Translate

Ijumaa, 11 Septemba 2020

13-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kutundika Kitu Kwa Ajili Ya Kinga, Kumlinganisha Allaah

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

13- Kutundika Kitu Kwa Ajili Ya Kinga Na Kumlinganisha Allaah

Alhidaaya.com

 

 

Katika kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni kutundika vitu ukatani au milangoni n.k. Itikadi ya kitendo hiki ni aina mbili;

 

Kwanza: kutundika kwa kuitakidi kwamba hicho kitu kilichotundikwa ni kinga ya jicho au husda n.k. Vinavyotundikwa huenda ikawa ni fremu za Aayah katika Qur-aan, au du’aa au Majina ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Au wengine hutundika vitu kama pilipili na ndimu, aina ya vijiwe vya buluu vyenye jicho n.k.  Yote haya ni shirki kwa hiyo haijuzu abadani kwa sababu hakuna baya lolote la kumdhuru mtu isipokuwa kama Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amelikidhia kama Anavyosema:

 

مَا أَصَابَ مِن مُّصِيبَةٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ ۗ وَمَن يُؤْمِن بِاللَّـهِ يَهْدِ قَلْبَهُ ۚ وَاللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ﴿١١﴾

Hausibu msiba wowote isipokuwa kwa idhini ya Allaah. Na yeyote   anayemuamini Allaah, (Allaah) Huuongoza moyo wake. Na Allaah kwa kila kitu ni Mjuzi. [At-Taghaabun: 11]

 

Na kinyume chake ni kukosa kutawakali Kwake Subhaanahu wa Ta’aalaa na kukosa kufuata kinga iliyothibiti. Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Hukaym ifuatayo imethibitisha katazo hilo:  

 

((مَنْ تَعَلَّقَ شَيْئًا؛ وُكِّلَ إِلَيْهِ)) رَوَاهُ أَحْمَدُ وَالتِّرْمِذِيُّ

((Atakayetundika kitu (kuitakidi ni kinga) basi amejiweka katika ulinzi wa hicho kitu alichokivaa)) [na kitamdhalilisha]. [Ahmad na At-Tirmidhiy. Hadiyth Marfu’w]

 

Tanbihi: Mifano ya vitu vinavyotundikwa kuitakidi kuwa kitamfaa au kumzuia shari ni: talasimu, hirizi, zindiko na vinginveyo kama ilivyobainishwa katika makala hizi.  

 

Haijuzu kabisa kutundikia kitu kuitakidi ni kinga, bali inatosha kabisa kutawakali kwa Allaah  kwani Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema  :

 

وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ فَهُوَ حَسْبُهُ

Na yeyote anayetawakali kwa Allaah, basi Yeye Humtosheleza.  [Atw-Twalaaq: 3]

 

Na mafunzo Swahiyh ya kujikinga ni kama ilivyothibiti katika Hadiyth ifuatayo:

 

 

عن خَوْلَةَ بِنْتَ حَكِيمٍ (رضي الله عنها) قالت: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ:  ((مَنْ نَزَلَ مَنْزلاَ ثُمَّ قَالَ: "أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللَّهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ" لَمْ يَضُرَّهُ شَيْءٌ حَتَّى يَرْتَحِلَ مِنْ مَنْزِلِهِ ذَلِكَ)) رواه مسلم

Imepokelewa toka kwa Khawlat bint Hakiym (Radhiwa Allaahuu ‘anhaa) kwamba kamsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Atakayefikia mahali kisha akasema: 

أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللَّهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ

 

A’uwdhu bikalimati-LLaahit-taammati min sharri maa Khalaq' (Najilinda kwa maneno ya Allaah yaliyotimia na shari ya Alichokiumba), hakuna kitakachomdhuru hadi atakapoondoka mahali pake hapo)). [Muslim]

 

 

Mafunzo mengine sahihi ni kusoma Adhkaar na nyiradi za asubuhi na jioni zilizothibiti.

 

Ama kuhusu kutundika Qur-aan, baadhi ya watu wanaona ni jambo la kupendeza lakini hakika haijuzu kwa sababu Qur-aan imeteremshwa kwa ajili ya Mwongozo, mawaidha, ukumbusho, na kusomwa na kufanyia kazi maamrisho yake na kuacha makatazo yake, na wala si kwa ajili ya kutundikwa. 

 

Ibnul-‘Arabiyy Al-Maalikiyy (Rahimahu Allaah) amesema:

“Kutundika Qur-aan si katika Sunnah, bali Sunnah ni kuisoma bila ya kuitundika.”

 

 

Aghlabu ya watu hutundika Aayatul-Kursiyy au Al-Maw’idhataan na Suwratul-Ikhlaasw ambazo ni nyepesi kabisa kuzihifadhi na kuzisoma na ndizo zilizothibiti katika mafunzo Swahiyh kwamba ni kinga ya Muislamu. Basi kwanini mtu atundike badala ya kuzisoma na kuzihifadhi?

 

Picha za baadhi ya vitu ambavyo baadhi ya watu wanavitundika wakiamini ni kinga:

 

                                       

 

 

     

                          

  

 

Pia kutundika vitu madukani au majumbani kama pilipili, ndimu n.k.

