Translate

Alhamisi, 6 Agosti 2020

Je wanawake huwa wanataka mwanaume adumu muda gani kitandani

Je wanawake huwa wanataka mwanaume adumu muda gani kitandani

Watu wengi wamekuwa wakiamini kwamba mwanaume anapochelewa sana kufika kileleni basi ndiyo tendo la ndoa linakuwa tamu jambo ambalo si kweli.

Umekuja hapa ukitafuta jibu la swali hili na usijifikirie upo peke yako ambaye umekuwa ukitaka kujuwa jibu la swali hili – ni wengi wamekuwa wakiniuliza mara kwa mara na leo nimeona niwatolee uvivu niwajibu wote kwa kirefu

Nikuambie tu mapema huwezi kuipata elimu kama hii popote shuleni wala chuoni ila hapa kwa bahati nzuri umeipata na unaweza kunizawadia chochote ikiwa maelezo haya yatakusaidia kuboresha maisha yako kwa namna moja au nyingine.

Tafiti mbalimbali zinasema wastani wa karibu ya zaidi ya asilimia 90 ya wanaume kote duniani hufika kileleni ndani ya dakika 2 mpaka 3.

Wapo baadhi ya wanaume wao wanawahi sana kiasi huwezi kuamini.

Yaani ni sekunde kadhaa tu tayari wazungu hao.

Na wengine wanadai yaani kile kitendo cha kumkumbatia tu mwanamke na kuhisi joto lake tayari ameshakojoa na mbaya zaidi hawezi kusimama tena mpaka kesho!

Hapa tunazungumzia muda ule ambao tayari kitendo kimeanza kufanyika kama ni kifo cha mende basi tayari mzee yupo juu ya ulingo!

Hatuhesabu muda wa maandalizi (foreplay).

Wanawake wengi wanajali sana muda wa maandalizi kuliko muda wa tendo lenyewe.

Kama unaweza kutumia dakika 40 kumuandaa mwanamke na ukamwingilia kwa dakika 10 kwake hapo utakuwa umefanya jambo la maana zaidi kuliko ungemwandaa dakika 10 na kumwingilia kwa dakika 40.

Wanawake ni watu wa hisia na ni jukumu lako kuhakikisha hisia zake zipo sehemu sahihi.

Je wanawake huwa wanataka mwanaume atumie muda gani kitandani?

Jibu la haraka ni kuwa wanawake wanapenda mwanaume atumie muda usiopungua dakika 13 katika tendo la ndoa.

Unaweza ukashangaa kusikia hivi na ukisoma dakika 13 unaweza kufikiri ni chache lakini ni nyingi sana hizo katika ule mchezo.

Kwa kawaida mwanaume anapoanza uhusiano mpya na mwanamke mpya anakuwa na hamasa na nguvu na shauku nyingi ya kutaka kushiriki naye tendo la ndoa lakini kwa bahati mbaya kadri siku zinavyozidi kwenda ndani ya huo uhusiano pole pole mwanaume huanza kupungua hiyo shauku na tamaa.

Ndiyo sababu watu wa jinsia zote mbili tunahimizwa ubunifu na kutafuta mbinu mpya kila mara katika uhusiano ili kuleta hamasa zaidi katika kitengo hiki cha kitandani.

Kwahiyo kinamama mliopo kwenye ndoa miaka mitano au kumi au zaidi msije mkafikiri mwanaume wa uchumba ndiyo mwanaume wa kwenye ndoa, hapana hapo utakuwa umechemka ndoa haiendi hivyo.

Kumbuka wakati wa uchumba hakuwa na majukumu kama aliyonayo sasa kwahiyo nguvu zake na vipaumbele vyake haviwezi kuwa sawa sasa na wakati ule wa uchumba au wakati mnaanza tu maisha ya ndoa.

Kuna uwezekano wakati wa uchumba mwanaume akawa na nguvu sana wakati wa tendo la ndoa na uwezo huo ukashuka hata zaidi ya nusu miaka kadhaa baadaye baada ya ndoa.

Miaka mitano au kumi baada ya ndoa kuna uwezekano mna mtoto au watoto tayari na ni jukumu kuu la baba kuhakikisha watoto wanakula vizuri, wanalala sehemu nzuri, wanaenda shule, wanaandaliwa pesa ya matibabu pembeni na kadharika.

Majukumu yote hayo humuondolea mwanaume hamasa, nguvu na uwezo wake wa awali wa kushiriki tendo la ndoa.

Kwahiyo ni jambo la kawaida kwa mwanaume kupungua uwezo wake wa awali wa kushiriki tendo la ndoa miaka kadhaa baada ya ndoa. Ni jambo la kawaida mwanamke mwenye akili tambua hilo na uishi kwa adabu na mmeo.

Ukiacha majukumu kuongezeka ni kwamba mwanaume anaona wewe mkewe upo hapo kila siku masaa 24 akikutaka anakupata muda wowote.

Sasa hiyo lazima itampungumzia hamasa tofauti na mwanzo mkiwa wachumba ulipokuwa unampa kwa nadra au mara chache tena kwa kuibana.

Kwa sasa anayo yote hapo hapo kwanini atumie nguvu nyingi wakati na baadaye na baadaye tena na baadaye tena na kesho ipo hapo hapo inamsubiri.

Kwahiyo wanaume wengi zaidi ya asilimia 90 wanafika kileleni ndani ya dakika 2 mpaka 3 dunia nzima siyo hapa Tanzania tu.

Utafiti mmoja uliofanywa na jarida liitwalo Journal of sexual medicine mwaka 2005 uliowahoji wataalamu wengi wa elimu ya tendo la ndoa (sex therapists) ulibaini kuwa wanawake wanachukulia muda mwanaume anaoweza kushiriki tendo la ndoa katika makundi yafuatayo:

a)Dakika 1 mpaka 3  > ni muda mchache mno. Lazima atakudharau

b)Dakika 3 mpaka 7 > muda wa wastani. Anakuona una afya

c)Dakika 7 mpaka 13 > Muda mzuri kwao. Anafurahi na kukuheshimu

d)Dakika 13 mpaka 25 > Muda MZURI SANA lazima atakuwa anakupa zawadi mara kwa mara

e)Dakika 25 kwenda juu > muda mrefu sana na ni kero kwao na anaweza kusitisha mahusiano na wewe.

