Translate

Ijumaa, 30 Novemba 2018

Majina ya Maswaha wanawake

                                  Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh


YAFUATAYO NI MAJINA YA MASWAHABA WANAWAKE (RADHI ZA ALLAAH ZIWE JUU YAO)


  • Aisha
  • Khawlah bint al-Azwar
  • Al-Nahdiah
  • Zunairah al-Rumiya
  • Al-Shifa' bint Abdullah
  • Arwa bint al-Harith
  • Asmā' bint Abi Bakr
  • Atiqa bint Zay
  • Fakhitah bint Abi Talib
  • Fatima bint Al-Aswad
  • Fatimah bint Asad
  • Fatimah
  • Habibah binte Ubayd-Allah
  • Umm Hakim

  • Halah bint Wuhayb
  • Halimah bint Abi Dhuayb
  • Hammanah bint Jahsh
  • Hind bint Awf
  • Hind bint Utbah
  • Hind the wife of Amr
  • Safiyya bint Huyayy
  • Jamila bint Thabit
  • Al-Khansa
  • Khawla bint Tha'labah
  • Layla bint al-Minhal
  • Lubaba bint al-Harith
  • Lubaynah
  • Khawlah bint Hakim


  • Maria al-Qibtiyya
  • Najiyah bint al-Walid
  • Nusaybah bint Ka'ab
  • Safiyyah bint Abd al-Muttalib
  • Salma bint Umays
  • Salma Umm-ul-Khair
  • Sirin bint Shamun
  • Sahla bint Suhail
  • Sumayyah bint Khabbat
  • Safiyyah bint Abd al-Muttalib
  • Salma bint Umays
  • Salma Umm-ul-Khair
  • Sirin bint Shamun
  • Sahla bint Suhail
  • Sumayyah bint Khabbat
  • Umama bint Hamza
  • Umamah bint Zainab
  • Asma bint Umais
  • Umm al-Darda
  • Umm Ayman
  • Umm Haram
  • Umm Kulthum bint Abi Bakr
  • Umm Kulthum bint Ali
  • Umm Kulthum bint Muhammad
  • Umm Kulthum bint Uqba
  • Umm Ma'bad
  • Umm Ruman
  • Umm Shareek
  • Umm Sulaym bint Milhan
  • Umm Ubays
  • Umm ul-Banin
  • Umm Waraqa
  • Zainab bint Muhammad
  • Zaynab bint Ali
  • Maymunah bint al-Harith
  • Qutayla ukht al-Nadr
  • Qutaylah bint Abd-al-Uzza
     
  •  Jumanah bint Abi Talib
          Rayta bint Abi Talib
  • Thuwaybah
  • Rufaida Al-Aslamia
  • Ruqayyah bint Muhammad

  • Jumanah bint Abi Talib
  • Rayta bint Abi Talib
  • Thuwaybah


  •                                                                    Na  Allaah  anajua Zaidi


from fisabilillaah.com https://ift.tt/2P9trgx
via IFTTT

Maswali na Majibu kuhusu Qur'an

Surat An-Nuwr Ndiyo Surah katika Qur'an iliyoanzishwa kwa neno la Surah yenyewe.


Abu Bakar Swidiq (Radhwiya Allahu Anhu) ndiye Swahaba aliyeamrisha Qur'an ikusanywe na kuwekwa kwa Maandishi katika Mswahafu.

 Surat An-Naswr Ndiyo Surah ya Mwisho Kuteremshwa.


Surat Asw-Swaff  ndio Surah pekee iliyotaja Jina la Ahmad kumkusudia Mtume Muhammad( Swallaah Allaahu Aleyhi wa Sallaam).


Swali   Je,Jina la Mtume Muhammad( Swallaah Allaahu Aleyhi wa Sallaam) limetajwa mara ngapi katika Qur'an likiwepo pia jina la Surah...?

Jibu  Limetajwa Mara 4 , (Surat Aal-Imraan , Surat Al-Ahzaab, Surat Muhammad na Surat Al-Fat-h )


Swali  Swahaba gani aliamrishwa Qur'an iandikwe kwa lahja moja ya Kiquraysh...?

Jibu  Uthman Bin Affaan (Radhwiya Allahu Anhu).


