Translate

Alhamisi, 4 Juni 2020

151-Aayah Na Mafunzo: Miongoni Mwa Aliyopewa Nabiy Ni Kutiwa Kizaazaa Maadui Ili Waislamu Wapate Nusra

 

Aayah Na Mafunzo

Aal-‘Imraan

 

Miongoni Mwa Aliyopewa Nabiy Ni Kutiwa Kizaazaa Maadui Ili Waislamu Wapate Nusra

 

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

سَنُلْقِي فِي قُلُوبِ الَّذِينَ كَفَرُوا الرُّعْبَ بِمَا أَشْرَكُوا بِاللَّـهِ مَا لَمْ يُنَزِّلْ بِهِ سُلْطَانًا ۖ وَمَأْوَاهُمُ النَّارُ ۚ وَبِئْسَ مَثْوَى الظَّالِمِينَ ﴿١٥١﴾

151. Tutavurumisha kizaazaa katika nyoyo za waliokufuru kwa sababu ya kumshirikisha Allaah na ambayo Hakuyateremshia mamlaka. Na makazi yao ni moto, na ubaya ulioje maskani ya madhalimu

 

Mafunzo:

 

Pindi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipopigana vita pamoja na Swahaba zake dhidi ya makafiri, na idadi ya makafiri ilikuwa ni wengi mno kulikoni idadi ya Waislamu, Allaah (سبحانه وتعالى)  Aliwateremshia Waislamu miujiza kadhaa kuwasaidia waweze kupambana na makafiri na wapate ushindi. Mfano wa muujiza mmojawapo ni pale Allaah (سبحانه وتعالى) Alipowafanya makafiri wawaone Waislamu katika macho yao kuwa ni wa idadi kubwa ilhali ni wachache mno. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَدْ كَانَ لَكُمْ آيَةٌ فِي فِئَتَيْنِ الْتَقَتَا ۖ فِئَةٌ تُقَاتِلُ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ وَأُخْرَىٰ كَافِرَةٌ يَرَوْنَهُم مِّثْلَيْهِمْ رَأْيَ الْعَيْنِ ۚ وَاللَّـهُ يُؤَيِّدُ بِنَصْرِهِ مَن يَشَاءُ ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبْرَةً لِّأُولِي الْأَبْصَارِ ﴿١٣﴾

Kwa hakika ilikuwa ni Aayah (ishara) kwenu katika makundi mawili; yalipokutana (vita vya Badr). Kundi linapigana katika njia ya Allaah na jingine ni makafiri ambao wanawaona (Waislamu) mara mbili yao kwa mtazamo wa macho. Na Allaah Humsaidia kwa nusura Yake Amtakaye. Hakika katika hayo bila shaka ni zingatio kwa wenye utambuzi. [Aal-‘Imraan: 13]

 

Hali kadhalika muujiza mwenginewe ni kutiwa kiwewe, kizaazaa, khofu kubwa nyoyoni mwa makafari, waogope na iwafanye wawe dhaifu na hivyo ushindi upatikane kwa Waislamu:

 

Abuu Huraryah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Nimefadhilishwa juu ya Manabii kwa mambo sita: nimepewa; ‘Jawaami’al-Kalimi’ (mukhtasari unaojumuisha maneno mengi) na nimenusuriwa kwa (kutiwa) kizaazaa (katika nyoyo za maadui) na nimehalalishiwa ghanima na nimefanyiwa ardhi kuwa kitwaharishi na Masjid (mahali pa kuswali) na nimetumwa kwa viumbe wote, na Manabii wamekhitimishwa kwangu.” [Muslim].

 

 

 

 

 

 

 



084-Asbaabun-Nuzuwl: At-Tawbah: Aayah: 84

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Suwrah At-Tawbah: Aayah 84

 

Alhidaaya.com

 

 

Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَا تُصَلِّ عَلَىٰ أَحَدٍ مِّنْهُم مَّاتَ أَبَدًا وَلَا تَقُمْ عَلَىٰ قَبْرِهِ ۖ إِنَّهُمْ كَفَرُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَمَاتُوا وَهُمْ فَاسِقُونَ﴿٨٤﴾

Na wala usimswalie yeyote abadani miongoni mwao akifa; na wala usisimame kaburini kwake. Hakika wao wamemkufuru Allaah na Rasuli Wake, na wakafa hali wao ni mafasiki.  [At-Tawbah: 84]

 

Na pia kuhusiana na Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لَا تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِن تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً فَلَن يَغْفِرَ اللَّـهُ لَهُمْ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ كَفَرُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ ۗ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ﴿٨٠﴾

