Translate

Jumanne, 21 Aprili 2020

Tabia 7 zinazokuchelewesha kupona bawasiri

Tabia 7 zinazokuchelewesha kupona bawasiri

Tabia 7 zinazokuchelewesha kupona bawasiri

1. Kutokunywa maji ya kutosha kila siku

Tafiti zinasema kutokunywa maji ya kutosha kila siku kunaweza kukuletea ugonjwa wa bawasiri.

Kama haunywi maji mengi ya kutosha kila siku ni rahisi sana wewe kupatwa na tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu kila mara na mwisho wake ni bawasiri.

Maji ni maji. Juisi, chai, soda au pombe haviwezi kuwa mbadala wa maji na tena vinywaji hivi vinaweza kukausha zaidi hata yale maji machache uliyonayo tayari mwilini.

Haijalishi uwe unaishi sehemu zenye joto au sehemu za baridi jizoeshe tabia ya kupenda kunywa maji mengi ya kutosha kila siku kwa mjibu wa uzito wako.

2. Kukaa tu chini au kwenye kiti masaa mengi

Kwenye dunia hii ya sasa ya kidigitali unaweza kupata vitu vingi ukiwa umekaa tu kwenye computer, simu au runinga (TV).

Wakati maisha yanaweza kuonekana rahisi kuishi kwa namna hii bado aina hii ya maisha inaweza kudhoofisha misuli ya mwili wako na kukuletea Zaidi bawasiri.

Unapokaa tu masaa mengi ni rahisi kuongezeka uzito na unene ni moja ya sababu kuu inayosababisha ugonjwa wa bawasiri.

Mazoezi ya viungo mara nyingi ni dawa ya uhakika kwa magonjwa mengi yatokanayo na tabia.

Kukaa mua mrefu kwenye kiti au chini kunavuruga na kuharibu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula na kukuletea magonjwa kama bawasiri, vidonda vya tumbo, gesi kujaa tumboni na mengine mengi yanayohusiana na tumbo.

Tazama TV kwa vipindi vile mhimu tu hasa taarifa ya habari, tofauti na hapo usitumie zaidi ya saa moja ukiwa umekaa tu ili kuepuka kuongeza zaidi tatizo la bawasiri.

3. Kula Zaidi vyakula feki

Kama unaishi mjini basi ni ukweli usiopingika kwamba unakula Zaidi vyakula feki (junk foods) na tena vingine vyenye kusisimua (spiced).

Vyakula hivi huongeza msukumo au presha sehemu ya eneo la misuli ya haja kubwa. Jambo hili linaweza kukuletea bawasiri au kuchelewesha uponyaji wa bawasiri uliyonayo tayari.

Vyakula feki ni vyakula vya madukani, vya kwenye makopo au vya kwenye migahawa (fast foods restaurants).

Pendelea kula vyakula vya asili zaidi na vinywaji vya asili zaidi kama unataka kupona haraka ugonjwa huu mbaya wa bawasiri.

4. Kushiriki tendo la ndoa kinyume na maumbile

Hii dunia sijuwi inaelekea wapi.

Kuna tabia mpya imeibuka kwenye kizazi cha sasa watu wanapenda kufanya tendo la ndoa kinyume na maumbile na wengine wanaimba mpaka nyimbo za muziki kabisa kujaribu kuhamasisha na kuwaonyesha wengine kwamba hilo ni jambo la kawaida.

Mapenzi kinyume na maumbile ni sababu nyingine inayokukwamisha usipone bawasiri yako kwa haraka na isijirudie tena.

Kwahiyo kama unataka kupona bawasiri amua kuachana na tabia hii mbaya haraka iwezekanavyo.

5. Kukaa muda mrefu chooni

Kama wewe ni mmoja wa wale ambao ukiwa chooni unaendelea kutumia simu na kuangalia picha facebook basi ujuwe unachelewesha uponyaji wa bawasiri yako bila kufahamu.

Kukaa muda mrefu chooni kunailazimisha damu kujaa na kusukumwa kwenye mishipa ya tundu la haja kubwa kitendo kinachoweza kuongeza uwezekano wa wewe kupatwa zaidi na bawasiri.

