Translate

Ijumaa, 23 Agosti 2019

28-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Atakuwa Wa Kwanza Kuingia Jannah Pamoja Na Ummah Wake

 

 

 

Fadhila Za  Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

28-Atakuwa Wa Kwanza Kuingia  Jannah Pamoja Na Ummah Wake

www.alhidaaya.com

 

 

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) atakuwa wa kwanza kuingia Jannah (Peponi):

 

 

عَنْ ثَابِتٍ، عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ، قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏ "‏ آتِي بَابَ الْجَنَّةِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ فَأَسْتَفْتِحُ فَيَقُولُ الْخَازِنُ مَنْ أَنْتَ فَأَقُولُ مُحَمَّدٌ ‏.‏ فَيَقُولُ بِكَ أُمِرْتُ لاَ أَفْتَحُ لأَحَدٍ قَبْلَكَ ‏" ‏مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Thaabit kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Nitaufikia mlango wa Jannah Siku ya Qiyaamah, utafunguliwa kisha mlinzi wake atauliza: “Nani wewe?” Nitasema: Mimi Muhammad. Atasema: Nimeamrishwa kukufungulia wewe tu si mwenginewe kabla yako)) [Muslim]

 

 Na katika Hadiyth nyengine atakuwa wa kwanza kugonga mlango wa Jannah:

 

 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ، قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏ "‏ أَنَا أَكْثَرُ الأَنْبِيَاءِ تَبَعًا يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَأَنَا أَوَّلُ مَنْ يَقْرَعُ بَابَ الْجَنَّةِ ‏"‏ ‏.‏مسلم

 

Kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Miongoni mwa Manabii, mimi nitakuwa ndiye mwenye wafuasi wengi kabisa Siku ya Qiyaamah na wa kwanza kuugonga mlango wa Jannah)) [Muslim]

 

Na pia Ummah wake tutakuwa wa kwanza kuingia Jannah:

 

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏ "‏ نَحْنُ الآخِرُونَ الأَوَّلُونَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَنَحْنُ أَوَّلُ مَنْ يَدْخُلُ الْجَنَّةَ بَيْدَ أَنَّهُمْ أُوتُوا الْكِتَابَ مِنْ قَبْلِنَا وَأُوتِينَاهُ مِنْ بَعْدِهِمْ فَاخْتَلَفُوا فَهَدَانَا اللَّهُ لِمَا اخْتَلَفُوا فِيهِ مِنَ الْحَقِّ فَهَذَا يَوْمُهُمُ الَّذِي اخْتَلَفُوا فِيهِ هَدَانَا اللَّهُ لَهُ - قَالَ يَوْمُ الْجُمُعَةِ - فَالْيَوْمُ لَنَا وَغَدًا لِلْيَهُودِ وَبَعْدَ غَدٍ لِلنَّصَارَى ‏"‏ ‏.‏ البخاري ، مسلم  

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Sisi ni (Ummah) wa mwisho lakini ni wa kwanza siku ya Qiyaamah. Sisi ni wa kwanza kuingia Jannah ingawa wao (Mayahudi na Manaswara) walipewa Kitabu kabla yetu nasi tumepewa baada yao. Allaah Ametuongoza katika haki katika waliyokhitilafiana kwa idhini Yake. Hii ni siku (Ijumaa) waliyokhitilafiana, nasi Allah Ametuongoza nayo Hivyo watu wanatufuata kwani kesho (Jumamosi) ni siku ya Mayahudi na inayofuatia (Jumapili) ni ya Manaswara)) [Al-Bukhaariy, Muslim  na wengineo]

 



086-Aayah Na Mafunzo: Tawbah Baada Ya Kuritadi Inakubalika

Aayah Na Mafunzo

Aal-‘Imraan

Tawbah Baada Ya Kuritadi Inakubalika

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa):

 

كَيْفَ يَهْدِي اللَّـهُ قَوْمًا كَفَرُوا بَعْدَ إِيمَانِهِمْ وَشَهِدُوا أَنَّ الرَّسُولَ حَقٌّ وَجَاءَهُمُ الْبَيِّنَاتُ ۚ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ ﴿٨٦﴾ 

86. Vipi Allaah Atawaongoza watu waliokufuru baada ya kuamini kwao na wakashuhudia kwamba Rasuli ni haki na zikawajia hoja bayana? Na Allaah Hawaongozi watu madhalimu.