Waombee maghfirah (ee, Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم), au usiwaombee maghfirah, hata ukiwaombea maghfirah mara sabini, Allaah Hatowaghufuria. Hivyo kwa kuwa wao wamemkufuru Allaah na Rasuli Wake. Na Allaah Haongoi watu mafasiki. [At-Tawbah: 80]

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

حَدَّثَنَا عُبَيْدُ بْنُ إِسْمَاعِيلَ، عَنْ أَبِي أُسَامَةَ، عَنْ عُبَيْدِ اللَّهِ، عَنْ نَافِعٍ، عَنِ ابْنِ عُمَرَ رضى الله عنهما قَالَ لَمَّا تُوُفِّيَ عَبْدُ اللَّهِ جَاءَ ابْنُهُ عَبْدُ اللَّهِ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَسَأَلَهُ أَنْ يُعْطِيَهُ قَمِيصَهُ يُكَفِّنُ فِيهِ أَبَاهُ فَأَعْطَاهُ، ثُمَّ سَأَلَهُ أَنْ يُصَلِّيَ عَلَيْهِ، فَقَامَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم لِيُصَلِّيَ فَقَامَ عُمَرُ فَأَخَذَ بِثَوْبِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ تُصَلِّي عَلَيْهِ وَقَدْ نَهَاكَ رَبُّكَ أَنْ تُصَلِّيَ عَلَيْهِ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏"‏ إِنَّمَا خَيَّرَنِي اللَّهُ فَقَالَ: ((اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لاَ تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِنْ تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً))‏ وَسَأَزِيدُهُ عَلَى السَّبْعِينَ ‏"‏‏.‏ قَالَ إِنَّهُ مُنَافِقٌ‏.‏ قَالَ فَصَلَّى عَلَيْهِ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَأَنْزَلَ اللَّهُ: ((‏وَلاَ تُصَلِّ عَلَى أَحَدٍ مِنْهُمْ مَاتَ أَبَدًا وَلاَ تَقُمْ عَلَى قَبْرِهِ‏))

 

Ametuhadithia ‘Ubayd bin Ismaa’iyl toka kwa Abuu Usaamah toka kwa ‘Ubaydullaah toka kwa Naafi’i toka kwa Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما)  amesema: Alipokufa ‘Abdullaah, alikuja mwanaye ‘Abdullaah bin ‘Abdillaah kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akamwomba ampe kanzu yake ili amkafinie baba yake, na Rasuli akampa. Kisha akamwomba amswalie, na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akasimama ili aswali. ‘Umar akasimama, akaikamata nguo ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na kusema: “Ee Rasuli wa Allaah! Unamswalia nailhali Rabb wako Amekukataza kumswalia?” Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Hakika Allaah Amenikhiyarisha Akisema:

 

اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لَا تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِن تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً  

Waombee maghfirah (ee, Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم), au usiwaombee maghfirah [At-Tawbah: 80]

 

Nami nitamzidishia zaidi ya mara sabiini.”  Akasema: “Hakika huyo ni mnafiki.” Akasema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamswalia, na hapo Allaah Akateremsha:

وَلَا تُصَلِّ عَلَىٰ أَحَدٍ مِّنْهُم مَّاتَ أَبَدًا وَلَا تَقُمْ عَلَىٰ قَبْرِهِ 

Na wala usimswalie yeyote abadani miongoni mwao akifa; na wala usisimame kaburini kwake. 

[Al-Bukhaariy Kitaab At-Tafsiyr]

 

Na pia,

 

 حَدَّثَنَا مُسَدَّدٌ، قَالَ حَدَّثَنَا يَحْيَى بْنُ سَعِيدٍ، عَنْ عُبَيْدِ اللَّهِ، قَالَ حَدَّثَنِي نَافِعٌ، عَنِ ابْنِ عُمَرَ رضى الله عنهما أَنَّ عَبْدَ، اللَّهِ بْنَ أُبَىٍّ لَمَّا تُوُفِّيَ جَاءَ ابْنُهُ إِلَى النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ أَعْطِنِي قَمِيصَكَ أُكَفِّنْهُ فِيهِ، وَصَلِّ عَلَيْهِ وَاسْتَغْفِرْ لَهُ، فَأَعْطَاهُ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم قَمِيصَهُ فَقَالَ ‏"‏ آذِنِّي أُصَلِّي عَلَيْهِ ‏"‏‏.‏ فَآذَنَهُ، فَلَمَّا أَرَادَ أَنْ يُصَلِّيَ عَلَيْهِ جَذَبَهُ عُمَرُ رضى الله عنه ـ فَقَالَ أَلَيْسَ اللَّهُ نَهَاكَ أَنْ تُصَلِّيَ عَلَى الْمُنَافِقِينَ فَقَالَ ‏"‏ أَنَا بَيْنَ خِيرَتَيْنِ قَالَ ‏ ((‏اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لاَ تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِنْ تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً فَلَنْ يَغْفِرَ اللَّهُ لَهُمْ)) ‏ فَصَلَّى عَلَيْهِ فَنَزَلَتْ: ((‏وَلاَ تُصَلِّ عَلَى أَحَدٍ مِنْهُمْ مَاتَ أَبَدًا‏))

