Translate

Jumatatu, 28 Januari 2019

07. Kulenga kusikika katika mambo ya ki-´Ibaadah ni shirki ndogo

Vivyo hivyo mtu kutaka kusikika. Ni kama kujionyesha. Kutaka kusikika ni kule mtu kupenda asikike na watu. Kwa mfano wasikie du´aa zake, kauli zake ambazo uinje wake ni nzuri na anaonekana anamdhukuru Allaah ilihali anachokusudia watu wamsifu na watu waseme kwa kweli fulani anamdhukuru Allaah sana, fulani anatafuta elimu, anafundisha elimu, fulani anafanya hivi na vile. Anaboresha sauti yake katika kisomo cha Qur-aan kwa ajili ya kutaka kusifiwa na watu. Yote haya ni katika aina za mtu kutaka kusikika. Mwenye kutaka kuonekana, basi Allaah atamfanya kweli aonekane. Kwa sababu malipo yanategemea na vile mtu alivyotenda. Mwenye kutaka kusikika, basi Allaah atamfanya kweli asikike.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2CMSvG8
via IFTTT

06. Kulenga kujionyesha katika mambo ya ki-´Ibaadah ni shirki ndogo

Miongoni mwa hayo ni yale yanayokuwa ndani ya moyo katika kujionyesha. Bi maana mtu akajionyesha kwa matendo. Mtu akafanya ´ibaadah uinje wake zikaonekana ni kwa ajili ya Allaah pamoja na kwamba anawaonyesha watu. Lengo anataka watu wamsifu, wamtape n.k. Huku ndio kujionyeasha. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Je, nisikwambieni kile ninachokukhofieni kuliko hata huyo al-Masiyh ad-Dajjaal?” Wakasema: “Ndio, ee Mtume wa Allaah!” Akasema: “Ni shirki iliyojificha.”

Shirki iliyojificha ni kujionyesha. Kwa sababu inakuwa ndani ya moyo na hakuna aijuaye isipokuwa Allaah pekee.

“Anasimama mtu kuswali na akaipamba swalah yake kwa kuwa anaona watu wanamwangalia.”[1]

Amesema (Ta´ala):

فَوَيْلٌ لِّلْمُصَلِّينَ الَّذِينَ هُمْ عَن صَلَاتِهِمْ سَاهُونَ الَّذِينَ هُمْ يُرَاءُونَ

“Basi adhabu kwa wanaoswali, ambao kuhusu swalah zao wanapuuza, ambao wanajionyesha.” (107:04-07)

Kujionyesha ni khatari. Ni jambo ambalo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kalikhofia juu ya Maswahabah zake. Kwa sababu kila mtu anapenda sifa, matapo, kuonekana kwa sura nzuri n.k., huenda hayo yakampelekea akaanza kujionyesha katika mambo ya ´ibaadah. Kujipamba mwili wake kwa mavazi na nguo nzuri, hili ni jambo linalotakikana kujipamba na kuvaa vizuri. Ama kuyapamba matendo yake mbele za watu ilihali hakusudii uso wa Allaah, bali kinyume chake anawakusudia watu, huu ndio msimba mkubwa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Kikubwa ninachokikhofia juu yenu ni shirki iliyojificha.” Wakasema: “Ni ipi hiyo, ee Mtume wa Allaah?” Akasema: “Ni kujionyesha.”

Imeitwa ´kujionyesha` (Riyaa`) kwa sababu malengo yake anataka watu wamuone.

[1] Ahmad (11270) na Ibn Maajah (4203). Nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Sunan Ibn Maajah” (3389).



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2RUi82h
via IFTTT

05. Mifano mbalimbali ya shirki ndogo

Miongoni mwa mambo yanayoitia kasoro ´Aqiydah ni shirki ndogo. Nayo inakuwa kwa matamshi ya dhahiri. Kwa mfano kuapa kwa jina la asiyekuwa Allaah (´Azza wa Jall). Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Atakayeapa kwa asiyekuwa Allaah amekufuru au amefanya shirki.”

“Msiape kwa baba zenu! Yule mwenye kutaka kuapa basi aape kwa jina la Allaah au anyamaze.”

Kuapa kwa asiyekuwa Allaah ni shirki. Lakini hata hivyo ni shirki ndogo isipokuwa tu ikiwa mtu huyo atakusudia kumuadhimisha yule anayemuapia kama anavyoadhimishwa Allaah (´Azza wa Jall) hapo itakuwa shirki kubwa. Hili hufanywa na watu wengi kuapa kwa asiyekuwa Allaah. Kwa mfano utawasikia wanasena ´naapa kwa Mtume` (wan-Nabiy), wanaapa kwa jina la Ka´bah na wanaapa kwa amana. Hii ni shirki. Inaweza kuwa shirki ndogo au kubwa itatokana na nia ya muapaji. Kuna watu wengi wasiojua uhakika wa Tawhiyd na wala hawasomi makatazo ya kuapa kwa ajili ya asiyekuwa Allaah.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2Sak0mB
via IFTTT

04. Kuchinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah ni shirki kubwa

Kuna watu wanaochinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah kwa ajili ya kujikurubisha kwa viumbe, kwa wafu, makaburi – wanachinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah. Wanamshirikisha Allaah shirki kubwa. Kwa sababu kujikurubisha kwa kuchinja inakuwa kwa ajili ya Allaah (´Azza wa Jalla) pekee. Haifai kwa mtu akajikurubisha kwa kitendo hicho kwa mwengine yeyote asiyekuwa Allaah. Amesema (Ta´ala):

قُلْ إِنَّ صَلَاتِي وَنُسُكِي وَمَحْيَايَ وَمَمَاتِي لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ لَا شَرِيكَ لَهُ ۖ وَبِذَٰلِكَ أُمِرْتُ وَأَنَا أَوَّلُ الْمُسْلِمِينَ

“Sema: “Hakika swalah yang na kichinjwa changu na uhai wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Allaah pekee, Mola wa walimwengu hali ya kuwa hana mshirika – na kwa hayo ndio nimeamrishwa nami ni muislamu wa kwanza.” (06:162-163)

Vilevile amesema (Ta´ala):

فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ

“Basi swali kwa ajili ya Mola wako na [pia ukichinja] na chinja [kwa ajili Yake].” (108:02)

Amefanya kuchinja ni mwenza wa swalah. Kama ambavyo haifai kwa mtu akaswali kwa ajili ya asiyekuwa Allaah hali kadhalika haifai kwake kuchinnja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah.

Baadhi ya watu wanachinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah. Wanawachinjia wafu kwa ajili wawanufaishe na wawaondoshee madhara, wawaponye maradhi walionayo au maradhi yaliyo na watoto wao. Anawachinjia kwa ajili ya ponyo na kujitibu kama alivyowapambia mashaytwaan wa kiwatu na wakijini. Wanachinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah (´Azza wa Jalla). ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Allaah amemlaani mwenye kuchinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah.”[1]

Shirki kubwa inaporomosha ´Aqiydah kuanzia msingi wake. Nayo ni pindi mtu atapofanya aina yoyote ya ´ibaadah kumfanyia asiyekuwa Allaah (´Azza wa Jall). Mfano wa ´ibaadah hizo ni kama du´aa, kuchinja, kuweka nadhiri na mengineyo. Na ni wingi ulioje wa watu ambao wametumbukia katika mambo haya katika makaburi yaliyoko katika miji mingi ya waislamu! Na huenda mjinga akadanganyika kwa hilo na khaswa pale anapopambiwa na kuambiwa:

“Utapata kadhaa na kadhaa.”

Matokeo yake akachinja na kuweka nadhiri kwa ajili ya asiyekuwa Allaah na akadanganywa na kuambiwa kwamba ni kwa ajili tu ya kufanya Tawassul kwa watu wema. Hii ni shirki. Hata kama wataita kuwa ni ´Tawassul`. Ni shirki. Majina hayabadilisha uhakika wa mambo.

[1] Muslim (1978).



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2HDlP7B
via IFTTT

03. Kumuomba asiyekuwa Allaah ni shirki kubwa

Miongoni mwa hayo ni shirki kubwa na ndogo. Shirki kubwa ni kama mfano wa kumuomba asiyekuwa Allaah katika mawalii, watu wema, wafu na wengineo. Kwa kuwa du´aa ndio ´ibaadah. Bi maana ndio aina kubwa ya ´ibaadah. Ndani yake kumekusanywa ´baadah nyingi ikiwa ni pamoja na unyenyekevu, kujidhalilisha kwa Allaah, kutambua ya kuwa hakuna anayenufaisha wala kudhuru ila Allaah pekee, kumtegemea Allaah na kurejea kwa Allaah. Du´aa inakuwa na mambo yote haya. Kwa ajili hii, ndio maana amesema (Jalla wa ´Alaa):

وَأَنَّ الْمَسَاجِدَ لِلَّـهِ فَلَا تَدْعُوا مَعَ اللَّـهِ أَحَدًا

“Kwamba sehemu zote za kuswalia ni kwa ajili ya Allaah, hivyo basi msiombe yeyote pamoja na Allaah.” (72:18)

Amesema (Subhaanah):

وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ ۚ إِنَّ الَّذِينَ يَسْتَكْبِرُونَ عَنْ عِبَادَتِي سَيَدْخُلُونَ جَهَنَّمَ دَاخِرِينَ

“Mola wenu anasema: “Niombeni Nitakuitikieni. Hakika wale wanaotakabari na ‘ibaadah Yangu, watauingika [Moto wa] Jahanam wadhalilike.” (40:60)

Amesema (Ta´ala):

فَادْعُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ وَلَوْ كَرِهَ الْكَافِرُونَ

“Basi mwombeni Allaah hali ya kumtakasia Yeye dini, japokuwa wanachukiwa makafiri.” (40:14)

Du´aa umuhimu wake ni mkubwa. Wako watu wengi wanaomba badala ya Allaah katika mambo muhimu, ya kutia huzuni na shida mbalimbali. Wanaomba, wanaita na wakitafuta uokozi kwa asiyekuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Ni azima kwa muislamu kutanabahi jambo hili. Hakika ni jambo la khatari sana.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2SicUgd
via IFTTT

´Umdat-ul-Ahkaam 17



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2B9QjbF
via IFTTT

´Umdat-ul-Ahkaam 19



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2CRF33X
via IFTTT

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...