 

 أُولَـٰئِكَ جَزَاؤُهُمْ أَنَّ عَلَيْهِمْ لَعْنَةَ اللَّـهِ وَالْمَلَائِكَةِ وَالنَّاسِ أَجْمَعِينَ ﴿٨٧﴾

87. Hao jazaa yao ni kwamba juu yao ipo laana ya Allaah na ya Malaika na ya watu wote.

 

خَالِدِينَ فِيهَا لَا يُخَفَّفُ عَنْهُمُ الْعَذَابُ وَلَا هُمْ يُنظَرُونَ ﴿٨٨﴾

88. Wenye kudumu humo hawatopunguziwa adhabu wala hawatopewa muda wa kuakhirishwa adhabu.

إِلَّا الَّذِينَ تَابُوا مِن بَعْدِ ذَٰلِكَ وَأَصْلَحُوا فَإِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٨٩﴾

89. Isipokuwa wale waliotubu baada ya hayo na wakatengenea, basi hakika Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu.

 

Mafunzo:

 

Aayah hizi (3: 86-89) ziliteremka kuhusu mtu mmoja katika Answaar ambaye alisilimu kisha akaritadi na akaingia katika shirki kisha akajuta kwa hilo tendo lake la kuritadi. Akatuma watu wake ili wamtumie ujimbe wa swali kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kuwa je, hivi anaweza kuleta tawbah kwa tendo lake hilo? Kisha baada ya swali hilo kuulizwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) zikateremka hizo Aayaat, akatumiwa, akasilimu [Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) imepokelewa aathaar hii na Ibn Jariyr, na pia imesimuliwa na Ahmad, Ibn Hibbaan na wengineo na ameiwafiki Adh-Dhahabiy na Al-Albaaniy katika Asw-Swahiyhah (3066)].

 

 

 



Alhamisi, 15 Agosti 2019

27-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Atakuwa Wa Kwanza Na Ummah Wake Kuvuka Swiraatw

Fadhila Za  Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

27-Atakuwa Wa Kwanza Na Ummah Wake Kuvuka Swiraatw

www.alhidaaya.com

 

Kutoka katika Hadiyth ndefu kabisa iliyothibiti kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Ummah wake tutakuwa wa kwanza kabisa kuvuka Asw-Swiraatw:

 

عَنْ عَطَاءِ بْنِ يَزِيدَ اللَّيْثِيِّ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، أَنَّ النَّاسَ، قَالُوا يَا رَسُولَ اللَّهِ هَلْ نَرَى رَبَّنَا يَوْمَ الْقِيَامَةِ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏"‏ هَلْ تُضَارُّونَ فِي الْقَمَرِ لَيْلَةَ الْبَدْرِ ‏"‏‏.‏ قَالُوا لاَ يَا رَسُولَ اللَّهِ‏.‏ قَالَ ‏"‏ فَهَلْ تُضَارُّونَ فِي الشَّمْسِ لَيْسَ دُونَهَا سَحَابٌ ‏"‏‏.‏ قَالُوا لاَ يَا رَسُولَ اللَّهِ‏.‏ قَالَ ‏"‏ فَإِنَّكُمْ تَرَوْنَهُ كَذَلِكَ، يَجْمَعُ اللَّهُ النَّاسَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ فَيَقُولُ مَنْ كَانَ يَعْبُدُ شَيْئًا فَلْيَتَّبِعْهُ‏.‏ فَيَتْبَعُ مَنْ كَانَ يَعْبُدُ الشَّمْسَ الشَّمْسَ، وَيَتْبَعُ مَنْ كَانَ يَعْبُدُ الْقَمَرَ الْقَمَرَ، وَيَتْبَعُ مَنْ كَانَ يَعْبُدُ الطَّوَاغِيتَ الطَّوَاغِيتَ، وَتَبْقَى هَذِهِ الأُمَّةُ فِيهَا شَافِعُوهَا ـ أَوْ مُنَافِقُوهَا شَكَّ إِبْرَاهِيمُ ـ فَيَأْتِيهِمُ اللَّهُ فَيَقُولُ أَنَا رَبُّكُمْ‏.‏ فَيَقُولُونَ هَذَا مَكَانُنَا حَتَّى يَأْتِيَنَا رَبُّنَا فَإِذَا جَاءَنَا رَبُّنَا عَرَفْنَاهُ فَيَأْتِيهِمُ اللَّهُ فِي صُورَتِهِ الَّتِي يَعْرِفُونَ فَيَقُولُ أَنَا رَبُّكُمْ‏.‏ فَيَقُولُونَ أَنْتَ رَبُّنَا‏.‏ فَيَتْبَعُونَهُ وَيُضْرَبُ الصِّرَاطُ بَيْنَ ظَهْرَىْ جَهَنَّمَ، فَأَكُونُ أَنَا وَأُمَّتِي أَوَّلَ مَنْ يُجِيزُهَا، وَلاَ يَتَكَلَّمُ يَوْمَئِذٍ إِلاَّ الرُّسُلُ، وَدَعْوَى الرُّسُلِ يَوْمَئِذٍ اللَّهُمَّ سَلِّمْ سَلِّمْ‏.‏