Ukienda chooni usiende na simu na usikae huko zaidi ya muda unaotakiwa kuwa huko na ukimaliza haja yako basi mara moja utoke.

6. Unapochelewa kwenda chooni

Kuna wakati inaweza kukutokea upo mbali kidogo na nyumbani na ukapatwa na hitaji la kutaka kupata choo lakini kwa sababu upo mbali na nyumbani unaweza kuamua kujizuia usiingie choo cha kulipia mpaka utakaporudi nyumbani.

Au wakati mwingine tu hata kama upo nyumbani unaweza kuwa upo bize na kazi au jambo fulani kiasi kwamba unapatwa na hitaji la kwenda chooni na bado hukimbii haraka kwenda chooni.

Kama utaendelea na tabia hii mbaya kwa kipindi kirefu inaweza kukuletea au kukuongezea zaidi uvimbe wa bawasiri na kama tabia hii haitadhibitiwa inaweza kukuletea dalili zenye maumivu za bawasiri.

7. Kutokula vyakula vya kutosha vyenye nyuzinyuzi kila siku

Vyakula vyenye nyuzi nyuzi ni mhimu na vya lazima hasa kwa mtu unayesumbuliwa na bawasiri.

Vyakula vyenye nyuzi nyuzi ni mhimu kwa ajili ya mwenendo wa kawaida wa tumbo.

Ukiona unapatwa na tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu kila mara ni ishara hauli vyakula vyenye nyuz nyuzi vya kutosha kila siku.

Unapopata choo kigumu kinaweza kukuletea maumivu sehemu ya haja kubwa na kukuletea dalili za bawasiri.

Kama unahitaji dawa ya asili kwa ajili ya kutibu bawasiri niachie ujumbe WhatsApp +255714800175

Kama unapenda kujifunza mengi zaidi kuhusu ugonjwa wa bawasiri bonyeza HAPA.

Mjulishe rafiki yako kwenye Twitter asome makala hii kwa kubonyeza maneno yafuatayo:

Tabia 7 zinazokuchelewesha kupona bawasiri Click To Tweet

SHARE post hii kwa ajili ya wengine.

Imesomwa mara 9

Let's block ads! (Why?)

Jumanne, 7 Aprili 2020

Namna mfumo wa kinga unavyopambana na virusi vya Corona

Virusi vya corona

CoronaVirus: Wanasayansi nchini Australia wanaonyesha namna mfumo wa kinga unavyopambana na virusi.

Wanasayansi nchini Australia wamesema kuwa wamegundua namna gani mfumo wa kinga mwilini unavyoweza kupambana na virusi vya Covid-19.

Utafiti wao, uliochapishwa kwenye jarida la Nature siku ya Jumanne, unaonesha kuwa watu wanapona maambukizi ya virusi, kama ambavyo wanavyopona mafua.

Duniani kote, mamlaka zimethibitisha maambukizi kwa zaidi ya watu 160,000 ya virusi vya corona na vifo karibu 6,500.

”Ugunduzi huu ni muhimu kwa sababu ni mara ya kwanza ambapo tunafahamishwa namna ambavyo kinga zetu zinavyopambana na virusi vya corona,” amesema mwandishi mwenza Profesa Katherine Kedzierska.

Taasisi ya utafiti ya magonjwa ya maambukizi na kinga ya Peter Doherty wa Melbourne imesifiwa na wataalamu wengine, mmoja akieleza kuwa ni ”mafanikio mapya”.

Soma hii pia > Dawa ya asili inayoongeza kinga ya mwili

Kilichobainika:

Watu wengi wamepona virusi vya Covid-19, ikimaanisha kuwa tayari ilijulikana kuwa mfumo wa kinga unaweza kupambana na virusi.

Lakini kwa mara ya kwanza, utafiti ulibaini aina nne za seli za kinga ambazo zinaweza kupambana na Covid-19.

Zilichunguzwa kwa kumfuatilia mgonjwa ambaye alikuwa na maambukizi ya virusi lakini ambaye hakuwa na matatizo ya kiafya hapo awali.

