Translate

Jumapili, 30 Desemba 2018

Kuelekea Qibla wakati wa Kuchinja

Swali


Je, ni lazima kuelekea Qiblah wakati wa kuchinja...?


Jibu


 Kuelekea Qiblah wakati wa kuchinja sio wajibu

Mtu anaweza kuchinja kichinjwa chake ijapokuwa hakuelekea Qiblah. Lakini wanachuoni (Rahimahumu Allaah) wamesema kuwa bora zaidi ni mtu aelekee Qiblah. Kwa sababu ni ´ibaadah. 

Lakini hata hivyo hawakusema kuwa ni sharti. Iwapo mtu atachinja kwa kuelekea upande usiokuwa Qiblah ni halali. Sio jambo limechukizwa. Hapana neno. 

Tofauti na wanavosema watu wasiokuwa na elimu. Baadhi yao wanasema kwamba ni lazima kuelekea Qiblah, jambo ambalo si sahihi.


Rejea : Al-Liqaa' ash-Shahriy (42)

from fisabilillaah.com http://bit.ly/2SvU024
via IFTTT

Hukumu ya Kufunga Mikono katika Swalah

                               HUKUMU  YA  KUFUNGA  MIKONO  KATIKA  SWALAH



Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh


Kufunga mikono katika Swalaah ni Sunnah iliyothibiti kutoka kwa Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na ni jambo alilolisisitiza sana katika Swalaah na hata kuwasahihisha wale waliokuwa wakikosea kufunga mikono yao ndani ya Swalaah. 

Isitoshe ni Sunnah sahihi iliyothibiti hata kwa Manabii  waliotangulia kama anavyotujulisha mwenyewe Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  katika Hadiyth zifuatazo.  

Hakuna ushahidi wala dalili wala mapokezi sahihi yoyote yanayoonyesha kinyume na kufunga mikono kwenye Swalaah kutoka kwake yeye Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  wala Maswahaba zake.


Hadiyth za Kufunga Mikono

Ama Hadiyth zinazoeleza juu ya Kufunga mikono ni nyingi sana na zinapatikana katika kitabu Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam). cha Shaykh Al-Albaaniy (Allaah Amrehemu) kilichopo ndani ya ALHIDAAYA kwa lugha ya Kiswahili Na pia ndani ya kitabu cha 'Al-Qawl Al-Mubiyn fiy Akhtwaa Al-Muswalliyn) kilichoandikwa na Shaykh Mash-huwr Hasan Salmaan na pia ndani ya kitabu cha Fiqhus Sunnah cha Sayyid Saabiq na kwenye kitabu cha Swahiyhu Fiqhus Sunnah cha Abu Maalik Kamaal kilichopo ALHIDAAYA Swahiyh Fiqhus Sunnah na ndani ya vitabu vingi sana vya Fiqh na vya Hadiyth sahihi.


Anasema 'Bahari ya elimu' Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kuwa;
"Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema;
"Sisi Manabii tumeamrishwa kuharakisha kula futari zetu na kuchelewesha kula daku letu, na kuweka mikono yetu ya kulia juu ya kushoto ndani ya Swalaah." 
[At-Twabaraaniy na Ibn Hibbaan]


Na katika Sunan za Abu Daawuwd Hadiyth iliyosahihishwa na Ibn Khuzaymah inasema;

"Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto."

Imepokelewa pia kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipomuona mtu mmoja akiswali huku ameweka mkono wake wa kushoto juu ya mkono wa kulia, akauondoa na kuuweka wa kulia juu ya kushoto."[Ahmad na Abu Daawuud].

Na imepokelewa kutoka kwa Swahaba Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kuwa katika Swalaah ya maiti Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  alinyanyua mikono yake juu akasema “Allahu Akbar:”, kisha akauweka mkono wake wa kulia juu ya wa kushoto." [At-Tirmidhiy katika ‘Baab maa jaa fiy raf’il yadayni.]


Imepokelewa katika Swahiyh Muslim na kutoka kwa Imam Ahmad na At-Twabaraaniy kuwa:
"Na alikuwa akiuweka mkono wake wa kulia juu ya sehemu ya nyuma (mgongo) ya mkono wa kushoto."