Wanawake wengi wanaweza kuwa wamefika kileleni muda wowote kuanzia dakika ya 8 kwenda juu tangu uanze kumwingia (siyo kumuandaa).

Kwahiyo chochote chini ya dakika 7 kuna uwezekano mkubwa ukamuacha njiani na asifurahie chochote.

Kuna jamaa anataka kucommnet hapo chini kuwa huwa anaenda dakika 40 au 60 vizuri tu kwahiyo mimi niache uongo.

Ni kweli unaweza kuwa upo sahihi hasa kama unashiriki tendo la ndoa na wanawake wasiojitambuwa wala hawajuwi thamani yao.

Mwanamke anayejitambuwa na kujuwa thamani yake haweza kukubali uende dakika 40. Atakumabia tu hapana imetosha hapo basi. Ila yule asiyejitambua atakaa tu kimya kukusubiri wewe umalize kulima shamba muda wote huo utadhani huna kazi zingine za mhimu za kufanya.

Kuna wanawake wa aina mbili. Wanawake wanaojitambua na wasiojitambuwa.

Wasiojitambua ukimwambia geukia huku anageuka, pandisha kule anapandisha, zunguka hivi anazunguka yaani lolote utakalomwambia au kumfanya yeye sawa tu hata kama anaumia.

Wanaojitambuwa hawezi kukubali kila unachomwamuru. Vingine atakuambia mhhh hapana mzee hilo siwezi au hilo hapana.

Kwahiyo kama huwa unaenda dakika 40 au 60 au masaa mawili huenda huwa umekutana na wale aina ya pili – wasiojitambuwa wala kujuwa thamani yao.

Hata wale wanawake wanaojiuza ukizidisha sana muda anakuambia wazi utaongeza hela au kama inashindikana chukua hela yako ondoka usinipotezee mimi muda!

Wanaume mtambuwe kila goli moja unalopiga unatoa mbegu Zaidi ya milioni 200 toka mwilini mwako na tendo hilo linauchosha sana mwili wako kuliko mwili wa mwanamke.

Ndiyo sababu wanaume wengi hutangulia kufa kabla ya wanawake.

Goli moja ni sawa na kazi ya kutembea kwa miguu kilomita 27.

Kwahiyo utaona wazi ni jinsi gani ukiendekeza tendo hilo unavyoweza kujidhuru afya yako bila mwenyewe kujuwa.

Wanawake ni watu wa hisia, kuwa bize zaidi kujenga hisia zake na siyo kutaka kushiriki naye tendo la ndoa na mtu hayupo hapo kifikra.

Na baadhi ya wanaume wana akili ndogo sana eti huwa wanawaza wanaweza kumkomoa mwanamke wakati wa tendo la ndoa kwa kufanya muda mrefu na kwa nguvu utadhani ugomvi wakati ni starehe.

Tambua huwezi kumkomoa mwanamke. Unajikomoa mwenyewe.

Unakuta mwanaume anatumia vilevi vikali na vyenye kuharibu afya yake na mwingine yupo bize kumeza vidonge vya kizungu ili tu eti akamkomoe mwanamke kitandani!

Huwezi kumkomoa mwanamke, unajikomoa mwenyewe na wewe ndiyo utaharibikiwa afya yako ukiendelea na huo ujinga.

Kumbuka wewe mwenyewe umezaliwa na mwanamke sasa sijuwi una ukubwa gani wa kumshinda mtoto anayezaliwa!

Shida moja ya baadhi ya wanaume wanaposhiriki tendo la ndoa ni kuwa wanajiwaza wao, wao wanajiona ndiyo madereva na wake zao ni abiria.

Mapenzi ni two way systems. Mapenzi ni njia mbili, wewe na yeye.

Kaa karibu na mkeo, mshirikiane mnaposhiriki tendo la ndoa, kila mmoja awe tayari na aonyeshe uhitaji na uwepo.

Usishiriki na mwenza wako tendo la ndoa, bali MSHIRIKI na mwenza wako tendo la ndoa.

Unao uwezo wa kumwambia mapema kabisa mkitaka kuanza kushiriki kwamba; ndugu mwenzio leo najiona wazi nitawahi sana hivyo usishangae.

Hakuna mwanaume anayeweza kuchelewa kila siku au kila mara atakaposhiriki tendo la ndoa. Inawezekana ana uchovu mwingi muda huo au na mawazo fulani yanamtatiza au hajapata chakula muda mrefu na kadharika.

Mwanaume kadharika mwanamke muulize mwenzio anapendaje, anatakaje, kipi kinamwamsha zaidi na kipi hapendi kabisa. Mwanaume usijichukulie madaraka na ufahamu wote peke yako.

Je wewe ni mwanaume na umekuwa ukisumbuliwa na tatizo la kuwahi sana kufika kileleni kwa muda mrefu? Kama jibu ni ndiyo pata suluhisho la tatizo lako kwa kubonyeza HAPA.

Mjulishe pia rafiki yako kwenye twitter naye asome post hii kwa kubonyeza maneno yafuatayo;

Je wanawake huwa wanataka mwanaume adumu muda gani kitandani Click To Tweet

Share na wengine uwapendao

Fadhili Paulo
Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
Imesomwa mara 140

Imehaririwa mwisho

Let's block ads! (Why?)

Jumatano, 29 Julai 2020

Ulaji wa chipsi umetajwa kuwa hatari kwa afya ya binadamu

ULAJI WA CHIPS umetajwa kuwa HATARI kwa afya ya Binadamu.

ULAJI WA CHIPS umetajwa kuwa HATARI kwa afya ya Binadamu, kwani husababisha maradhi mengi yasiyo ya kuambukiza hasa FIGO, MOYO , SHINIKIZO LA DAMU,KISUKARI NA SARATANI za aina zote.

SAHANI moja ya CHIPS kavu huwa na MAFUTA yanayokaribia NUSU kikombe cha CHAI ambayo ni sawa na ujazo wa mililita 250.

Kwahiyo WALAJI wengi wa CHIPS wapo katika HATARI ya kutengeneza SUMU kwenye MIILI yao bila kujua.

UTAFITI unaonyesha WATU wengi hupendelea KULA chips mayai, kuku, soseji au hata kwa mishikaki maana yake ni kwamba KIWANGO hicho cha MAFUTA huzidi kwa sababu na vyenyewe huwa VIMEKAANGWA.

