Translate

Alhamisi, 1 Novemba 2018

Tujifunzayo katika maisha ya Salmaan bin Alfaarisy MAISHA YA MASWAHABA: 4

Tunapoipitia sira ya kila Swahaba katika Maswahaba wa Mtume, tunakuta maajabu na mazingatio makubwa yanayogusa maisha yetu kiimani, kifamilia, kiutamaduni na kijamii. Hata hivyo, safari ya Maswahaba ya kuitafuta neema ya Uislamu hutofautiana sana.

kwa mfano, safari ya kuufikia Uislamu ya Maswahaba kama vile Abubakr, Uthman, Ali, Abdurahman bin Auf zilikuwa fupi sana, lakini safari ya Swahaba Salmaan [Allah amri- dhie] ilikuwa ndefu na yenye mlolongo wa matukio mviringo ambayo hutupa wingi vile vile wa mazingatio.

Bila shaka, mpendwa msomaji aliyekuwa akifuatilia kisa na mikasa ya Swahaba huyu mtukufu ataweza kubaini mafunzo mengi tunayopaswa kuyachukua. Hapa tutataja baadhi ya mafunzo hayo.

Udanganyifu wa baadhi ya viongozi wa dini

Viongozi wa dini wakikosa uaminifu kwa Waumini wao hujishushia hadhi na hukera. Pia, viongozi wa aina hiyo ni chanzo cha uchafuzi wa imani husika na kusababisha mtafaruku. Tumeona jinsi mwalimu wa kwanza wa Swahaba Salmaan alivyokosa uaminifu, ambapo alikuwa akizikunja sadaka za waumini wake kwa jina la dini huku akijilimbikizia makasiki ya dhahabu nyumbani mwake.

Tunaelezwa katika historia kwamba chanzo cha kuibuka dhana ya ukoministi duniani ilikuwa ni viongozi wa dini kujifunika mwamvuli wa dini na kutenda maovu hususan kuwadhulumu wafuasi waona kujinufaisha binafsi. Hali hiyo ilipelekea watu kutoona haja ya kuwepo dini kama mfumo wa maisha, na hivy owakakana uwepowa Muumba wa ulimwengu na vilivyomo na pia wakakana uwepo wa maisha baada ya kufa.

Walimkana Mwenyezi Mungu mmoja sio tu kwa lengo la kukwepa kuwajibika mbele kwake lakini pia kwa ajili ya kukwepa udanganyifu, ubabaishaji na dhuluma za walojipa ukubwa na uongozi wa dini kwa maslahi yao.

Utulivu wa moyo uko katika kuifuata dini ya haki

Jambo jingine tunalojifunza kutokana na maisha ya Swahaba Salmaan [Allah amridhie] ni kwamba, dini aliyoiteremsha Allah kwa waja wake humpatia mja faraja na utulivu wa moyo. Dalili ya hayo ni kule kutangatanga na hamahama inayoonekana kwa baadhi ya watu kutoka dini hadi dini nyengine, lakini akifika kwenye Uislamu moyo hutulia na
hukinaishwa na hoja na mafunzo yake safi matakatifu. Siri ya hayo yote ni kwamba Uislamu ndio dini ya Muumba, nyenginezo ni usanii wa mwanadamu.

Swahaba Salmaan, tokea siku alipowaona watu wakiabudu kinyume na utaratibu wa dini yao na katika safari yake kuitafuta dini ya haki alikosa utulivu wa kiroho, lakini alipokutana na Mtume [rehema za Allah na amani zimshukie] pamoja na Maswahaba zake na kuupata Uislamu, alipata utulivu wa nafsi na safari yake ilifika mwisho. Wala Mtume hakumuuliza tena Mtume kwamba akifariki aelekee kwa nani.

Utume wa Muhammad kuthibitishwa na wanadini

Watu wanaokataa utume wa Muhammad na kukubali utume wa waliomtangulia wanapaswa kuizingatia kwa makini historia ya Swahaba huyu mtukufu. Utume wa Muhammad [rehema na amani za Allah zimfikie] tumeona umethibitishwa na Padri [mtawa] wa mwisho kule Ammuuriya alikosoma.