Mwanamke mmoja mwenye miaka 47 kutoka mjini Wuhan, China aliyewasili hospitali nchini Australia alipona ndani ya siku 14.

Profesa Kedzierska ameiambia BBC kuwa timu yake imechunguza ”uwezo wa kinga kupambana na virusi” kwa mgonjwa huyu.

Siku tatu kabla mwanamke mmoja alianza kujisikia vizuri, seli zilioonekana kwenye mfumo wa damu. Katika wagonjwa wa maradhi ya mfumo wa upumuaji, seli hizi pia zinaonekana kabla ya kupona, Profesa Kedzierska alieleza.

‘Tulifurahia matokeo yetu na ukweli kuwa tunaweza kuona seli za kinga kwa mtu aliyegundulika, kabla ya afya yake kuimarika,” aliiambia BBC.

Wanasayansi walifanya uchunguzi wao kwa wiki nne ili kutathimini hilo, aliongeza.

Hatua hii imesaidia nini?

Kubaini wakati seli za kinga zinaingia zinaweza kusaidia “kutabiri mwenendo wa virusi”, alisema Prof Bruce Thompson, Mkuu wa kitivo cha sayansi ya afya katika Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Swinburne.

Waziri wa Afya wa Australia Greg Hunt alisema kupatikana kwa ukweli huu pia kunaweza kusaidia “kufuatilia kwa haraka” chanjo na tiba inayowezekana kwa wagonjwa walioambukizwa.

Prof Kedzierska alisema hatua inayofuata kwa wanasayansi ni kutazama kwa nini kinga ni dhaifu kwa wagonjwa walio katika hali mbaya.

“Ni muhimu sana sasa kuelewa ni nini kinachopungua au tofauti kwa wagonjwa ambao wamekufa au ambao wana ugonjwa ulio katika hali mbaya – kwa hivyo tunaweza kuelewa jinsi ya kuwalinda,” alisema.

Mnamo Januari, taasisi hiyo ikawa ya kwanza ulimwenguni kuunda tena virusi nje ya Uchina.

Kituo hicho kimepokea fedha zaidi kutoka kwa serikali ya Australia na pia michango kutoka kwa wafanyabiashara na bilionea wa Kichina Jack Ma.

Mjulishe rafiki yako kwenye twitter naye asome post hii kwa kubonyeza ujumbe ufuatao:

Namna mfumo wa kinga unavyopambana na virusi vya Corona Click To Tweet

Habari hii ilichapishwa na BBC Tarehe 17 Machi 2020

SOURCE

Imesomwa mara 4

Let's block ads! (Why?)

Jumatano, 18 Machi 2020

Uhusiano wa vidonda vya tumbo na saratani ya tumbo

Uhusiano wa vidonda vya tumbo na saratani ya tumbo

Kwa kawaida vidonda vya tumbo husababishwa na bakteria aitwaye Helicobacter pylori au kwa kifupi H. pylori. Watu wawili katika kila watu watatu hapa duniani wana huyu bakteria tumboni mwao Click To Tweet

Na ingawa wengi wa watu hawa wenye huyu bakteria hawaonyeshi dalili yoyote ya kuumwa vidonda vya tumbo bado baadhi yao wanatokewa kuumwa.

Karibu asilimia 2 mpaka 20 ya watu wenye H. pylori wanaugua vidonda vya tumbo.

Ukiacha uwezo huo wa huyu bakteria H. pylori wa kusababisha vidonda vya tumbo, bakteria huyu huyu anahusika na ugonjwa mwingine mbaya wa saratani ya tumbo.

Ukweli ni kuwa bakteria huyu H. pylori hushambulia ulinzi asili unaolinda ukuta wa tumbo jambo ambalo ni mhimu sana na kutokea kwa saratani ya tumbo.