JAMBO la KUSIKITISHA ni kwamba WAFANYABIASHARA wengi wamekuwa hawazingatii UMUHIMU wa kutumia MAFUTA mara moja katika kukaanga VITU hivyo.

WENGI huwa wanapikia MAFUTA kwa zaidi ya mara mbili na hivyo kuzidisha HATARI zaidi.

“Wanazidisha HATARI kwa sababu… kawaida MAFUTA yanapaswa KUPIKIWA mara moja. Kadri unavyounguza MAFUTA ndivyo ambavyo ule MFUMO wa MAFUTA MASAFI ambayo yanatakiwa kwa MWILI wa MWANADAMU unabadilika na kuwa MACHAFU, maana yake ni kwamba unapopikia MAFUTA zaidi ya mara mbili tayari yanakuwa yametengeneza SUMU ambayo haitakiwi MWILINI ,”

MAFUTA ambayo yametumika kukaangia VYAKULA zaidi ya mara mbili hubadilika na kutengeneza UTANDO MWEUPE ambao huweza kuonekana iwapo MTU atayatazama kwa MACHO yake.

Ule UTANDO MWEUPE utakaouona unatoa ISHARA kwamba MAFUTA hayo HAYAFAI kwa MATUMIZI ya BINADAMU, lakini WATU wanataka kufanya BIASHARA hivyo huendelea KUYATUMIA bila KUJALI au pengine KUTOKUJUA kwamba wanaziweka AFYA za WALAJI katika HATARI ya kupata MAGONJWA .”

PAMOJA na KIWANGO hicho cha MAFUTA ambacho huingia MWILINI kwa ULAJI wa SAHANI moja pekee ya CHIPSI kavu, MLAJI hula CHUMVI nyingi iliyopo ndani ya NYANYA maalumu iliyosagwa (tomato).

TOMATO SAUCE jinsi ilivyotengenezwa ina CHUMVI nyingi, sasa umekula MAFUTA mengi jumlisha na hiyo CHUMVI nyingi na ninavyofahamu WALAJI wengi wa CHIPSI hupendelea KUSHUSHIA na KINYWAJI chenye SUKARI nyingi maana yake unakuwa umetengeneza SUMU ndani ya MWILI wako.

TAKWIMU zinaonesha kuwa idadi ya WAGONJWA wanaougua MAGONJWA yasiyokuwa ya KUAMBUKIZA nchini inaongezeka.

HATARI hii inaweza KUEPUKWA iwapo WATU watazingatia ULAJI unaofaa.

Ulaji wa chipsi umetajwa kuwa hatari kwa afya ya binadamu 1

WENGI hatuzingatii ULAJI wa CHAKULA BORA, tunakula mradi tule na hatuzingatii kupima AFYA zetu.

Wakati UMEFIKA tunapaswa TUBADILIKE kwa sababu WAGONJWA wanaongezeka.

UTAFITI unaonyesha KATI ya WATU 100 wenye UMRI wa kati ya MIAKA 25 na kuendelea, 9 kati yao tayari wanaugua UGONJWA wa KISUKARI huku WAWILI wakiwa hawajijui kuwa wana MARADHI hayo.

Kila MWAKA duniani WATU milioni 12 HUGUNDULIKA kuwa wana SARATANI , na ASILIMIA 60% ya MAGONJWA ya SARATANI yanasababishwa na MFUMO MBOVU wa MAISHA hasa ULAJI usiofaa.

Wenzetu WAZUNGU ni wajanja sio kwamba hawali CHIPS, wanakula lakini WANAZINGATIA ‘menu’ ya SAHANI wanayokula kwamba inakuwa na VIAZI kidogo, MBOGAMBOGA nyingi na MATUNDA.

SISI kwetu ni KINYUME Kabisa.

WATU wanapenda TOMATO sauce kwa wingi.

ULAJI wa MBOGAMBOGA ni jambo la MSINGI kwani huenda kusaidia kurahisisha MFUMO wa umeng’enywaji wa CHAKULA tumboni.

Kama unapenda chipsi basi usile kila siku na ikiwezekana upike mwenyewe nyumbani na mafuta yanayotumika kupikia yatumike mara moja tu vile vile unaweza kujiandalia kachumbali au hata pili pili au tomato sauce wewe mwenyewe nyumbani.

AFYA BORA KWA MAISHA MAREFU !!

Soma hii pia 👇

Kukaa muda mrefu kwenye kiti husababisha kufa mapema

Mjulishe rafiki yako kwenye twitter naye asome post hii kwa kubonyeza ujumbe ufuatao:

Ulaji wa chipsi umetajwa kuwa hatari kwa afya ya binadamu Click To Tweet
Fadhili Paulo
Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
Imesomwa mara 1

Imehaririwa mwisho

Let's block ads! (Why?)

Jumanne, 21 Julai 2020

Namna rahisi ya kuzuia na kudhibiti magonjwa ya virusi

Namna rahisi ya kuzuia na kudhibiti magonjwa ya virusi

Mimi sijuwi ni virusi vya ugonjwa upi vimekuwa vikikusumbuwa au unasumbuliwa navyo bali katika makala hii nitakuonyesha namna rahisi kabisa ya kuzuia au kudhibiti ugonjwa wowote utokanao na virusi.

ILI KUDHIBITI VIRUSI

Tafuta namna unaweza kupunguza au kuondoa sumu katika mwili wako na hakuna kirusi wala ugonjwa wowote wa virusi utakusumbua tena.

Ukiweza tu kupunguza au kuondoa sumu katika mwili wako ninakuhakikishia hakuna ugonjwa wowote utokanao na virusi utakaokusumbuwa tena na ikiwa habari hizi zinaleta matokeo mazuri kwako usisahau kuwashirikisha na wengine na hata kuniletea ushuhuda kwa namna ya comment hapo chini kwenye makala hii.

Kabla ya kujifunza namna gani ya kuondoa au kupunguza sumu mwilini tuangalie kwanza namna sumu zenyewe zinavyojitokeza mwilini.

Kinachosababisha mwili kuwa na sumu au taka taka

SUMU ni kitu chochote ambacho kinaweza kuingia mwilini na kusababisha mifumo ya mwili ishindwe kufanya kazi ipasavyo.

Sizungumzii sumu za kung’atwa na nyoka, wala sizungumzii sumu zinazohitaji matibabu ya dharura.