 

         

 

 

        

 

 

 

Pili: Kutundika Jina la Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ukutani mifano kama ifuatavyo:

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Haijuzu kutundika picha kama hizo, kwani haiwezekani kuwa Muumba na aliyeumbwa wawe katika daraja moja, hata kama niyyah ni kupamba nyumba au kudhihirisha mapenzi yao, kwa sababu wengi hudai kuwa hawakusudii kumlinganisha sawa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Basi kujiepusha na hilo ni bora hata kama mtu haitakidi hilo, kwani kukaa mbali na utata ndio njia ya salama katika Dini ya mtu.

 

Kadhaalika, Wanachuoni wamekemea jambo hili kama ifutavyo:

 

Fatwa ya 1 - Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah Lil-Buhuwth Al-'Ilmiyyah Wal-Iftaa imepitia yaliyofikishwa kwa Mufti Mkuu kutoka kwa muulizaji Humuwd ‘Abdul-Aziyz As-Saayigh kwa marejeo Nambari 6860 9/11/1421H.

 

Muulizaji ameuliza swali na haya hapa maelezo yake:

“Allaah Akuhifadhini, na kukhofia yanayojiri katika Dini hii na kutilia mkazo yanayofisidi ‘Aqiydah na ambayo yanaenea kwa Ummah huu kutoka kwa maadui wa Allaah na wa Dini Yake na wepesi wa watu kufuata mambo wanayodhania ni madogo mno lakini kumbe ni makubwa mno na ikawa kuondosha madhara yake ni vigumu. Kama ilivyokuwa hali katika watu wa Nuwh na masanamu yao; walivyoanza kuweka picha za waja wema wakaanza kuziabudu wakidhania ni jambo jema kumbe ni shirki iliyowasababisha watu waliofuata kuabudu masanamu.

 

Tunadhihirisha mbele yenu aina mbali mbali za picha zilizotayarishwa kuwekwa pande mbili; upande kuna Jina la Allaah (’Azza wa Jalla) na upande wa jina la Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Wala sijui lipi bado litakalojiri baada ya haya! Na baadhi ya ndugu wamewaandikia Baraza la Fatwa maombi haya ili kufuatilia maovu ya ‘Aqiydah wakitaraji mtoe maoni yenu ambayo huenda ikiwa ni sababu ya ufumbuzi na tiba ya kuondosha uovu huu, Allaah Awathibitishieni na Akulipeni kwa kuwanufaisha waja Wake Katika utiifu Wake.”

 

Jibu la Baraza la Fatwa:

 

Haijuzu kuandika Jina la Allaah Aliyetukuka [Allaah] pamoja na [Muhammad] jina la Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) sambaba katika karatasi au kwenye ubao [au vitambaa], au kutundika ukutani [kwa hali yoyote]. Huko ni kupindukia mipaka kwa haki yake Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), na kumlinganisha yeye sawa na Allaah. Haya ni mas-alah miongoni mwa masuala ya shirki na hali yeye mwenyewe amekataza katika kauli yake, aliposema:

“Msinitukuze kama Manaswara walivyomtukuza Masiyh mwana wa Maryam, hakika mimi ni mja kwa hiyo semeni mja wa Allaah na Rasuli Wake.”

 

Na hivyo ni wajibu kuondosha picha hizo au karatasi na kufutilia mbali maandishi kama hayo katika kuta au popote penye aina hizo za picha, ili tuilinde ‘Aqiydah na kufuata wasia wa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). 

Wa biLLaahi At-tawfiyq. Wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyinaa wa ‘alaa aalihi wa swahbihi wa sallam.

 

[Fataawa Al-Lajnah Ad-Daaimah Lil-Buhuwth Al-'Ilmiyyah Wal-Iftaa]

 

 

Fatwa ya 2:  Fatwa ya Shaykh Ibn ‘Uthaymin (Rahimahu Allaah):  

Hakika kuandikwa Jina la Allaah (الله) upande mmoja na jina la (محمد) upande wa pili, yakiwa majina hayo yako sambamba na kama hivi:

 الله   ***  محمد     yanamfanya anayetazama kuona kwamba wako katika cheo kimoja na hali Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimjibu mtu mmoja aliyemwambia Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) “Atakavyotaka (au Akipenda) Allaah [In Shaa Allaah) na ukataka wewe.” Akamjibu: ((Je umenilinganisha mimi kuwa sawa Allaah? Bali sema: Akipenda Allaah [In Shaa Allaah] pekee)).

 

Na ikiwa maandishi kama hayo yamewekwa hivyo mbele ya wanaoswali, yatakuwa ni sababu ya kuwashughulisha watu na Swalaah zao. Pia ‘Ulamaa wakubwa wamechukizwa [na kukataza] kuandikwa kitu mbele ya Qiblah kwa sababu kitamshughulisha na kumshawishi mwenye kuswali. Hivyo, haipasi kuandikwa hivyo; namaanisha الله   ***  محمد    Na popote palipoandikwa hivyo panapaswa kufutiliwa mbali!

