allaah Anatosheleza kuwa Mdhamini. [Al-Ahzaab: 45-48]

 

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ بَلِّغْ مَا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ ۖ وَإِن لَّمْ تَفْعَلْ فَمَا بَلَّغْتَ رِسَالَتَهُ ۚ وَاللَّـهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ ﴿٦٧﴾

Ee Rasuli! Balighisha yale yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Rabb wako. Na usipofanya, basi utakuwa hukubalighisha ujumbe Wake. Na Allaah Atakuhifadhi dhidi ya watu. Hakika Allaah Haongoi watu makafiri [Al-Maaidah: 67]

 

 

Bonyeza kiungo kifuatacho upate faida  inayohusiana na maudhui ya fadhila hii:

 

 

02-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Ametumwa Kwa Walimwengu Wote

 

 

 

 



08-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Zuhd Yake: Njaa Ilimtoa Nje

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

08-Zuhd Yake: Njaa Ilimtoa Nje

 

Alhidaaya.com

 

 

Siku moja au usiku mmoja, pindi njaa ilipomzidi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alitoka nje, akakutana na Swahaba zake ambao nao pia wametoka nje kwa sababu ya kubanwa na njaa:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، قَالَ خَرَجَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ذَاتَ يَوْمٍ أَوْ لَيْلَةٍ فَإِذَا هُوَ بِأَبِي بَكْرٍ وَعُمَرَ فَقَالَ ‏"‏ مَا أَخْرَجَكُمَا مِنْ بُيُوتِكُمَا هَذِهِ السَّاعَةَ ‏"‏ ‏.‏ قَالاَ الْجُوعُ يَا رَسُولَ اللَّهِ ‏.‏ قَالَ ‏"‏ وَأَنَا وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ لأَخْرَجَنِي الَّذِي أَخْرَجَكُمَا قُومُوا ‏"‏ ‏.‏ فَقَامُوا مَعَهُ فَأَتَى رَجُلاً مِنَ الأَنْصَارِ فَإِذَا هُوَ لَيْسَ فِي بَيْتِهِ فَلَمَّا رَأَتْهُ الْمَرْأَةُ قَالَتْ مَرْحَبًا وَأَهْلاً ‏.‏ فَقَالَ لَهَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏"‏ أَيْنَ فُلاَنٌ ‏"‏ ‏.‏ قَالَتْ ذَهَبَ يَسْتَعْذِبُ لَنَا مِنَ الْمَاءِ ‏.‏ إِذْ جَاءَ الأَنْصَارِيُّ فَنَظَرَ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَصَاحِبَيْهِ ثُمَّ قَالَ الْحَمْدُ لِلَّهِ مَا أَحَدٌ الْيَوْمَ أَكْرَمَ أَضْيَافًا مِنِّي  قَالَ - فَانْطَلَقَ فَجَاءَهُمْ بِعِذْقٍ فِيهِ بُسْرٌ وَتَمْرٌ وَرُطَبٌ فَقَالَ كُلُوا مِنْ هَذِهِ ‏.‏ وَأَخَذَ الْمُدْيَةَ فَقَالَ لَهُ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏"‏ إِيَّاكَ وَالْحَلُوبَ ‏"‏ ‏.‏ فَذَبَحَ لَهُمْ فَأَكَلُوا مِنَ الشَّاةِ وَمِنْ ذَلِكَ الْعِذْقِ وَشَرِبُوا فَلَمَّا أَنْ شَبِعُوا وَرَوُوا قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم لأَبِي بَكْرٍ وَعُمَرَ ‏"‏ وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ لَتُسْأَلُنَّ عَنْ هَذَا النَّعِيمِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ أَخْرَجَكُمْ مِنْ بُيُوتِكُمُ الْجُوعُ ثُمَّ لَمْ تَرْجِعُوا حَتَّى أَصَابَكُمْ هَذَا النَّعِيمُ ‏"‏ ‏.‏ مسلم

 