Ametuhadithia Musaddad, amesema ametuhadithia Yahyaa bin Sa’iyd toka kwa ‘Ubaydullaah amesema: “Amenihadithia Naafi’i toka kwa Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما)  ya kuwa alipofariki ‘Abdullaah bin Ubayya, mtoto wake alikwenda kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  na kumwambia: Ee Rasuli wa Allaah, nipe kanzu yako nikamkafinie, na mswalie na mwombee maghfirah. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akampa kanzu yake na kumwambia: “Nipe idhni nimswalie.” Naye akampa. Na aliposimama kumswalia, ‘Umar (رضي الله عنه)   alimvuta na kumwambia: “Hivi kwani Allaah Hakukukataza kuwaswalia wanafiki?” Akasema: “Mimi niko kati ya khiyari mbili, Akasoma:

اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لَا تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِن تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً  

Waombee maghfirah (ee, Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم), au usiwaombee maghfirah [At-Tawbah: 80]

Akamswalia, na hapo ikamteremkia:

وَلَا تُصَلِّ عَلَىٰ أَحَدٍ مِّنْهُم مَّاتَ أَبَدًا

Na wala usimswalie yeyote abadani miongoni mwao akifa.

[Al-Bukhaariy – Kitaab Al-Janaaiz]

 

Na pia,

حَدَّثَنِي إِبْرَاهِيمُ بْنُ الْمُنْذِرِ، حَدَّثَنَا أَنَسُ بْنُ عِيَاضٍ، عَنْ عُبَيْدِ اللَّهِ، عَنْ نَافِعٍ، عَنِ ابْنِ عُمَرَ رضى الله عنهما أَنَّهُ قَالَ لَمَّا تُوُفِّيَ عَبْدُ اللَّهِ بْنُ أُبَىٍّ جَاءَ ابْنُهُ عَبْدُ اللَّهِ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَأَعْطَاهُ قَمِيصَهُ وَأَمَرَهُ أَنْ يُكَفِّنَهُ فِيهِ ثُمَّ قَامَ يُصَلِّي عَلَيْهِ، فَأَخَذَ عُمَرُ بْنُ الْخَطَّابِ بِثَوْبِهِ فَقَالَ تُصَلِّي عَلَيْهِ وَهْوَ مُنَافِقٌ وَقَدْ نَهَاكَ اللَّهُ أَنْ تَسْتَغْفِرَ لَهُمْ‏.‏ قَالَ ‏"‏ إِنَّمَا خَيَّرَنِي اللَّهُ أَوْ أَخْبَرَنِي فَقَالَ ‏((‏اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لاَ تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِنْ تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً فَلَنْ يَغْفِرَ اللَّهُ لَهُمْ‏)) ‏ فَقَالَ سَأَزِيدُهُ عَلَى سَبْعِينَ ‏"‏‏.‏ قَالَ فَصَلَّى عَلَيْهِ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَصَلَّيْنَا مَعَهُ ثُمَّ أَنْزَلَ اللَّهُ عَلَيْهِ: ((‏وَلاَ تُصَلِّ عَلَى أَحَدٍ مِنْهُمْ مَاتَ أَبَدًا وَلاَ تَقُمْ عَلَى قَبْرِهِ إِنَّهُمْ كَفَرُوا بِاللَّهِ وَرَسُولِهِ وَمَاتُوا وَهُمْ فَاسِقُونَ‏))

Amenihadithia Ibraahiym bin Al-Mundhir, ametuhadithia Anas bin ‘Iyaadhw toka kwa ‘Ubaydullaah toka kwa Naafi’i toka kwa Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما)  kwamba amesema: Alipokufa ‘Abdullaah bin Ubayya, mwanawe ‘Abdullaah bin ‘Abdillaah alikuja  kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  na Rasuli akampa kanzu yake na kumwamuru amkafinie kwayo, kisha akasimama kumswalia. ‘Umar bin Al-Khattwaab akaikamata nguo yake na kumwambia: “Unamswalia naye ni mnafiki, nailhali Allaah Amekukataza kuwaombea maghfirah!?” Akasema: “Hakika Allaah Amenikhiyarisha au Amenijulisha, Akasema:

اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لَا تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِن تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً فَلَن يَغْفِرَ اللَّـهُ لَهُمْ

Waombee maghfirah (ee, Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم), au usiwaombee maghfirah, hata ukiwaombea maghfirah mara sabini, Allaah Hatowaghufuria.