Katika mlango huu zimepokelewa Hadiyth zaidi ya ishirini kutoka kwa Maswahaba kumi na nane pamoja na waliowafuatilia (Taabi’iyn), zote hizo zikitoka moja kwa moja  kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)

Kutoka kwa Swahaba Waail bin Hujr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kuwa amesema;
"Kama kwamba namtazama Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) namna alivyokuwa akiswali", akasema:
"Nikamtazama! akatoa takbiyr, kisha akanyanyua mikono yake mpaka ikakaribia masikio yake, kisha akauweka wa kulia juu ya upande wa nyuma wa mkono wa kushoto." 
[Ibn Khuzaymah katika Swahiyh yake na An-Nasaaiy na Abu Daawuwd katika Sunan yake na Ahmad katika Musnad yake 4/318 na Ibn Maajah katika Sunan yake 1/266 na Ad-Daarimiy katika Sunan yake 1/314 na Ibnul Jaruud katika Al-Muntaqaa Hadiyth nambari 208 na katika vitabu vingi vingine"].


Anasema Imaam Maalik (Allaah Amrehemu) katika kitabu cha Al-Muwattwaa, na huyu ni Imaam wa watu wa Madiynah mji alioishi na kuswali ndani yake Mtume wa Allaah zaidi ya miaka kumi, na Maswahaba wake watukufu (Radhwiya Allaahu ‘anhum) wakaendelea kuswali hapo miaka mingi iliyofuata.


Katika ukurasa wa 122 na 123 mlango wa "Mwenye kuswali aweke mkono mmoja juu ya mwengine",  imeandikwa katika kitabu hicho cha Imaam Maalik katika Hadiyth nambari 133 kama ifuatavyo:

"Katika maneno ya Manabii ni kuwa usipokuwa na haya basi fanya utakalo, na pia (katika maneno ya Mitume) ni kuweka mkono mmoja juu ya mwengine katika Swalaah."

Haya ni maneno ya Imaam Maalik ndani ya kitabu chake cha Al-Muwattwaa.
 
Na katika kitabu hicho hicho cha Al-Muwattwaa Imaam Maalik ameandika Hadiyth kutoka kwa Sahl bin Sa’ad Al Saa’idiy kuwa:
“Watu walikuwa wakiamrishwa kuweka mkono wao wa kulia juu ya mkono wa kushoto katika Swalaah."

Anasema Abu Haazim;
"Naelewa kuwa anakusudia hapa wakati wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)". [Al-Bukhaariy Juz. 1 ukurasa wa 397 Imaam Maalik katika Al-Muwattwaa na Imaam Ahmad katika Musnad.]

Na katika kuisherehesha Hadiyth hiyo amesema Imaam Maalik (Allaah Amrehemu);
"Kuweka (mkono) wa kulia juu ya kushoto na kuharakisha futari na kuchelewesha daku."
Haya ameyasema katika kuisherehesha Hadiyth iliyotangulia ya Abul Mukhariq.

Baadhi ya watu wakasema kuwa katika Hadiyth iliyomo ndani ya Al-Muwattwaa yumo Abul Mukhariq na huyu anajulikana kuwa ni dhaifu katika elimu ya Hadiyth, lakini inaeleweka pia katika elimu ya Hadiyth kuwa udhaifu wa wapokezi unakhitalifiana darja, na kwamba daraja inayokubalika Hadiyth zao katika madhaifu ni wale waliodhoofishwa kwa ajili ya udhaifu wao wa kuhifadhi ikiwa wao si watu waongo wala si wenye kupenda kuongeza maneno.

Madhaifu wa aina hii anasema Dr. Muhammad Ajjaaj Al-Khatwiyb katika kitabu chake cha 'Al-Mukhtasar Al-Wajiyz fiy Uluwm Al-Hadiyth kuwa;
"Mtu aliyedhoofishwa kwa ajili ya kuhifadhi kwake, au kwa ajili ya kutoweza kudhibiti maneno vizuri, ikiwa hatuhumiwa kwa ila nyingine, na ikiwa zitapokewa Hadiyth zake kwa njia nyingi, basi Hadiyth itapanda na kufikia darja ya Hadiyth 'Hasan', na kwa ajili hiyo udhaifu wake unatoweka kwa kupokelewa Hadiyth kwa njia nyingine."
Anasema Imaam Muhammad bin Al Hassan Al Shaybaniy kuwa;
"Anatuhumiwa Abul Mukhariq kwa udhaifu wake wa kuhifadhi tu."

