Translate

Ijumaa, 28 Agosti 2020

Aina za vidonda vya tumbo

Vidonda vya tumbo vimegawanyika katika makundi matatu makuu na leo nitajadili kwa kina aina hizo za magonjwa haya ya tumbo kama ifuatavyo:

1. Vidonda vya tumbo kubwa (Gastric Ulcers):

Aina hii ya vidonda vya tumbo hutokea kwenye mfuko wa kuhifadhia chakula yaani tumbo.

Vidonda hivi hutokea katika utumbo kwa sababu mbalimbali kama vile mtu kupata maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori.

Imegundulika kuwa zaidi ya asilimia 50 ya watu duniani wana vimelea hivi katika utumbo na huwa ni vigumu kuonesha dalili yoyote ya kuugua maradhi haya.

Aina hii ya vimelea vya bakteria husababisha karibu asilimia 60 ya vidonda vinavyotokea kwenye tumbo na huitwa kitaalam Gastric Ulcers.

2. Vidonda vya sehemu ya juu ya tumbo (Duodenal Ulcers):

Hivi ni vidonda ambavyo hutokea kwenye utumbo mdogo.

Aina hii huwapata watu kutokana na kushindwa kwa mfumo wa kinga mwilini ambao huua na kuondoa kabisa vimelea vya kinga ndani ya mwili.

Matokeo ya kushindikana huko kunasababisha kuwepo kwa uambukizi wa kudumu katika kuta za tumbo ambao kitaalam huitwa Chronic Active Gastritis, hivyo kuharibu mfumo na uwezo wa kuta za tumbo kutunza homoni ya Gastrin ambayo kazi yake ni kuhakikisha tumbo linakuwa na tindikali (acid) inayotakiwa tumboni.

Acid hii iitwayo Gastric Acid, ikizalishwa kwa wingi tumboni husababisha kuchubuka kwa ukuta wa tumbo na mtu huyo kuambiwa ana vidonda vya tumbo.

Lakini ukuta wa utumbo hujilinda na madhara yatokanayo na tindikali ya utumbo yaani Gastric Acid kwa kuwa na utando laini (mucus) ambao hutolewa na vichocheo vijulikavyo kama Prostaglandins.

Hata hivyo, kuna dawa ambazo huharibu mfumo wa kutengeza vichocheo hivi yaani Prostaglandins na hivyo kufanya kuta za tumbo kukosa mucus za kuzilinda na mashambulizi ya tindikali, hali ambayo hufanya vidonda vya tumbo kuibuka.

3. Vidonda vya utumbo mdogo (Ulcers in small intestine):

Kundi hili ni wale wagonjwa wanaougua ugonjwa wa vidonda kwenye sehemu ya kwanza ya utumbo mdogo yaani Small Intestine na maumivu yao makali husikia wanapokuwa na njaa na hupata nafuu pindi anapokula.

Soma zaidi kuhusu vidonda vya tumbo kwa kubonyeza hapa.

Fadhili Paulo
Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
Imesomwa mara 3

Let's block ads! (Why?)

Jumanne, 25 Agosti 2020

Aina 4 za wanawake ambao hawawezi kuolewa

AINA 4 ZA WANAWAKE AMBAO HAWAWEZI KUOLEWA

Makala hii inaeleza juu ya aina 4 za wanawake ambao hawawezi kuolewa au wanaolewa kwa kuchelewa sana.

Vitu vingi ninavyojadili hapa ni tabia na zinaweza kurekebishika iwapo mhusika atakuwa tayari kubadilika.

Kwenye maisha hakuna kitu kizuri au hakuna silaha kubwa unaweza kupata kama kupata ufahamu na uwezo wa kutambua udhaifu wako.

Watu wengi hawapendi kujipeleleza na kujitafiti wapi wanakosea au wapi wana mapungufu. Wengi wanapenda kuonekana ni wakamilifu na namna au tabia yoyote yakutaka kuwaonyesha udhaifu wao inaweza kukuletea shida wewe uliyeanza kutaka kumuonyesha shida zake.

Watu wengi wanapenda kusifiwa tu na siyo kukosolewa. Hili ni jambo baya sana kama wewe ni mtu unayependa kujirekebisha na kuwa bora zaidi ya ulivyo.

Vile vile nitowe angalizo mapema kwamba haina maana kwamba ukiwa mwanamke ni lazima uolewe, au ili uwe umekamilika kama mwanamke basi lazima uolewe au hata mwanaume siyo lazima uwe umeoa ndiyo uwe umekamilika, HAPANA sina maana hiyo.

Wapo wanawake wengi tu hawajaolewa na wana msaada mkubwa katika familia, katika jamii na kwa taifa kwa ujumla.

Kuolewa ni bahati na kwa bahati mbaya ukweli utabaki pale pale kwamba si wanawake wote watapata nafasi ya kuolewa.

Takwimu zinaonyesha kila watoto 10 wanaozaliwa watoto 7 kati yao ni wa kike!

Kuna mambo mengi unayoweza kufanya na jamii inayokuzunguka ikaona fahari kuwa na wewe hata kama hujaolewa au huna mme.

Jikubali

Kusema hivyo bado siwezi kupinga ukweli pia kwamba wapo wanawake ambao wanalala usiku na mchana wakiomba Mungu waweze kupata wenza wa maisha yao na waanzishe familia kama mme na mke na kuwa na watoto.

Siyo jambo baya kuolewa kwani kwa kawaida hakuna taifa linaweza kuwepo kama watu hawaoani.

Hata hivyo kuna baadhi ya tabia unazoweza kuwa nazo kwa kujuwa au hata bila kujuwa zinazoweza kuwa zinazuia wewe kuolewa au kudumu kwenye ndoa na leo nimeona bora nikuandikie tabia hizo ili kama unaweza kuzifanyia marekebisho unaweza kumpata mwanaume umtakaye na ukadumu kwenye ndoa yako.