Amehadithia Abuu Hurayrayh (رضي الله عنه) kwamba: Siku moja Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alitoka mchana mmoja, au usiku, akakutana na Abuu Bakr na ‘Umar (رضي الله عنهما) akawauliza: “Jambo gani lililokutoeni majumbani mwenu wakati huu?”  Wakasema: “Ni njaa ee Rasuli wa Allaah!” Akasema: “Nami naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mkononi Mwake, nami pia lililonitoa ni kama lililowatoa nyinyi. Twendeni!”  Wakafuatana naye hadi nyumbani kwa mtu miongoni mwa Answaariy, lakini hawakumkuta nyumbani kwake. Mkewe alipomuona (Rasuli wa Allaah) alimwambia: “Marhaban wa Ahlan” (Karibu). Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwambia: “Yuko wapi fulani?” Akajibu: Amekwenda kututafutia maji matamu.” Mara yule Answaariy akaja akamtazama Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na Swahaba zake akasema: “AlhamduliLLaah! Leo hakuna mwenye wageni watukufu kama mimi!” Akaondoka kisha akarudi na kichala cha tende tosa, tende kavu na tende mbivu, Akwaambia: “Kuleni!” Akachukua kisu lakini Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwambia: “Usichinje mbuzi wa maziwa.” Akawachinjia wakala mbuzi yule na wakala katika kile kichala cha tende na wakanywa. Waliposhiba na wakamaliza kiu chao, Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akawaambia Abuu Bakar na ‘Umar (رضي الله عنهما): “Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mkononi Mwake, mtaulizwa Siku ya Qiyaamah juu ya neema hii. Njaa imewatoa majumbani mwenu, kisha hamkurejea mpaka mkapata neema hii.” [Muslim]

 

Na alifundisha du’aa ya kumumobea mtu anayekupa chakula au kinywaji useme:

 

اللّهُـمَّ أَطْعِمْ مَن أَطْعَمَني، وَاسْقِ مَن سَقانِي

Allaahumma Atw-’im man atw-’amaniy Wasqi man saqaaniy

Ee Allaah Mlishe aliyenilisha na Mnywishe aliyeninyweisha  [Hadiyth ya Al-Miqdaad bin Al-Aswad  (رضي الله عنه) - Muslim (3/126) [2055], Ahmad]

 

 

 



010-Aayah Na Mafunzo: Kula Mali Ya Yatima Ni Miongoni Mwa Mambo Saba Yanayoangamiza

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Kula Mali Ya Yatima Ni Miongoni Mwa Mambo Saba Yanayoangamiza

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الَّذِينَ يَأْكُلُونَ أَمْوَالَ الْيَتَامَىٰ ظُلْمًا إِنَّمَا يَأْكُلُونَ فِي بُطُونِهِمْ نَارًا ۖ وَسَيَصْلَوْنَ سَعِيرًا ﴿١٠﴾

10. Hakika wale wanaokula mali ya mayatima kwa dhulma hapana shaka kwamba wanakula katika matumbo yao moto, na watauingia moto uliowashwa vikali mno”

 

Mafunzo:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه عن النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((اجْتَنِبُوا السَّبْعَ الْمُوبِقَاتِ)) قَالُوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ وَمَا هُنَّ؟  قَالَ: ((الشِّرْكُ بِاللَّهِ وَالسِّحْرُ وَقَتْلُ النَّفْسِ الَّتِي حَرَّمَ اللَّهُ إِلاَّ بِالْحَقِّ وَأَكْلُ الرِّبَا وَأَكْلُ مَالِ الْيَتِيمِ وَالتَّوَلِّي يَوْمَ الزَّحْفِ وَقَذْفُ الْمُحْصَنَاتِ الْمُؤْمِنَاتِ الْغَافلاَتِ)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:((Jiepusheni na mambo saba yanayoangamiza!)) Wakauliza: Ni yepi hayo ee Rasuli wa Allaah? Akasema: ((Ni kumshirikisha Allaah, sihri [uchawi], kuua nafsi Aliyoiharamisha Allaah isipokuwa kwa haki, kula ribaa, kula mali ya yatima, kukimbia wakati wa kupambana na adui na kuwatuhumu uzinifu wanawake Waumini waliohifadhika walioghafilika)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 



110-Asbaab Nuzuwl: An-Nahl: Kisha Wale Waliohajiri Baada Ya Kutiwa Katika Mitihani

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

016- Suwrah An-Nahl Aayah: 110

 