 

Akasema: Nitamzidishia zaidi ya mara sabiini. Akasema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamswalia nasi tukaswali pamoja naye. Kisha Allaah Akamteremshia:

وَلَا تُصَلِّ عَلَىٰ أَحَدٍ مِّنْهُم مَّاتَ أَبَدًا وَلَا تَقُمْ عَلَىٰ قَبْرِهِ ۖ إِنَّهُمْ كَفَرُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَمَاتُوا وَهُمْ فَاسِقُونَ

Na wala usimswalie yeyote abadani miongoni mwao akifa; na wala usisimame kaburini kwake. Hakika wao wamemkufuru Allaah na Rasuli Wake, na wakafa hali wao ni mafasiki.

[Al-Bukhaariy - Kitaab  At-Tafsiyr]

 

Na pia,

حَدَّثَنَا أَبُو بَكْرِ بْنُ أَبِي شَيْبَةَ، حَدَّثَنَا أَبُو أُسَامَةَ، حَدَّثَنَا عُبَيْدُ اللَّهِ، عَنْ نَافِعٍ، عَنِ ابْنِ عُمَرَ، قَالَ لَمَّا تُوُفِّيَ عَبْدُ اللَّهِ بْنُ أُبَىٍّ ابْنُ سَلُولَ جَاءَ ابْنُهُ عَبْدُ اللَّهِ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَسَأَلَهُ أَنْ يُعْطِيَهُ قَمِيصَهُ أَنْ يُكَفِّنَ فِيهِ أَبَاهُ فَأَعْطَاهُ ثُمَّ سَأَلَهُ أَنْ يُصَلِّيَ عَلَيْهِ فَقَامَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم لِيُصَلِّيَ عَلَيْهِ فَقَامَ عُمَرُ فَأَخَذَ بِثَوْبِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ أَتُصَلِّي عَلَيْهِ وَقَدْ نَهَاكَ اللَّهُ أَنْ تُصَلِّيَ عَلَيْهِ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏"‏ إِنَّمَا خَيَّرَنِيَ اللَّهُ فَقَالَ: ((اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لاَ تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِنْ تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً‏)) وَسَأَزِيدُ عَلَى سَبْعِينَ‏"‏ ‏.‏ قَالَ إِنَّهُ مُنَافِقٌ ‏.‏ فَصَلَّى عَلَيْهِ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَأَنْزَلَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ: ((وَلاَ تُصَلِّ عَلَى أَحَدٍ مِنْهُمْ مَاتَ أَبَدًا وَلاَ تَقُمْ عَلَى قَبْرِهِ‏))‏

Ametuhadithia Abuu Bakri bin Abiy Shaybah, ametuhadithia Abuu Usaamah, ametuhadithia ‘Ubaydullaah toka kwa Naafi’i toka kwa Ibn ‘Umar amesema: “Alipokufa ‘Abdullaah bin Ubayya bin Saluwl, mtoto wake ‘Abdullaah bin ‘Abdillaah alikuja kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akamwomba ampe kanzu yake amkafinie baba yake naye akampa. Kisha akamwomba amswalie, na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasimama ili amswalie. ‘Umar akasimama, akaikamata nguo ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Ee Rasuli wa Allaah: Unamswalia nailhalli Allaah Amekukataza kumswalia?” Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Hakika Allaah Amenikhiyarisha Akasema:

اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لَا تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِن تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً

Waombee maghfirah (ee, Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم), au usiwaombee maghfirah, hata ukiwaombea maghfirah mara sabini.

Nami nitazidisha zaidi ya sabiini.” Akasema (‘Umar): “Hakika yeye ni mnafiki.” Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamswalia, na Allaah (عز وجل) Akateremsha:

وَلَا تُصَلِّ عَلَىٰ أَحَدٍ مِّنْهُم مَّاتَ أَبَدًا وَلَا تَقُمْ عَلَىٰ قَبْرِهِ

Na wala usimswalie yeyote abadani miongoni mwao akifa; na wala usisimame kaburini kwake.