Nazungumzia sumu ambazo zinatuua pole pole na kimya kimya bila ya sisi kujua wala kutambua chochote. Nazungumzia sumu ambazo kila kuchapo tuko kwenye mlango wa daktari.

Mwili unaweza kupatwa na sumu au takataka zisizohitajika na mwili kwa namna mbili, ama kupitia mazingira tunayoishi (viwanda, migodi nk) au kupitia vyakula na vinywaji ambavyo tunatumia kila siku.

Sumu au taka pia zinaweza kuingia mwilini kupitia dawa mbalimbali hasa za kizungu tunazotumia kujitibia magonjwa mbalimbali.

Mwili huzalisha hizi sumu au takataka (free radicals) kila mara kunapofanyika mmeng’enyo wa chakula mwilini mwako.

Utajuwaje kama una sumu nyingi katika mwili wako?

Ishara zitakazokuonyesha mwili wako una sumu nyingi:

  • Uchovu sugu
  • Maumivu ya maungio
  • Msongamano puani
  • Kuumwa kichwa kila mara
  • Tumbo kujaa gesi
  • Kufunga choo au kupata choo kigumu
  • Kukosa utulivu
  • Matatizo mbalimbali ya ngozi ikiwemo chunusi
  • Pumzi mbaya
  • Mzunguko wa hedhi usio sawa
  • Kuishiwa nguvu
  • Kushindwa kupungua uzito
  • Kupenda kula kula kila mara
  • Kupatwa na ganzi sehemu mbalimbali mwilini

Kinachosababisha mwili kuwa na sumu au taka taka

1. Kutokula matunda na mboga za majani

Matunda na mboga za majani ni vitu viwili mhimu sana ili kusafisha mwili wako na kukukinga dhidi ya sumu na taka taka mbalimbali.

Kama huna tabia ya kula matunda na mboga za majani kila siku ni wazi mwili wako utatengeneza sumu za kutosha.

2. Kula vyakula vya viwandani

Kama unataka kuepuka sumu au takataka nyingine kirahisi kuingia katika mwili wako basi pendelea zaidi kula vyakula vya asili vinavyopikwa nyumbani kuliko kula vya kwenye makopo au vya dukani au vya kwenye migahawa (fast foods).

3. Kutokunywa maji mengi kila siku

Sababu kubwa ya watu wengi kutengeneza sumu au taka mwilini mwao ni kutokunywa maji mengi kila siku. Maji ni uhai, bila kunywa maji mengi kila siku ni sawa na kwenda dukani bila hela mfukoni.

Haijalishi upo mazingira gani kama ni ya baridi au ni ya joto ni LAZIMA UNYWE MAJI YA KUTOSHA KILA SIKU IENDAYO KWA MUNGU.

Unahitaji maji glasi 8 mpaka 10 kila siku. Watu wengi wanahangaika namna ya kuondoa sumu kusafisha miili yao bila kujua kuwa maji pekee ya kunywa yanatosha kwa kazi hiyo.

Kumbuka asilimia 94 ya damu yako ni maji, asilimia 85 za ubongo wako ni maji, hivyo kama huna mazoea ya kupenda kunywa maji kila siku ni rahisi mwili wako kutengeneza sumu. .

4. Vinywaji vyenye kaffeina

Kama tayari imethibitika una sumu au takataka nyingi mwilini nakushauri uache kunywa chai ya rangi na kahawa.

Badala yake hamia kutumia chai yenye tangawizi au mdalasini au mchaichai.

Chai ya rangi na kahawa vina kaffeina ambayo kwanza huyasukuma maji nje ya mwili kwa haraka na kuuacha mwili bila kuwa na maji ya kutosha kwa ajili ya kazi zake.

Kaffeina pia ni madawa ya kulevya kundi la madawa yanayosisimua mwili (stimulants drugs).

5. Kutopata usingizi wa kutosha kila siku

Moja ya vitu vinaweza kukupelekea kuwa na sumu mwilini au takataka nyingi ni pamoja na kutokulala muda wa kutosha kila siku. Usingizi haukopwi na huwezi kuwa na ufanisi katika kazi zako kama hupati usingizi wa kutosha kila siku.

Usingizi siyo jambo la starehe tu, ni sehemu mhimu sana katika afya yako ya kila siku.

Bila kupata usingizi wa kutosha unaweza kuwa karibu na matatizo kama kuongezeka uzito, kushuka kwa kinga ya mwili na nguvu zako za mwili kwa ujumla zinaweza kushuka.

Unapopata muda wa kutosha wa kulala masaa 7 mpaka 8 kwa siku unaupa mwili wako nafasi ya kutosha ya kupumzika na kujiripea upya na hivyo ndivyo sumu na takataka nyingine zinavyoweza kukutoka kirahisi.

Ingia kulala mapema walau saa tatu usiku ingia kulala siyo unakaa unaangalia tamthiliya au mpira mpaka saa sita za usiku!

6. Mazingira tunayoishi

Kuna mazingira yanajulikana wazi kuwa ni vyanzo vya sumu mwilini. Maeneo ya migodi ya madini, maeneo yenye viwanda vingi, maduka yanayouza dawa za kilimo nk

Maeneo haya yanafaa kukaa mbali na makazi ya binadamu kwa usalama wa afya zetu.

7. Vyakula vilivyokobolewa

Ili kuwa na mwili msafi kabisa epuka kula mkate mweupe, sukari na vyakula vinavyopikwa katikati ya mafuta mengi kama vile chipsi, maandazi na vingine vyote vinavyochomwa katikati ya mafuta mengi.

Mkate upo mkate mweusi (brown bread), sukari ipo asali mbichi, vyakula vinavyopikwa katikati ya mafuta mengi unaweza kuamua kuwa unavioka (bake) au uvichemshe (boiling). Uchaguzi ni wako.

8. Mfadhaiko (stress)

Kile tayari unajuwa ni kuwa mfadhaiko au stress ni jambo baya kwa afya yako. Kile unatakiwa kujua kuanzia sasa ni kuwa ili kubaki na afya bora kabisa yenye TBS basi ukae mbali na stress.

Kama utaruhusu stress kutawala maisha yako basi ujuwe mwili wako hauwezi kufanya kazi zake vizuri ikiwemo ya kuondoa taka au sumu mbalimbali mwilini.

Stress peke yake inaweza kupelekea magonjwa mbalimbali mwilini zaidi ya 50. Unapokuwa na mfadhaiko mwili wako hauwezi kutoa taka nje kirahisi na kinga yako ya mwili inashuka matokeo yake unakuwa karibu na magonjwa mengine mengi.

