Translate

Jumatano, 1 Mei 2019

Kundi lenye kuokoka na Moto 01 – Masjid Firdaws Ifakara Morogoroja



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2WlYXww
via IFTTT

Kundi lenye kuokoka na Moto 02 – Masjid Firdaws Ifakara Morogoroja



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2DI7en1
via IFTTT

Nasaha kwa wanawake wa Kiislamu 02 – Masjid Firdaws Ifakara Morogoro



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2Lcl8Ut
via IFTTT

Nasaha kwa wanawake wa Kiislamu 01 – Masjid Firdaws Ifakara Morogoro



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2VBJyee
via IFTTT

42. Hukumu ya mwenye kufa wakati wa kujitetea

Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) amesema:

“Na ikitokea yeye ndiye akafa wakati yuko anaitetea nafsi yake na mali yake, kunatarajiwa kwake kufa shahidi. Hivyo ndivyo ilivyotajwa katika Hadiyth na mapokezi. Vinaamrisha tu kujitetea na wala haviamrishi yule mshambulizi kuuawa wala kufuatwa. Wala usimalize uhai wake endapo ataanguka chini au akapata majeraha. Hafai vilevile kwake kumuua wala kumsimamishia adhabu iwapo atamkamata. Badala yake anatakiwa kumpeleka mahakamani na awaache wamuhukumu.”

MAELEZO

Hayo ni kutokana na Hadiyth kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesema:

“Kuna mtu alikuja kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Ee Mtume wa Allaah! Unaonaje iwapo atakuja mtu anayetaka kuchukua mali yangu?” Akasema: “Usimpe.” Akauliza: “Akinipiga vita?” Akajibu: “Mpige vita.” Akauliza: “Akiniua?” Akajibu: “Basi wewe utakuwa shahidi.” Akauliza: “Nikimuua?” Akajibu: “Basi yeye ataingia Motoni.”[1]

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema vilevile:

“Atakayeuawa kwa ajili ya kutetea nafsi yake ni shahidi. Atakayeuawa kwa ajili ya kutetea mali yake ni shahidi. Atakayeuawa kwa ajili ya kutetea dini yake ni shahidi.”[2]

Haijuzu kuwaua majeruhi wao, kuwafuata wasaliti wao, kuchukua mali zao wala kuwateka wanawake wao – kwa sababu ni waislamu.

[1] Muslim (140).

[2] Abu Daawuud (4772), at-Tirmidhiy (1421) na an-Nasaa’iy (4094). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1411).



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2WcuQr4
via IFTTT

41. Inafaa kuwapiga vita wezi na Khawaarij

Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) amesema:

“Inafaa kuwapiga vita wezi na Khawaarij. Wakimshambulia mtu au mali yake basi inafaa kwake kupambana kwa ajili ya nafsi yake na mali yake. Ajitetee kwa yote ayawezayo. Hata hivyo haifai kwake kuwafuata au kuwatafuta wakimuacha. Hakuna mwingine isipokuwa kiongozi au mtawala wa waislamu ndiye anayeweza kufanya kitu kama hicho. Ana haki tu ya kujitetea mahala hapo. Anuie kutomuua yeyote. Ikitokea wakati wa kuitetea nafsi yake akamuua yule mshambulizi, basi atajaza yule mshambulizi.”

MAELEZO

Kuwapiga vita waasi, wezi na Khawaarij inafaa pindi watapomvamia mtu au mali yake. Wakitaka kuvunja heshima ya familia ya mtu basi ni lazima kwake kuitetea. Inafaa kwake kuitetea nafsi yake na mali yake na ni lazima kuitetea familia yake kwa njia zote anazoweza.

Katika kipande hichi Imaam Ahmad ametilia mkazo kwamba mtu asifuatilie nyayo zao wakimwacha salama yule mshambuliwaji na wakakimbia. Kwa sababu ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) wakati alipopigana na Khawaarij aliamrisha wasifuatiliwe iwapo watakimbia[1]. ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) ni mmoja katika wale makhaliyfah waongofu ambaye mwenendo wake unatakiwa kufuatwa.

[1] al-Bayhaqiy katika ”as-Sunan al-Kubraa” (16521).



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2DIGUck
via IFTTT

40. Haifai kufanya mapambano na uasi dhidi ya mahakama

Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) amesema:

“Si halali kumpiga vita mtawala. Asiwepo mtu yeyote atakayemfanyia uasi. Atakayefanya hivo basi ni mtu wa Bid´ah aliye mbali na Sunnah na njia iliyonyooka.”

MAELEZO

Allaah (´Azza wa Jall) ameamrisha kumtii kiongozi midhali ni muislamu. Haijuzu kumfanyia uasi ijapokuwa atadhulumu, atakupiga mgongo wako na kuchukua mali yako. Hudhayfah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Msikilizeni na mumtii kiongozi hata kama atakupiga mgongo wako na kuchukua mali yako. Msikilizeni na mumtii!”[1]

Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wanaona kuwa haijuzu kufanya uasi dhidi ya kiongozi midhali hajaingia katika ukafiri wa wazi kabisa ambao kuna dalili kutoka kwa Allaah. Ahl-ul-Bid´ah tu kama Khawaarij na Mu´tazilah ndio wenye kujuzisha kufanya uasi dhidi ya kiongozi.

Hivyo basi kuwa pamoja na wale wenye kufuata na jiepushe mbali na wale wenye kuzusha. Njia yao ndio njia iliyonyooka na inahusiana na kushikamana barabara na mapokezi.

[1] Muslim (1847).



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2WfGbH3
via IFTTT

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...