Soma hii pia > Dawa ya asili inayotibu saratani ya tezidume

H. pylori siyo sababu pekee ya kuugua saratani ya utumbo, sababu nyingine zinazoweza kuleta saratani ya tumbo ni pamoja na zifuatazo:

  • Umri. Watu wengi wenye saratani ya tumbo wana miaka 70 na kuendelea
  • Kuwa na maumivu ya tumbo yasiyoisha
  • Ukiwa ni mwanaume
  • Uvutaji sigara, tumbaku, bangi na vingine kama hivyo
  • Kurithi
  • Kula sana vyakula vilivyokaushwa kwa moshi na kuongezwa chumvi
  • Pombe
  • Vyakula na vinywaji vingi vya viwandani
  • Nyama choma
  • Sukari

Habari njema ni kuwa ukiwa na mazoea ya kula mara kwa mara vyakula vyenye beta-carotene na vitamini C, vyakula kama vile matunda na mboga za majani kunaweza kukupunguzia uwezekano wa kupatwa na saratani ya tumbo.

Majani mabichi ya mti wa mlonge yana vitamini C mara 7 zaidi ya ile ya kwenye chungwa. Unaweza kula ujazo wa kiganja kimoja cha mkono wako kutwa mara moja kwenye kachumbali au usage sambamba na juisi yoyote ya matunda.

Majani fresh ya mlonge

Saratani yoyote siyo hii ya tumbo tu, ni matokeo ya mwisho ya asidi kuzidi na kudumu mwilini kwa kipindi kirefu.

Tunatambuwa kwamba asidi inahusika pia na kutokea kwa vidonda vya tumbo.

Zaidi ya nusu ya watu wote wenye vidonda vya tumbo vidonda vyao ni matokeo ya asidi kuzidi mwilini na siyo H. pylori  bakteria moja kwa moja.

Ukiacha mboga za majani, matunda na maji ya kunywa vyakula na vinywaji karibu vyote vina asidi.

Kinyume cha asidi ni alkalini. Asidi hujulikana pia kama tindikali.

Vyakula na vinywaji vingi ambavyo mgonjwa wa vidonda vya tumbo anakatazwa kula na kunywa vina asidi nyingi ndani yake.

Tafiti za hivi karibuni zinathibitisha kwamba vidonda vya tumbo vinao uwezo wa kukuletea saratani ya tumbo ikiwa hutachukuwa hatua ya kuvitibu kwa muda mrefu.

Vitu vyote viwili vinavyoleta vidonda vya tumbo yaani huyo bakteria na asidi vinahusika moja kwa moja na kutokea kwa saratani ya tumbo.

Vidonda vya tumbo ni vidonda vinavyojitokeza ndani ya mwili kwenye kuta za tumbo. Vidonda hivi vinaunda uwazi kwenye ukuta wa tumbo wakati ulinzi wa ukuta wa tumbo unapokuwa dhaifu kama matokeo ya bakteria au asidi kuzidi mwilini.

Huo uwazi unaojitengeneza (yaani kidonda) ndiyo njia ambayo bakteria H.Pylori anaitumia kuziingia kuta za tumbo na kuleta saratani.

Bakteria huyu anapoziingia kuta za tumbo kupitia hivyo vidonda anasababisha mabadiliko kwenye kinasaba (DNA) na kusababisha kudhurika kwa seli za tumbo

Kwa wagonjwa wa vidonda vya tumbo wanaopata maumivu ya tumbo, kujisikia vibaya au kutokewa na kutapika mara kwa mara wanashauriwa kuwahi mapema hospitali kwa ajili ya vipimo haraka iwezekanavyo.

Dalili hizi zinaweza kuwa ni dalili za saratani ya tumbo na siyo vidonda vya tumbo pekee.

Ukiona miguu inavimba, inawaka moto au inachomachoma kwenye nyayo ni dalili za wazi za mwili wako kuzidiwa na asidi au sumu. Matokeo ya mwisho kabisa ya dalili hizi ni saratani.

Ni ishara unatumia muda mwingi kukaa kwenye kiti hivyo damu inashuka chini kwenye miguu na kubaki huko bila kurudi juu ya mwili ili ibadilike na kusafishwa na ndiyo mwisho inakuletea asidi kisha miguu kuwaka moto na mwisho kabisa kama hutajitibia mapema ni saratani.