Isitoshe ndani ya kitabu hicho cha Al-Muwattwaa ipo pia Hadiyth iliyosimuliwa na Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhuma) na kunukuliwa pia na Maimaam Ahmad na Al-Bukhaariy na wengineo, inayosema;
"Watu (wakati wa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)) walikuwa wakiamrishwa kuweka mikono yao ya kulia juu ya kushoto katika Swalaah."



Je, Imaam Maalik Alikuwa Akiaachia Mikono Na Alisema Watu Waachie Mikono Kwenye Swalaah?

Yaliyoandikwa ndani ya kitabu cha Bidaayatul Mujtahid si kukanusha kufunga mikono bali ni kuthibitisha, isipokuwa tu imenukuliwa ndani ya kitabu hicho kuwa Imaam Maalik amejuzisha kufunga katika Swalaah ya Sunnah na hakujuzisha katika Swalah ya fardhi akihofia watu wasiwe wanafunga kwa ajili ya kujipumzisha tu na wasidhani kuwa ni nguzo mojawapo ya Swalaah na kwamba Swalaah inabatilika iwapo mtu atafanya kinyume cha hivyo (hii ikiwa kweli imethibiti kuwa Imaam Maalik amesema hayo), lakini yaliyomo ndani ya kitabu chake cha Al-Muwattwaa ni kinyume na hayo yaliyoelezwa.

Na yanayofanywa na baadhi ya wafuasi wa Imaam Maalik wanaoachia mikono kwenye Swalah zao kama wafanyavyo baadhi ya watu wenye itikadi zisizo za Ahlus Sunnah wal Jama’ah, ni jambo ambalo halina dalili kwenye Sunnah ya Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  wala Maswahaba zake wala hata Imaam Maalik mwenyewe.

Hivyo, tumeona kuwa hapana Hadiyth Swahiyh hata moja kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inayosema watu waachie mikono katika Swalaah au kuonyesha kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akifanya kinyume na kufunga mikono kwenye Swalaah, na hii ni kauli ya wengi sana katika Maswahaba na Taabi’iyna (Radhwiya Allaahu ‘anhum) na haya ndiyo aliyonukuu Imaam Maalik katika Al-Muwattwaa.


Na  Allaah  anajua  zaidi


from fisabilillaah.com http://bit.ly/2Sofhe8
via IFTTT

Uharamu wa Mwaka Mpya

               MUISLAMU  USISHIRIKI  KATIKA  KUSHEHEREKEA  MWAKA  MPYA



Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh


Naam,Ndugu zangu katika Imaani, na leo tena nachukua fursa hii kuwahusia Nafsi zenu pamoja na kuihusia Nafsi yangu juu ya Kumcha  Allaah(Subhaana wa Taala) na Salamu zimfikie Kipenzi cha Ummah huu na Maswahaba zake, Amabad.


Ndugu zangu katika Imaani, Leo ni Tarehe 31/12/2018 katika Tarehe za Kikafiri na ni Ada zao katika Tarehe kama ya leo ikifika kuanzia jioni huwa wanajiandaa katika kuukaribisha Mwaka Mpya wao wa Kikafiri ambao umetengenezwa tu watu.

Kwahiyo Muislamu anatakiwa ajitenge na wala asishiriki nao katika sherehe hizi za Kikafiri maana wengi huwa wanakesha kwa kuukaribisha na kupiga mabaruti na wengine kucheza miziki nakadhalika.