Watu wengine wenye uelewa mdogo wakiwa na stress hukimbilia kutumia vilevi wakidhani zitapungua kumbe ndiyo wanazidi kuongeza tatizo bila kujua.

9. Dawa za kizungu

Dawa nyingi za hospitali huwa zina matokeo chanya (positive) na matokeo hasi (negative) pia ambayo ndiyo matokeo mabaya.

Kama unalazimika kutumia antibiotic kila mara au unameza dawa za kuondoa maumivu kila mara unaweza kuwa unaongeza sumu na taka mwilini bila kujua na bila sababu yoyote ya lazima.

Kuepuka hilo jaribu kutumia mitishamba au mimea ya asili kwa baadhi ya magonjwa ambayo si lazima uende hospitali. Siyo mafua tu mtu ameenda kuchoma sindano!

10. Vilevi

Moja ya vitu vinavyoweza kuleta sumu au taka mwilini moja kwa moja ni vilevi. Vilevi kama pombe, madawa ya kulevya, sigara, bangi na vinginevyo ni vitu vinavyopelekea mwili kuwa na taka moja kwa moja.

Namna pekee ya kuondoa sumu kutokana na vilevi ni kuviacha hivyo vilevi, ndiyo kuviacha.

Usitegemee asubuhi utumie dawa kuondoa sumu mwilini halafu jioni ukanywe pombe au ukavute sigara utegemee tu ile dawa uliyotumia asubuhi kwamba itafanya kazi, hapana unajidanganya, dawa ni kuacha vilevi moja kwa moja.

Vingine vya kuacha kama tayari imegundulika una sumu nyingi mwilini ni pamoja na vinywaji baridi vyote, juisi zote za dukani, chai ya rangi na kahawa.

Je unatafuta dawa ya asili isiyo na madhara ya kutoa sumu mwilini kwa uhakika? kama jibu ni ndiyo basi bonyeza HAPA.

Mjulishe rafiki yako kwenye twitter naye asome post hii kwa kubonyeza ujumbe ufuatao:

Namna rahisi ya kuzuia na kudhibiti magonjwa ya virusi Click To Tweet

Tafadhali SHARE post hii na wengine uwapendao

Fadhili Paulo
Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
Imesomwa mara 41

Imehaririwa mwisho

Let's block ads! (Why?)

Alhamisi, 16 Julai 2020

10-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kumhusisha Rasuli wa Allaah Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam Katika Kumshirikisha Allaah.

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

10-Kumhusisha Rasuli wa Allaah Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam

Katika Kumshirikisha Allaah. 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Baadhi ya Waislamu wanamhusisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwa namna mbali mbali. Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na Rasuli wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wamekemea mno kwa dalili kadhaa miongoni mwazo ni: 

 

Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba ilipoteremshwa kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ ﴿٢١٤﴾

Na onya (ee Muhammad Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) jamaa zako wa karibu. [Ash-Shu’araa: 214]

 

 

Alisimama Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema:

 

 ((يَا مَعْشَرَ قُرَيْشٍ!)) أَوْ كَلِمَةً نَحْوَهَا ((اشْتَرُوا أَنْفُسَكُمْ، لاَ أُغْنِي عَنْكُمْ مِنَ اللَّهِ شَيْئًا، يَا بَنِي عَبْدِ مَنَافٍ لاَ أُغْنِي عَنْكُمْ مِنَ اللَّهِ شَيْئًا، يَا عَبَّاسُ بْنَ عَبْدِ الْمُطَّلِبِ لاَ أُغْنِي عَنْكَ مِنَ اللَّهِ شَيْئًا، وَيَا صَفِيَّةُ عَمَّةَ رَسُولِ اللَّهِ لاَ أُغْنِي عَنْكِ مِنَ اللَّهِ شَيْئًا ، وَيَا فَاطِمَةُ بِنْتَ مُحَمَّدٍ سَلِينِي مَا شِئْتِ مِنْ مَالِي لاَ أُغْنِي عَنْكِ مِنَ اللَّهِ شَيْئًا))

((Enyi maashara Quraysh!)) Au mfano wa maneno hayo ((Uzeni nafsi zenu, mimi sitowafaa chochote mbele ya Allaah! Enyi Baniy ‘Abdi Manaaf! Mimi sitowafaa chochote mbele ya Allaah!  Ee ‘Abbaas bin ‘Abdil-Mutwalib! Sitokufaa  chochote mbele ya Allaah! Na ee Faatwimah bint Muhammad! Niombe utakacho katika mali, lakini sitokufaa chochote mbele ya Allaah)) [Al-Bukhaariy (2753), Muslim (206)].

 

 

Amesema Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) katika Majmuw’ Fataawa wa Rasaail (9/285- 288):

 

“Ikiwa ujamaa wa karibu na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hautowafaa chochote jamaa zake, ni dalili hiyo kukatazwa tawassul kwa jaha ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa kuwa jaha ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hainufaishi kwayo isipokuwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Na ndivyo ikawa kauli sahihi kabisa ya Wanachuoni ni uharamu wa tawassul kwa jaha ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).”

 

 

Na Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah) amesema katika Majmuw’ Fataawaa (3/98):

 

“Mwongozo na kipimo cha hakika ni kufuata yaliyokuja katika Qur-aan Al-Kariym na Sunnah Al-Mutwaharrah kwa kauli na na vitendo na kuitakidi. Ama unasaba, hakika hautofaa (mtu) wala hauna umuhimu kama alivyosema Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam:  

 

وَمَنْ بَطَّأَ بِهِ عَمَلُهُ لَمْ يُسْرِعْ بِهِ نَسَبُهُ

((…na ambaye kazorotesha ‘amali zake, haitomharakisha nasaba yake)). [Muslim]

 

Akasema: ((Enyi maashara Quraysh! Uzeni nafsi zenu, mimi sitowafaa chochote mbele ya Allaah!)). Hivyo ndivyo alivyomwambia ‘Ammi yake na ‘Ammat (shangazi) yake, na binti yake Faatwimah. Basi ingekuwa unasaba utamfaa mtu, ungewafaa hao.”

 

 

Baadhi ya vitendo vinavyomhusisha    Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni kama ifuatavyo:  

 

 

1-Kumtukuza mno Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mpaka kumfikisha daraja ya Allaah!