 

Kutoka kwa ‘Atwaa’ bin Yaziyd Al-Laythiy kuwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Watu (yaani Maswahaba) walisema:  “Ee Rasuli wa Allaah! Je, tutamuona Rabb wetu Siku ya Qiyaama?” Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  akasema: ((Je, mna shida yoyote ya kuuona mwezi usiku ambao mwezi ni mpevu?)) Wakasema: “Hapana ee Rasuli wa Allaah.” Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Je, mna shida ya kuliona jua siku isiyokuwa na mawingu?)) Wakasema: “Hapana  ee Rasuli wa Allaah.”  Akasema: ((Hakika nyinyi mtamuona, kama hivyo. Allaah Atawakusanya watu wote Siku ya Qiyaamah, Naye Atasema: “Yeyote aliyekuwa akiabudu kitu (duniani) akifuate hicho (kitu)”  Kwa hiyo, yule aliyekuwa akiabudu jua atalifuata jua; na yeyote aliyekuwa akiuabudu mwezi ataufuata mwezi; na yeyote aliyekuwa akiabudu twaghuti  atamfuata twaghuti. Na utabakia Ummah huu peke yake na watu wake wazuri na wanafiki miongoni mwao)). Allaah Atakuja kwao na kusema: “Mimi Ndiye Rabb wenu.” Wao (watu watamkanusha) kwa kusema: “Hii ni sehemu yetu, nasi tutaketi hapa mpaka atakapokuja Rabb wetu. Pindi Atakapokuja tutamjua.” Kwa hivyo, Allaah Atakuja kwao katika Surah Yake ambayo wataijua, Naye Atasema: “Mimi Ndiye Rabb wenu.” Watu watasema: “Wewe Ndiye Rabb wetu.” Nao (watu) watamfuata. Kisha Asw-Swiraatw (Njia) itawekwa juu ya Moto (wa Jahannam).. Mimi na Ummah wangu tutakuwa wa kwanza kuivuka na hakuna atakayezungumza Siku hiyo isipokuwa Rusuli. Na Du‘aa ya Rusuli Siku hiyo itakuwa:

اللَّهُمَّ سَلِّمْ سَلِّمْ

 

Allaahumma Sallim (Ee Allaah! Jaalia salama, Jaalia salama)) [Al-Bukhaariy]

 

 

 



27-Sifa Akhlaaq Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Akiomba Kuishi Umasikini Na Kufishwa Pamoja Na Masikini Na Akinasihi Kuwa Karibu Nao

 

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

27-Akiomba Kuishi Umasikini Na Kufishwa Pamoja Na Masikini

Na Akinasihi Kuwa Karibu Nao

 

www.alhidaaya.com

 

عَنْ أَنَسٍ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ ‏"‏ اللَّهُمَّ أَحْيِنِي مِسْكِينًا وَأَمِتْنِي مِسْكِينًا وَاحْشُرْنِي فِي زُمْرَةِ الْمَسَاكِينِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ‏"‏ ‏.‏ فَقَالَتْ عَائِشَةُ لِمَ يَا رَسُولَ اللَّهِ قَالَ ‏"‏ إِنَّهُمْ يَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ قَبْلَ أَغْنِيَائِهِمْ بِأَرْبَعِينَ خَرِيفًا يَا عَائِشَةُ لاَ تَرُدِّي الْمِسْكِينَ وَلَوْ بِشِقِّ تَمْرَةٍ يَا عَائِشَةُ أَحِبِّي الْمَسَاكِينَ وَقَرِّبِيهِمْ فَإِنَّ اللَّهَ يُقَرِّبُكِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ‏"‏

Kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameomba: ((Ee Allaah Nijaalia uhai wa umaskini na nifishe nikiwa maskini na nifufue pamoja na kundi la masaakini Siku ya Qiyaamah)).  ‘Aaishah akasema: “Kwa nini ee Rasuli wa Allaah?”  Akasema: ((Hakika wao wataingia Jannah kabla ya matajiri kwa miaka arubaini. Ee ‘Aaishah usimrudishe maskini (bila kumpa kitu, umpe) hata kipande cha tende. Ee ‘Aaishah kurubiana nao kwani Allaah Atakukurubisha Siku ya Qiyaamah)) [At-Tirmidhiy]

 



085-Aayah Na Mafunzo: Jibriyl ('Alayhis-Salaam) Amekuja Kukufundisheni Dini Yenu

Aayah Na Mafunzo

Aal-‘Imraan

Jibriyl ('Alayhis-Salaam) Amekuja Kukufundisheni Dini Yenu

www.alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَمَن يَبْتَغِ غَيْرَ الْإِسْلَامِ دِينًا فَلَن يُقْبَلَ مِنْهُ وَهُوَ فِي الْآخِرَةِ مِنَ الْخَاسِرِينَ ﴿٨٥﴾

Na yeyote anayetaka dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitokubaliwa kwake; naye katika Aakhirah atakuwa miongoni mwa waliokhasirika. [Aal-'Imraan: 85]

 

 

 

Mafunzo:

 

Umar (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: Siku moja tulikuwa tumekaa na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) hapo alitokea mtu ambaye nguo zake zilikuwa nyeupe pepe na nywele zake zilikuwa nyeusi sana; hakuwa na alama ya machofu ya safari na wala hapakuwa na hata mmoja katika sisi aliyemtambua. Alienda akakaa karibu na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akaweka magoti yake karibu na magoti yake na akaweka viganja vyake juu ya mapaja yake kisha akasema; Ee Muhammad! Niambie kuhusu Uislamu.  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Uislamu ni kukiri laa ilaaha illa Allaah na kwamba Muhammad ni Rasuli wa Allaah. Na kusimamisha Swalaah, kutoa Zakaah, kufunga Swiyaam Ramadhwaan na kwenda kuhiji (Makkah) ukiweza.” (Akasema yule mtu yaani Jibriyl) Umesema kweli. Tulipigwa na mshangao kwa kumuuliza kwake Rasuli na kumsadikisha.  Na akasema tena: Niambie kuhusu Iymaan.  Akasema “Ni kumwamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Rasuli Wake na Siku ya Qiyaamah, na kuamini ya kuwa kheri na shari zinatoka Kwake.” (Akasema Jibriyl): Umesema kweli. Akasema hebu nielezee kuhusu Ihsaan.  Akasema: “Ni kumuabudu Allaah kama vile unamuona na kama humuoni basi Yeye Anakuona” Akasema (Jibriyl):  Niambie    kuhusu Qiyaamah.  Akajibu: “Muulizwaji si mjuzi kama asivyo vilevile Muulizaji.” Kisha akamwambia: Nijulishe alama zake: Akajibu: “Kijakazi atazaa bibi yake, na utaona wachunga wenda miguu chini, wenda uchi (wasio na uwezo wa kumiliki hata mavazi), mafukara (wasiokuwa hata na sehemu ya kuishi kwa umaskini) wakishindana kujenga majumba ya fahari.” Kisha akaondoka (Jibriyl) na nilitulia kidogo (nikitafakari). Kisha akasema: “Ee 'Umar! Je, unamjua ni nani yule aliyekuwa akiuliza?” Nikasema: Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi.  Akasema: “Ni Jibriyl, alikuja kuwafundisha Dini yenu.” [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 



058-Asbaabun-Nuzuwl: Suwrah Al-Mujaadalah: Aayah 14

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

058-Suwrah Al-Mujaadalah: Aayah 14

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ تَوَلَّوْا قَوْمًا غَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِم مَّا هُم مِّنكُمْ وَلَا مِنْهُمْ وَيَحْلِفُونَ عَلَى الْكَذِبِ وَهُمْ يَعْلَمُونَ﴿١٤﴾

14. Je, hukuona wale waliofanya urafiki na watu ambao Allaah Ameghadhibika nao, wao si miongoni mwenu na wala si miongoni mwao na wanaapia uongo nao wanajua.