Imepokelewa toka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy  (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 لَتَتَّبِعُنَّ سَنَنَ مَنْ قَبْلَكُمْ شِبْرًا بِشِبْرٍ وَذِرَاعًا بِذِرَاعٍ حَتَّى لَوْ سَلَكُوا جُحْرَ ضَبٍّ لَسَلَكْتُمُوهُ, قُلْنَا يَا رَسُولَ اللَّهِ, الْيَهُودَ وَالنَّصَارَى؟ قَال: فَمَنْ

“Mtafuata nyendo za watu waliokuwa kabla yenu, kiganja kwa kiganja, mkono kwa mkono, hata wakiingia kwenye shimo la kenge mtawafuata)).  Tukasema: “Ee Rasuli wa Allaah, Je, Unamaanisha Mayahudi na Manaswara?” Akasema: “Kwani nani zaidi ya wao?” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Tunakaribia kuingia mwaka mpya wa Kikristo (wa kalenda ya Papa Gregory ijulikanayo kama ‘Gregorian Calendar’), na kuna Waislamu wengi wanaosherehekea mwaka huo mpya kama wanavyofanya makafiri, jambo ambalo halimo katika mafundisho ya Kiislamu.

Imekuwa ni kawaida Waislamu kujiunga na wafanyakazi wenzao au marafiki zao au majirani zao na kusherehekea sherehe hizi potofu, na kuwa na tabia isiyoendana na mwendo na mafundisho ya dini yetu tukufu. Hivyo tumeona ni muhimu tuwatumie ujumbe huu ndugu zetu popote walipo wajiepushe na mambo haya ya uzushi ya kuiga makafiri.

Swali ni kwamba, Vipi Muislamu ajitengee siku kama hizo na kusherehekea?  

Jibu kutoka kwa Mwanachuoni wa Ummah, Shaykhul Islaam Ibn Taymiyyah kwamba: 

"Sisi Waislamu tusifanye jambo lolote lilokuwa si la kawaida katika siku hizi. Iwe kama siku yoyote nyingine katika maisha yetu bila ya kuwa imekhusishwa na lolote kama mfano wao watu wa Vitabu walivyokuwa hawasherehekei wala kuzifanya siku zetu za ‘Iyd kuwa ni khaswa (maalum) kwao."  

Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Ametuonyesha ubaya wa makafiri katika Aayah nyingi kama:

إِنَّ الْكَافِرِينَ كَانُواْ لَكُمْ عَدُوًّا مُّبِينًا
Hakika makafiri ni maadui zenu walio wazi wazi.” [An-Nisaa: 101]


Vile vile Amewaita kuwa ni jamaa wa mashaytwaan na vikosi vyao.

Kuungana na Ahlul-Kitaab katika sherehe zao imekatazwa kama ilivyokatazwa kuungana na washirikina vile vile. Asibishe mtu kusema kuwa imemaanishwa ni washirikina peke yao na kwamba watu wa Vitabu wana mielekeo au mila kama ya Waislamu takriban.

Shaykhul Islaam Ibn Taymiyyah ametoa dalili za kuharamishwa kusherehekea Krismasi, sherehe za wafursi kama Neyrouz, Sherehe za Mayahudi na nyinginezo (kama hizi za mwaka mpya) kwa kusema kwamba zote zinakuja katika hukumu hiyo hiyo moja.

Muislamu anapaswa kukataa mwaliko huo wa kusherehekea mwaka mpya hata kama mwaliko huo umetoka kwa Muislamu mwenzake. 

Vile vile kaelezea Shaykhul Islaam kuhusu wakati na sehemu za sherehe. Amesema: “Mfano, Muislamu asiuze chakula, nguo au chochote ambacho kitamtia shauku Muislamu awe kama Ahlul-Kitaab katika sherehe zao.”

Kutokana na hili tunafahamu kwamba ikiwa kuuza vitu kama hivyo imeharamishwa, seuze kuuza kadi ambazo zina picha za msalaba, (au picha zinazodaiwa ni za Mama Maryam (‘Alayhas-Salaam) kabeba mtoto ambaye ni ‘Iysa (‘Alayhis-Salaam) au kanisa, kwa ajili ya kutumiana salaam na pongezi katika sherehe hizo. Na baya zaidi kujiunga na kuhusika na upotofu huo mkubwa. Makatazo yanaenea pia kwa kila jambo linalohusu sherehe  hizo kama vile kusalimiana (kama kusema “Merry Christmas”  au “Happy New Year” n.k.), kupeana zawadi, vyakula na kadhalika kwani haya ndiyo mambo yanayotendwa na kuwepo katika sherehe hizo.

Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametukamilishia dini yetu kabla ya kufa kwake na hakuna jambo lililokuwa jema ila ametujulisha na hakuna jambo baya ila ametukataza. Kwa hiyo katika mafundisho yake ya Sunnah hakuna hata mwaka mmoja uliothibitika kwamba Maswahaba walisherehekea mwaka mpya unapoingia hata wa Kiislam sembuse huo wa kikafiri!

Katika Sunnah, Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema:
“Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuja Madiynah na walikuwa wana siku mbili ambazo walikuwa wakipumzika na kustarehe na kucheza. Akasema: "Hizi ni siku gani?" Wakasema: Ni siku ambazo tulikuwa tukicheza na kustarehe katika Ujaahiliya". Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Allaah Amekupeni zilizo bora kuliko hizo; Yawmul-Adhwhaa (‘Iydul-Adhwhaa) na Yawmul-Fitwr (‘Iydul-Fitr) )) [Abu Daawuwd]

Hii inaonyesha dhahiri kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameharamisha Ummah wake kusherehekea sherehe za makafiri na amefanya hima kuzifuta kwa kila njia.

Sababu mojawapo ya kuharamishwa sherehe zao kama za mwaka mpya ni kwa sababu ya maovu, uchafu na fitna zinazotokea humo. Na hata kama hakuna maovu yanayotendeka humo lakini kusherehekea kutasababisha uzushi huu kuendelea katika vizazi vyetu na kusababisha kuingiza mila za kikafiri ndani ya Uislamu.  


 ‘Umar Ibnil-Khatwtwaab amesema:"Jiepusheni na maadui wa Allaah katika sherehe zao"

Imeripotiwa katika mapokezi sahihi kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr akisema: “Yeyote anayeishi katika nchi isiyo ya Kiislam na akasherehekea sherehe yao ya mwaka mpya, na kuwaiga na akafa katika hali hiyo, basi atakusanywa pamoja nao siku ya Qiyaamah.”


Wa biLLaahit-tawfiyq


from fisabilillaah.com http://bit.ly/2Su60kP
via IFTTT

74. Matamshi ya Tashahhud – Tamko la Ibn ´Umar

3- Tashahhud ya Ibn ´Umar. Ibn ´Umar amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

التحيات لله، [و]الصلوات [و]الطيبات، السلام عليك أيها النبي و رحمة الله، السلام علينا و على عباد الله الصالحين، أشهد أن لا إله إلا الله و أشهد أن محمداً عبده و رسوله

“Maadhimisho, swalah na mazuri yote yanamstahikia Allaah. Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yako, ee Mtume[1]! Amani ishuke juu yetu na juu ya waja wema wa Allaah. Nashuhudia ya kwamba hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah[2] na nashuhudia ya kwamba Muhammad ni mja na Mtume Wake.”[3]

[1] Ibn ´Umar amesema:

“Niliongeza:

و بركاته

“… na baraka Zake… “

[2] Ibn ´Umar amesema:

“Niliongeza juu yake:

وحده لا شريك له

“… hali ya kuwa yupekee, hana mshirika… “

Nyongeza mbili hizi katika Tashahhud zimethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ibn ´Umar hakuziongeza kutoka kwake mwenyewe. Asingeweza kamwe kufanya kitu kama hicho. Nyongeza mbili hizo alijifunza nazo kutoka kwa Maswahabah wengine waliozisikia kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akaziongeza katika Tashahhud yake aliyoisikia moja kwa moja kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

[3] Abu Daawuuud na ad-Daaraqutwniy ambaye ameisahihisha.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2EWreDJ
via IFTTT

73. Matamshi ya Tashahhud – Tamko la Ibn ´Abbaas

2- Tashahhud ya Ibn ´Abbaas. Ibn ´Abbaas amesema:

“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akitufunza Tashahhud kama anavyotufunza [Suurah katika] Qur-aan: Alikuwa akisema:

التحيات المباركات الصلوات الطيبات لله، [ال]سلام عليك أيها النبي و رحمة الله و بركاته، [ال]سلام علينا و على عباد الله الصالحين، أشهد أن لا إله إلا الله و [أشهد]أن محمداً رسول الله

“Maadhimisho, baraka, swalah na mazuri yote yanamstahikia Allaah[1]. Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yako, ee Mtume! Amani ishuke juu yetu na juu ya waja wema wa Allaah. Nashuhudia ya kwamba hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah na [nashuhudia] ya kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah.”