[Muslim – Kitaab Swifaat Al-Munaafiqiyn Wa Ahkaamihim]

 

 



042-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Haingii Jannah Mtu Ila Kwa Iymaan, Kupendana na Kutoleana Salaam

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya  42

 

Haingii Jannah Mtu Ila Kwa Iymaan, Kupendana na Kutoleana Salaam

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ لاَ تَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ حَتَّى تُؤْمِنُوا، وَلاَ تُؤْمِنُوا حَتَّى تَحَابُّوا، أَوَلاَ أَدُلُّكُمْ عَلَى شَيْءٍ إِذَا فَعَلْتُمُوهُ تَحَابَبْتُمْ؟  أَفْشُوا السَّلاَمَ بَيْنَكُمْ)) مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake! Hamtoingia Jannh mpaka muamini, wala hamtoamini mpaka mpendane. Je, niwajulishe jambo mtakapolifanya mtapendana? Enezeni Salaam baina yenu)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kutekeleza amri ya kuamkiana kwa maamkizi ya Kiislamu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٍ فَحَيُّوا بِأَحْسَنَ مِنْهَا أَوْ رُدُّوهَا ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ حَسِيبًا ﴿٨٦﴾

Na mtapoamkiwa kwa maamkizi yoyote, basi itikieni kwa yaliyo mazuri zaidi kuliko hayo au yarudisheni hayo hayo. Hakika Allaah daima ni Mwenye kuhesabu kila kitu. [An-Nisaa: 86]

 

2. Maamkizi ya Kiislamu yana kheri na baraka, ndio maana Allaah (سبحانه وتعالى) Akaamrisha mtu anapoingia nyumbani kwake ayatamke, hata kama hakuna mtu ndani ya nyumba. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  ۚ فَإِذَا دَخَلْتُم بُيُوتًا فَسَلِّمُوا عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ تَحِيَّةً مِّنْ عِندِ اللَّـهِ مُبَارَكَةً طَيِّبَةً ۚ  

Mtakapoingia majumbani toleaneni salaam; maamkizi kutoka kwa Allaah, yenye Baraka, mazuri.  [An-Nuwr (24: 61)]

 

3. Jannah haipatikani ila kuweko na Iymaan, na Iymaan haikamiliki ila Muislamu ampendelee nduguye anayoyapenda nafsi yake. [Rejea Hadiyth namba 21].

 

 

4. Iymaan haikamiliki ila kwa matendo na amri zake.

 

 

5. Maamkizi ya Kiislamu katika shariy’ah na inavyopasa kuamkiana ni “Assalaamu ‘Alaykum” Au: “Assalaamu ‘alaykum wa RahmatuLLaah” Au: “Assalaamu ‘alaykum wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh”  na si vinginevyo kutokana na Hadiyth:

 

عَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَيْنٍ  رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا  قَالَ: جَاءَ رَجُلٌ إِلَى النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ: "السَّلامُ عَلَيْكُمْ" فَرَدَّ عَلَيْهِ ثُمَّ جَلَسَ فَقَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((عَشْرٌ))  ثُمَّ جَاءَ آخَرُ فَقَالَ: "السَّلامُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللَّهِ"  فَرَدَّ عَلَيْهِ فَجَلَسَ فَقَالَ: ((عِشْرُونَ)) ثُمَّ جَاءَ آخَرُ فَقَالَ: "السَّلامُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللَّهِ وَبَرَكَاتُهُ" فَرَدَّ عَلَيْهِ فَجَلَسَ فَقَالَ : ((ثَلاثُونَ)) رواه ابو داود والترمذي و قال حديث حسن

'Imraan bin Al-Huswayn (رضي الله عنهما) amesimulia: "Mtu mmoja alikuja kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: "Assalaamu 'Alaykum." Akamrudishia (Salaam) kisha yule mtu akaketi. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Kumi)) [Kwa maana amepata thawabu kumi]. Kisha akaja mtu mwengine, akasema: "Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLLaah." Naye akamrudishia, kisha yule mtu akaketi, Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Ishirini)). Kisha akaja mtu mwingine akasema: "Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh." Naye akamrudishia kisha akasema ((Thelathini)) [Imesimuliwa na Abu Daawuwd na At-Trimidhiy na akasema Hadiyth Hasan na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Abiy Daawuwd (5195), Swahiyh At-Tirmidhiy (2869)]

 

 

Na haifai kuyafupisha katika maandishi kama ilivyozoeleka katika mitandao ya kijamii; baadhi ya watu kuandika: (AA) na vinginevyo. ‘Ulamaa wetu wamekemea jambo hili kwamba ni kinyume na maamrisho ya Qur-aan na Sunnah, na pia ni kujikosesha thawabu na fadhila zake.

 

 

5. Kutoleana Salaam ni sababu au chanzo cha kutambulisha na kujuana baina ya Waislamu, na kutoa Salaam kwa mtu mmoja kunaweza kuwafikia maelfu ya Waislamu na kupata fadhila, thawabu, na manufaa yake.