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

ثُمَّ إِنَّ رَبَّكَ لِلَّذِينَ هَاجَرُوا مِن بَعْدِ مَا فُتِنُوا ثُمَّ جَاهَدُوا وَصَبَرُوا إِنَّ رَبَّكَ مِن بَعْدِهَا لَغَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿١١٠﴾

Kisha hakika Rabb wako, kwa wale waliohajiri baada ya kutiwa katika mitihani, kisha wakafanya jihaad na wakasubiri; hakika Rabb wako baada ya hayo bila shaka ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [An-Nahl: 110]

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

عن ابن عباس قال: كان قوم من أهل مكة أسلموا وكانوا يستخفون بالإسلام، فأخرجهم المشركون يوم بدر معهم، فأصيب بعضهم وقتل بعض، فقال المسلمون: كان أصحابنا هؤلاء مسلمين وأكرهوا فاستغفروا لهم فنزلت ((إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلائِكَةُ ظَالِمِي أَنْفُسِهِمْ)) إلى آخر الآية.  قال: وكتب إلى من بقي بمكة من المسلمين هذه الآية لا عذر لهم قال: فخرجوا فلحقهم المشركون فأعطوهم الفتنة فنزلت هذه الآية ((وَمِنَ النَّاسِ مَنْ يَقُولُ آمَنَّا بِاللَّهِ فَإِذَا أُوذِيَ فِي اللَّهِ جَعَلَ فِتْنَةَ النَّاسِ كَعَذَابِ اللَّهِ)) إلى آخر الآية. فكتب المسلمون إليهم بذلك فخرجوا وأيسوا من كل خير ثم نزلت فيهم ((ثُمَّ إِنَّ رَبَّكَ لِلَّذِينَ هَاجَرُوا مِنْ بَعْدِ مَا فُتِنُوا ثُمَّ جَاهَدُوا وَصَبَرُوا إِنَّ رَبَّكَ مِنْ بَعْدِهَا لَغَفُورٌ رَحِيمٌ)) فكتبوا إليهم بذلك إن الله قد جعل لكم مخرجا ، فخرجوا فأدركهم المشركون فقاتلوهم ثم نجا من نجا وقتل من قتل.
 

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas kwamba kulikuwepo watu wa Makkah waliosilimu wakawa wanaficha Uislamu wao. Washirikina wakawatoa siku ya vita vya Badr pamoja nao, na wakajeruhiwa baadhi yao na wengineo wakauawa. Waislamu wakasema: “Hawa walikuwa marafiki zetu wa Kiislamu.”  Basi walilazimishwa (kutoka kupigana),  wakawaombea maghfirah ikateremka:

 

إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ ظَالِمِي أَنفُسِهِمْ قَالُوا فِيمَ كُنتُمْ ۖ قَالُوا كُنَّا مُسْتَضْعَفِينَ فِي الْأَرْضِ ۚ قَالُوا أَلَمْ تَكُنْ أَرْضُ اللَّـهِ وَاسِعَةً فَتُهَاجِرُوا فِيهَا ۚ فَأُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا ﴿٩٧﴾

Hakika wale ambao Malaika wamewafisha, hali wamejidhulumu nafsi zao; (Malaika) watawaambia: Mlikuwa katika hali gani? Watasema: Tulikuwa tukikandamizwa katika ardhi.  (Malaika) Watasema: Je, kwani ardhi ya Allaah haikuwa ya wasaa mkahajiri? Basi hao makazi yao yatakuwa ni Jahannam, na uovu ulioje mahali pa kuishia [An-Nisaa: 97]

 

Akasema: Ikatolewa hukumu kwa Waislamu waliobakia Makkah kuwa hawana udhuru kutokana na Aayah hii. Wakatoka, wakakutana na washirikina wakawatia katika fitnah (mitihani) ikateremka Aayah ifuatayo:

 

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَقُولُ آمَنَّا بِاللَّـهِ فَإِذَا أُوذِيَ فِي اللَّـهِ جَعَلَ فِتْنَةَ النَّاسِ كَعَذَابِ اللَّـهِ وَلَئِن جَاءَ نَصْرٌ مِّن رَّبِّكَ لَيَقُولُنَّ إِنَّا كُنَّا مَعَكُمْ ۚ أَوَلَيْسَ اللَّـهُ بِأَعْلَمَ بِمَا فِي صُدُورِ الْعَالَمِينَ ﴿١٠﴾