Katika upokezi mwingine imekuja:

و أن محمداً عبده و رسوله

“… na kwamba Muhammad ni mja na Mtume Wake.”[2]

[1] an-Nawawiy amesema: ”Hadiyth inafahamisha kwamba maadhimisho na yote yaliyo baada yake yanamstahikia Allaah (Ta´ala) pekee na si mwengine.”

[2] Muslim, Abu ´Awaanah, ash-Shaafi´iy na an-Nasaa’iy.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2EXMud1
via IFTTT

72. Matamshi ya Tashahhud – Tamko la Ibn Mas´uud

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwafunza Maswahabah sampuli mbalimbali za Tashahhud:

1- Tashahhud ya Ibn Mas´uud. Ibn Mas´uud amesema:

“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alinishika mkono wangu kwa mikono yake miwili na akanifunza Tashahhud kama anavyonifunza Suurah katika Qur-aan:

التحيات لله، و الصلوات و الطيبات، السلام عليك أيها النبي و رحمة الله و بركاته، السلام علينا و على عباد الله الصالحين، أشهد أن لا إله إلا الله و أشهد أن محمداً عبده و رسوله

“Maadhimisho, swalah na mazuri yote yanamstahikia Allaah. Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yako, ee Mtume! Amani ishuke juu yetu na juu ya waja wema wa Allaah [pindi anaposema hivo basi inamgusa kila mja mwema mbinguni na ardhini]. Nashuhudia ya kwamba hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah na nashuhudia ya kwamba Muhammad ni mja na Mtume Wake.”

Tulikuwa tukisema hivo wakati (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) bado yupamoja nasi. Alipofariki tukawa tunasema:

السلام على النبي

“Amani iwe juu ya Mtume.”[1]

[1] al-Bukhariy, Muslim, Ibn Abiy Shaybah (2/90/1), as-Sarraaj na Abu Ya´laa katika ”al-Musnad” (2/258). Imetajwa katika ”al-Irwaa’” (321). Maneno ya Ibn Mas´uud “Tulikuwa tukisema hivo wakati (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) bado yupamoja nasi. Alipofariki tukawa tunasema:

السلام على النبي

“Amani iwe juu ya Mtume.”

ni dalili inayoonyesha kuwa Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) walikuwa wakisema katika Tashahhud ya kwanza wakati wa uhai wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

السلام عليك أيها النبي و رحمة الله و بركاته

“Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yako, ee Mtume!”

Baada ya kufa kwake wakabadilisha matamshi na kusema:

السلام على النبي

“Amani iwe juu ya Mtume.”

Hilo pasi na shaka ni lazima liwe limetokana na kuridhia kwake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Nadharia hiyo inaungwa mkono vilevile na ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) na jambo la hakika ni kuwa naye alifunza Tasahhhud kama ifuatavyo:

السلام على النبي

“Amani iwe juu ya Mtume.” (as-Sarraaj katika ”al-Musnad” (2/1/9) na al-Mukhallas katika ”al-Fawaa-id” (1/54/11) kwa cheni mbili za wapokezi kupitia kwake)

Haafidhw Ibn Hajar (Rahimahu Allaah) amesema:

“Nyongeza hii udhahiri wake ni kwamba walikuwa wakisema:

السلام عليك أيها النبي و رحمة الله و بركاته

“Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yako, ee Mtume!”

wakati (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa bado yuko hai. Alipofariki (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndipo wakaacha aina ya kumlenga na wakawa wanasema:

السلام على النبي

“Amani iwe juu ya Mtume.””

Ibn Hajar amesema vilevile:

“as-Subkiy amesema katika “Sharh-ul-Minhaaj” baada ya kutaja nyongeza hii kwa Abu ´Awaanah: “Ikiwa haya yamesihi kutoka kwa Maswahabah basi inafahamisha kwamba sio wajibu kusema kwa aina ya kumlenga Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) baada ya kufa kwake. Kwa hiyo mtu anaweza kusema:

السلام على النبي

“Amani iwe juu ya Mtume.””