 

Amekemea Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

لا تُطْرُونِي كَمَا أَطْرَتْ النَّصَارَى ابْنَ مَرْيَمَ فَإِنَّمَا أَنَا عَبْدُهُ فَقُولُوا عَبْدُ اللَّهِ وَرَسُولُهُ) رواه البخاري

Msinitukuze Kama Manaswara [Wakristo] walivyomtukuza Masiyh mwana wa Maryam, hakika mimi na mja kwa hiyo semeni, ‘mja wa Allaah na Mjumbe Wake’)). [Al-Bukhaariy na Muslim.]

 

Na pia Hadiyth:

 

 عَنْ أَنَسٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ نَاسًا قَالُوا: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! يَا خَيْرَنَا وَابْنَ خَيْرِنَا, وَسَيِّدَنَا وَابْنَ سَيِّدِنَا! فَقَالَ: ((يَا أَيُّهَا اَلنَّاسُ! قُولُوا بِقَوْلِكُمْ، وَلاَ يَسْتَهْوِيَنَّكُمْ اَلشَّيْطَانُ، أَنَا مُحَمَّدٌ عَبْدُ اَللَّهِ وَرَسُولُهُ، مَا أُحِبُّ أَنْ تَرْفَعُونِي فَوْقَ مَنْزِلَتِي اَلَّتِي أَنْزَلَنِي اَللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ)) رَوَاهُ النَّسَائِيُّ بِسَنَدٍ جَيِّدٍ

Imepokelewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: kwamba watu walisema: “Ee Rasuli wa Allaah! Ee mbora wetu na mwana wa mbora wetu, na bwana wetu, na mwana wa bwana wetu!.” Akasema: ((Enyi watu! Semeni msemayo, asikupambieni shaytwaan hawaa zenu. Mimi ni Muhammad mja wa Allaah na Rasuli Wake. Sipendi mnipandishe cheo kuliko cheo changu ambacho Ameniteremshia Allaah Ázza wa Jalla)). [An-Nasaaiy kwa isnaad nzuri]

 

Na kutukuzwa kwengine ni vile kusifiwa mno kwa uzushi na pia kutajwa kwa sifa ambazo ni Sifa za Allaah Pekee. Mfano katika Mawlid mbalimbali kama Barzanjiy, Nuwn, Al-Hibshiy (Sumtud-Durar), Burdah n.k. Vilevile kwenye nyiradi mbalimbali miongoni mwa nyiradi za Kisufi kama, Swalaatun-Naariyah, Wasiylatush-Shaafi’, Dalaail Al-Khayraat, n.k.

 

i) Maneno ya shirki yaliyomo katika Swalaatun-Naariyah:

 

للهم صلي صلاةً كاملة وسلم سلاما تاما على سيدنا محمد الذي تنحل به العقد، وتتفرج به الكرب، وتقضى به الحوائج ، وتنال به الرغائب، وحسن الخواتيم ويستسقى الغمام بوجهه الكريم وعلى آله وصحبه في كل لمحة ونفس بعدد معلوم لك

 

 Ee Allaah, Mswalie  Swalaah iliyotimu bwana wetu Muhammad ambayo kwa fadhila zake, vizuizi vyote vinaondoka, mazonge (misukosuko) yanapoa, shida zote zinafarijika, na mahitaji yanakidhika, na inafikisha kwa yanayotamaniwa, na mwisho mwema wapatikana, na kwa fadhila zake yule mwenye uso mtukufu mawingu (mvua) huombwa kunyesha, na Swalah na Salaam ziwe juu ahli zake na Maswahaba wake kwa kila muda na kila pumzi kwa idadi ya kadiri ya Ujuzi Wako)

 

 

ii) Baadhi ya sifa za kumtukuza mno katika Mawlid ya Barzanjiy:

 

“Katika saa ya kuzaliwa Mtume alihudhuria Aasiyah na Maryam kutoka Mbinguni.”

 

“Wanyama walitamka kwa Kiarabu kuwa leo imechukuliwa mimba ya Mtume.”

 

“Wanyama wakapeana khabari ya kuchukuliwa mimba ya Mtume.”

 

“Majini wakatoa khabari kwa watu kuwa imechukuliwa mimba ya Mtume.”

 

“Katika saa ya kuzaliwa Mtume alihudhuria Aasiyah na Maryam kutoka Mbinguni.”

 

“Wanavyuoni wameona ni jambo zuri watu kusimama wakati inapotajwa kuzaliwa Mtume.”

 

“Akamwona Allaah kwa macho yake.”

 

 

iii) Baadhi ya maneno ya shirki kwenye Mawlid Ya Nuwn

 

“Lau kuwa si Mtume asingepatikana Aadam wala Ibraahiym….. na ufalme wa Nabii Sulaymaan…”

 

“Manabii wote ni manaibu wa Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakimwendeshea kazi yake.”

 

 

iv) Baadhi ya maneno ya shirki katika uradi wa Nabhaaniy: 

 

“Lau kuwa si Nabii Muhammad tusingekuja ulimwenguni wala tusingeishi!”

 

 

 

2-Kumuomba du’aa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) badala ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 

Du’aa huelekezwa kwake kama kusema: “Ee Rasuli nisaidie”, “Ee Rasuli niondoshee dhiki, shida zangu”. Hakuna kiumbe yeyote mwenye uwezo wa hayo isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa). Angekuwa na uwezo huo basi yasingemfika madhara, mateso, maudhi mbali mbali yaliyomsibu kutoka kwa makafiri. Allaah Alimuamrisha awaambie washirikina:

 

قُل لَّا أَمْلِكُ لِنَفْسِي نَفْعًا وَلَا ضَرًّا إِلَّا مَا شَاءَ اللَّـهُ ۚ وَلَوْ كُنتُ أَعْلَمُ الْغَيْبَ لَاسْتَكْثَرْتُ مِنَ الْخَيْرِ وَمَا مَسَّنِيَ السُّوءُ ۚ إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ وَبَشِيرٌ لِّقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ﴿١٨٨﴾

Sema: “Siimilikii nafsi yangu manufaa yoyote wala dhara yoyote isipokuwa Apendavyo Allaah. Na lau ningekuwa najua ya ghayb, bila shaka ningelijikithirishia ya kheri, na wala lisingelinigusa ovu. Mimi si chochote isipokuwa ni mwonyaji na mbashiriaji kwa watu wanaoamini.” [Al-A’raaf: 188]

 

 

Na Akamwambia tena aseme:

قُلْ إِنَّمَا أَدْعُو رَبِّي وَلَا أُشْرِكُ بِهِ أَحَدًا﴿٢٠﴾

Sema: (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika mimi namuomba Rabb wangu na wala simshirikishi na yeyote.”

