Translate
Ijumaa, 27 Septemba 2019
Utulivu Wa Nafsi (Sakiynatun-Nafs) - 1
Alhamisi, 26 Septemba 2019
33-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Ana Ujira Usiokatika Anasifika Na Maarufu Mno
Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)
33-Ana Ujira Usiokatika Anasifika Na Maarufu Mno
Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):
وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ ﴿٣﴾
Na hakika wewe bila shaka una ujira usiokatika. [Al-Qalam: 3]
Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):
وَرَفَعْنَا لَكَ ذِكْرَكَ ﴿٤﴾
Na Tukanyanyulia juu utajo wako (ukawa mwenye kusifika mno)? [Ash-Sharh: 4]
Allaah (سبحانه وتعالى) Amemfadhilisha na kumkirimu Nabiy Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa kutajwa mno na kusifiwa na akawa maarufu ulimwenguni. Hutajwa katika kila Adhaana ya Swalaah, katika Iqaamah, katika khutbah za Ijumaa, katika kutamka Shahaadah, na hutajwa ndani ya Swalaah na kila zinapotajwa Hadiyth zake, na anaswaliwa katika kuomba du’aa ambapo du’aa haitaqabaliwi bila ya kumswalia yeye kwanza, na huswaliwa pia inapomalizika du’aa, na katika hali nyingi mbali mbali, na Hadiyth zifuatazo zinathibitisha:
عن ابي سعيد الخدري رضي الله عنه ان رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: أتاني جبريلُ فقال: إنَّ ربِّي وربَّك يقولُ لك: كيف رفَعْتُ ذِكْرَك ؟ قال: اللهُ أعلَمُ قال: إذا ذُكِرْتُ ذُكِرْتَ معي
Imepokelewa kutoka kwa Sa’idy Al-Khudriyy (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Amenijia Jibriyl akasema: Hakika Rabb wangu na Rabb Wako Anasema: Vipi umenyanyuliwa juu utajo wako? Akasema: Allaah Anajua zaidi. Akasema: (Allaah Anasema): Kila nnapotajwa, nawe unatajwa pamoja nami.” [Ibn Jariyr, Ibn Abiy Haatim, Ibn Hibbaan na Ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Ibn Hibbaan 3382]
Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amesema ) (kuhusu maana ya): “Sitajwi isipokuwa unatajwa pamoja Nami”; katika Adhaan, Iqaamah, Tashahhud, Siku ya Ijumaa, kwenye Minbari (khutbah), Siku ya ’Iydul-Fitwr, Siku ya ’Iydul- Adhw-haa, Ayyaamut-Tashriyq, Siku ya ’Arafah, katika Jamarah, katika Swafaa Wal Marwah, katika Khutbah za Nikaah, Mashariki ya ardhi na Magharibi, na kwamba lau mtu akamwabudu Allaah akaamini Jannah na Moto na kila kitu lakini hashuhudii kwamba Muhammad ni Rasuli wa Allaah, basi hakuna kitakachomfaa na atakuwa ni kafiri. [Tafsiyr Al-Qurtwubiy]
Naye Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:
((الْبَخِيلُ مَنْ ذُكِرْتُ عِنْدَهُ فَلَمْ يُصَلِّ عَلَيَّ))
((Bakhili ni yule ambaye nikitajwa haniswalii)) [Hadiyth ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (رضي الله عنه) - At-Tirmidhiy (5/551) [3546], na wengineo na angalia: Swahiyh Al-Jaami’ (3/25) [2787] na Swahiyh At-Tirmidhiy (3/177)]
33-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Unyenyekevu Wake Akinyenyekea Kwa Ahli Zake
Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)
33-Unyenyekevu Wake Akinyenyekea Kwa Ahli Zake
عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ، عَنِ النَّبِيِّ ـ صلى الله عليه وسلم ـ قَالَ " خَيْرُكُمْ خَيْرُكُمْ لأَهْلِهِ وَأَنَا خَيْرُكُمْ لأَهْلِي " رواه الترمذي
Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mbora wenu ni yule aliye mbora kwa mke wake, na mimi ni mbora kwa watu wangu wa nyumbani [ahli])) [Ibn Maajah na Ad-Daarimiy].
