Translate

Jumatano, 1 Mei 2019

19. Ni ipi hukumu ya mwenye kula katika Ramadhaan na wakati huohuo hapingi uwajibu wake?

Swali 19: Ni ipi hukumu ya mwenye kula katika Ramadhaan na wakati huohuo hapingi uwajibu wake? Je, ametoka nje ya Uislamu kwa kule kuacha kwake kufunga kwa sababu ya kuzembea zaidi ya mara moja?

Jibu: Mwenye kula katika Ramadhaan kwa makusudi bila ya udhuru wa Kishari´ah amefanya dhambi kubwa. Lakini hakufuru kwa mujibu wa maoni sahihi zaidi ya wanachuoni. Ni lazima kwake kutubia kwa Allaah (Subhaanah) pamoja na kulipa. Zipo dalili nyingi zinazothibitisha kwamba kuacha kufunga sio kufuru kubwa midhali mtu hapingi kuwa ni wajibu na bali ameacha kufunga kwa sababu ya ivivu na kuzembea. Ni lazima kwake kulisha maskini kwa kila siku moja aliyochelewesha kulipa mpaka akaingiliwa na Ramadhaan nyingine pasi na kuwa na udhuru wa Kishari´ah kutokana na yale yaliyotangulia katika jibu la swali la kumi na saba[1]. Kadhalika kuacha kutoa zakaah na kuhiji mtu hakufuru kwa vitendo hivyo. Lakini ni lazima kwake kutoa zakaah juu ya ile miaka iliyompita na akawa hakutoa ambapo alizembea. Vilevile ni lazima kwake kuhiji pamoja na kutubu tawbah ya kweli kwa sababu ya kuchelewesha. Hayo ni kutokana na ujumla wa zile dalili za Kishari´ah katika hayo ambazo zimefahamisha juu ya kutokukufuru midhali mtu hapingi kuwa ni wajibu. Miongoni mwa dalili hizo ni ile Hadiyth kuhusu kuadhibiwa kwa aliyeacha kuitolea mali yake zakaah siku ya Qiyaamah mpaka hatimaye ataona njia yake ima kuelekea Peponi au Motoni.

[1] Tazama http://firqatunnajia.com/17-ni-ipi-hukumu-ya-aliyechelewesha-kulipa-mpaka-akaingiliwa-na-ramadhaan-nyingine/



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2GRioGZ
via IFTTT

Msafiri kuswali Maghrib nyuma ya anayeswali ´Ishaa

Swali: Mimi ni msafiri na sijaswali Maghrib wala ´Ishaa. Nikaingia msikitini na wao ndio wanaanza kuswali ´Ishaa. Nikajichelewesah Rak´ah moja katika swalah ya ´Ishaa na nikakamilisha zilizobaki kwa nia ya Maghrib. Ndugu mmoja ananikataza na kwamba eti kitendo changu kinapingana na Sunnah na kwamba ni kosa. Ni yepi maoni yako juu ya swalah yangu?

Jibu: Mtu akija hali ya kuwa ni msafiri na akaingia msikitini akakuta watu wanaswali ´Ishaa, akiwakuta katika Rak´ah ya pili basi anuie Maghrib na atoe Tasliym pamoja na imamu. Kwa sababu katika hali hiyo atakuwa ameswali Rak´ah tatu. Akiwakuta katika Rak´ah ya tatu, anuie Maghrib na kuswali pamoja nao Rak´ah mbili kisha imamu akitoa Tasliym asimame katika Rak´ah ya tatu. Akijiunga nao katika Rak´ah ya kwanza aingie nao kwa kunuia Maghrib. Pindi imamu ataposimama kwa ajili ya Rak´ah ya nne basi yeye abaki chini na anuie kujitenga, asome Tashahhud, atoe Tasliym kisha ajiunge pamoja na imamu katika yale yatayokuwa yamebaki katika swalah ya ´Ishaa.



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2ZMPhx1
via IFTTT

Ahkaam-ul-Janaa-iz 27



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2IUaoIK
via IFTTT

Ahkaam-ul-Janaa-iz 26



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2J6lcTh
via IFTTT

Ahkaam-ul-Janaa-iz 25



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2IQeLV3
via IFTTT

Ahkaam-ul-Janaa-iz 24



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2J5R3TX
via IFTTT

Ahkaam-ul-Janaa-iz 23



from Firqatu Nnajia http://bit.ly/2IUadx4
via IFTTT

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...