Aina 4 za wanawake ambao hawawezi kuolewa

1. Mwanamke mkamilifu

Hapa haina maana kwamba msichana mwenyewe ni mkamilifu, hapana. Huyu ni msichana au ni mwanamke ambaye mawazo yake yote ni kupata na kuolewa na mwanaume wa ndoto zake.

Vigezo vyake vya aina ya mwanaume anayemtaka mara nyingi ni vingi mno kiasi kwamba mwanaume wa sifa hizo anaweza asipatikane.

Mara nyingi mwanamke huyu anaweza kumpata mwanaume mwenye sifa hizo lakini bahati mbaya mwanaume huyo anaweza asimpende huyu mwanamke.

Mwanamke huyu anakuwa na sifa na vigezo kichwani kwake vya aina ya mwanaume anayemtaka. Anataka kuwa na mwanaume mrefu, tajiri, mpole na mzuri sana (Handsome man).

Mwanamke huyu anaweza kuendelea kung’ang’ania vigezo hivi kwa kipindi kirefu sana akimtafuta mwanaume asiye na kasoro na mwenye sifa anazotaka yaani mwanaume mrefu, tajiri, anayejali na mzuri sana kwa umbile.

Tatizo la tabia hii : Shida kubwa ya wanawake wa aina hii ni kuwa wanaishia kulipenda BOKSI (container) badala ya kupenda VILIVYOMO ndani ya boksi (content). Unaishia kupenda vitu vya nje vya mtu badala ya kumpenda yeye kama yeye.

Ushauri: Mpende mwanaume kwa jinsi alivyo na punguza hivyo vigezo walau mpaka nusu yake na mengine yatakaa sawa pole pole mkiendelea kuishi.

Kwa mfano ukipata mwanaume mrefu na siyo tajiri unaweza kuolewa naye, utajiri ni vitu vinavyotafutwa na mtu wa aina yoyote anaweza kuupata wakati wowote bila kujali ni mfupi au ni mbaya usoni.

2. Mwanamke mrembo sana

Mwanamke mrembo sana anapendwa na kila mwanaume.

Kuna mwanamke hawezi kumaliza kukatisha njia hajaitwa au hajatongozwa. Ni mzuri kila mwanaume anayemuona anamtamani na kumtaka.

Mwanamke au msichana wa namna hii ni vigumu kuolewa au kudumu kwenye ndoa.

Mara nyingi wanawake na wasichana wa namna hii hujikuta kwenye mahusiano ambayo si sahihi kwao.

Huu ndiyo ukweli mchungu.

Anaweza kupata mwanaume wa kumuoa kirahisi sana na akaolewa mapema sana katika umri wake lakini itakuwa vigumu kudumu kwenye ndoa kwa sababu ya udhaifu wake wa asili yaani uzuri uliopitiliza aliopewa na Mungu.

Umeona eeehhh?

Wanaume wengi wanaotembea au kuanzisha mahusiano na wanawake wa namna hii hufanya hivyo kwa lengo moja la BURUDANI TU na siyo kingine.

Uzuri wako mwenyewe unaweza kukuponza na ukaishia kutumika kama chombo cha starehe tu na ukashuhudia wenzio wenye sura mbaya au za kawaida wakiolewa na kuwekwa ndani kila siku.

Uzuri wake unamfanya kuwa mgumu kujitunza na kujiheshimu kwa ajili ya mwanaume mmoja. Haya ni matokeo ya kuhitajika na kila mwanaume kila kona kulia, kushoto, katikati kila akigeuka anahitajika.

Tatizo lilivyo hasa : Tatizo kubwa la wanawake na wasichana wa namna hii ni kuwa hakuna mwanaume anayetokea kumpenda mwanamke huyu kwa jinsi alivyo na wanaume wengi huwa na viulizo vingi kichwani wakihofu ikiwa kweli msichana au mwanamke huyu anaweza kuwa mama na kuendesha familia kwa utulivu.

Hili linawasilisha hatari kubwa kwa mwanamke kushindwa kuolewa au kuolewa mapema na kuachika kirahisi au mapema zaidi.

Hakuna mwanaume anaweza kuendeleza mahusiano na wewe akiwa na uhakika kabisa kichwani kwamba wewe ni cha wote au ni chama la wana.

Suluhisho kwa tatizo hili : Kuwa na picha ya mwanaume unayemhitaji kuwa naye maishani.

Una bahati kwamba umezaliwa ni mrembo na uwe na uhakika kuolewa kwako haitakuwa shida ila utapata raha zaidi ukichukuwa hatua nyingine ya pili ya kumheshimu huyo mwanaume mmoja aliyekupa Mungu, kuwa mwaminifu kwake na atakuwa na furaha kwa uamuzi wake wa kukuoa.

Wanaume hawataacha kukutongoza, hawataacha kukuhitaji.

Thamani yako ya kweli itaonekana pale tu utakapokataa kutumia uzuri wako kuishi maisha ya kijinga kwani hakuna mwanaume atakayevumilia ujinga wako sababu tu wewe ni mzuri.

Subutu yako! Utaliwa na kuachwa kila mara kama boga.

3. Msichana kutoka familia tajiri

Msichana au mwanamke ambaye baba yake ni tajiri sana naye anaweza kupata wakati mgumu kuolewa.

Akili yake mara nyingi ipo bize na utajiri wa baba yake. Na mara nyingi anaweza kumchukulia baba yake kama vile ni malaika au mungu wa pili.

Akili yake yote ni baba yake na baba yake ndiye shujaa wake kwakuwa kwenye kuishi kwake hakuna alichowahi kuhitaji akakikosa. Akitaka ada analipiwa ya mwaka mzima tangu januari, akitaka simu ya milioni mbili ananunuliwa.

Na wazazi wengi wenye mali hudhani kuwapenda sana watoto wao ndiyo kuwajali kumbe wanawaharibu bila wao kujuwa.