MAZOEZI MAALUMU KWA ANAYESUMBULIWA NA MIGUU KUWAKA MOTO AU ASIDI KUZIDI MWILINI

Unalala chali, nyoosha mikono chini. Kisha nyanyua mguu mmoja juu unyooke, shusha chini mguu na unyanyue wa pili hivyo hivyo juu kisha chini. Endelea hivyo hivyo kwa mara kumi kumi kwa round 5. Zoezi lichukuwe dk 10

Kisha simama, chuchumaa simama, chuchumaa simama, hivyo hivyo mara 15 kwa round 5. Zoezi hili linaondoa asidi mwilini haraka kuliko zoezi lingine lolote

Pia unasimama wima, nyoosha mikono yote juu na uishushe mabegani. Hivyo hivyo mikono juu mikono mabegani mara 15 kwa round 5

Mwisho jipigie saluti mwenyewe ukianzia mkono wa kulia mara 15 hamia mkono wa kushoto mara 15 tena kwa round 5

Fanya hivi mara 4 mpaka 5 kwa wiki.

Asidi ni sumu au takataka zilizomo ndani ya mwili zinazoweza kukuletea magonjwa na maumivu mbalimbali mwilini ikiwemo miguu kuwaka moto, vidonda vya tumbo na maumivu yoyote mwilini ambayo hayajaletwa na ajali au jeraha nje ya mwili

Vidonda vya tumbo ni ugonjwa unaotibika na hata saratani ya tumbo ni ugonjwa unaotibika hasa katika hatua za mwanzo.

Kitakachokuletea saratani ya tumbo ni kitendo cha wewe kuwa na vidonda vya tumbo na ukaamua kuishi navyo. Ni kitendo cha wewe kuwa na vidonda vya tumbo na ukakubali viwe ni sehemu ya maisha yako ndiko kunakopelekea saratani ya tumbo.

Kama unahitaji dawa ya asili inayotibu kabisa vidonda vya tumbo niachie tu ujumbe WhatsApp +255714800175 (nimesema niachie ujumbe WhatsApp, sijaandika nipigie simu).

Kama unapenda kujifunza mengi kuhusu vidonda vya tumbo bonyeza HAPA.

Jiunge na mimi na watu wengine zaidi ya 94000 kwenye ukurasa wangu wa facebook kwa kubonyeza hapa

Share post hii na watu wengine uwapendao.

Imesomwa mara 31

Let's block ads! (Why?)

Madhara zaidi ya Kisukari katika mwili

Kupenda vitu vitamu hususani jamii ya sukari huwa ni tamu sana kwenye ulimi lakini changamoto inakuja kule inakoelekea kwa ajili ya kutunzwa na kutumika, hapo ndo husababisha changamoto mbalimbali mwilini hasa kwenye baadhi ya viungo vya mwili.

Madhara ya muda mrefu ya ugonjwa wa kisukari huanza taratibu, kadiri unavyo kuwa na sukari na unavyo shindwa kuchukua hatua juu ya sukari hiyo ndivyo hatari ya kupata madhara makubwa huongezeka.

Pia ikumbukwe madhara yatoka nayo na kisukari huweza kuhatarisha maisha ya mtu.

Yafuatayo ni madhara ya sukari inapozidi mwili na kiwango sahihi cha sukari inayotakiwa mwili pale unapokuwa umekula chakula:

1. Vidonda vya miguuni

Ugonjwa wa kisukari huathiri miguuni hasa pale unapopata ganzi inapelekea kushindwa kuhisi maumivu hivyo hata ukipata jeraha au mchubuko unakuwa huhisi maumivu ya aina yoyote.

Unakuwa hauna tofauti na aliechomwa sindano ya ganzi kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji.