 

 

6. Maamkizi ya Kiislamu ni funguo za mapenzi baina ya Waislamu.

 

 

7. Maamkizi ya Kiislamu ndiyo yanayotofautisha baina ya Waislamu na makafiri.

 

 

8. Maamkizi ya Kiislamu yanalingana sawa na maana ya ‘Uislamu’ yaani amani.  

 

 

9. Fadhila ya Iymaan ni kumuingiza mtu Jannah.

 

 

 

 



04-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Shirki Inabatilisha ‘Amali

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno

 

04- Shirki Inabatilisha ‘Amali

 

Alhidaaya.com

 

 

‘Amali za Muislamu bila ya kuwa na niyyah safi kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) au ikhlaasw, huwa hazina thamani mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa dalili zifuatazo:

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

 

وَقَدِمْنَا إِلَىٰ مَا عَمِلُوا مِنْ عَمَلٍ فَجَعَلْنَاهُ هَبَاءً مَّنثُورًا ﴿٢٣﴾

Na Tutayaendea yale waliyoyatenda ya ‘amali yoyote ile, Tutayafanya   chembechembe za vumbi zinazoelea hewani zinazotawanyika. [Al-Furqaan: 23]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ﴿٦٥﴾

Kwa yakini umefunuliwa Wahy na kwa wale walio kabla yako kwamba: “Ukifanya shirki bila shaka zitaporomoka ‘amali zako na bila shaka utakuwa miongoni mwa waliokhasirika.” [Az-Zumar: 65]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٨٨﴾

Na kama wangemshirikisha bila shaka yangeporomoka yale waliyokuwa wakitenda. [Al-An’aam: 88]

 

 

 

Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametaja katika Hadiyth Al-Qudsiy:

 

 

عنْ ابي هريرة رضي الله عنه أنَّه صلَّى الله عليه وسلَّم قال: ((قال الله تعالى: أنا أغْنى الشُّركاء عن الشِّرْك، فمَن عمل عملاً أشْرَك فيه معي غيري تركتُه وشِرْكه))    

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam amesema: ((Allaah Ta’aalaa Anasema: ‘‘Mimi ni mwenye kujitosheleza kabisa, sihitaji msaada wala mshirika. Kwa hiyo, yule afanyaye ‘amali kwa kunishirikisha na mtu, nitaikanusha pamoja na mshirika wake.”)) Yaani: hatopata ujira wowote kwa ‘amali hiyo. [Muslim (2985), Ibn Maajah (4202)]

 

 

Mfano bayana wa kubatilika ‘amali za mtu kwa anayetoa swadaqah kwa riyaa ni kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُبْطِلُوا صَدَقَاتِكُم بِالْمَنِّ وَالْأَذَىٰ كَالَّذِي يُنفِقُ مَالَهُ رِئَاءَ النَّاسِ وَلَا يُؤْمِنُ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ۖ فَمَثَلُهُ كَمَثَلِ صَفْوَانٍ عَلَيْهِ تُرَابٌ فَأَصَابَهُ وَابِلٌ فَتَرَكَهُ صَلْدًا ۖ لَّا يَقْدِرُونَ عَلَىٰ شَيْءٍ مِّمَّا كَسَبُوا ۗ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ ﴿٢٦٤﴾

 Enyi walioamini! Msibatilishe swadaqah zenu kwa masimbulizi na udhia kama yule ambaye anatoa mali yake kwa kujionyesha kwa watu wala hamwamini Allaah na Siku ya Mwisho. Basi mfano wake ni kama jabali juu yake pana udongo, kisha likapigwa na mvua kubwa ikaliacha tupu. Hawana uwezo juu ya lolote katika waliyoyachuma. Na Allaah Haongoi watu makafiri.  [Al-Baqarah: 264]

 

 



42-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Ni Kigezo Kizuri Kwa Anayetaka Kufaulu Aakhirah

 

Fadhila Za  Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

42-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Ni Kigezo Kizuri Kwa Anayetaka Kufaulu Aakhirah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Amemjaalia Nabiy Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) kuwa na tabia njema zilokamilika nazo ni kigezo kwa yeyote yule anayetaka kufuzu Aakhirah kwa kuingizwa Jannah (Peponi) na kuepushwa na Moto. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّـهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ لِّمَن كَانَ يَرْجُو اللَّـهَ وَالْيَوْمَ الْآخِرَ  

Kwa yakini mna kigezo kizuri kwa Rasuli wa Allaah kwa mwenye kumtaraji Allaah na Siku ya Mwisho  [Al-Ahzaab: 21]

 

Imaam As-Sa’dy (رحمه الله) amesema kuhusu kauli hiyo ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