Hakuna mwanaume anaweza kuwa mbadala wa baba yake au mama yake.

Wasichana wengi wa namna hii huwa wanadhani kila mwanaume anayemhitaji anafanya hivyo kwa sababu ya utajiri alionao baba mkwe (baba wa msichana) na wanakuwa hawapatikani kirahisi mbele ya macho ya wanaume.

Wanaume wengi wanaojitambuwa hawawezi kukubali upumbavu wa namna hii. Yaani hata uwe tajiri vipi mwanaume anabaki kuwa mwanaume.

Chochote kinachoweza kumfanya huyu mwanaume asijione mwanaume na mwenye kauli ya mwisho kitakuzuia usiolewe.

Tatizo lilivyo : Wasichana wengi ambao baba zao ni matajiri huolewa kwa kuchelewa sana au huolewa na mwanaume ambaye siyo sahihi kwao.

Suluhisho la tatizo : Tambua mali za kidunia ni ubatili na upumbavu mtupu.

Hela ni kitu cha mhimu sana hakuna mtu hata mmoja atakayepinga hili bali uelewe kuwa HELA PEKE YAKE SIYO KILA KITU.

Hela, majumba, magari, utajili vyote utaviacha hapa hapa duniani, ulivikuta na utaviacha wala visikupe homa kila mtu anaweza kuwa navyo.

Wanaume wanaweza kuvutiwa na wewe sababu ya uhakika wa kuishi maisha yasiyo ya kimaskini lakini ujuwe kuwa uzuri wako utakuwa ni kitu cha pili watakachokupendea jambo ambalo si sahihi.

Kuwa mpole tu dunia tunapita.

4. Mwanamke shupavu :

Hawa ndiyo wale unawasikia kwenye mitandao wanajiita kina strong woman, wanajiita kina boss lady, mwanamke mpambanaji, single woman na kadharika.

Hawa wana kila dalili za kufanana na wanaume. Hawa wanaamini wanajiweza wenyewe na hawahitaji kuwa chini ya mwanaume.

Wengi wao wana biashara zao binafsi, ni waajiriwa wa serikali kwenye vitengo mhimu au wanafanya kazi kwenye makampuni makubwa na hawana shida yoyote.

Unaweza kumkuta mwanamke tayari ana nyumba yake, kazi nzuri, gari lake, hela ya kutosha, ni mzuri hata kwa umbile lakini kuolewa inakuwa vigumu.

Mara nyingi wanapenda kuwa wanaharakati, ni waumini wazuri wa kauli mbiu ya haki sawa na usimtegemee mwanaume ndiyo kauli zitokazo kwenye midomo yao mara nyingi.

Kwa bahati mbaya ndoa haipo hivyo.

Hakuna haki sawa kwenye ndoa na haitakaa itokee hivyo leo wala kesho wala kesho kutwa, kwa kifupi sahau hilo kichwani kwako.

Ndoa kama ndoa kwao siyo tatizo, mara nyingi wanabahatika kupata wanaume wazuri. Tatizo ni kazi wanazofanya.

Tatizo lao kubwa : Tatizo lao kubwa hawa wadada ni MUDA. Hawana muda na wanaendesha kila kitu kwenye maisha yao kama vile biashara hata mahusiano wanayachukulia kama vile ni kuendesha biashara au kampuni fulani.

Wanaweza kuajiri mpishi na akaishi hata mwaka mzima bila kuingia jikoni japo kuandaa chai ya mmewe. Yupo bize.

Wanapenda kuwa mabosi kwenye kila kitu na hili ni jambo wanaume wengi hawawezi kuvumilia.

Kadri mwanamke anavyojitahidi kutaka kuwa kama au kufanana kimajukumu na mwanaume ndivyo anavyokuwa anapoteza mvuto kwa wanaume.

Hakuna mwanaume yupo tayari kuishi na mwanaume mwenzake ndani ya nyumba moja.

Wanaume wanapenda wanawake wenye sauti ya chini na wanaoonyesha dalili fulani ya kunyenyekea na kujishusha. Ndiyo asili yao wanaume na huwezi kuibadili.

Suluhisho la tatizo : Endelea kuwa mwanamke bila kujali kazi yako, mali zako na uwezo wako wa kujimudu.

Unapoolewa haina maana huwezi kuishi peke yako au huwezi kujimudu, bali hiyo ndivyo tulivyoumbwa kwamba peke yetu hatujiwezi na mara zote tunahitaji misaada ya wengine hata kama siyo misaada ya hela lakini tumeumbwa kutegemeana.

Kuwa mpole, jishushe, cheka na watu, kuwa mtoto.

Je wewe ni mwanamke na unaishiwa au umepoteza kabisa hamu ya kutaka kushiriki tendo la ndoa?

Kama ndiyo jibu la tatizo lako ninalo, ninayo dawa nzuri ya asili ya kukurudishia mudi yako kama zamani na ukaendelea kufurahia maisha yako ya ndoa, tuwasiliane WhatsApp +255714800175

Aina 4 za wanawake ambao hawawezi kuolewa 1

.

SHARE na wengine uwapendao

Fadhili Paulo
Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
Imesomwa mara 23

Let's block ads! (Why?)

Vitu 6 wanawake wanatakiwa kufanya ili kujikinga na uvimbe kwenye kizazi

Vitu 6 wanawake wanatakiwa kufanya ili kujikinga na uvimbe kwenye kizazi

Inakadiriwa asilimia 70 mpaka 80 ya wanawake wanaweza kupatwa na ugonjwa huu katika safari yao ya kuishi.

Hata hivyo si wanawake wote wenye uvimbe kwenye kizazi wanaweza kuonyesha dalili kwamba wanao au wanahitaji matibabu.

Uvimbe katika mfuko wa kizazi wa mwanamke hujulikana kama ‘uterine myoma’ au fibroid.