Na miongoni mwa watu wako wasemao: Tumemwamini Allaah; lakini wanapoudhiwa kwa ajili ya Allaah, hufanya fitnah za watu kama kwamba ni adhabu ya Allaah. Na inapowajia nusura kutoka kwa Rabb wako husema: Hakika sisi tulikuwa pamoja nanyi. Je, kwani Allaah Hayajui yale yaliyomo katika vifua vya walimwengu? [Al-‘Ankabuwt: 10]

 

Wakaandikiwa hukumu Waislamu kwa hayo, wakatoka na wakaacha kufanya kheri zote ikawateremkia:

 

ثُمَّ إِنَّ رَبَّكَ لِلَّذِينَ هَاجَرُوا مِن بَعْدِ مَا فُتِنُوا ثُمَّ جَاهَدُوا وَصَبَرُوا إِنَّ رَبَّكَ مِن بَعْدِهَا لَغَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿١١٠﴾

Kisha hakika Rabb wako, kwa wale waliohajiri baada ya kutiwa katika mitihani, kisha wakafanya jihaad na wakasubiri; hakika Rabb wako baada ya hayo bila shaka ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [An-Nahl: 110]

 

Wakaandikiwa hukumu kwa hiyo kwamba Allaah Amekujaalieni njia. Wakatoka wakakutana na washirikina wakapigana, na baadhi kuuwawa na baadhi kupona.   

 

[Ibn Jariyr]

 



052-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Muumin Angelijua Adhabu Za Allaah Asingelitarajia Jannah, Kafiri Angelijua Rahma Ya Allaah Asingelikata Tamaa Nayo

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 52

Muumin Angelijua Adhabu Za Allaah Asingelitarajia Jannah,

Kafiri Angelijua Rahma Ya Allaah Asingelikata Tamaa Nayo

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ  (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لَوْ يَعْلَمُ الْمُؤْمِنُ مَا عِنْدَ اللَّهِ مِنْ الْعُقُوبَةِ مَا طَمِعَ بِجَنَّتِهِ أَحَدٌ. وَلَوْ يَعْلَمُ الْكَافِرُ مَا عِنْدَ اللَّهِ مِنْ الرَّحْمَةِ مَا قَنَطَ مِنْ جَنَّتِهِ أَحَدٌ)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Lau Muumin angalijua adhabu zilioko kwa Allaah, hakuna yeyote angelitarajia kuingia katika Jannah Yake. Na Lau kafiri angalijua Rahma zilioko kwa Allaah, hakuna yeyote angekata tamaa ya Jannah Yake)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kukhofia adhabu za Allaah (سبحانه وتعالى) na kutaraji Rahma Zake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

غَافِرِ الذَّنبِ وَقَابِلِ التَّوْبِ شَدِيدِ الْعِقَابِ ذِي الطَّوْلِ ۖ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ إِلَيْهِ الْمَصِيرُ﴿٣﴾

Mwenye kughufuria dhambi, Anayepokea tawbah, Mkali wa kuakibu, Mwenye wingi wa Ukarimu, hakuna Mwabudiwa wa haki ila Yeye, Kwake ndio mahali pa kuishia. [Ghaafir (40: 3)

 

Rejea pia: Al-Maaidah (5: 98), Az-Zumar (39: 53).

 

 

2. Muumin anapaswa kuwa katika hali ya khofu na matarajio hata anapotenda mema. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):  

 

وَالَّذِينَ يُؤْتُونَ مَا آتَوا وَّقُلُوبُهُمْ وَجِلَةٌ أَنَّهُمْ إِلَىٰ رَبِّهِمْ رَاجِعُونَ ﴿٦٠﴾

Na ambao wanatoa vile walivyopewa na huku nyoyo zao zinakhofu kwamba hakika watarejea kwa Rabb wao.

