Translate

Ijumaa, 1 Februari 2019

Kitaab-ul-Buyu´ 01



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2DOoHKU
via IFTTT

al-Ikhlaasw



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2MLei5q
via IFTTT

al-Falaq



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2DNe6jv
via IFTTT

Namna ya kujibu salamu ya kafiri

Swali: Akikujia kafiri na akaanza kukutolea salamu. Je, inafaa kumrudishia kwa kusema “wa ´alayakas-Salaam”? Ni vipi mtu amjibu? Je, inajuzu kwa mtu kuanza kumtolea salamu? Ni yepi maoni yako?

Jibu: Haijuzu kuanza kumtolea kafiri salamu kwa kumwambia: “as-Salaam ´alaykum”. Lakini akitutolea salamu basi mjibu kwa tamko lifuatalo “wa ´alayakum”. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndivo kaamrisha inapokuja kwa mayahudi na manaswara. Mbali na hawa wana hukumu moja kama wao kama wao watakuwa sio duni kuliko wao.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2SnaI6Q
via IFTTT

Mtu amewalaani wazazi wake wawili

Swali: Ni ipi hukumu ya mtu mwenye kuwalaani wazazi wake wawili kwa sababu ya hasira au akawalaani kwa kukusudia? Je, laana hiyo – ni mamoja kwa kukusudia au pais na kukusudia – ina kafara? Je, afanye nini aliyelaani?

Jibu: Kuwalaani wazazi wawili ni katika madhambi makubwa. Kwani imethibiti kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amemlaani yule mwenye kuwalaani wazazi wawili. Ni mamoja kuwalaani huko ikawa ni moja kwa moja au mtu yeye ndiye amesababisha. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliulizwa:

“Hivi kweli mtu atawalaani wazazi wake wawili?” Akajibu: “Ndio. Ni pale ambapo atamtusi baba wa mwingine na yeye amtukanie baba yake na amtukanie mama yake na yeye amtukanie mama yake.”

Kwa hivyo kuwatukana wazazi wawili – ni mamoja mtu amefanya hivo moja kwa moja au amesababisha – ni dhambi kubwa. Hakuna tofauti hayo yametokea pasi na sababu au kwa sababu ya hasira. Isipokuwa kuhusiana na hasira mtu hasira ikimfikisha kiwango cha kwamba hajui kile anachokisema, katika hali hiyo hana dhambi. Kwa sababu hakitambui anachokisema. Allaah anamlipa mja kwa kile anachokitambua na si kwa kile asichokitambua. Pamoja na kwamba inatakiwa kwa mtu pale anapokuwa na hasira au kama yeye ni mwenye kushikwa na hasira haraka, basi afanye sababu zinazomwondosha katika hali hiyo au kumpunguzia. Kwa sababu kuna mtu alimuomba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amuusie ambapo akamwambia:

“Usikasirike!”

Akakariri ausiwe akamwambia:

“Usikasirike!”

Mtu akihisi hasira basi aombe kinga dhidi ya shaytwaan aliyefukuzwa na atawadhe. Kwani hayo ni miongoni mwa sababu zinazoondosha hasira. Miongoni mwa sababu vilevile mtu aondoke na aende mbali na hasimu wake ili kusitokee kitu katika madhara.

Swali: Upande wa tawbah inakubaliwa tawbah yake?

Jibu: Kuhusiana na tawbah yuko na tawbah. Hakuna dhambi yoyote isipokuwa ikiwa na tawbah. Amesema (Tabaarak wa Ta´ala):

قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَى أَنْفُسِهِمْ لا تَقْنَطُوا مِنْ رَحْمَةِ اللَّهِ إِنَّ اللَّهَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعاً إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ

“Sema: “Enyi waja Wangu ambao mmepindukia juu ya nasfi zenu: “Msikate tamaa na rehema za Allaah. Kwani hakika anasamehe madhambi yote. Kwani hakika Yeye ni mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu.” (39:53)

Lakini ilipokuwa dhambi hii inahusiana na haki ya kiumbe basi ili tawbah iweze kusili basi ni lazima amuombe msamaha yule aliyemfanyia vibaya ili tawbah yake iweze kutimia.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2GdcSQ9
via IFTTT

Inafaa kumpiga mnyama?

Swali: Sisi tunaishi kwenye kijiji chenye milima na kinachotisha sana na mara nyingi tunatumia wanyama kama vipando kwenda huku na kule. Mfano wa wanyama hao ni ngamia, punda, nyumbu na wengineo. Ni mamoja tunapoenda masomoni ambayo yako mbali kidogo na kijiji chetu kwa takriban 10 km. Tunawapiga kipigo cha kuumiza ili waweze kutembea na wachapue kwenda masomoni. Ni ipi hukumu ya kuwapiga wanyama ili wachapue na masafa yawe mafupi au kumpiga kwa kukusudia? Kwa sababu nimesoma Hadiyth kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba wanyama watamlipiza kisasi mtu siku ya Qiyaamah. Tunaomba faida na Allaah akujaze kheri.

Jibu: Hapana shaka kwamba wanyama wana roho na hisia. Wanaumia na wanahisi ugumu na uzito kwa yale yenye kushinda uwezo wao. Hivyo haifai kwa muislamu kumbebesha mnyama asichokiweza. Ni mamoja kitu hicho kiwe kinabebwa mgongoni mwake, kitu anachokibeba kwenda mahali fulani asipoweza au hali nyinginezo ambazo hawezi.

Kuhusu kumpiga inafaa wakati wa haja kwa sharti asimuumize. Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kupitia kwa Jaabir kuhusu kisa cha ngamia ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikutana naye na ndani yake imetajwa kwamba alikuwa akimpiga ngamia. Kimsingi ni kwamba kuwapiga wanyama, midhali mtu hawaumizi, inafaa. Dalili katika Sunnah ni Hadiyth ya Jaabir. Ama ikiwa ni pasi na haja, ikawa ni kipigo cha kuumiza au ikawa ni kipigo kitachomfikisha mnyama katika jambo zito kwake, hapo haitofaa.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2TosOCJ
via IFTTT

Vibao vilivyoandikwa (الله) na (محمد)

Jengine ni kwamba vibao vilivyoandikwa “Allaah” na pembezoni mwake “Muhammad” ni aina fulani ya ushirikiano na kumlinganisha Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), jambo ambalo halifai. Kuna mtu alisema kumwambia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

ما شاء الله وشئت

“Akitaka Allaah na wewe.”

 Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema:

“Je, umenifanya kuwa mshirika wa Allaah? Sema: “Akitaka Allaah pekee.”



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2MGEtdA
via IFTTT

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...