Uvimbe huu hutokea katika sehemu mbalimbali juu au ndani ya mji wa uzazi wa mwanamke.

Jambo la mhimu kufahamu kuhusu uvimbe huu ni kuwa si kweli kwamba unaweza kupelekea saratani kama hatua zake za mwisho za ugonjwa kama baadhi ya watu wanavyoweza kukutisha.

Jambo la mhimu kufahamu kuhusu uvimbe huu ni kuwa si kweli kwamba unaweza kupelekea saratani kama hatua zake za mwisho za ugonjwa kama baadhi ya watu wanavyoweza kukutisha. Click To Tweet

Vile vile si kweli kwamba ni upasuwaji tu ndiyo njia pekee ya uhakika ya kutibu uvimbe kwenye kizazi.

Zipo dawa rafiki zinazoweza kutumika na ukapona bila kulazimika kufanya upasuwaji.

Uponyaji wake kwa kawaida huwa ni wa pole pole lakini kwa uvumilivu na kuendelea kuzingatia maelezo na ushauri wa daktari ni ugonjwa unaotibika.

Ingawa uvimbe kwenye kizazi unaweza kuwa ni moja ya sababu inayokuzuia usipate ujauzito, bado wapo baadhi ya wanawake wana uvimbe kwenye kizazi na ujauzito wanapata.

Vitu 6 wanawake wanatakiwa kufanya ili kujikinga na uvimbe kwenye kizazi (Fibriod)

1. Weka sawa homoni zako

Ili kuepuka kupata uvimbe kwenye mji wako wa uzazi unahitajika kuhakikisha homozi zako zipo sawa kila mara.

Wakati wowote usawa wa homoni ya ‘estrogen’ unapozidi mwilini mwako ni wakati huo pia uvimbe kwenye mji wako wa uzazi unaweza kujitokeza.

Kuongezeka zaidi kwa usawa wa homoni ya ‘estrogen’ mara nyingi kunaweza kuwa ni matokeo ya matumizi ya mara kwa mara ya dawa za uzazi wa mpango au inaweza kutokea pia unapopata ujauzito.

Soma pia hii 👇

Dawa ya asili ya kuweka sawa homoni

2. Dhibiti uzito wako

Vitu 6 wanawake wanatakiwa kufanya ili kujikinga na uvimbe kwenye kizazi 1

Kuwa makini na uzito wako wa mwili ili kujikinga na tatizo la uvimbe kwenye mji wa uzazi (fibroids).

Uzito uliozidi ni sababu nyingine inayoweza kurahisisha kutokea kwa ugonjwa huu mwilini mwako.

Tabia zifuatazo zitakusaidia kupunguza uzito wako;

  • Kupunguza kiasi cha chakula unachokula,
  • Kufunga kula mara kwa mara,
  • Kupunguza kukaa chini au kwenye kiti masaa mengi, na
  • Mazoezi ya viungo ya mara kwa mara

Soma hii pia 👇

Dawa ya asili ya kupunguza uzito, unene na kitambi

Unataka kujuwa ikiwa una uzito sawa au uliozidi?

Tumia kikokotoo cha BMI (BMI calculator) hiki hapa chini.

Bonyeza Nataka Kupima Uzito kisha andika urefu wako katika sentimita na uzito katika kilogramu kisha bonyeza KOKOTOA itakuambia kama una uzito sawa au umezidi au una uzito pungufu.

Pima uzito hapa

BMI yako ni ......

BMI Maelezo ya Majibu
BMI chini ya 18.5: Uzito Upo Chini
BMI 18.5 Mpaka 24.9: Una uzito wa kawaida
BMI 25 Mpaka 29.9: Uzito wako umezidi Kidogo
BMI 30 Mpaka 34.9: Uzito unaanza kuwa juu
BMI 35 Mpaka 39.9: Uzito wako upo juu
BMI zaidi ya 40 : Uzito wako upo juu SANA

.

3. Acha baadhi ya vipodozi

    Ili kujikinga, kuzuia au kujiongezea nafasi ya kupona haraka uvimbe kwenye kizazi kama mwanamke utahitaji kuacha kutumia vipodozi ambavyo vimekatazwa wazi na wizara ya afya na hata vile ambavyo vimeruhusiwa lakini siyo vya asili zaidi.

    Losheni, krimu na vipodozi vingi vya dukani vina kemikali ambazo zinaweza kuuingia mwili wako kirahisi kupitia ngozi yako na kukuletea wewe usawa usio sawa wa homoni (endocrine imbalance) na uwezekano mkubwa wa kupatwa na uvimbe kwenye kizazi.

    Ndiyo sababu tatizo hili la uvimbe kwenye kizazi limeongezeka sana miongo mitatu iliyopita sababu ndiyo wakati wanawake wengi wamekuwa bize sana na vipodozi kuliko miaka ya nyuma.

    4. Weka sawa shinikizo lako la juu la damu

    Utatakiwa pia kupunguza na ikiwezekana kutibu shinikizo lako la juu la damu (high blood pressure – BP) kama unalo.

    Tafiti nyingi zinathibitisha kwamba wanawake wanaoumwa shinikizo la juu la damu wanapatwa kirahisi zaidi pia tatizo la uvimbe kwenye kizazi.

    Pengine umeshaambiwa kuwa shinikizo la juu la damu halina dawa ya kutibu na hivyo utatakiwa kuwa mtumwa wa kumeza dawa miaka yote!

    Ningependa kukuambia habari mpya kwamba shinikizo la juu la damu linaweza kutibika na kuisha kabisa hasa kwa kutumia dawa za asili na kuzingatia vyakula na mazoezi ya viungo.