Vidonda vya mtu mwenye kisukari ni vigumu sana kupona kwa sababu damu inakuwa haifiki ya kutosha kwenye kidonda na asilimia kubwa bakteria wabaya huanza kukishambulia kwa kasi kwa sababu kinakuwa ni kitamu 

Kwa kuwa kidonda kina bakteria na kinaonekana kuwa na malengelenge ya mafuta na hao bakteria hushambulia kwa kasi hivyo kusababisha kuongezeka kwa kidonda na mwishowe kukatwa endapo hutawahi huduma mapema ya kujikinga. ·        

2. Kutokuona vizuri au mtoto wa jicho

Mishipa ya kwenye macho huwa ni midogo midogo sana na iko laini sana ukiliganisha na mishipa ya sehemu zingine za mwili hivyo inapoingiliwa na sukari damu hushidwa kupita ya kutosha sehemu za macho na kumfanya mtu awe anaona ukungu ukungu au kutokuona kabisa. ·        

3. Madhara ya figo

Figo inapokuwa imezidiwa na kiwago kingi cha sukari hulazimika kupunguza maji ya ziada na utengenezaji wa calcium kwa ajili ya kulinda mifupa hivyo sukari nyingi kukimbilia kwenye damu na baadaye huwa sumu mwilini. ·        

4. Kiharusi (stroke)

Kwa kuwa madhara ya sukari mojawapo ni kudhoofisha mishipa kwenye mwili hivyo mtu wa kisukari ana hatari kubwa ya kupata stroke kwa sababu baadhi ya mishipa kwenye ubongo huathiriwa na kukosa uwezo wa kupitisha damu ya kutosha na mwishoe kupasuka na kusababisha kiharusi. ·        

5. Maradhi ya moyo

Vyanzo vya mishipa huanzia kwenye moyo na kusambaa pande zingine za mwili, moyo huathiriwa na ugonjwa wa kisukari kwa sababu sukari hudhoofisha mishipa na kumfanya mtu kuwa dhaifu hivyo kama damu haipiti ya kutosha kwenye mishipa inakuwa ni kirahisi kupata magonjwa ya moyo kama vile moyo kupanuka, moyo kuwa na tundo pamoja na kuongezeka kwa mapigo ya moyo. ·        

6. Kwa wanaume kuishiwa nguvu za kiume

Hili ni tatizo kubwa kwa wanaume kwa sababu mfumo wa uzazi wa mwanaume umeundwa kwa mishipa na misuli, kama patakuwa hakupati ujazo mzuri wa damu inakuwa ni rahisi sana kushidwa kushiriki tendo ndoa na wengi wao wanapopatwa na hali kama hii huigiwa na presha au msongo wa mawazo na kuibua matatizo mengine tena.  

Hayo ni baadhi ya madhara anayopatwa mtu mwenye kisukari japo anaweza kupatwa na changamoto zingine nyingi kwenye mwili wake na kumpelekea kupata shida awe mtoto au mtu mzima, lakini kwa kukosa uelewa na umakini zaidi kundi la watu wengi huishia kukatwa baadhi ya viungo na mwishowe kifo.

7. Kuvurugika kwa vichocheo vya mwili

8. Hatari ya kupata maambukizi kutokana na kushindwa kufanya kazi vizuri kwa seli nyeupe za damu

9. Kwa wamama wenye kisukari kinacho tokana na ujauzito kupata  aina ya pili ya kisukari

10. Kifafa Cha mimba

11. Matatizo ya ganzi na kupooza endapo kisukari kitaathiri mishipa ya fahamu

Soma hii pia > Chakula cha mgonjwa wa kisukari aina ya pili

Kama unahitaji dawa ya asili inayotibu kisukari aina ya pili, niachie tu ujumbe WhatsApp +255714800175.

Makala hii inaendelea kuboreshwa kwa kuongeza picha na maelezo zaidi, endelea kuja …

Tafadhali SHARE kwa ajili ya wengine uwapendao.

Imesomwa mara 23

Let's block ads! (Why?)

Hadithi 8 za uongo kuhusu bawasiri

Hadithi 8 za uongo kuhusu bawasiri

Hadithi namba 1: Ukiugua bawasiri hata ukipona utarudia kuugua tena na tena.

Ukweli ni upi: Madai haya hayana ukweli wowote hasa kwa yule ambaye amepata ugonjwa huu kwa sababu za muda mfupi tu kama vile ujauzito.  