Na katika sharh yake ya Kitabu cha Buluwghul-Maraam, Kitabu cha Swalaah, Mlango wa Misikiti, Mkanda namba 16 upande wa pili, anasema Shaykh kuwa, kwa uchache maandishi kama haya ni shirk ndogo.”

Ameandika: Muhammad Bin Swaalih Al-‘Uthaymiyn 9/1/1420H.

 

 

Basi ndugu Waislamu tutahadhari kutundika vitu kama hivyo au chochote kile mfano wa hivyo kwa kuitakidi ni kinga au baraka.

 

 

 

 



51-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Amefunuliwa Wahyi Mbingu Ya Saba; Suwrah Na Aayah Mbili Ambazo Hajapewa Nabii Yoyote Kabla Yake

Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

51-Amefunuliwa Wahyi Mbingu Ya Saba; Suwrah Na Aayah Mbili

Ambazo Hajapewa Nabii Yoyote Kabla Yake  

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) amepewa katika Qur-aan Suwrah Al-Faatihah na Aayah mbili za mwisho wa Suwratul-Baqarah, ambazo hajapatapo kupewa mfano wa kama Aayah hizo Nabiy mwenginewe kabla yake.  Juu ya hivyo, Aayah hizo amefunuliwa nazo Wahyi akiwa mbingu ya Saba katika safari ya Israa wal-Mi’raaj:

 

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ، قَالَ بَيْنَمَا جِبْرِيلُ قَاعِدٌ عِنْدَ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم سَمِعَ نَقِيضًا مِنْ فَوْقِهِ فَرَفَعَ رَأْسَهُ فَقَالَ: ((هَذَا بَابٌ مِنَ السَّمَاءِ فُتِحَ الْيَوْمَ لَمْ يُفْتَحْ قَطُّ إِلاَّ الْيَوْمَ، فَنَزَلَ مِنْهُ مَلَكٌ فَقَالَ: هَذَا مَلَكٌ نَزَلَ إِلَى الأَرْضِ لَمْ يَنْزِلْ قَطُّ إِلاَّ الْيَوْمَ، فَسَلَّمَ وَقَالَ أَبْشِرْ بِنُورَيْنِ أُوتِيتَهُمَا لَمْ يُؤْتَهُمَا نَبِيٌّ قَبْلَكَ، فَاتِحَةُ الْكِتَابِ وَخَوَاتِيمُ سُورَةِ الْبَقَرَةِ لَنْ تَقْرَأَ بِحَرْفٍ مِنْهُمَا إِلاَّ أُعْطِيتَهُ)) ‏.‏

Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما)   amehadithia kwamba: Jibriyl   (عليه السلام)  alipokuwa na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  alisikia sauti kutoka juu. Jibriyl   (عليه السلام) akatazama juu akasema: “Huu mlango wa mbinguni umefunguliwa na haujapatapo kufunguliwa isipokuwa leo.” Malaika akateremka humo akasema: “Huyu Malaika ameteremka ardhini, hajapatapo kuteremka kamwe isipokuwa leo.” Akasalimia kisha   akasema: “Pokea bishara ya nuru mbili ulizopewa ambazo hakuna Nabiy aliyepewa kabla yako; Ufunguo wa Kitabu (Al-Faatihah), na Aayah (mbili) za mwisho wa Suwratul-Baqarah.  Hutosoma herufi humo ila utapewa barakah zake ziliomo.” [Muslim]

 

 

Imaam Muslim amenukuu katika Swahiyh yake kuwa Aayah hizi mbili alipewa Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) alipofika kikomo mbingu ya saba katika Safari ya Al-Israa Wal-Mi’raaj pamoja na kupewa Swalaah tano na msamaha kwa mtu asiyemshirikisha Allaah na yeyote au chochote.

 

 

 



07-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Zuhd Yake: Akifunga Jiwe Tumboni Mwake Kwa Sababu Ya Njaa

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

07-Zuhd Yake: Akifunga Jiwe Tumboni Mwake Kwa Sababu Ya Njaa

 

Alhidaaya.com

 

 

Njaa ni jambo gumu mtu kulivumilia kwani huenda likampeleka mtu kula yaliyokuwa ya haraam pindi akikosa chakula. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akifunga tumbo lake kwa kitambaa ili kuzuia njaa:

 

عن أَنَس بْن مَالِكٍ قال:  جِئْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَوْمًا فَوَجَدْتُهُ جَالِسًا مَعَ أَصْحَابِهِ يُحَدِّثُهُمْ وَقَدْ عَصَّبَ بَطْنَهُ بِعِصَابَةٍ ، قَالَ أُسَامَةُ وَأَنَا أَشُكُّ  عَلَى حَجَرٍ ، فَقُلْتُ لِبَعْضِ أَصْحَابِهِ:  لِمَ عَصَّبَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم بَطْنَهُ؟ فَقَالُوا: مِنَ الْجُوعِ ‏.‏ فَذَهَبْتُ إِلَى أَبِي طَلْحَةَ وَهُوَ زَوْجُ أُمِّ سُلَيْمٍ بِنْتِ مِلْحَانَ فَقُلْتُ يَا أَبَتَاهُ ، قَدْ رَأَيْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم عَصَّبَ بَطْنَهُ بِعِصَابَةٍ فَسَأَلْتُ بَعْضَ أَصْحَابِهِ فَقَالُوا مِنَ الْجُوعِ ‏.‏ فَدَخَلَ أَبُو طَلْحَةَ عَلَى أُمِّي فَقَالَ هَلْ مِنْ شَىْءٍ فَقَالَتْ نَعَمْ عِنْدِي كِسَرٌ مِنْ خُبْزٍ وَتَمَرَاتٌ فَإِنْ جَاءَنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَحْدَهُ أَشْبَعْنَاهُ وَإِنْ جَاءَ آخَرُ مَعَهُ قَلَّ عَنْهُمْ ‏.‏  