    Soma na hii pia 👇

    Ukweli kuhusu chumvi na maajabu yake

    Vitu vingine viwili unavyotakiwa kuvifanya ili kujikinga au kujiongezea nafasi ya kuweza kupona uvimbe kwenye kizazi ni pamoja na

    5. Utaacha kula nyama nyekundu ikiwemo nyama choma na mishikaki

    6. Utaacha pia vilevi vyote

    Soma zaidi kuhusu uvimbe kwenye kizazi kwa kubonyeza hapa.

    Jiunge na mimi na watu wengine zaidi ya 94000 kwenye ukurasa wangu wa facebook kwa kubonyeza hapa

    Mjulishe rafiki yako kwenye twitter naye asome post hii kwa kubonyeza ujumbe ufuatao:

    Vitu 6 wanawake wanatakiwa kufanya ili kujikinga na uvimbe kwenye kizazi Click To Tweet

    Share post hii na wengine uwapendao

    Fadhili Paulo
    Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
    Imesomwa mara 17

    Let's block ads! (Why?)

    Jumatano, 19 Agosti 2020

    Dawa ya vidonda

    Dawa ya vidonda

    Kama umekuwa ukisumbuliwa na tatizo la vidonda iwe ni miguuni, mikononi au sehemu nyingine yoyote ya mwili dawa yake ni rahisi kama kumsukuma mlevi

    Pakaa (mimina kwenye kidonda) mafuta orijino ya nazi mara mbili mpaka tatu kwa siku na kidonda chako kitaanza kupona na kufunga siku chache tangu uanze kutumia dawa

    Mafuta original kabisa ya nazi yale yanayoruhusiwa kunywa pia

    Kama huwezi kupata mafuta ya nazi orijino kabisa unaweza kununua dukani mafuta ya nazi yanaitwa parachute yanatoka India

    Mafuta ya nazi yana uwezo wa kuua na kudhibiti bakteria, virusi na vijidudu vingine nyemelezi

    Mafuta ya nazi ni dawa kwa matatizo mengine mengi ya ngozi

    Vile vile ikiwa unasumbuliwa na magonjwa ya virusi mara kwa mara kunywa tui la nazi glasi moja kutwa mara mbili asubuhi na jioni kabla ya chakula kila siku mpaka utakapoona upo vizuri

    .

    Mawasiliano yangu ni WhatsApp +255714800175

    Share na wengine uwapendao

    Fadhili Paulo
    Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
    Imesomwa mara 6

    Let's block ads! (Why?)

    Chanzo cha kufunga au kupata choo kigumu wakati wa ujauzito

    CHANZO CHA KUFUNGA AU KUPATA CHOO KIGUMU WAKATI WA UJAUZITO

    Kipindi cha ujauzito ni kipindi cha furaha kubwa kwa mwanamke yoyote.

    Hata hivyo kuna baadhi ya mabadiliko ya kiafya yanayoweza kukutokea unapokuwa na ujauzito ambayo yanaweza kukuondolea furaha hiyo ikiwemo tatizo la kupata choo kigumu sana au kufunga choo kabisa na kupelekea tatizo la ugonjwa wa bawasiri.

    Kwa afya nzuri kabisa kila mtu anahitaji kupata choo walau mara moja mpaka mara tatu kwa siku.

    Baadhi ya wanawake wanapokuwa katika kipindi cha ujauzito wanatokewa kupata tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu na chenye maumivu.

    Wanawake wengi wanaoumwa ugonjwa wa bawasiri ninapowasiliana nao huniambia walipata ugonjwa huo wakati wakiwa wajawazito au mara tu baada ya kujifungua.

    Bawasiri ni matokeo ya kupata choo kigumu kwa muda mrefu na mwishoni hukuletea maumivu wakati unajisaidia haja kubwa, kutoa damu wakati unajisaidia na kukuletea vinyama kwenye njia ya haja kubwa ambavyo vinaweza kukuletea maumivu zaidi wakati unajisaidia.

    Soma hii pia 👇

    Tiba ya bawasiri bila upasuwaji

    Nini chanzo cha kufunga au kupata choo kigumu wakati wa ujauzito?

    Kufunga choo au kupata choo kigumu ni tatizo linalowatokea wajawazito wengi.

    Ni moja kati ya matatizo makuu yanayolalamikiwa na wanawake wengi wawapo wajawazito.

    Karibu asilimia 38 ya wanawake wote wanaopata ujauzito hupatwa na tatizo hili wakati wa ujauzito au baada ya kujifungua.

    Chanzo cha kufunga au kupata choo kigumu wakati wa ujauzito

    Zipo sababu nyingi za kutokea kwa tatizo hili kwa wamama wajawazito ambazo ni pamoja na zifuatazo:

    1. Mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito – Mabadiliko haya hupelekea misuli ya kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula kulegea na kusababisha mwendo wa pole pole wa chakula tumboni na kuleta kufunga choo au kupata choo kigumu.
    2. Kupungua kwa kazi za mwili – Wakati wa ujauzito wanawake wengi hutumia muda mwingi kupumzika.

    Hawajishughulishi na mazoezi wala shughuli nyingine za kuuchosha mwili kama vile mazoezi ya viungo.

    Mara nyingi kufunga choo au kupata choo kigumu ni matokeo ya kupenda kukaa tu chini au kwenye kiti masaa mengi jambo ambalo ni kawaida kwa wanawake wengi wanapokuwa wajawazito.

    1. Baadhi ya dawa wanazotumia wakati wa ujauzito – Wakati wa ujauzito wanawake huanza kutumia dawa na vidonge mbalimbali ili kujilinda na kumlinda mtoto.

    Dawa hizo kwa ajili ya madini na vitamini mbalimbali anazotumia zinaweza pia kumsababishia tatizo la kukosa choo au kupata choo kigumu.

    Vitu unavyoweza kufanya ili kuzuia na kutibu tatizo:

    Nyingi ya njia zinazotumika kuzuia usipate choo kigumu au kufunga choo ndiyo hizo hizo unaweza kuzitumia kutibu tatizo kama tayari unalo.