 

أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُمْ عَذَابًا شَدِيدًا ۖ إِنَّهُمْ سَاءَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿١٥﴾

15. Allaah Amewaandalia adhabu kali, hakika uovu ulioje waliyokuwa wakiyatenda.

 

 

Sababun-Nuzuwl: 

  ثنا محمد بن جعفر ثنا شعبة عن سماك بن حرب عن سعيد بن جبير عن ابن عباس قال: قال رسول الله صلى الله عليه وعلى آله وسلم: "يدخل عليكم رجل ينظر بعين شيطان أو بعيني شيطان". قال فدخل رجل أزرق فقال: يا محمد علام سببتني أو شتمتني أو نحو هذا قال وجعل يحلف، قال: ونزلت هذه الآية في المجادلة ((وَيَحْلِفُونَ عَلَى الْكَذِبِ وَهُمْ يَعْلَمُونَ)) والآية الأخرى.

 

Ametuhadithia Muhammad bin Ja’far, ametuhadithia Shu’bah toka kwa Simaak bin Harb toka kwa Sa’iyd bin Jubayr toka kwa Ibn ‘Abbaas amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Atawajieni mtu anayeangalia kwa jicho la shaytwaan au macho mawili ya shaytwaan)). Akasema: Akaingia mtu wa kibuluu akasema: Ee Muhammad! Umenitukania nini au umenitusia nini, au mfano wa hivi. Akasema: Akaendelea kuapa, na ikashuka Aayah hii katika Al-Mujaadalah:

 

أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ تَوَلَّوْا قَوْمًا غَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِم مَّا هُم مِّنكُمْ وَلَا مِنْهُمْ وَيَحْلِفُونَ عَلَى الْكَذِبِ وَهُمْ يَعْلَمُونَ﴿١٤﴾

 

Je, hukuona wale waliofanya urafiki na watu ambao Allaah Ameghadhibika nao, wao si miongoni mwenu na wala si miongoni mwao na wanaapia uongo nao wanajua.

 

أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُمْ عَذَابًا شَدِيدًا ۖ إِنَّهُمْ سَاءَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿١٥﴾

Allaah Amewaandalia adhabu kali, hakika uovu ulioje waliyokuwa wakiyatenda.

 

Hadiyth hii ameitaja vile vile katika ukurasa wa 267 na ukurasa 350. Al-Haythamiy amesema katika Majma’u Az Zawaaid kuwa Ahmad na Al-Bazzaar wameisimulia, na wapokezi wake wote ni watu wa kuaminika wasio na shaka yoyote, lakini katika Hadiyth hii inaeleza kuwa Rasuli ndiye aliyemwambia (mtu huyo): ((Unanitukania nini wewe na wenzako?)) [Al-Musnad ukurasa wa 267 na 350. Al-Haakim ameikhariji katika Al-Mustadrak katika mjeledi wa pili ukurasa wa 482. Amesema: Hii ni Hadiyth Swahiyh kwa sharti ya Muslim, na wao hawakuikhariji, na Ibn Jariyr katika mjeledi wa pili ukurasa wa 25]

 

Katika Muwattwa Maalik:  Kitaab An Nudhuwr Wal Iymaan:

 

حَدَّثَنِي يَحْيَى، عَنْ مَالِكٍ، عَنْ هِشَامِ بْنِ عُرْوَةَ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ عَائِشَةَ أُمِّ الْمُؤْمِنِينَ، أَنَّهَا كَانَتْ تَقُولُ لَغْوُ الْيَمِينِ قَوْلُ الإِنْسَانِ لاَ وَاللَّهِ بَلَى وَاللَّهِ ‏.‏ قَالَ مَالِكٌ أَحْسَنُ مَا سَمِعْتُ فِي هَذَا أَنَّ اللَّغْوَ حَلِفُ الإِنْسَانِ عَلَى الشَّىْءِ يَسْتَيْقِنُ أَنَّهُ كَذَلِكَ ثُمَّ يُوجَدُ عَلَى غَيْرِ ذَلِكَ فَهُوَ اللَّغْوُ ‏.‏ قَالَ مَالِكٌ وَعَقْدُ الْيَمِينِ أَنْ يَحْلِفَ الرَّجُلُ أَنْ لاَ يَبِيعَ ثَوْبَهُ بِعَشَرَةِ دَنَانِيرَ ثُمَّ يَبِيعَهُ بِذَلِكَ أَوْ يَحْلِفَ لَيَضْرِبَنَّ غُلاَمَهُ ثُمَّ لاَ يَضْرِبُهُ وَنَحْوَ هَذَا فَهَذَا الَّذِي يُكَفِّرُ صَاحِبُهُ عَنْ يَمِينِهِ وَلَيْسَ فِي اللَّغْوِ كَفَّارَةٌ ‏.‏ قَالَ مَالِكٌ فَأَمَّا الَّذِي يَحْلِفُ عَلَى الشَّىْءِ وَهُوَ يَعْلَمُ أَنَّهُ آثِمٌ وَيَحْلِفُ عَلَى الْكَذِبِ وَهُوَ يَعْلَمُ لِيُرْضِيَ بِهِ أَحَدًا أَوْ لِيَعْتَذِرَ بِهِ إِلَى مُعْتَذَرٍ إِلَيْهِ أَوْ لِيَقْطَعَ بِهِ مَالاً فَهَذَا أَعْظَمُ مِنْ أَنْ تَكُونَ فِيهِ كَفَّارَةٌ ‏.‏