Swali  Je,Qur'an iliteremshwa kwa Herufi (Lahaja) ngapi za Ki Quraysh ...?

Jibu Herufi 7

Swali Qur'an iliteremshwa kwa miaka mingapi kwa Mtume Muhammad( Swallaah Allaahu Aleyhi wa Sallaam)..?

Jibu Miaka 23


Swali Kuna Maeneo mangapi ya Sajdah ya Kisomo katika Qur'an ....?

Jibu Maeneo 15


Surat Al-Baqarah Ndiyo Surah Ndefu kuliko Zote katika Qur'an.


Katika Qur'an Kuna jumla ya Ayah 6236 na Katika Qur'an Kuna Surah 114 na Qur'an ina jumla ya Juzuu 30.


Surah zilizoteremshwa MAKKAH ndio zilizo nyingi Kuliko Surah zilizoteremshwa MADIYNAH.


Surat Al-Kawthar Ndio Surah Fupi kuliko Surah zote ndani ya Qur'an Tukufu.


Swali Nini Maana ya Qur'an...?

Jibu KINACHOSOMWA



Surat At-Tawbah Ndiyo Surah Pekee ndani ya Qur'an isiyoanza na BISMILLAAH.


Aayah Tano za Mwanzo Surat 'Alaq ndio Ayah za Mwanzo kuteremshwa kwa Mtume Muhammad( Swallaah Allaahu Aleyhi wa Sallaam)


Swali Mara ngapi Bismillaah imerudia katika Qur'an..?

Jibu Mara 114


Swali Surah ipi ambayo Allaah Ameiapia kuhusu Wakati ,ambayo Imaam Shaaffiiy amesema: "Kama isingeteremshwa Surah nyingine ila hii ingeliwatoshelewa watu.."?

Jibu Surat Al-Aswr


Surat An-Naml Ndiyo SURAH ambayo BismilLaah imejirudia mara mbili


Surat Al-Kahf   Ndiyo SURAH ambayo inakiwa Kusomwa katika Siku ya Ijumaa.


Ayaah Ndefu kuliko Zote zinajulikana kwa jina la Ayyaatul-Mudayyanah au Ayyaatud-Dayn



Mwezi wa Ramadhwaan Ndiyo Mwezi pekee katika Miezi 12 ya Kiislamu uliotajwa katika Qur'an


Surat Al-Hadiyd Ndiyo Surah Pekee iliyokusanya Majina na Sifa za Allaah( Subhaana wa Taala) zipatazo 27.


Surat Al-Ikhlaasw Ndiyo Surah Pekee ambayo Ukiisoma utapata Thawabu (1/3) ya Qur'an.


Surat Al-Faatiha ndiyo surah inayojulikana kama "Mama wa Qur'an"


Shirk Ndiyo Dhambi kubwa iliyotajwa kuwa haitosehemewa katika Qur'an ikiwa Mtu hatotubia(Hatofanya Tawbah)

Al-Qiyaamah Ndiyo Surah ambayo ALLAAH ameitaja kuwa WAUMINI watamuona Allaah Al-Jaannah (Peponi).


Surat Al-Hujuraat na Surat Al-Humazah Ndiyo Surah ambazo zinazomkemea Msengenyaji.


Surat Al-Baqarah Aya 281 Ndiyo Ayah ya Mwisho Kuteremshwa katika Qur'an.

Malaika wa Msimamizi wa Moto ametajwa katika Qur'an kwa jina la Maalik


Swali Malaika wangapi wametajwa katika Qur'an kuwa wataibeba 'Arsh ya Allaah(Subhaana wa Taala) na wametjwa katika Surah gani..?

Jibu Malaika 8 wametajwa katika Surat Al-Haaqah.


Kuna Jumla ya Surah 37 katika Juzuu 30.



NA  ALLAAH  ANAJUA  ZAIDI

from fisabilillaah.com https://ift.tt/2QvJOZD
via IFTTT

MENDE: wadudu wastahamilivu, waishio kwenye hali zote za hewa

Naam ndugu yangu msomaji wa safu hii ya ‘Fahamu Usiyoyajua’ juma hili nataka tukajifunze kuhusu mdudu aina ya mende.