    Matatizo ya kufunga choo

    Matunda

    Baadhi ya njia zinazotumika kushughulika na tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu kwa mama mjamzito ni pamoja na;

    1. Kula zaidi vyakula vyenye nyuzinyuzi (fiber) – Mboga za majani na matunda uwe ndiyo mlo wako mkuu.

    Asilimia 80 ya chakula chako kwa siku iwe ni matunda na mboga za majani. Matunda kama parachichi na ndizi ni mhimu sana kwa mama mjamzito.

    Chagua mlo wako mmoja katika milo yako mitatu ya siku uwe ni matunda pekee. Unaweza kuamua chakula cha asubuhi au cha usiku kuwa ni matunda pekee mpaka utakaposhiba.

    2. Kunywa maji ya kutosha kila siku: Mama mjamzito au unayenyonyesha unahitaji kuongeza kiasi cha maji unachokunywa kila siku.

    Unahitaji maji glasi 8 mpaka 10 za majai kila siku na pengine zaidi ya hapo kama unaishi maeneo yenye joto.

    Unaweza pia kunywa juisi ya matunda uliyotengeneza mwenyewe nyumbani. Ni vizuri kutumia asali kidogo katika hiyo juisi badala ya sukari.

    3. Punguza au acha kabisa vinywaji vyenye kaffeina – Soda, energy soda, kahawa, chai ya rangi, chokoleti nyeusi, cocoa, nk. Punguza sana matumizi ya sukari na vyakula vigumu kama vile mikate, chapati, viazi vitamu, wali na vingine kama hivyo.

    4. Fanya mazoezi – Unaweza kutumia muda mwingi kupumzika hasa miezi miwili mpaka mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuzuia mimba isitoke kirahisi au kizembe.

    Lakini kuanzia mwezi wa nne wa ujauzito unahimizwa kuwa bize na mazoezi ya viungo hasa ya kutembea tembea kwa miguu na kusimama hapa na hapa na siyo kukaa tu chini au kwenye kiti masaa yote.

    Huhitaji mazoezi mazito au ya kukimbia riadha, mazoezi tu ya kutembea tembea hapa na pale, kuogelea, kucheza muziki wa pole pole na mmeo, kufagia uwanja, kumtembelea jirani yako na mazoezi mengine madogo madogo.

    5. Usitumie simu uwapo chooni – Ukiwa chooni usitumie simu na ni vizuri usitumie choo cha kukaa badala yake utumie cha kuchuchumaa.

    Kwenda chooni na kukaa tu muda mrefu huku unachat na mtu kwenye simu kunaweza kukupotezea hitaji la kupata choo na kukuletea kufunga au kupata choo kigumu.

    6. Kuwa makini na baadhi ya dawa unazotumia – Baadhi ya dawa unazotumia unapokuwa mjamzito kama vile multivitamins, dawa za kuondoa maumivu, dawa za kuondoa gesi au kiungulia, dawa za kuongeza madini chuma na kalsiamu zinaweza kukuongezea uwezekano wa wewe kupata choo kigumu au kukufunga kabisa usipate choo uwapo mjamzito.

    Kubadili aina ya hizo dawa au namna zinavyotumika kunaweza kusaidia kuzuia tatizo la kufunga choo.

    Ni mhimu kwamba unawasiliana na kuonana na daktari wako wa karibu uso kwa uso kwa msaada na maelekezo zaidi juu ya tatizo lako na siyo kuishia facebook.

    Usitumie dawa yoyote unapokuwa mjamzito bila ushauri na uangalizi wa karibu wa daktari.

    Je umekuwa ukitafuta ujauzito bila mafanikio? Kama jibu lako ni ndiyo pata suluhisho la tatizo lako kwa kubonyeza hapa.

    Mjulishe rafiki yako kwenye twitter naye asome post hii kwa kubonyeza ujumbe ufuatao:

    Chanzo cha kufunga au kupata choo kigumu wakati wa ujauzito Click To Tweet

    SHARE post hii na wengine uwapendao

    Fadhili Paulo
    Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
    Imesomwa mara 2

    Let's block ads! (Why?)

    Jumanne, 18 Agosti 2020

    Jinsi ya kuimarisha afya ya mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula

    Jinsi ya kuimarisha afya ya mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula

    Ili kuimarisha mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula unahitaji kula zaidi vyakula vyenye bakteria wazuri.

    Tumboni kwako kuna bakteria wa aina mbili, bakteria wazuri na bakteria wabaya na kwa bahati mbaya mwili au tumbo lako linawahitaji bakteria wote wawili yaani bakteria wazuri na bakteria wabaya ili uendelee kuishi.

    Hata hivyo kwa bahati mbaya watu wengi wanakuwa na bakteria wabaya wengi kuliko bakteria wazuri na hapo ndiyo huwa chanzo kikuu cha magonjwa mengi mwilini kama PID, vidonda vya tumbo, bawasiri, amiba, magonjwa ya virusi, kushuka kwa kinga ya mwili na mengine mengi.

    Ili kuepuka yote hayo unahitaji kuwa unakula vyakula vyenye bakteria wazuri mara kwa mara ili kuweka usawa mzuri wa bakteria tumboni mwako.

    Asilimia zaidi ya 70 ya kinga yako yote ya mwili ipo kwenye kuta za tumbo lako.

    Hii ni kusema linapokuja suala la kuwa na kinga nzuri ya mwili na inayofanya kazi kukulinda unahitaji kuwa makini namna unavyotunza usawa huu wa hawa bakteria tumboni mwako.

    Tumbo lako ndiyo injini ya mwili wako. Maisha yako yote yapo tumboni na kila chakula na kinywaji hufika kwanza tumboni kabla hakijameng’enywa na kusambazwa sehemu zingine za mwili.