Kwa kawaida ukitibiwa ugonjwa huu na ukapona kitakachosababisha upate tena ugonjwa huu ni kutokuzingatia masharti unayopewa juu ya vyakula na namna ya kuishi kwa ujumla ili kujikinga na tatizo lisijirudie tena.

Hata baada ya kupona bado unatakiwa uendelee kula vizuri na kuishi vizuri wakati wote ili kwamba usipate tena ugonjwa huu.

Ni ugonjwa wa tabia na hivyo kadri unavyojiepusha na tabia zinazopelekea ugonjwa huu ndivyo unavyojiweka mbali na kuugua tena.

Hadithi: Bawasiri inaweza kuleta saratani ya utumbo mpana

Ukweli ni upi: Bawasiri kama bawasiri haiwezi kukuletea saratani ya utumbo mpana.

Hata hivyo dalili za bawasiri zinafanana sana na zile za ugonjwa wa saratani ya utumbo mpana (colon cancer).

Kwahiyo ni mhimu sana kwamba unahangaika kwa vyovyote utakavyoweza kupata matibabu kwa ajili ya bawasiri mapema wakati inapojitokeza na siyo kusubiri mpaka hali iwe mbaya kiasi cha kufananishwa na saratani.

Hadithi: Ninakula vyakula vya nyuzinyuzi hivyo siwezi kuugua bawasiri

Ukweli ni huu: Wakati kula vizuri hasa kupendelea kula vyakula vyenye nyuzinyuzi ni hatua nzuri ya kujikinga usipatwe na bawasiri bado hilo pekee halizuii wewe kuugua ugonjwa huu.

Kuna sababu zingine kuu zinazoleta ugonjwa huu ikiwemo tabia ya kukaa tu chini au kwenye kiti masaa mengi, kula ugali wa sembe na kutokunywa maji mengi ya kutosha kila siku.

Hadithi: Kuendesha baiskeli muda mrefu kunaweza kusababisha bawasiri.

Ukweli: Miaka mingi mababu zetu wamekuwa wakitegemea baiskeli kama usafiri wao mkuu na hawakuugua bawasiri kama tunavyoteseka sisi miaka ya sasa.

Kuendesha baiskeli kunaweza kusikuletee bawasiri moja kwa moja ila kunaweza kuwa ni sababu mojawapo ya kutokea kwa dalili au hatua za mwanzo za bawasiri.

Kama unaendesha baiskeli lakini unakula vizuri na baadaye unakuwa unatumia muda mwingi kusimama au kutembeatembea na siyo kukaa tu kwenye kiti kuna uwezekano mdogo wa wewe kupatwa na bawasiri.

Kinachosaidia ni kwamba baiskeli tofauti na pikipiki au gari baiskeli ni sehemu ya mazoezi pia kwa mwili hivyo kuna faida za kiafya unaweza kuzipata ambazo zitakusaidia usipate bawasiri kirahisi kama vile ungekuwa boda boda au dereva wa gari.

Hadithi: Ni watu wazima tu ndiyo hupata bawasiri

Ukweli: Ingawa ni kweli ugonjwa huu kwa sehemu kubwa umekuwa ukionekana mara nyingi ukiwatokea watu wazima bado haimaanishi kwamba ni watu wazima tu ndiyo wanaougua ugonjwa huu.

Ukweli ni kuwa mtu wa umri wowote ambaye muda mwingi anatumia kukaa chini au kwenye kiti, hali vyakula vingi vya nyuzinyuzi (fiber) na anakula zaidi vyakula feki anaweza kupata ugonjwa huu bila kujali umri wake.

Kwahiyo watoto na hata watu wazima wazee sana pia wote wanaweza kupatwa na ugonjwa huu.

Ugonjwa huu unaonekana kuwatesa zaidi wanawake kuliko wanaume sababu ya tabia yao ya kupenda kukaa muda mrefu kwenye kiti na wengine kwa sababu zinazotokana na ujauzito.

Hadithi: Mara zote bawasiri huambatana na kutoka damu

Ukweli unasemaje: Madai haya tena hayana ukweli. Dalili za bawasiri zinaweza kutokea bila kuhusisha kutoka damu wakati wa kujisaidia.