Anas bin Maalik (رضي الله عنه) amesema:  Nilimtembelea Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) siku moja na nikamkuta amekaa pamoja na Swahaba zake akiongea nao, na alikuwa amejifunga tumbo lake kwa kitambaa. Usaamah alisema: “Nina shaka kama kulikuwa na jiwe juu yake (tumbo lake) au la. Niliuliza baadhi ya Swahaba zake: Kwanini Rasuli amejifungakitambaa tumboni mwake?” Wakasema: “Kutokana na   njaa.” Nikaenda kwa Abuu Twalhah ambaye ni mume wa Umm Sulaym binti Milhaan, nikamwambia: “Ee Baba, nimemuona Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amefunga tumbo lake kwa kitambaa. Nikawauliza baadhi ya Swahaba zake wamesema ni kwa sababu ya njaa. Hapo Abuu Twalhah akamwendea mama yangu akamuuliza: “Je kuna chochote cha kula?” Akasema: “Naam nnavyo vipande vya mkate na baadhi ya tende. Atakapotujia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  pekee yake tutaweza kumpa na vitamshibisha, lakini   ikiwa atakuja pamoja wenginewe basi havitawatosheleza.”   [Muslim]

 

Na alikuwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akiomba du’aa ifuatayo ya kujikinga na njaa:

 

اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنَ الْجُوعِ فَإِنَّهُ بِئْسَ الضَّجِيعُ وَأَعُوذُ بِكَ مِنَ الْخِيَانَةِ فَإِنَّهَا بِئْسَتِ الْبِطَانَةُ

Ee Allaah, hakika mimi najikinga Kwako na njaa kwani hiyo ni mbaya mno kulala nayo, na najikinga Kwako khiyana kwani hiyo ni dhamira ovu. [Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy, Ibn Maajah, Swahiyh An-Nasaaiy (3/1112)]

 

Na miongoni mwa mambo matatu aliyoyaomba katika Hadiyth mojawapo, amwaombea Ummah wake wasiangamizwe kwa sababu ya njaa:

 

قَالَ صلى الله عليه وسلم ‏ "‏ سَأَلْتُ رَبِّي ثَلاَثًا فَأَعْطَانِي ثِنْتَيْنِ وَمَنَعَنِي وَاحِدَةً سَأَلْتُ رَبِّي أَنْ لاَ يُهْلِكَ أُمَّتِي بِالسَّنَةِ فَأَعْطَانِيهَا وَسَأَلْتُهُ أَنْ لاَ يُهْلِكَ أُمَّتِي بِالْغَرَقِ فَأَعْطَانِيهَا وَسَأَلْتُهُ أَنْ لاَ يَجْعَلَ بَأْسَهُمْ بَيْنَهُمْ فَمَنَعَنِيهَا ‏"‏ ‏

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Nilimuomba Rabb Wangu mambo matatu, Amenipa mawili, na Amenikatalia moja. Nilimuomba Rabb wangu Asiuangamize Ummah wangu kwa sababu ya njaa, Akanitakabalia hili, nikamuomba Ummah wangu usiangamizwe kwa kugharikishwa (mafuriko) Akanitakabalia hili,  na nikamuomba Rabb wangu  kwamba kusimwagwe  damu yoyote miongoni mwa watu wa Ummah wangu, lakini Hakunitakabalia hili.”  [Muslim]

 



001-Aayah Na Mafunzo: Fadhila Za Swillatur-Rahm (Kuunga Undugu) Na Matahadharisho Ya Kukata Undugu

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Fadhila Za Swillatur-Rahm (Kuunga Undugu) Na Matahadharisho Ya Kukata Undugu

 

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالًا كَثِيرًا وَنِسَاءً ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا ﴿١﴾ 

 Enyi watu! Mcheni Rabb wenu Ambaye Amekuumbeni kutokana na nafsi moja (Aadam) na Akaumba kutoka humo mke wake (Hawwaa) na Akaeneza kutoka hao wawili wanaume na wanawake wengi. Na mcheni Allaah Ambaye Kwake mnaombana (haki zenu kwa kuunga) undugu. Hakika Allaah ni Mwenye kuwachunga daima. [An-Nisaa: 1]

 

Mafunzo:

 

Swillatur-Rahm = Kuunga Undugu Na Jamaa Wenye Uhusiano Wa Damu:

 

Fadhila kadhaa zimetajwa katika Qur-aan na Sunnah za mwenye kuunga undugu na jamaa wenye uhusiano wa damu. Miongoni mwazo ni:

 

عن أنسٍ رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( من أحَبَّ أنْ يُبْسَطَ لَهُ في رِزْقِهِ ، ويُنْسأَ لَهُ في أثَرِهِ ، فَلْيَصِلْ رَحِمَهُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa na Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anayependa akunjuliwe riziki yake, na arefushiwe maisha yake basi aunge kizazi chake." [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuud] 

 

Matahadharisho ya kukata undugu: Rejea tanbihi (2: 27) Pia miongoni mwa Hadiyth alizokataza Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kukata undugu ni zifuatazo:

 

عن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إنَّ اللهَ تَعَالَى خَلَقَ الخَلْقَ حَتَّى إِذَا فَرَغَ مِنْهُمْ قَامَتِ الرَّحِمُ ، فَقَالَتْ : هَذَا مُقَامُ العَائِذِ بِكَ مِنَ القَطِيعةِ ، قَالَ : نَعَمْ ، أمَا تَرْضَيْنَ أنْ أصِلَ مَنْ وَصَلَكِ ، وَأقْطَعَ مَنْ قَطَعَكِ ؟ قَالَتْ : بَلَى ، قَالَ : فَذَلِكَ لَكِ ، ثُمَّ قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( اقْرَؤُوا إنْ شِئْتمْ : ( فَهَلْ عَسَيْتُمْ إِنْ تَوَلَّيْتُمْ أَنْ تُفْسِدُوا فِي الأَرْضِ وَتُقَطِّعُوا أَرْحَامَكُمْ أُولَئِكَ الَّذِينَ لَعَنَهُمُ اللهُ فَأَصَمَّهُمْ وَأَعْمَى أَبْصَارَهُمْ  ) [ محمد : 22 - 23 ] مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية للبخاري : فَقَالَ الله تَعَالَى : (( مَنْ وَصَلَكِ ، وَصَلْتُهُ ، وَمَنْ  قَطَعَكِ ، قَطَعْتُهُ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) baada ya kuumba viumbe vyote, mpaka Alipomaliza (kukamilisha), yalisimama matumbo (kizazi) na kusema: "Hii ni nafasi ya mtu anayetaka ulinzi  na kinga kutoka  Kwako kwa mwemye kukata (kizazi, na kihitaji ulinzi)." Akasema: "Ndio je huridhiki Kwangu kumuunga anayekuunga, na kumkata mwenye kukukata?" Kikasema: "Ndio (naridhika)." Akaambiwa: "Hilo ni lako." Kisha akasema  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Someni mkitaka: "Basi huenda nyinyi mkigeuka ndio mfanye ufisadi katika ardhi na kukata jamaa zenu wa uhusiano wa damu? Hao ndio ambao Allaah Amewalaani; Akawafanya viziwi na Akawapofua macho yao." [Muhammad: 22-23] [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy: Akasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa): "Anayekuunga, Nitamuunga na anayekukata Nitamkata."

 

 

Pia:

 

عن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لَيْسَ الوَاصِلُ بِالمُكَافِىء ، وَلكِنَّ الوَاصِلَ الَّذِي إِذَا قَطَعَتْ رَحِمُهُ وَصَلَهَا )) رواه البخاري .

Na kutoka kwake Ibn 'Amr bin al-'Aasw (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa):  Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anayeunga si yule anayetoa anapopewa, lakini anayeunga jamaa ni ambaye jamaa zake wanapomkata, yeye huwaunga." [Al-Bukhaariy, Abu Daawuud na At-Tirmidhiy]

 

Pia,

 

وعن عائشة ، قَالَتْ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( الرَّحِمُ مُعَلَّقَةٌ بِالعَرْشِ تَقُولُ : مَنْ وَصَلَنِي ، وَصَلَهُ اللهُ ، وَمَنْ قَطَعَنِي ، قَطَعَهُ اللهُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aa'ishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kizazi kimetundikwa katika 'Arshi, kinasema: "Anayeniunga, Allaah atamuunga, na anayenikata, Allaah Atamkata." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 



103-Asbaab Nuzuwl: An-Nahl: Kwa Yakini Tunajua Wasemayo Kuwa Kuna Mtu Anamfundisha...