    Kwahiyo jambo lolote linaloharibu afya yako ya tumbo ujuwe linaharibu pia kinga yako ya mwili na kukuweka karibu na magonjwa mengine mabaya kama vidonda vya tumbo, bawasiri, saratani ya tumbo, kuishiwa kinga ya mwili na mengine mengi.

    Jinsi ya kuimarisha afya ya mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula

    Ili kuimarisha mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula unahitaji kula zaidi vyakula vyenye bakteria wazuri.

    Vyakula vyenye bakteria wazuri vimegawanyika mara mbili.

    Kuna vyakula vyenyewe vyenye hao bakteria wazuri ambavyo hujulikana kwa kiingereza kama ‘Probiotics’ na kuna vyakula ambavyo ni chakula cha hao bakteria wazuri ambavyo kwa kiingereza hujulikana kama ‘Prebiotics’.

    Probiotics ni vyakula vyenye bakteria wazuri na Prebiotics ni chakula ambacho hao bakteria wazuri wanakula.

    Probiotics ni jeshi, wakati Prebiotics ni chakula cha hao wanajeshi.

    Probiotics ambao ni bakteria wazuri wanaulinda mji wako wa tumbo na kukuimarishia kinga yako ya mwili na ubongo.

    Bakteria wazuri wanahusika pia kushusha msongo wa mawazo (depression) na kuimarisha afya ya moyo.

    Bakteria hawa wazuri pia tafiti mbalimbali zinasema wanaweza pia kukufanya uonekane una ngozi nzuri na ya kuvutia.

    Vipo vidonge vyenye hawa bakteria wazuri (supplements) lakini bado nakushauri uwapate kupitia chakula moja kwa moja.

    VYAKULA VYENYE BAKTERIA WAZURI – PROBIOTICS

    Kwa bahati mbaya kwa hapa kwetu Tanzania vyakula vyenye bakteria wazuri na vinavyopatikana kirahisi ni chakula kimoja tu nao ni MTINDI.

    Mtindi pekee ndiyo chakula chenye bakteria wazuri kinachopatikana kirahisi hapa Tanzania.

    Mtindi ni moja ya vyakula vizuri kabisa vyenye bakteria wazuri ambao wanaweza kuimarisha afya ya mmeng’enyo wako wa chakula.

    Mtindi unatokana na maziwa ya ng’ombe.

    Kula mtindi mara kwa mara kuna uhusiano wa kuimarisha afya yako ya mwili ikihusisha afya ya mifupa. Mtindi una faida nyingi pia kwa watu wenye shinikizo la juu la damu.

    Kwa watoto wadogo mtindi unaweza kusaidia kupunguza tatizo la kuharisha lililotokana na matumizi ya dawa za antibiotics.

    Mtindi pia unaweza kutumika kwa watu wenye aleji na maziwa fresh ya kawaida (lactose intolerance).

    Mtindi mzuri kabisa ni ule uliotengeneza mwenyewe nyumbani.

    Lakini unaweza kutumia pia mtindi wa dukani hasa mtindi wa Tanga Fresh nakuruhusu unaweza kutumia.

    Kama utatumia mtindi wa dukani uwe ni wenyewe peke yake usiwe umeongezwa rangi wala sukari au kingine chochote.

    Robo lita (ml 250) kwa siku ni kiasi sahihi cha mtindi kwa watu wengi.

    Vyovyote itakavyokuwa usizidishe Zaidi ya mtindi nusu lita (ml 500) kwa siku.

    Watu wenye vidonda vya tumbo wanaruhusiwa kula mtindi isipokuwa maziwa fresh ndiyo hawatakiwi kunywa.

    VYAKULA VYA BAKTERIA WAZURI – PREBIOTICS

    Jinsi ya kuimarisha afya ya mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula 1

    Kitunguu Swaumu

    Hivi ni vyakula sasa kwa ajili ya hao bakteria wazuri na unavihitaji kwa wingi ili hao bakteria wazuri wawe na nguvu za kufanya kazi zao vizuri kama inavyowapasa.

    Prebiotics vinatoka katika baadhi ya vyakula vya wanga hasa wanga wenye nyuzinyuzi (fiber) navyo ni pamoja na vyakula vifuatavyo;

    • Mboga za majani
    • Ndizi. Ndizi zenyewe kama zilivyo au ukipata unga wake unaweza kutengeneza uji wa unga wa ndizi
    • Maharage
    • Kitunguu swaumu
    • Kitunguu maji
    • Vyakula jamii ya kunde

    Vitu vingine vinavyoimarisha afya ya mmeng’enyo wa chakula:

    Pia unaweza kuimarisha afya ya mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula kwa kufanya yafuatayo (namba 6 ni mhimu zaidi)

    1. Kunywa maji glasi 2 (nusu lita) mara tu uamkapo kutoka kitandani kila siku. Kunywa tena kiasi hiki cha maji kila nusu saa kabla ya chakula cha asubuhi, mchana na cha jioni kila siku.
    2. Kula chakula kichache milo mingi. Kula hata mara 5 kwa siku lakini chakula kidogo kidogo siyo kingi kwa wakati mmoja.
    3. Kula pole pole ulapo chakula
    4. Hakikisha unapokula chakula huna mawazo mawazo (stress) yoyote.
    5. Kula zaidi vyakula vyenye nyuzi nyuzi
    6. Punguza kukaa chini au kwenye kiti masaa mengi

    Mawasiliano yangu ni WhatsApp +255714800175

    Mjulishe rafiki yako kwenye Twitter naye asome makala hii kwa kubonyeza maneno yafuatayo;

    Jinsi ya kuimarisha afya ya mfumo wako wa mmeng’enyo wa chakula Click To Tweet

    SHARE POST HII NA WENGINE UWAPENDAO

    Fadhili Paulo
    Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
    Imesomwa mara 7

    Let's block ads! (Why?)