 

قُلْ إِنِّي لَا أَمْلِكُ لَكُمْ ضَرًّا وَلَا رَشَدًا﴿٢١﴾

Sema: “Hakika mimi sikumilikieni dhara na wala uongofu.”

 

قُلْ إِنِّي لَن يُجِيرَنِي مِنَ اللَّـهِ أَحَدٌ وَلَنْ أَجِدَ مِن دُونِهِ مُلْتَحَدًا﴿٢٢﴾

Sema: “Hakika hakuna yeyote awezaye kunilinda na Allaah na wala sitoweza kupata mahali pa kukimbilia. [Al-Jinn: 20-22]

 

 

Na pia Akamuamrisha Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) :

 

قُلْ إِنَّمَا أَنَا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ يُوحَىٰ إِلَيَّ أَنَّمَا إِلَـٰهُكُمْ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۖ فَمَن كَانَ يَرْجُو لِقَاءَ رَبِّهِ فَلْيَعْمَلْ عَمَلًا صَالِحًا وَلَا يُشْرِكْ بِعِبَادَةِ رَبِّهِ أَحَدًا ﴿١١٠﴾

 Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika mimi ni mtu kama nyinyi, nafunuliwa Wahy kwamba: Hakika Muabudiwa wa haki wenu ni Ilaah Mmoja Pekee. Hivyo anayetaraji kukutana na Rabb wake, basi na atende ‘amali njema na wala asimshirikishe yeyote katika ‘ibaadah za Rabb wake.” [Al-Kahf: 110]

 

 

3-Kumuomba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mbele ya kaburi lake:

 

Kuna wanaoelekea kaburi lake wanapofika Masjid Nabawiy Madiynah na kumuomba. Inavyopasa ni kuelekea Qiblah. Allaah Anakataza wazi kumshirikisha Yeye ndani ya Misikiti na hata penginepo, pale Anaposema:

 

وَأَنَّ الْمَسَاجِدَ لِلَّـهِ فَلَا تَدْعُوا مَعَ اللَّـهِ أَحَدًا﴿١٨﴾

Na kwamba Misikiti ni kwa ajili ya Allaah, basi msiombe yeyote pamoja na Allaah. [Al-Jinn: 18]

 

Naye Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam amekataza:

((لا تجعلوا قبري عيدًا))

((Msifanye kaburi langu ni sehemu ya kurudiwa rudiwa [kuendewa kila mara])). [Musnad Ahmad, Muswannaf 'Abdur-Razzaaq]

 

Na akasema:

 

   لعنة الله على اليهود والنصارى اتخذوا قبور أنبيائهم مساجد

((Allaah Amewalaani Mayahudi na Manaswara, wamefanya makaburi ya Manabii wao kuwa misikiti)). [Al-Bukhaariy  (425) Muslim (531)]

 

 

4-Kutawassul (kujikurubisha) kwa du’aa kupitia kwake:

 

Mfano kusema: “Ee Allaah, hakika mimi nakuomba kwa jaha ya Rasuli Wako Unikidhie haja zangu kadhaa, au Uniokoe na janga au balaa fulani, Unighufurie dhambi zangu n.k.”

 

Baada yakufariki Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) haipasi kutawasali kwake. Maswahaba waliacha kutawasali kwake bali walitawasali kwa ami yake ‘Abbaas kwa kuwa alikuwa hai wakati huo kama ilivyothibiti katika Hadiyth ifuatayo:

 

 عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ  (رضي الله عنه)  أَنَّ عُمَرَ بْنَ الْخَطَّابِ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) كَانَ إِذَا قَحَطُوا اسْتَسْقَى بِالْعَبَّاسِ بْنِ عَبْدِ الْمُطَّلِبِ فَقَالَ:  "اللَّهُمَّ إِنَّا كُنَّا نَتَوَسَّلُ إِلَيْكَ بِنَبِيِّنَا فَتَسْقِينَا وَإِنَّا نَتَوَسَّلُ إِلَيْكَ بِعَمِّ نَبِيِّنَا فَاسْقِنَا"  قَالَ" فَيُسْقَوْنَ

Kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba ‘Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu) aliomba mvua kulipokuwa na ukame kwa kutawasali kwa ‘Abbaas bin ‘Abdil-Muttwalib akisema: “Ee Allaah, tulikuwa tunatawasali Kwako kupitia Nabiy wako, Ukatunyeshea mvua, na sasa tunatawasali Kwako kupitia ‘ami wa Nabiy Wako basi tunyweshee mvua”. Akasema: Wakanyweshewa mvua. [Al-Bukhaariy]

 

 

 

 



48-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Amepewa Funguo Za Hazina Za Ulimwengu Wote

 

Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

48-Amepewa Funguo Za Hazina Za Ulimwengu Wote

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ عُقْبَةَ بْنِ عَامِرٍ، أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم خَرَجَ يَوْمًا فَصَلَّى عَلَى أَهْلِ أُحُدٍ صَلاَتَهُ عَلَى الْمَيِّتِ، ثُمَّ انْصَرَفَ إِلَى الْمِنْبَرِ فَقَالَ ‏ "‏ إِنِّي فَرَطٌ لَكُمْ، وَأَنَا شَهِيدٌ عَلَيْكُمْ، وَإِنِّي وَاللَّهِ لأَنْظُرُ إِلَى حَوْضِي الآنَ، وَإِنِّي أُعْطِيتُ مَفَاتِيحَ خَزَائِنِ الأَرْضِ ـ أَوْ مَفَاتِيحَ الأَرْضِ ـ وَإِنِّي وَاللَّهِ مَا أَخَافُ عَلَيْكُمْ أَنْ تُشْرِكُوا بَعْدِي، وَلَكِنْ أَخَافُ عَلَيْكُمْ أَنْ تَنَافَسُوا فِيهَا ‏"‏‏.‏

 

Kutoka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir (رضي الله عنه) amesema: Siku moja Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikwenda nje na akaongoza Swalaah za maiti; Mashuhadaa wa Uhd, kisha akapanda katika Minbar akasema: “Mimi nitaandaa njia kwa ajili yenu kama muasisi na nitakuwa Shahidi kwa ajili yenu. Na wa-Allaahi, ninaiona Al-Hawdhw (chemchemi ya Al-Kawthar) sasa hivi na nimepewa funguo za hazina zote za ardhi (au funguo za ardhi). Na Wa-Allaahi, hakika mimi sikhofu kuwa mtamshirikisha Allaah baada ya kufa kwangu, lakini nakhofu kuwa mtagombana baina yenu kwa ajili ya vitu vya kidunia.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Kupewa Hazina Za Ulimwengu: Ni kuongezeka na kupanuka Uislamu, na kujaaliwa ushindi mkubwa na mateka ya mali, kwa sababu unapopatikana ushindi wa nchi ni sawa na kumiliki mali na hazina zake.