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

016- Suwrah An-Nahl Aayah: 103

 

 

Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

وَلَقَدْ نَعْلَمُ أَنَّهُمْ يَقُولُونَ إِنَّمَا يُعَلِّمُهُ بَشَرٌ ۗ لِّسَانُ الَّذِي يُلْحِدُونَ إِلَيْهِ أَعْجَمِيٌّ وَهَـٰذَا لِسَانٌ عَرَبِيٌّ مُّبِينٌ﴿١٠٣﴾

Na kwa yakini Tunajua kwamba wao wanasema: Hakika hapana isipokuwa mtu anamfundisha (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم Qur-aan). Lisani wanayomnasibishia nao ni ya kigeni, na hii ni lisani ya Kiarabu bayana. [An-Nahl: 103]

 

 

Sababun-Nuzuwl:   

 

 

عَنْ عَبْد اللَّه بْن مُسْلِم الْحَضْرَمِيّ قال:  كَانَ لَنَا غُلَامَانِ نَصْرَانِيَّانِ مِنْ أَهْلِ عَيْنِ التَّمْرِ، اسْمُ أَحَدِهِمَا يَسَارٌ وَاسْمُ الْآخَرِ جَبْرٌ ، وَكَانَا يَقْرَآنِ كِتَابًا لَهُمْ. (التَّوْرَاةَ) فَكَانَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم  يَمُرُّ بِهِمَا وَيَسْمَعُ قِرَاءَتَهُمَا، وَكَانَ الْمُشْرِكُونَ يَقُولُونَ: يَتَعَلَّمُ مِنْهُمَا، فَأَنْزَلَ اللَّهُ هَذِهِ الْآيَةَ:

لِّسَانُ الَّذِي يُلْحِدُونَ إِلَيْهِ أَعْجَمِيٌّ وَهَـٰذَا لِسَانٌ عَرَبِيٌّ مُّبِينٌ﴿١٠٣﴾

 

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Muslim Al-Hadhwramiyy amesema:  Tulikuwa na  vijana wawili Manaswara kutoka Watu wa ‘Ayn At-Tamar, mmojawapo akiitwa Yasaar na mwenginewe Jabr, na walikuwa wakiwasomea Kitabu (Tawraat) na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akiwapitia na kuwasikia Qiraa chao, basi washirikina wakawa wanasema:  “Anajifunza kutoka kwa hao wawili.”  Hapo Allaah Akateremsha:

 لِّسَانُ الَّذِي يُلْحِدُونَ إِلَيْهِ أَعْجَمِيٌّ وَهَـٰذَا لِسَانٌ عَرَبِيٌّ مُّبِينٌ﴿١٠٣﴾

Lisani wanayomnasibishia nao ni ya kigeni, na hii ni lisani ya Kiarabu bayana.

 

[Qurtwubiy – Jaami’ Ahkaam Al-Qur-aan, Ibn Jariyr]

 

 



051-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Muumin Anahimiza Jeneza Lake, Kafiri Anakhofia Na Kupiga Mayoe!

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 51

Muumin Anahimiza Jeneza Lake, Kafiri Anakhofia Na Kupiga Mayowe!

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيَّ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِذَا وُضِعَتْ الْجِنَازَةُ وَاحْتَمَلَهَا النَّاسُ – أوِ الرِّجَالُ عَلَى أَعْنَاقِهِمْ، فَإِنْ كَانَتْ صَالِحَةً قَالَتْ: قَدِّمُونِي. وَإِنْ كَانَتْ غَيْرَ صَالِحَةٍ قَالَتْ: يَا وَيْلَهَا! أَيْنَ يَذْهَبُونَ بِهَا؟ يَسْمَعُ صَوْتَهَا كُلُّ شَيْءٍ إلاَّ الإِنْسَانَ وَلَوْ سَمِعَهُ صَعِقَ)) البخاري

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه)   kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Linapowekwa jeneza na likabebwa na watu au wanaume shingoni mwao, basi anapokuwa [maiti] ni mwema husema: Nikadimisheni [nitangulizeni]. Lakini ikiwa si mtu mwema husema: Ole wake! Wanalipeleka wapi? Sauti yake inasikika na kila kitu isipokuwa binaadamu. Na lau angeisikia angelizimia)). [Al-Bukhaariy]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Muumin anatamani ayafikie mema aliyoahidiwa na Allaah (سبحانه وتعالى) baada ya kufariki kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَعَدَ اللَّـهُ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَمَسَاكِنَ طَيِّبَةً فِي جَنَّاتِ عَدْنٍ ۚوَرِضْوَانٌ مِّنَ اللَّـهِ أَكْبَرُ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ﴿٧٢﴾

Allaah Amewaahidi Waumini wanaume na Waumini wanawake Jannaat zipitazo chini yake mito, ni wenye kudumu humo na makazi mazuri katika Jannaat za kudumu milele. Na radhi kutoka kwa Allaah ndio kubwa zaidi. Huko ndiko kufuzu adhimu. [At-Tawbah (9: 72)]

 

Rejea pia: An-Nisaa (4: 122), Al-Maaidah (5: 9), At-Tawbah (9: 111), Luqmaan (31: 8-9), Az-Zumar (39: 20)

 

 

2. Kafiri au mtu muovu anakhofia adhabu aliyotishiwa nayo ambayo hakuiamini duniani.  Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَوْ تَرَىٰ إِذِ الظَّالِمُونَ فِي غَمَرَاتِ الْمَوْتِ وَالْمَلَائِكَةُ بَاسِطُو أَيْدِيهِمْ أَخْرِجُوا أَنفُسَكُمُ ۖ الْيَوْمَ تُجْزَوْنَ عَذَابَ الْهُونِ بِمَا كُنتُمْ تَقُولُونَ عَلَى اللَّـهِ غَيْرَ الْحَقِّ وَكُنتُمْ عَنْ آيَاتِهِ تَسْتَكْبِرُونَ ﴿٩٣﴾