103-Aayah Na Mafunzo: Allaah Anaridhia Mshikamane Kwa Kamba Yake Msifarikiane
Aayah Na Mafunzo
Aal-‘Imraan
Allaah Anaridhia Mshikamane Kwa Kamba Yake Msifarikiane
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):
وَاعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللَّـهِ جَمِيعًا وَلَا تَفَرَّقُوا ۚ وَاذْكُرُوا نِعْمَتَ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ إِذْ كُنتُمْ أَعْدَاءً فَأَلَّفَ بَيْنَ قُلُوبِكُمْ فَأَصْبَحْتُم بِنِعْمَتِهِ إِخْوَانًا وَكُنتُمْ عَلَىٰ شَفَا حُفْرَةٍ مِّنَ النَّارِ فَأَنقَذَكُم مِّنْهَا ۗ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَهْتَدُونَ ﴿١٠٣﴾
103. Na shikamaneni kwa kamba ya Allaah nyote pamoja, wala msifarikiane. Na kumbukeni neema ya Allaah juu yenu, pale mlipokuwa maadui (kati yenu); kisha Akaunganisha nyoyo zenu, mkawa kwa neema Yake ndugu; na mlikuwa ukingoni mwa shimo la moto Akakuokoeni humo. Hivyo ndivyo Allaah Anavyokubainishieni Aayaat Zake mpate kuongoka.
Mafunzo:
Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hakika Allaah Anawaridhia mambo matatu na Anachukia kwenu mambo matatu; Anawaridhia mumwabudu Yeye, wala msimshirikishe kwa chochote, na mshikamane nyote na kamba ya Allaah wala msifarikiane. Na anachukia kwenu uvumi, kuuliza sana na kupoteza mali.” [Muslim, na katika riwayaah: “Na muwanasihi wenye kuwatawalia mambo yenu.” Swahiyh Adaab Al-Mufrad (343)].
049-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Hujuraat: 9
أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com
049-Al-Hujuraat Aayah 9
Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):
وَإِن طَائِفَتَانِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ اقْتَتَلُوا فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا ۖ فَإِن بَغَتْ إِحْدَاهُمَا عَلَى الْأُخْرَىٰ فَقَاتِلُوا الَّتِي تَبْغِي حَتَّىٰ تَفِيءَ إِلَىٰ أَمْرِ اللَّـهِ ۚ فَإِن فَاءَتْ فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا بِالْعَدْلِ وَأَقْسِطُوا ۖ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ﴿٩﴾
Na ikiwa makundi mawili ya Waumini yakipigana, basi suluhisheni baina yao. Lakini mojawapo likikandamiza jengine, basi piganeni na ambalo linakandamiza mpaka lielemee kwenye amri ya Allaah. Likishaelemea, basi suluhisheni baina yao kwa uadilifu, na timizeni haki. Hakika Allaah Anapenda wanaotimiza haki.
إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ﴿١٠﴾
Hakika Waumini ni ndugu, basi suluhisheni baina ya ndugu zenu. Na mcheni Allaah ili mpate kurehemewa. [Al-Hujuraat: 9-10]
Sababun-Nuzuwl:
عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ قَالَ قِيلَ لِلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم لَوْ أَتَيْتَ عَبْدَ اللَّهِ بْنَ أُبَىٍّ قَالَ فَانْطَلَقَ إِلَيْهِ وَرَكِبَ حِمَارًا وَانْطَلَقَ الْمُسْلِمُونَ وَهِيَ أَرْضٌ سَبِخَةٌ فَلَمَّا أَتَاهُ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم قَالَ إِلَيْكَ عَنِّي فَوَاللَّهِ لَقَدْ آذَانِي نَتْنُ حِمَارِكَ . قَالَ فَقَالَ رَجُلٌ مِنَ الأَنْصَارِ وَاللَّهِ لَحِمَارُ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَطْيَبُ رِيحًا مِنْكَ - قَالَ - فَغَضِبَ لِعَبْدِ اللَّهِ رَجُلٌ مِنْ قَوْمِهِ - قَالَ - فَغَضِبَ لِكُلِّ وَاحِدٍ مِنْهُمَا أَصْحَابُهُ - قَالَ - فَكَانَ بَيْنَهُمْ ضَرْبٌ بِالْجَرِيدِ وَبِالأَيْدِي وَبِالنِّعَالِ - قَالَ - فَبَلَغَنَا أَنَّهَا نَزَلَتْ فِيهِمْ ((وَإِنْ طَائِفَتَانِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ اقْتَتَلُوا فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا))
Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maalik (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliambiwa: Unaonaje umwendee ‘Abdullaah bin Ubayy (umlinganie Uislamu). Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwendea akiwa amepanda punda, na (kundi la) Waislamu walienda (naye) wakitembea katika ardhi kavu iliyo na chumvi. Pindi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipomfikia, (‘Abdullaah bin Ubayy) alisema: “Jiepushe mbali nami! Naapa kwa Allaah harufu mbaya ya punda wako imenikera.” Mtu mmoja katika Answaariy akasema (kumwambia ‘Abdullaah bin ‘Ubayy): “Naapa kwa Allaah punda wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ana harufu nzuri zaidi kulikoni yako!” Hapo mtu mmoja katika kabila ya ‘Abdullaah akaghadhibika kwa ajili ya aliyoaambiwa ‘Abdullaah, kisha hao watu wawili wakawa wanashutumiana ikasababisha maswahibu wa hao wawili kughadhibika. Makundi mawili ya watu hao yakaanza kupigana kwa vitawi, viatu na makofi. Tukajulishwa kwamba imeteremshwa:
وَإِن طَائِفَتَانِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ اقْتَتَلُوا فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا ۖ
Na ikiwa makundi mawili ya Waumini yakipigana, basi suluhisheni baina yao….
033-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kutaja Jina La Allaah Katika Chakula Na Kula Kilichoko Mbele Yako
Lu-ulu-un-Manthuwrun
(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)
Hadiyth Ya 33
Kutaja Jina La Allaah Katika Chakula Na Kula Kilichoko Mbele Yako
عَنْ عُمَرَ بْن أَبِي سَلَمَةَ عَبْدُ الله رَبيب رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَال: كُنْتُ غُلاَمًا فِي حَجْرِ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ وَكَانَتْ يَدِي تَطِيشُ فِي الصَّحْفَةِ فَقَالَ لِي رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((يَا غُلاَمُ سَمِّ اللَّهَ تَعَالى، وَكُلْ بِيَمِينِكَ، وَكُلْ مِمَّا يَلِيكَ)) فَمَا زَالَتْ تِلْكَ طِعْمَتِي بَعْدُ. متفق عليه
Imepokelewa kutoka kwa ‘Umar bin Abi Salamah, ambaye ni mwanakambo wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: Nilikuwa kijana mdogo chini ya ulezi wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), na mkono wangu ulikuwa ukizungukazunguka katika sinia (ya chakula). Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akaniambia: ((Ee ghulamu! Taja jina la Allaah (Ta’aalaa) na kula kwa mkono wako wa kulia, na ule kilicho mbele yako)). Basi huo ukawa ndio mtindo wangu wa kula baadaye. [Al-Bukhaariy, Muslim]
Mafunzo na Mwongozo:
1. Kuwajibika kuwafunza watoto kila aina mojawapo wa tabia njema za Kiislamu na kuwatanabahisha makosa yao wanapoanza kuyatenda.
2. Miongoni mwa adabu za kuanza jambo lolote, kama kula chakula ni kuanza kwa ‘BismiLlaah’ (Naanza kwa Jina la Allaah), na kula kwa mkono wa kulia, na kula kilicho mbele ya sahani.