Amenihadithia Yahyaa toka kwa Maalik toka kwa Hishaam bin ‘Urwah toka kwa baba yake toka kwa ‘Aaishah Mama wa Waumini kwamba alikuwa anasema: “Laghwu Al-Yamiyn”, ni mtu kusema: “Laa Wa-Allaahi, Balaa Wa-Allaahi”  Maalik kasema: Zuri zaidi nililolisikia kuhusiana na hili ni kuwa “Al-Laghw” ni kiapo cha mtu juu ya kitu ambacho ana uhakika kuwa kiko hivyo kisha kinakutwa kinyume na hivyo, basi hiyo ni “Al-Laghwu”. Maalik kasema: Na kufunga kiapo ni mtu kuapa kuwa hatouza nguo yake kwa dinari kumi, kisha akaiuza kwa bei hiyo, au kuapa kuwa lazima atampiga kijana wake, kisha asimpige na mfano wa hivi. Kiapo hichi ndicho ambacho mwapaji hukitolea kafara, lakini katika “Al-Laghw” hakuna kafara. Maalik amesema: Ama yule anayeapia kitu naye anajua kuwa ni mwenye kufanya dhambi, na anaapia la uongo huku anajua ili kumridhisha kwao mtu, au kuomba udhuru kwao kwa mkosewa, au kudhulumu kwao mali, basi hiki ni kikubwa zaidi kuweza hata kuwa na kafara ndani yake.

 



028-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kuvumiliana Tabia Mbaya Katika Maisha Ya Ndoa Kwa Kukumbuka Tabia Zilizo Nzuri

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 28

Kuvumiliana Tabia Mbaya Katika Maisha Ya Ndoa Kwa Kukumbuka Tabia Zilizo Nzuri

www.alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((لاَ يَفْرَكْ مُؤْمِنٌ مُؤْمِنَةً إِنْ كَرِهَ مِنْهَا خُلُقًا رَضِيَ مِنْهَا آخَرَ))  مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Muumin [mume] asimchukie Muumin [mke]. Asipompendelea kwa tabia fulani ataridhika naye kwa tabia nyingine)) [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Hakuna binaadamu aliyekamilika kwa tabia njema. Kila mmoja ana kasoro zake; huenda zikawa ni tabia zinazolingana; nzuri au mbaya. 

 

 

2. Kuishi pamoja kunadhihirisha tabia baina ya watu.

 

 

3. Inapasa kuvumiliana katika maisha ya ndoa, kwani kila mmoja ni mtihani kwa mwenziwe. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَجَعَلْنَا بَعْضَكُمْ لِبَعْضٍ فِتْنَةً أَتَصْبِرُونَ ۗ وَكَانَ رَبُّكَ بَصِيرًا ﴿٢٠﴾

Na Tumejaalia baadhi yenu nyinyi kwa nyinyi kuwa ni majaribio je mtasubiri? Na Rabb wako ni Mwenye kuona daima. [Al-Furqaan: 20]

 

 

4. Uislamu unamsisitiza mume kumfanyia wema mke.

 

Rejea: An-Nisaa (4: 19).

 

Rejea pia Hadiyth namba (29).

 

 

5. Hadiyth hii ni suluhisho mojawapo la kutatua matatizo baina ya mume na mkewe.

 

Rejea An-Nisaa (4: 128).

 

 

6. Inasisitizwa Muislamu kuchagua mke mwema, kwani ndio sababu ya furaha yake duniani na Aakhirah.

 

Rejea Hadiyth namba (35), (40).

 

 

7. Hii Hadiyth inamtaka mume awe makini wala asichukue hatua za haraka kama talaka ambayo huenda ikamletea majuto.

 



20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...