Na lau ungeliona madhalimu pale wakiwa katika mateso makali ya mauti, na Malaika wamenyosha mikono yao (wakiwaambia): “Toeni nafsi zenu! Leo mnalipwa adhabu ya kudhalilisha kwa yale mliyokuwa mkiyasema juu ya Allaah pasi na haki, na mlikuwa mkitakabari kuhusu Aayaat Zake.” [Al-An’aam (6: 93)]

 

Na pia:

 

وَعَدَ اللَّـهُ الْمُنَافِقِينَ وَالْمُنَافِقَاتِ وَالْكُفَّارَ نَارَ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ هِيَ حَسْبُهُمْ ۚ وَلَعَنَهُمُ اللَّـهُ ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ مُّقِيمٌ﴿٦٨﴾

Allaah Amewaahidi wanafiki wanaume na wanafiki wanawake na makafiri moto wa Jahannam, ni wenye kudumu humo; unawatosheleza Na Allaah Amewalaani, na watapata adhabu ya kudumu.  [At-Tawbah (9: 68)]

 

Rejea pia:  Al-Jaathiyah (45: 28)

 

 

3. Ni Sunnah kuharakiza Jeneza.

 

 

4. Jeneza linabebwa na wanaume na si wanawake.

 

 

5. Baadhi ya sauti zinasikika kwa viumbe isipokuwa binaadamu na pia vitu vinginevyo visivyokuwahai. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَإِنَّكَ لَا تُسْمِعُ الْمَوْتَىٰ وَلَا تُسْمِعُ الصُّمَّ الدُّعَاءَ إِذَا وَلَّوْا مُدْبِرِينَ ﴿٥٢﴾

Basi hakika wewe huwezi kusikilizisha wafu, na wala huwezi kusikilizisha viziwi wito wanapokengeua wakigeuza migongo yao. [Ar-Ruwm (30: 52)]

 

Rejea pia: An-Naml (27: 80)

 

 

6. Dalili kwamba maiti anasikia ila hawezi kuongea.

 

 

7. Uthibitisho wa hali ya maisha ya Barzakh na matokeo ya adhabu za kaburi au neema zake.

 

 

 

 

 

 

 

 



Jumapili, 6 Septemba 2020

Chakula cha mgonjwa mwenye Kisukari aina ya kwanza

CHAKULA CHA MGONJWA MWENYE KISUKARI AINA YA KWANZA

Kisukari ni ugonjwa wa kongosho, wakati uzarishaji wa Insulini au utolewaji wake haufanyi kazi vizuri, na ikiwa hali hii haitadhibitiwa, inaweza kusababisha matatizo makubwa kwenye macho, figo, neva, mishipa ya damu, Ini na moyo.

Kisukari aina ya kwanza, ambapo Insulini inakuwa tegemezi (insulin-dependent); hapa kongosho halitengenezi kabisa insulini au linaitengeneza kwa kiasi kidogo sana kiasi kwamba mgonjwa analazimika kuchomwa sindano ya insulini au kutumia pampu za insulini.

Aina ya kwanza ya kisukari inaweza kutokea kwa watu kuanzia utotoni mpaka kwa watu wa umri wa miaka 30. Aina hii ya kisukari hushambulia kwa haraka sana, kwa kawaida ndani ya majuma mpaka miezi kadhaa.

Kwakuwa kongosho halifanyi kazi vizuri, usawa wa damu sukari lazima upewe uangalizi wa karibu. Watu wenye kisukari aina hii ya kwanza pia huwa na uzito pungufu (underweight).

Ni mhimu kula vyakula vyenye afya unapokuwa na kisukari aina ya kwanza. Hata hivyo hii haina maana kwamba unalazimika kuacha kila chakula ukipendacho sababu tu una kisukari.

Aina ya kwanza ya kisukari inaweza kutokea kwa watu kuanzia utotoni mpaka kwa watu wa umri wa miaka 30. Aina hii ya kisukari hushambulia kwa haraka sana, kwa kawaida ndani ya majuma mpaka miezi kadhaa.

Kwakuwa kongosho halifanyi kazi vizuri, usawa wa damu sukari lazima upewe uangalizi wa karibu. Watu wenye kisukari aina hii ya kwanza pia huwa na uzito pungufu (underweight).

Ni mhimu kula vyakula vyenye afya unapokuwa na kisukari aina ya kwanza. Hata hivyo hii haina maana kwamba unalazimika kuacha kila chakula ukipendacho sababu tu una kisukari.

KWANINI NI MHIMU KUZINGATIA CHAKULA

Unapokuwa na kisukari aina ya kwanza mwili wako unaacha kutengeneza insulini. Hivyo unalazimika kuchomwa sindano za insulini kila siku.

Ni mhimu pia kufuatilia kiasi cha damu sukari katika mwili wako kila siku.

Insulini ni sehemu tu ya mambo mhimu ya kuzingatia.

Mlo sahihi na kamili pia mazoezi ya viungo vina umhimu mkubwa kwa mtu mwenye kisukari aina ya kwanza.