3. Ruhusa ya kula pamoja au pekee. Lakini Hadiyth inaashiria kula katika sahani moja ni bora zaidi, na bila shaka inaleta baraka katika chakula. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):
لَّيْسَ عَلَى الْأَعْمَىٰ حَرَجٌ وَلَا عَلَى الْأَعْرَجِ حَرَجٌ وَلَا عَلَى الْمَرِيضِ حَرَجٌ وَلَا عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ أَن تَأْكُلُوا مِن بُيُوتِكُمْ أَوْ بُيُوتِ آبَائِكُمْ أَوْ بُيُوتِ أُمَّهَاتِكُمْ أَوْ بُيُوتِ إِخْوَانِكُمْ أَوْ بُيُوتِ أَخَوَاتِكُمْ أَوْ بُيُوتِ أَعْمَامِكُمْ أَوْ بُيُوتِ عَمَّاتِكُمْ أَوْ بُيُوتِ أَخْوَالِكُمْ أَوْ بُيُوتِ خَالَاتِكُمْ أَوْ مَا مَلَكْتُم مَّفَاتِحَهُ أَوْ صَدِيقِكُمْ ۚ لَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَأْكُلُوا جَمِيعًا أَوْ أَشْتَاتًا ۚ فَإِذَا دَخَلْتُم بُيُوتًا فَسَلِّمُوا عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ تَحِيَّةً مِّنْ عِندِ اللَّـهِ مُبَارَكَةً طَيِّبَةً ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمُ الْآيَاتِ لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ ﴿٦١﴾
Si vibaya kwa kipofu, na wala si vibaya kwa kilema, na wala si vibaya kwa mgonjwa, na wala nyinyi wenyewe kama mtakula majumbani mwenu, au majumbani mwa baba zenu, au majumbani mwa mama zenu, au majumbani mwa kaka zenu, au majumbani mwa dada zenu, au majumbani mwa ‘ammi zenu, au majumbani mwa shangazi zenu, au majumbani za wajomba wenu, au majumbani mwa makhalati zenu au za mliowashikia funguo zao, au rafiki yenu. Hakuna ubaya kama mkila pamoja au mbali mbali. Mtakapoingia majumbani toleaneni salaam; maamkizi kutoka kwa Allaah, yenye Baraka, mazuri. Hivyo ndivyo Anavyokubainishieni Allaah Aayaat ili mpate kutia akilini. [An-Nuwr (24: 61)]
4. Hima ya Maswahaba kufuata Sunnah, maamrisho na muongozo wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) tokea udogoni mwao.
5. Umuhimu wa kumfunza mtoto angali mdogo.
6. Kurekebisha kosa pale pale linapotokea kwa wakati wake munaasib na kwa upole.
7. Kutumia utaratibu na mfumo mzuri wa kumrekebisha mtu bila ya yeye kujihisi vibaya au kumfedhehesha. Hapa tunaona kuwa tatizo la mtoto lilikuwa ni mkono kuzungukazunguka katika sahani, lakini hilo lilitajwa mwisho na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم).
8. Kuwa makini katika kurekebisha jambo na kujali hisia za mtu japo za mtoto mdogo.
9. Maswahaba walikuwa makini katika kuyafikisha waliyopewa, kufundishwa na kunasihiwa na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), kwani walifahamu kuwa hayo hayakuwa yao pekee yao bali ni kwa Ummah wote.
10. Hadiyth inatupatia fundisho kujuzu kwa mwanamme kuwalea watoto wa mke wake aliyezaa na mume mwengine.
11. Mwanamme anayelea watoto wa kambo anatakiwa awalee kwa njia nzuri kama watoto wake wa uhusiano wa damu.
Jumatano, 25 Septemba 2019
Kila Nafsi Itaonja Mauti Na Hakuna Atakayebakia Isipokuwa Allaah سبحانه وتعالى
20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah
إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! 20 - Isti’aadhah (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah ...
-
إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! 20 - Isti’aadhah (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah ...
-
Dalili 18 zinazoashiria una ujauzito wa mtoto wa kiume Awali ya yote nitoe pongezi kwa mama K na Baba K wote popote walipo kwa kazi nzuri ...