“Mwenye kufuata kigezo chake amefuata njia ya kumfikisha katika Utukufu wa Allaah na hiyo ndio Njia Iliyonyooka. Na kigezo hicho kizuri hukifuata  na kupata tawfiyq kwa mwenye kumtaraji Allaah na Siku ya Mwisho, kwa sababu ya kuwa kwake na iymaan, khofu ya Allaah, kutaraji thawabu na khofu ya adhabu Yake, basi hujihimiza kufuata kigezo cha Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم).” [Tafsiyr As-Sa’dy]

 

 

 

 



42-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Unyenyekevu Wake Katika Ibaadah: Hakujitukuza Kwa Kujitanguliza Yeye Katika Jamaraat (Kurusha Vijiwe Minaa)

 

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

46-Unyenyekevu Wake Katika Ibaadah Hakujitukuza Kwa  Kujitanguliza Yeye

Katika Jamaraat (Kurusha Vijiwe Minaa)

 

www.alhidaaya.com

 

 

Ingawa kawaida ya viongozi hutangulia kutekeleza jambo, na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa ni kiongozi wa Swahaba katika kutekeleza taratibu za Hajj, lakini hakujipa umbele kama kiongozi, bali alifanya nao pamoja bila ya kujitukuza.  

 

 

 عَنْ قُدَامَةَ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ، قَالَ رَأَيْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَرْمِي جَمْرَةَ الْعَقَبَةِ يَوْمَ النَّحْرِ عَلَى نَاقَةٍ لَهُ صَهْبَاءَ لاَ ضَرْبَ وَلاَ طَرْدَ وَلاَ إِلَيْكَ إِلَيْكَ ‏.‏

 

Amehadithia Qudaamah bin ‘Abdillaah kwamba: “Nilimuona Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akiwa juu ya ngamia aliyechanganyika rangi nyekundu na kahawia, akirusha vijiwe katika Jamarah ya Al-‘Aqabah (Minaa) Siku ya An-Nahr (Siku ya Iydul-Adhw-haa), bila kumpiga mtu yeyote au kumfukuza." [At-Tirmidhiy na amesema Abuu ‘Iysaa Hadiyth Hasan Swahiyh. Imekusanywa pia na An-Nasaaiy na Ibn Maajah]

 

 

 



Jumatano, 3 Juni 2020

Fangasi ukeni na tiba yake

Fangasi ukeni na tiba yake

fangasi ukeni na tiba yake

Kwa kawaida mwanamke hutokwa na majimaji mepesi (vaginal fluids) yenye rangi nyeupe au ya njano.

Inapotokea anatokwa na majimaji yenye ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali na muwasho, hiyo huwa ni ishara ya ugonjwa uitwao wa kutokwa uchafu ukeni ujulikanao kwa kitaalamu kama ‘Vaginosis’.

Mwanamke mwenye tatizo hili hujisikia vibaya na anaweza akaacha kushiriki tendo la ndoa ama kwa kuhofia maumivu au kwa kuona aibu kwani mwanaume ni vigumu kuvumilia harufu hiyo au hata kuuona tu huo ute ute kwani humjengea hisia kwamba mwenza wake atakuwa na magonjwa ya zinaa au si mwaminifu kwa ujumla.

Kinachosababisha kutokwa na uchafu ukeni:

• Kuwa na wapenzi wengi
• Baadhi ya dawa za uzazi wa mpango
• Kusafisha uke kwa kutumia dawa zenye kemikali
• Uchafu
• Uvutaji sigara
• Pombe
• Maambukizi ya Bakteria au bakteria wabaya wanapozidi ukeni

Dalili:

• Kutokwa na uchafu usio wa kawaida
• Kutokwa na uchafu wenye harufu kali kama shombo ya samaki au kitu kilichooza
• Kuwashwa sehemu za siri na ndani ya uke
• Uke unaweza kubadilika na kuwa na rangi nyekundu
• Maumivu sehemu za siri wakati wa kukojoa
• Maumivu makali chini ya kitovu
• Kutokwa uchafu uliochanganyika na damu

Fangasi ukeni na tiba yake

Matibabu

Dawa ya asili ya fangasi ukeni  > Palimaua
Ili kutibu aina yoyote ya maambukizi ya ndani ya mwili ambayo yanahusu bakteria, virusi au fangasi kunategemea sana na uimara na ubora wa kinga yako ya mwili.

Kinga yako ya mwili inajumuisha aina ya seli nyeupe maalumu ambazo hutafuta na kuua bakteria na vijidudu vingine nyemelezi ambavyo husababisha magonjwa.