Haya yamesihi pasi na shaka na nimepata upokezi wenye nguvu mwingine unaotilia nguvu. ´Abdur-Razzaaq amesema: “Ibn Jurayj amenikhabarisha: ´Atwaa amenikhabarisha ya kwamba Maswahabah walikuwa wakisema wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) bado yuhai:

السلام عليك أيها النبي و رحمة الله و بركاته

“Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yako, ee Mtume!”

Alipofariki wakasema:

السلام على النبي

“Amani iwe juu ya Mtume.””

Mlolongo wa wapokezi ni Swahiyh. Hata hivyo Sa´iyd bin Mansuur amepokea kupitia kwa Abu ´Ubaydah bin ´Abdillaah bin Mas´uud kutoka kwa baba yake ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwafunza Tashahhud. Baada ya kutaja tamko Ibn ´Abbaas akasema: “Wakati bado Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yuko hai ndipo tulikuwa tukisema:

السلام عليك أيها النبي و رحمة الله و بركاته

“Amani, rehema na baraka za Allaah ziwe juu yako, ee Mtume!”

Ndipo akasema Ibn Mas´uud: “Hivo ndivyo tulivyojifunza na hivo ndivyo tunavyofunza.”

Ni kama kwamba Ibn ´Abbaas alisema hivo kwa lengo la kuhakiki na kwamba Ibn Mas´uud hakurejea kwake. Lakini upokezi wa Abu Ma´mar [kwa al-Bukhaariy] ni Swahiyh zaidi kwa sababu Abu ´Ubaydah hakuwahi kusikia kutoka kwa baba yake. Pamoja na hivyo cheni ya wapokezi mpaka kwake ni dhaifu.”

Wanachuoni wengi wahakiki, akiwemo al-Qastwalaaniy, az-Zarqaaniy na al-Luknawiy, wameyanukuu maneno haya ya Haafidhw Ibn Hajar kwa kuyakubali bila kuyapinga. Rejea katika asili kuhusu zaida juu ya maudhui haya.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2EW0rrc
via IFTTT

71. Uwajibu wa ile Tashahhud ya kwanza na du´aa zake zilizowekwa katika Shari´ah

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisoma Tashahhud kila baada ya Rak´ah mbili[1]. Kitu cha kwanza anachosema punde tu baada ya kukaa chini:

التحيات لله

“Maadhimisho yote yanamstahiki Allaah.”[2]

Akisahau (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) Tashahhud ya kwanza, basi huleta Sujuud-us-Sahuw[3]. Aliamrisha Tashahhud na akasema:

“Mnapokaa chini kila baada ya Rak´ah mbili basi semeni:

…التحيات لله

“Maadhimisho yote yanamstahiki Allaah… “

na chagueni du´aa inayokupendezeni na mumuombe Allaah (´Azza wa Jall).”[4]

Katika upokezi mwingine imekuja:

“Semeni katika kila kitako:

…التحيات لله

“Maadhimisho yote yanamstahiki Allaah… “[5]

Vivyo hivyo alimwamrisha yule mtu aliyeswali kimakosa, kama ilivyotangulia punde tu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiwafunza Tashahhud kama anavyowafunza Suurah kutoka katika Qur-aan[6]. Sunnah ni kuisoma kimyakimya[7].

[1] Muslim  na Abu ´Awaanah.

[2] al-Bayhaqiy kupitia kwa ´Aaishah kwa cheni ya wapokezi nzuri, amesema Ibn-ul-Mulaqqin (2/28).

[3] al-Bukhaariy na Muslim. Imetajwa katika ”Irwaa’-ul-Ghaliyl” (338).

[4] an-Nasaa’iy, Ahmad na at-Twabaraaniy katika ”al-Mu´jam al-Kabiyr” (1/25/3) kwa cheni Swahiyh. Udhahiri ni kwamba imewekwa katika Shari´ah kuomba katika kila Tashahhud hata kama sio Rak´ah ya mwisho. Haya pia ndio maoni ya Ibn Hazm (Rahimahu Allaah).

[5] an-Nasaa’iy kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.

[6] al-Bukhaariy na Muslim.

[7] Abu Daawuud na al-Haakim ambaye ameisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2EYoAhJ
via IFTTT

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...