Unapochagua kula vyakula vyenye afya kila siku vinaweza kukusaidia kuweka sukari katika kiwango kinachotakiwa.

Kula mlo sahihi kunaweza pia kukusaidia kuepuka na matatizo mengine yahusianayo na kisukari kama ugonjwa wa moyo, magonjwa ya ini, na kudhurika kwa neva.

Chakula cha mgonjwa mwenye Kisukari aina ya kwanza

Baadhi ya wataalamu wamekuwa wakifikiri kwamba kuna lishe au chakula maalumu kwa ajili ya mtu mwenye kisukari.

Wamekuwa wakidhani kwamba mtu mwenye kisukari hatakiwi kabisa kutumia vyakula au vinywaji vyenye sukari na baadhi ya vyakula.

Lakini unapokuwa na kisukari aina ya kwanza unaweza kula vyakula vyovyote vyenye afya kama mtu mwingine yoyote.

Fuata huu muongozo wa jumla:

  1. Punguza kutumia mafuta yasiyo na afya (saturated fats).

Haya ni mafuta yatokanayo na wanyama, maziwa, siagi ya wanyama, nk. Mafuta yasiyo na afya yanaongeza uwezekano kwako wa kupatwa na ugonjwa wa moyo.

Unapokuwa na kisukari hatari ya kupata ugonjwa wa moyo inakuwa kubwa zaidi. Hivyo kuwa makini na chaguo la chakula chako ili kupunguza hatari hiyo.

  1. Kula vyakula vingi vyenye nyuzinyuzi.

Vyakula vyenye nyuzinyuzi vinaweza kukusaidia kudhibiti sukari yako.

Unaweza kupata nyuzinyuzi toka katika vyakula ambavyo havijakobolewa, maharage, matunda na mboga za majani. Jitahidi upate gramu 25 mpaka 30 kila siku za nyuzinyuzi.

Vyakula hivyo vyenye nyuzinyuzi kwa wingi ni bora zaidi kwa mgonjwa wa kisukari aina ya kwanza kuliko vile vyenye nyuzinyuzi chache kama vile vilivyokobolewa na vile vyenye sukari nyingi vya dukani.

KUTAMBUA KIASI CHA WANGA UNACHOKULA

Vyakula vya wanga ndiyo vyakula pekee ambavyo ni chanzo kikuu cha nguvu cha mwili. Unavipata hivyo katika vyakula vingi unavyokula kama mikate, tambi, mboga za majani, matunda, maziwa, viazi, ugali, wali, sukari nk

Vyakula vya wanga vinapandisha sukari yako kuliko vyakula vingine vyovyote.

Kiasi gani na ni vyakula aina gani hasa hivyo vyenye wanga unavyokula vinaweza kuathiri jinsi gani unadhibiti kisukari chako.

Kujua ni kiasi gani cha wanga unakula ni namna nzuri ya kudhibiti kisukari.

Unaweza kushirikiana na daktari wako au na mtaalamu yoyote wa lishe kufanya hesabu kujua ni kiasi gani cha wanga mwili wako unahitaji kila siku.

MBADALA WA SUKARI

Baadhi ya watu hudhani kuwa sukari husababisha kisukari na hivyo mtu mwenye kisukari eti asitumie kabisa sukari.

Lakini kisukari aina ya kwanza husababishwa na sababu za kijenetiki na mambo mengine yasiyohusu sukari moja kwa moja.

Hata hivyo vyakula vingi vitamu vina wanga mwingi ambao unaweza kuathiri sukari katika damu yako.

Ukiambiwa chakula au kinywaji hakina sukari ndani yake hasa hivyo vya kwenye makopo haina mana kwamba havina wanga au nishati .

Soma vizuri maelezo kwenye vifungashio ya kila unachonunua na kula au kunywa ili ujuwe ni wanga kiasi gani unatumia kila siku.

Pamoja na hayo bado nashauri upendelee kutumia vyakula au vinywaji vyenye nishati kidogo na visiwe vimeongezwa sukari ya kutengenezwa (artificial sweeteners).

VYAKULA VIZURI ZAIDI KWA MWENYE KISUKARI AINA YA KWANZA

Vyakula vifuatavyo vina wanga mchache na vina viinilishe mhimu kama kalsiamu, potasiamu, nyuzinyuzi, magnesiamu na vitamini zingine mhimu. Navyo ni pamoja na:

  1. Maharage
  2. Mboga za majani zenye rangi ya kijani
  3. Matunda jamii ya machungwa
  4. Viazi vitamu
  5. Nyanya
  6. Samaki
  7. Vyakula ambavyo havijakobolewa
  8. Mbegu za maboga
  9. Mtindi usio na mafuta ndani yake

1o. Maziwa yasiyo na mafuta ndani yake

Kama unatafuta dawa ya asili kwa ajili ya kutibu kisukari niachie tu ujumbe WhatsApp +255714800175

Je Umeipenda makala hii?

Share post hii kwa ajili ya wengine

Fadhili Paulo
Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
Imesomwa mara 18

Let's block ads! (Why?)

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...