    Jumatatu, 17 Agosti 2020

    Vyakula vinavyoondoa maumivu wakati wa hedhi kwa wanawake

    VYAKULA VINAVYOONDOA MAUMIVU WAKATI WA HEDHI KWA WANAWAKE

    KILA mwanamke hupitia hatua ya kupatwa na hedhi mara moja kwa mwezi, ikiwa ni maumbile ya kawaida waliyoumbwa nayo.

    Lakini wanawake wengi husumbuliwa na matatizo kadhaa siku chache kabla au wakati wa siku zao, matatizo hayo hutofautiana kati ya mtu na mtu kutegemeana na afya ya muhusika.

    DALILI ZA MATATIZO YA HEDHI

    Siku chache kabla ya hedhi, baadhi ya wanawake hupatwa na hofu na huwa wenye hasira.

    Husumbuliwa na mfadhaiko wa akili, huumwa na kichwa, matiti hujaa maziwa, hukosa usingizi na kuvimba sehemu za siri.

    Hali hii husababishwa na kukosekana kwa uwiano wa homoni (Homone imbalance) na hali hii huweza kukoma ndani ya saa 24 baada ya kuanza hedhi.

    MAUMIVU MAKALI YA HEDHI

    Wengine hupatwa na maumivu makali sana wakati wa hedhi. Maumivu hayo huwapata akina mama ama siku mbili ama tatu kabla au mara tu waanzapo siku zao.

    Hali hii pia inasababishwa na kutokuwepo kwa uwiano wa homoni mwilini, ambako kumesababishwa na ukosefu wa virutubisho fulani.

    Wengine hutokwa na damu nyingi kuliko kawaida au kukaa katika siku za hedhi kwa kipindi kirefu kuliko kawaida.

    Kuna sababu nyingi zinazoweza kuchangia hali hii, ikiwemo kuugua kwa muda mrefu, kupatwa na hofu, huzuni, mshtuko na sababu nyingine za kitabibu.

    JUISI YA MBOGA ZIFUATAZO HUTIBU

    Kwa kutumia vyakula asilia unaweza kuepukana na maumivu ya mara kwa mara wakati wa siku zako.

    Katika orodha ndefu ya juisi za mboga zinazotibu kwa uhakika matatizo yote ya hedhi, ni Kotimiri (Parsley), mboga ya majani ambayo upatikanaji wake ni rahisi.

    Kwa mujibu wa watafiti, Kotimiri ina uwezo wa kurekebisha uwiano wa homoni hivyo kuondoa matatizo kadhaa ya hedhi.

    Inaelezwa kuwa uwezo wa Kotimiri kurekebisha matatizo ya hedhi unatokana na kuwa na aina ya kirutubisho kiitwacho ‘Apiol’ ambacho pia kimo miongoni mwa homoni za jinsia ya kike (estrogen).

    Maumivu na mvurugiko wa siku hurejea katika hali ya kawaida kwa kunywa juisi ya Kotimiri mara kwa mara.

    Aidha, juisi hiyo inapochanganywa na juisi ya viazi pori (Beet Root), karoti au matango huwa na nguvu zaidi. Kiwango kinachoshauriwa kuchanganya kiwe na ujazo sawa kwa kila aina ya juisi utakayochanganya.

    Juisi yenye mchanganyiko huo ni rahisi kutengeneza na ni dawa inayoweza kumsaidia mwanamke wakati wote wa maisha yake bila kuhitaji kutumia dawa zingine kali za kuzuia maumivu (pain killers) ambazo huwa na madhara baadaye.

    TANGAWIZI NAYO HUTIBU

    Tangawizi nayo ni dawa nzuri sana ya kutibu matatizo yatokanayo na hedhi, hasa katika tatizo la maumivu makali na kutokupata hedhi.

    Chukua kipande cha tangawizi mbichi, kiponde na kiweke kwenye kikombe cha maji ya moto kwa dakika chache, kisha tia sukari kiasi na unywe mchanganyiko huo, kwa siku mara mbili kila baada ya mlo.

    UFUTA NAO NI DAWA

    Ufuta (Sesame) nao ni miongoni mwa mbegu za asili unazoweza kula na kutibu matatizo ya hedhi.

    Saga ufuta na pata unga wake kisha uchanganye na maji ya moto, kunywa mara mbili kwa siku.

    Kinywaji hiki huondoa maumivu wakati wa hedhi kwa wasichana wadogo.

    Ukitumia mara kwa mara kinywaji hiki cha ufuta, hutibu pia tatizo la kupata hedhi kidogo.

    Pia unaweza kuchangaya maji ya kuoga ya uvuguvugu na mbegu za ufuta zilizopondwa pondwa kiasi cha kiganja kimoja, nayo hutoa nafuu kubwa kwa wanaosumbuliwa na maumivu, hasa ukitumia siku mbili kabla ya siku zako.

    PAPAI NALO NI DAWA

    Mungu ametuumba na kutupa mazao mengi ambayo yana uwezo wa kutatua matatizo yetu ya kiafya, iwapo tutagundua siri hiyo.

    Papai bichi nalo linaelezwa na watafiti wetu kuwa lina uwezo wa kulainisha misuli ya njia ya uzazi hivyo kufanya utokaji wa hedhi kuwa mwepesi usio na maumivu.

    Papai huwa na manufaa zaidi kwa wasichana haswa kwa wale wenye tatizo la kutopata siku zao kutokana na kuwa na ‘stress’ au mawazo.

    Utapata faida hiyo kwa kula mara kwa mara tunda hilo bichi (ambalo halijaiva lakini limekomaa)

    Mawasiliano yangu ni WhatsApp +255714800175

    Share na wengine uwapendao

    Fadhili Paulo
    Latest posts by Fadhili Paulo (see all)
    Imesomwa mara 1

    Let's block ads! (Why?)

    20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

      Ø¥ِÙ†َّ الشِّرْÙƒَ Ù„َظُÙ„ْÙ…ٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...