 

 



04-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Zuhd Yake: Alikosa Chakula Nyumbani Mwake Hadi Kufikia Miezi Miwili

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

04-Zuhd Yake: Alikosa Chakula Nyumbani Mwake Hadi Kufikia Miezi Miwili

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

Kulifikia ukosekanaji wa chakula nyumbani mwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa siku nzima au masiku au hadi miezi kupita! Basi hakika hii pia ni sifa ya Zuhd ya ajabu mno kuimiliki mtu!

 

 

وعن النعمان بن بشير رضي الله عنهما ، قَالَ : ذَكَرَ عُمَرُ بْنُ الخَطَّابِ رضي الله عنه ، مَا أَصَابَ النَّاسُ مِنَ الدُّنْيَا ، فَقَالَ : لَقَدْ رَأيْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم يَظَلُّ الْيَوْمَ يَلْتَوِي مَا يَجِدُ مِنَ الدَّقَلِ مَا يَمْلأ بِهِ بَطْنَهُ . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa An-Nu'maan bin Bashiyr (رضي الله عنهما)   ambaye amesema: Alitaja 'Umar bin Al-Khattaab (رضي الله عنه)  yale yaliyowafikia watu katika hii dunia, akasema: "Hakika nilimuona Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akipitisha siku zake akiwa na njaa hana hata tende (hata) mbaya ya kuondoa njaa yake." [Muslim] 

 

Mpaka katika hali yake ya kuaga dunia hakuwa na chakula nyumbani mwake:

 

 

عن عائشة رضي الله عنها ، قالت : تُوفي رسول الله صلى الله عليه وسلم، وَمَا في بَيْتِي مِنْ شَيْءٍ يَأكُلُهُ ذُو كَبِدٍ إِلاَّ شَطْرُ شَعِيرٍ في رَفٍّ لي ، فَأكَلْتُ مِنْهُ حَتَّى طَالَ  عَلَيَّ ، فَكِلْتُهُ فَفَنِيَ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah  (رضي الله عنها) amesema: "Aliaga dunia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na hakukuwa katika nyumba chakula cha sawa (kwa watu kula) isipokuwa mtama kidogo katika stoo yangu ambao nilikuwa nikiutumia kwa muda. Baadae nilitaka kuupima lakini ukawa umemalizika." [Al-Bukhaariy na Muslim

 

Bali alikosa chakula nyumbani mwake hadi kufikia siku tatu:

 

عن عَائِشَة رضي الله عَنْهَا قالت : (مَا شَبِعَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ثَلَاثَةَ أَيَّامٍ تِبَاعًا مِنْ خُبْزِ بُرٍّ حَتَّى مَضَى لِسَبِيلِهِ) رواه البخاري ومسلم  

 

‘Aaishah (رضي الله عنها) amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) hakupatapo kula mkate wa ngano mpaka kufariki kwake.” [Muslim na wengineo]

 

 

Na pia,

 

  فاطِمةَ ناوَلَتْ رسولَ اللهِ صلَّى اللهُ عليه وسلَّمَ كِسْرةً مِن خُبزِ شَعيرٍ، فقال: هذا أوَّلُ طعامٍ أكَلَهُ أبوكِ مِن ثَلاثةِ أيَّامٍ.

 

Na pia pindi mwanawe Faatwimah (رضي الله عنها) alipompatia kipande cha mkate wa shayiri alisema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Hiki ni chakula cha kwanza baba yako anakula tokea siku tatu.” [Hadiyth ya Anas bin Maalik ameikusanya Imaam Ahmad -Hadiyth Hasan]

 

Bali kulikosekana chakula nyumbani mwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) hadi kufikia miezi!

 

 عَنْ عُرْوَةَ، عَنْ عَائِشَةَ، أَنَّهَا كَانَتْ تَقُولُ: "وَاللَّهِ يَا ابْنَ أُخْتِي إِنْ كُنَّا لَنَنْظُرُ إِلَى الْهِلاَلِ ثُمَّ الْهِلاَلِ ثُمَّ الْهِلاَلِ ثَلاَثَةَ أَهِلَّةٍ فِي شَهْرَيْنِ وَمَا أُوقِدَ فِي أَبْيَاتِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم نَارٌ"   قَالَ: قُلْتُ: يَا خَالَةُ فَمَا كَانَ يُعَيِّشُكُمْ؟ قَالَت: الأَسْوَدَانِ التَّمْرُ وَالْمَاءُ إِلاَّ أَنَّهُ قَدْ كَانَ لِرَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم جِيرَانٌ مِنَ الأَنْصَارِ وَكَانَتْ لَهُمْ مَنَائِحُ فَكَانُوا يُرْسِلُونَ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم مِنْ أَلْبَانِهَا فَيَسْقِينَاهُ ‏.‏

 

 

Amehadithia ‘Urwah kuwa ‘Aaishah (رضي الله عنها) alikuwa akimwambia: “Ee mwana wa dada yangu!  Tulikuwa tukiutazama mwandamo wa mwezi, kisha mwezi mwengine kisha mwezi mwengine, miandamo mitatu katika miezi miwili na ilhali katika nyumba  za Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) hakujaashwa moto (wa kupikia chakula). (‘Urwaa) Akasema: Nikamuuliza: “Ee Khaalat yangu, je, mliweza kuishi kwa vipi?” Akasema: “Vyeusi viwili: tende na maji isipokuwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa ana jirani katika Answaariy walikuwa wana mbuzi na walikuwa wakimletea Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) maziwa yake akawa anatunywesha.”  [Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo]

 



20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...