Kinga yako ya mwili inapokuwa ni dhaifu bakteria wabaya wanaweza kuongezeka na kujirundika mwilini na kusambaa mpaka kwenye via vya uzazi kwa njia ya damu.

Kwahiyo ili kutibu na kukinga P.I.D unahitaji kuwa na dawa ya uhakika ya kuboresha kinga yako ya mwili ifanye kazi kwa kiwango chake cha juu kabisa.

  • Palimaua ni mchanganyiko wa dawa kadhaa za asili maalumu kwa kuimarisha kinga ya mwili nzuri kuliko dawa nyingine yoyote unaifahamu au uliyowahi kutumia.
  • Ni dawa nzuri ya asili inayondoa sumu mwilini.
  • Ina Vitamini C. Vitamini C ni mhimu katika kurejesha kinga ya mwili kwa sababu ni vitamini inayofanya kazi ya kuripea seli za mwili na kinga ya mwili.
  • Vitamini C huimarisha ngozi ya mwili, nywele, fizi, macho na kuongeza nguvu ya jumla ya mwili
  • Ina Vitamini A ambayo ni moja ya vitamini zinazotajwa kuwa mhimu sana katika kuimarisha kinga ya mwili.
  • Vitamini A ni mhimu kwa watu wanaosumbuliwa na matatizo kama ya kuharisha, upungufu wa kinga mwilini, surua na malaria.
  • Palimaua husafisha mwili wako wote, inasafisha ini, figo, moyo, macho, inaimarisha meno, ngozi na nywele.
  • Ni dawa bora ya asili yenye nguvu dhidi ya bakteria (anti-bacteria), ni dawa dhidi ya virusi (anti-virus) na ni dawa pia dhidi ya fangasi (anti-fungus).
  • Pia ni dawa nzuri kwa mtu mwenye tatizo la kukosa usingizi.
  • Usingizi ni kitu mhimu katika kuongeza, kutunza na kuimarisha kinga ya mwili.
  • Kama hupati usingizi mzuri na wa kutosha kila siku ni vigumu mwili wako kuwa na kinga nzuri ya mwili na hivyo utashambuliwa kirahisi na magonjwa ya bakteria, virusi na fangasi.
  • Ikiwa ni mjamzito usitumie dawa hii.
  • Inatibu pia vidonda vya tumbo
  • Mara zote pata ushauri toka kwa tabibu kabla ya kuanza kutumia dawa yoyote

Mara uonapo dalili hizo unashauriwa kwenda kumuona daktari haraka iwezekanavyo kwa vipimo zaidi na dawa zaweza kuwa ni za kunywa au za kupaka.

Mpaka hapo nimekupa hii Elimu BURE pia nimekuandikia maelezo namna ya kutumia BURE hujanilipa hata sh 100. Hela haitibu mtu ndiyo maana hata matajiri hufariki.

Je unahitaji dawa ya asili ya kutibu fangasi ukeni? Kama ndiyo niachie tu ujumbe WhatsApp +255714800175

MAMBO MHIMU YA KUZINGATIA:

Zingatia dawa peke yake haitofaa kitu bila kuzingatia ushauri au masharti mhimu yafuatayo:

1. Kunywa maji mengi kila siku kuanzia glasi 8 hadi 10
2. Tumia zaidi vyakula vyenye vitamini B, C, D na E
3. Tumia sana matunda hasa machungwa, limau, ndizi na vitunguu
4. Punguza vyakula vyenye wanga
5. Acha kutumia vidonge vya uzazi wa mpango, hii ni kwa sababu vidonge hivi vinasemwa huwa vinasababisha kushuka kwa kinga ya mwili na kukufanya mrahisi kupata maambukizi ya fangasi.
6. Epuka mapenzi kinyume na maumbile
7. Acha kutumia sukari na badala yake tumia asali
8. Usitumie chokoleti na vitu vingine vya namna hiyo
9. Kuwa na mpenzi mmoja tu
10. Pendelea kujiweka msafi muda wote
11. Oga maji ya moto
12. Acha vinywaji baridi, acha pia chai ya rangi na kahawa
13. Acha vilevi
14. Acha matumizi ya pafyumu hasa maeneo ya huko

MHIMU: Kama unahitaji USHAURI TU niandikie hapo kwenye comment nitakujibu, nitafute WhatsApp ikiwa tu unahitaji dawa toka kwangu moja kwa moja.

Mjulishe pia rafiki yako kwenye twitter naye asome post hii kwa kubonyeza maneno yafuatayo;

Fangasi ukeni na tiba yake Click To Tweet

Tafadhali SHARE post hii na wengine uwapendao

Fadhili Paulo
Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
Imesomwa mara 9

Let's block ads! (Why?)

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...