 

أُولَـٰئِكَ يُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَهُمْ لَهَا سَابِقُونَ ﴿٦١﴾

Hao wanakimbilia katika mambo ya kheri; na wao ndio wenye kuyatanguliza.  [Al-Muuminuwn (23: 60-61)]

 

 

3. Muumin anatakiwa akimbilie kutenda mema apate Rahma na malipo mema ya Rabb wake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَالَّذِينَ هَاجَرُوا وَجَاهَدُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ أُولَـٰئِكَ يَرْجُونَ رَحْمَتَ اللَّـهِ ۚ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٢١٨﴾

Hakika wale walioamini na wale waliohajiri na wakapigana jihaad katika njia ya Allaah, hao wanataraji rahmah ya Allaah, na Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Al-Baqarah (2: 218)]

 

 

4. Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى) ni pana mno, na adhabu Yake ni kali mno. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَالَ عَذَابِي أُصِيبُ بِهِ مَنْ أَشَاءُ ۖ وَرَحْمَتِي وَسِعَتْ كُلَّ شَيْءٍ ۚ فَسَأَكْتُبُهَا لِلَّذِينَ يَتَّقُونَ وَيُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَالَّذِينَ هُم بِآيَاتِنَا يُؤْمِنُونَ ﴿١٥٦﴾

 (Allaah) Akasema: “Adhabu Yangu Nitamsibu nayo Nimtakaye. Na rahmah Yangu imeenea kila kitu. Basi Nitawaandikia wale wenye taqwa na wanaotoa Zakaah na ambao wao wanaziamini Aayaat (ishara, dalili) Zetu.” [Al-A’raaf (6: 156)]

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَإِن كَذَّبُوكَ فَقُل رَّبُّكُمْ ذُو رَحْمَةٍ وَاسِعَةٍ وَلَا يُرَدُّ بَأْسُهُ عَنِ الْقَوْمِ الْمُجْرِمِينَ ﴿١٤٧﴾

Wakikukadhibisha (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم); basi sema: “Rabb wenu ni Mwenye rahmah iliyoenea. Na wala haizuiliwi adhabu Yake kwa watu wahalifu.” [Al-An’aam (6: 147)]

 

 

Rejea pia: Al-A’raaf (7: 56).

 

 

5. Allaah (سبحانه وتعالى) Amewapa fursa makafiri wataraji Rahma na Jannah Yake, lakini ni chaguo lao kukubali haki au kubakia katika upotofu.

 

 

6. Jannah imejaa mazuri yasiyoweza kutambulikana katika akili ya binaadamu. Hadiyth: Al-Qudsiy: ((Nimewatayarishia waja Wangu wema kile ambacho jicho lolote halijapata kuona, na sikio lolote halijapata kusikia, na wala haijapata kupita katika moyo wa binaadamu)). [Al-Bukhaariy na Muslim]  Akasema Abuu Hurayrah: Kwa hivyo, soma ukitaka: ((Basi nafsi yoyote haijui  yaliyofichiwa katika yanayoburudisha macho)). [As-Sajdah (32: 17)]

 

 

7. Moto wa Jahannam na adhabu zake ni kali mno. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

فَالَّذِينَ كَفَرُوا قُطِّعَتْ لَهُمْ ثِيَابٌ مِّن نَّارٍ يُصَبُّ مِن فَوْقِ رُءُوسِهِمُ الْحَمِيمُ ﴿١٩﴾

Basi wale waliokufuru watakatiwa nguo za moto watamwagiwa juu ya vichwa vyao maji yachemkayo.

 

يُصْهَرُ بِهِ مَا فِي بُطُونِهِمْ وَالْجُلُودُ ﴿٢٠﴾

Yatayeyusha kwayo (maji hayo) yaliyomo matumboni mwao na ngozi zao.

 

وَلَهُم مَّقَامِعُ مِنْ حَدِيدٍ ﴿٢١﴾

Na watapata marungu ya vyuma.

 

كُلَّمَا أَرَادُوا أَن يَخْرُجُوا مِنْهَا مِنْ غَمٍّ أُعِيدُوا فِيهَا وَذُوقُوا عَذَابَ الْحَرِيقِ ﴿٢٢﴾

Kila watakapotaka kutoka humo kwa dhiki, watarudishwa humo; na (wataambiwa): “Onjeni adhabu ya kuunguza.” [Al-Hajj (22: 19-22)]

 

 

Rejea pia: An-Nisaa (4: 560, Ibraahiym (14: 15-17), (49-50), Al-Muuminuwn (23: 103-108), Al-Furqaan (25:  65), Asw-Swaaffaat (37: 62-68), Ad-Dukhaan (44: 43-50)  

 

 

  

 



20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...