Translate
Jumatatu, 28 Januari 2019
Mume afanye nini ikiwa mkewe hataki kuswali?
*Swali*
Mume achukue hatua gani ikiwa mke hataki kuswali?
*Jibu*
✅Mara nyingi kama vile wanawake wanashindwa kufuata maagizo ya kuchagua mume wa sawa Kidini ndivyo wanaume wanavyofanya makosa hayo hayo.
➡Mume wa Kiislamu anatakiwa amchague mke mwenye Dini na Imani, maadili na tabia nzuri.
✅Kukosa kufuata maagizo hayo ya Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ndio kunatokea matatizo kama hayo.
➡Hata hivyo, kosa lishatokea na inabidi tupate suluhisho kwa suala hilo nyeti.
➡Kulingana na maelezo yako ni kuwa mkeo inaonyesha bado ana Uislamu na Imani, hivyo anataka msukumo wa kuweza kutekeleza wajibu huo bila ya tatizo.
➡Jambo ambalo unatakiwa mwanzo kabisa kufanya ni kumnasihi mkeo kwa njia nzuri, kwani Allaah (Subhaana wa Taala) Anatuambia⤵
“Waite waelekee kwenye Njia ya Mola wako Mlezi kwa hikima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora”
↪Rejea Qur'an 16: 125.
➡Inatakiwa utumie mbinu tofauti za kuweza kumvutia katika kuswali bila ya yeye kuwa na kinyongo juu ya suala hilo.
➡Mpatie vipeperushi kuhusu umuhimu wa Swalah na madhara ya kuacha, vitabu, kanda, kaseti na njia nyingine.
✅Ikiwa imeshindikana hilo, itabidi sasa uingize mkono wa wazazi wenu kama inavyotaka sheria.
➡Allaah (Subhaana wa Taala) Anasema kwamba⤵
“Na ambao mnachelea kutoka katika utiifu wanasihini, muwahame katika malazi na wapigeni. Wakikutiini msiwatafutie njia ya kuwaudhi bure. Hakika Allaah ndiye Aliye juu na Mkuu. Na mkichelea kutakuwapo mfarakano baina ya mke na mume basi pelekeni muamuzi kutokana na jamaa za mume, na muamuzi kutokana na jamaa za mke. Wakitaka mapatano Allaah Atawawezesha. Hakika Allaah ni Mjuzi Mwenye khabari”
↪Rejea Qur'an 34 – 35.
➡Hivyo Mume inatakiwa ufuate mfumo ufuatao⤵
1⃣Kuwanasihi katika ya haki na ukweli.
2⃣Mhame(Jitenge naye katika Kitanda) katika malazi.
3⃣Mpige mkeo kipigo ambacho hakitamuumiza bali cha kumtisha wala usimpige uso.
4⃣Kuwe na suluhisho kwa kutumia waamuzi kutoka upande wa mke na mume ili waamue hilo.
✅Ikiwa hakukupatikana suluhisho lolote na wala mkeo hakubadilika basi itabidi umuache.
➡Na ikiwa itatokea hilo itabidi usirudie kosa tena unapotaka kuoa mwingine. Hata hivyo, tunaamini kuwa haitofikia hapo, In Shaa Allaah
Na Allaah Anajua zaidi
Imeandaliwa na *Imaam Masjid Tawbah*
from fisabilillaah.com http://bit.ly/2CL0y68
via IFTTT
Hukmu ya Mke Asiyeswali
SWALI
Ni ipi hukmu ya mke asiyeswali, kwa kutambua kuwa nimeshambainishia adhabu anayopata mwenye kuacha kuswali, kuna baadhi ya nyakati anaswali na wakati mwengine anaacha. Kwa mfano anaswali Adhuhuri na anaacha (Swalaah) zote za Faradhi zilizobaki?
JIBU
Hukmu yake ni Kafiri.
Na haijuzu kuendelea kubaki naye katika hifadhi yako. Inapasa kuwa naye mbali, isipokuwa kama atatubu tawbah ya kweli, la sivyo, ni waajib kuwa naye mbali (kuachana naye).
Kwa sababu kuacha Swalaah ni ukafiri mkubwa.
Anasema Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
“Baina ya mtu na baina ya ushirikina na ukafiri ni kuacha Swalaah.” [Muslim]
Na anasema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
“Agano (Kinachotutofautisha) baina yetu (Waumini) na baina yao (Washirikina, Makafiri na Wanafiki) ni Swalaah, anayeiacha (Swalaah) amekufuru.” [At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na An-Nasaaiy]
Hii ndio kauli sahihi katika kauli za Wanachuoni; kwamba kuiacha (Swalaah) ni ukafiri mkubwa.
Na Allaah anajua zaidi
from fisabilillaah.com http://bit.ly/2WqkhkE
via IFTTT
Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe
Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake.
Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika Swahiyh yake wenye kichwa cha habari, “Elimu Kabla Ya ‘Amali”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.
Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo.
Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi, kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema:
“Wakikutiini, basi msiwatafutie njia” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii inamaanisha kuwa lau wake zenu watakutiini kwa mnayowaamrisha basi msiwatafutieni njia za kuwadhuru.
Na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
“Mbora wa wanawake wote ni yule ambaye unapomuangalia hukufurahisha, na unapomuamrisha hukutii na unapokuwa haupo naye, hukulindia nafsi yake na mali yako” (Abu Daawuud).
Hivyo, mke wako anafaa kishari’ah awe ni mwenye kukutii na asiwe ni mwenye kutoka bila ya ruhusa yako.
Na Allaah Anajua zaidi
from fisabilillaah.com http://bit.ly/2RlWxKT
via IFTTT
20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah
إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! 20 - Isti’aadhah (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah ...
-
إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! 20 - Isti’aadhah (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah ...
-
Dalili 18 zinazoashiria una ujauzito wa mtoto wa kiume Awali ya yote nitoe pongezi kwa mama K na Baba K wote popote walipo kwa kazi nzuri ...