Kuna bawasiri za aina mbili hasa ambazo ni bawasiri ya ndani na bawasiri ya nje na zote mbili siyo lazima zipelekee kuvuja damu.

Kwenye bawasiri ya nje uvimbe unaweza kusikika na kuonekana sehemu ya nje ya tundu la haja kubwa na inaweza kuleta maumivu wakati unajisaidia lakini siyo lazima iambatane na damu.

Ikikutokea kwamba bawasiri yako inaambatana na kutokwa damu utahitaji matibabu ya haraka zaidi kwani unaweza kupatwa na madhara mengine mabaya zaidi kiafya yatokanayo na damu kupungua kwa kupotea hivyo pole pole kila siku.

Hadithi: Bawasiri haiponi mpaka ufanye upasuwaji.

Ukweli ni: Upasuwaji (operation) siyo njia pekee ya kutibu tatizo hili. Upasuaji ni njia ya haraka (quick fix) ya kuondoa uvimbe wa bawasiri ya nje. Hapa unakuwa umeondoa uvimbe uliotokana na bawasiri na siyo bawasiri yenyewe.

Bawasiri ni ugonjwa unaoanzia ndani ya mwili tumboni kwenye mmeng’enyo wa chakula.

Uonapo uvimbe kwenye sehemu ya tundu la haja kubwa hiyo siyo bawasiri, huo ni uvimbe kama matokeo ya bawasiri.

Pamoja na upasuaji ili kuondoa uvimbe bado utahitaji kula vizuri na kutumia baadhi ya dawa za kunywa ili kwamba chanzo cha ugonjwa wenyewe kilichojiunda tumboni kiweze kupotea ili kwamba usiendelee tena kuugua ugonjwa huu.

Utakuwa shuhuda hapa kwamba umeshawahi kufanya upasuaji na bado wiki kadhaa mbeleni uliona uvimbe ukijirudia tena na ukabaki unashangaa.

Hadithi: Bawasiri ni ugonjwa usiotibika

Ukweli upoje: Bawasiri siyo UKIMWI. Ni ugonjwa wa kawaida na unatibika na kupotea.

Inawezekana umeshatumia dawa za kila namna na huoni dalili zozote za kupona.

Bado kuna watu wanapona bawasiri hasa wale wanaozingatia maelezo wanayopewa na matabibu juu ya vyakula na namna ya kuishi kwa ujumla.

Ni wale tu wanaoweka matumaini yote kwenye dawa bila kujibidiisha kubadili vyakula na mifumo yao ya maisha inayopelekea ugonjwa wa bawasiri ndiyo hawaponi.

Hata kwa upande wa vidonda vya tumbo kuna imani za namna hii kwamba ni ugonjwa usiotibika. Siyo kweli, wapo wanaopona na mimi ninazo shuhuda za watu wanaopona bawasiri hata vidonda vya tumbo. Usikae tu na kuishi na ugonjwa wowote, chukua hatua.

Hitimisho

Bawasiri ni ugonjwa wa kawaida na unatibika.

Tofauti na unavyoweza kufikiri na pengine hata kuona aibu, ni kuwa ugonjwa huu wanaugua watu wengi sana na hauchagui maskini wala tajiri.

Ni ugonjwa wa pili unaotesa watu wengi baada ya U.T.I na una uhusiano wa karibu na vidonda vya tumbo.

Upatapo ugonjwa huu usione aibu, chukua hatua mapema ili kuweza kupona kirahisi kuliko ukisubiri hali iwe mbaya zaidi kiasi cha matibabu kukugharimu zaidi na kuchukuwa muda mrefu kuliko kawaida.

Kama unahitaji dawa ya asili kwa ajili ya kutibu bawasiri niachie ujumbe WhatsApp +255714800175

Kama unapenda kujifunza mengi zaidi kuhusu ugonjwa wa bawasiri bonyeza HAPA.

SHARE post hii kwa ajili ya wengine.

Imesomwa mara 29

Let's block ads! (Why?)

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...