Kwa wale wasiomfahamu, mende hawa ni wadudu wenye miguu sita, upande wa kushoto miguu mitatu, na upande wa kulia miguu mitatu.

Mende wana taya za kutafunia, miili iliyokuwa bapa, na kichwa kidogo. Wengi wao wana rangi nyekundu, kahawia mpaka nyeusi. Macho ya mende ni kama macho ya inzi, yaani ana jicho ndani ya jicho. Maana yake ni kuwa, ndani ya jicho lake moja kuna macho madogo madogo mengi.

Pia, mende wana antena mbili na mwili wao umegawanyika katika vipande vitatu yaani sehemu ya kichwa, kifua (kati kati) na sehemu ya nyuma. Kadhalika, katika kila kipande kuna jozi za miguu.

Mende ni kundi la wadudu linalofahamika kwa Jina la ‘blattodea,’ kundi ambalo pia wapo mchwa. Wataalaamu wa elimu ya viumbe wanasema kuwa, kuna aina 4,600 za mende lakini wanaopatikana katika mazingira binadamu ni aina 30. Aina nne kati ya hao 30 ni mende waharibifu. Katika bara la Amerika Kaskazini kuna aina 50 na kule Australia kuna aina 450.

Aina nyingi za mende wanapatikana sehemu za joto. Kwa ujumla, aina nyingi za mende wanapenda kuishi kijamii. Hakika, viumbe hawa, mende, wameonekana katika mazingira wanayopatikana binadamu kwa karne nyingi. Watu wengi wanawatazama mende kama wadudu wachafu lakini si kuwa wanakula uchafu kila wakati.

Ukubwa wao wengi ni kama kucha ya dole gumba ila kuna aina moja ya mende inapatikana Australia inaitwa ‘giant burrowing cockroach’ ana urefu wa sentimita tisa.

Chakula

Katika chakula, mende ni ‘omnivuorous’ wanakula kila kitu ikiwemo matunda, nafaka, karatasi, ngozi, nywele, mimea iliyokufa, mbao zilizooza, mkate nk. Inatajwa katika matumbo yao kuna bacteria fulani ambao husaidia kusaga vyakula.

Uzazi

Katika uzazi, mende wanataga kati ya mayai 300-400 kulingana na aina. Mende huchukua masaa matano kwa kutaga. Kadhalika kuna hatua anapitia mende kabla ya kuwa mende kamili kama vile yai, nyimphi kisha mende kamili.

Kutoka kuwa yai hadi mende, inachukua miezi mitatu hadi minne. Muonekano wa mayai yao ni kama gundi fulani, yananata na madogo.

Mambo 10 usiyoyajua kuhusu mende

  • Mende ni wadudu wavumilivu sana wanaoweza kuishi kwenye hali zote; kwenye joto sana na hata baridi sana, yaani hata kule ncha ya Kaskazini kwenye theluji pia wanapatikana.
  • Allah Aliyetukuka amejaalia katika miili ya mende kuwa wana uwezo wa kutengeneza kitu fulani kinaitwa ‘anti freeze’ ambayo inawakinga wasigande hata kwenye baridi kali.
  • Mende huwa wanatambuana baina ya kundi moja na jingine kwa harufu zao,  yaani mende wa kundi fulani anaweza akatambua hili si kundi lake kwa harufu.
  • Kila kundi la mende lina harufu yake.
  • Maisha ya mende wengi ni usiku.
  • Mwanga ukiwaelekea, mende huwa wanakimbia, ingawa kuna aina moja ya mende inapatikana Asia, yeye anapenda mwanga.
  • Mende wanapokutana (kujamiiana) kipekee sana. Huwa mmoja anaangalia huku mwingine kule, yaani hawatazamani.
  • Jike la mende huwa ndio hasa linavutiwa na dume baada ya dume kufanya mchezo fulani wa madaha.
  • Dume hufanya hivyo baada ya kupata harufu ya jike ya anapojiona kuwa yupo tayari.
  • Ipo aina moja ya mende jike huwa linajamiiana mara moja tu katika maisha yake yote.



from TIF https://ift.tt/2Rm7pt6
via IFTTT

Kufuga Ndevu


Kuachilia ndevu ni wajibu kwa wanaume kwa dalili zifuatazo:


1- Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameamuru kuziachilia. Amri hii ni ya lazima, kwani hakuna kiashirio chochote kinachoigeuza na kuipeleka katika usunnah. Na kati ya amri hizo ni neno lake Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 خالفوا المشركين: وفروا اللحى، وأحفوا الشوارب
((Kuweni kinyume na washirikina; fugeni ndevu kwa wingi na punguzeni masharubu)) [Hadiyth Sahihi: Imetolewa na Al-Bukhaariy (5892) na Muslim (259)]


Na neno lake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 جزوا الشوارب، وأرخوا اللحى، خالفوا المجوس
((Kateni masharubu na ziachilieni ndevu; nendeni kinyume na wanaoabudu moto)) [Hadiyth Sahihi: Imetolewa na Muslim (260)]


2- Ni kwamba kuzinyoa ni sawa na kujifananisha na makafiri kama inavyoonekana katika Hadiyth mbili zilizotangulia.


3- Ni kwamba kuzinyoa ni sawa na kuubadilisha Uumbaji wa Mwenyezi Mungu na kumtii Shaytwaan asemaye:

وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللَّـهِ ۚ  
…na nitawaamrisha watabadili maumbile ya Allaah.”  [An-Nisaa: 119]

4- Ni kwamba kuzinyoa ni sawa na kujifananisha na wanawake. Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amewalaani wanaume wanaojifananisha na wanawake [Hadiyth Sahihi: Imetolewa na Al-Bukhaariy (5885) na At-Tirmidhiy (2935)]


Na kwa ajili hiyo, Shaykh wa Uislamu amesema:
“Na inaharamishwa kunyoa ndevu zake” [Kitabu cha “Al-Ikhtiyaaraat Al-Fiqhiyyah” cha ‘Alaau Ddiyn Al-Ba’aly (uk.10). Angalia pia kitabu cha“Al-Furu’u” cha Ibn Muflih (1/291).]

Ibn Hazm na wengineo, wamenukulu Ijmaa’ ya Maulamaa juu ya uharamu wa kunyoa ndevu.


Je, Inajuzu Kupunguza Ndevu Zilizozidi Mshiko Wa Kiganja?

Baadhi ya Maulamaa wamefuata mwelekeo wa kujuzu kuondosha ndevu zilizozidi mkamato wa kiganja. Wao wameshikilia Hadiyth ya Ibn ‘Umar ambaye wakati wa kuhiji au kufanya ‘Umrah, alikuwa akizikamata ndevu zake, kilichozidi alikuwa akikiondosha.

Wamesema: “Yeye ndiye mpokezi wa Hadiyth yenye kuamuru kuachilia ndevu kwa wingi, hivyo basi yeye ndiye ajuaye zaidi upokezi wake!

Katika kaulipokezi hii, wao hawana hoja yoyote kwa dalili zifuatazo:

1- Kwamba Ibn ‘Umar Allah Amridhie, alikuwa akifanya hivyo wakati anapojifungua na ihraam ya Hija au ‘Umrah, wakati wao (Maulamaa hao) wanalijuzisha hilo nyakati zote.


2- Kwamba kitendo hiki cha Ibn ‘Umar kimefahamika kutokana na yeye kuliawilisha neno Lake Subhaanah:
   مُحَلِّقِينَ رُءُوسَكُمْ وَمُقَصِّرِينَ

… wenye kunyoa vichwa vyenu na wenye kupunguza, [Al-Fat-h: 27]

Katika ‘amali za Hijjah, kichwa hunyolewa na ndevu hupunguzwa.

3- Ni kwamba Swahaba akisema au kutenda kinyume na alivyohadithia, basi kinachozingatiwa ni maneno yake na wala si ufahamu wake wala kitendo chake. Kwani mazingatio ni kile kilichorufaishwa moja kwa moja kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).

Na kutokana na yaliyotangulia, lililo sawa ni wajibu wa kuachia ndevu na kutozikata kwa kuutumia ujumuishi wa amri zilizokuja katika Hadiyth sahihi kama vile: (( Fugeni kwa wingi…, ziachilieni…, zifanyeni nyingi….)) kama walivyoeleka kwa hilo jamhuri ya Maulamaa. 



Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.



from fisabilillaah.com https://ift.tt/2DT1WWB
via IFTTT

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...