Tumeona jinsi padre yule alivyomuhakikishia kwamba hakuna tena msomi yoyote aliye juu ya dini sahihi kwa zama zile lakini tayari zimefika zama za kuja Mtume wa mwisho na kumpa wasifu wake. Ikiwa limethibitishwa hilo na wasomi wa Ukristo tokea zamani,.Mkristo wa leo ama mfuasi wa dini yoyote, kama ni mkweli wa nafsi yake, inafaa awe makini sana katika kuihakiki dini inayomkataa Mtume huyu wa mwisho, Muhammad [rehema za Allah na amani zimshukie] kwa usalama wake mbele ya Mwenyezi Mungu.

Mwenyezi Mungu anasema: “Hakika dini ya kweli mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu….” [Qur’an, 3:19].

Pia anasema: “Je wanataka dini isiyokuwa ya Mwenyezi Mungu, na hali kila kilichomo mbinguni na ardhini kinamtii yeye kikipenda kisipende; na kwake mtarejeshwa.” [Qur’an 3:83].

Na anasema: “Na atakayetaka dini isiyokuwa Uislamu, basi hatokubaliwa na huko akhera atakuwa miongoni mwa wenye khasara.” [Qur’an, 3:85].

Mvuto wa dini ya haki hauzuiliki

Watu wanaposafiri ndani ya maisha ya kila siku kwa malengo mbalimbali, safari zao huhusisha muda, maeneo pamoja na roho. Safari ya Muirani huyu, Salmaan ilikuwa ya kiroho zaidi. Licha ya kutumia muda kukata masafa, pia alisafiri baada ya kukata kamba na minyororo aliyotatizwa na baba yake.

Alisafiri huku moyoni mwake kukiwa na kitu kizito mithili ya chuma, haki ikiwa mbele naye akiwa nyuma yake. Kwa ajili ya hili, moyo wake ulipata msukumo wa ajabu, na haukutulia mpaka alipoikamata dini ya haki.

 

Udanganyifu wa baadhi ya viongozi wa dini

Viongozi wa dini wakikosa uaminifu kwa Waumini wao hujishushia hadhi na hukera. Pia, viongozi wa aina hiyo ni chanzo cha uchafuzi wa imani husika na kusababisha mtafaruku. Tumeona jinsi mwalimu wa kwanza wa Swahaba Salmaan alivyokosa uaminifu, ambapo alikuwa akizikunja sadaka za waumini wake kwa jina la dini huku akijilimbikizia makasiki ya dhahabu nyumbani mwake.

Tunaelezwa katika historia kwamba chanzo cha kuibuka dhana ya ukoministi duniani ilikuwa ni viongozi wa dini kujifunika mwamvuli wa dini na kutenda maovu hususan kuwadhulumu wafuasi waona kujinufaisha binafsi. Hali hiyo ilipelekea watu kutoona haja ya kuwepo dini kama mfumo wa maisha, na hivyo wakakana uwepowa Muumba wa ulimwengu na vilivyomo na pia wakakana uwepo wa maisha baada ya kufa.

Walimkana Mwenyezi Mungu mmoja sio tu kwa lengo la kukwepa kuwajibika mbele kwake lakini pia kwa ajili ya kukwepa udanganyifu, ubabaishaji na dhuluma za walojipa ukubwa na uongozi wa dini kwa maslahi yao.

Utulivu wa moyo uko katika kuifuata dini ya haki

Jambo jingine tunalojifunza kutokana na maisha ya Swahaba Salmaan [Allah amridhie] ni kwa heshima yake na kukubali usumbufu mkubwa, ikiwemo kuingia katika utumwa zaidi ya mara moja. Pia alitekwa na watu makhaini aliyewapa wanyama wake kama malipo ya kumpeleka alikoelekezwa na mwalimu wake.

Yote haya yanatufunza kuwa, haki ni kitu ghali zaidi, na mtu anayeitafuta ataipata. Muhimu ni kuwa, mtu akipata imani ya kweli hana budi kuitunza na kuishikilia kisawasawa kwani haifanani na kitu chochote chengine kwa thamani.

Dini ya haki huthibiti kwa hoja

Baadhi ya watu huridhika na imani walizozirithi kutoka kwa wazee wao. Watu hawa Allah anawaelezea kama ifuatavyo: “Na wanapoambiwa fuateni aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu husema,

Bali tunafuata tuliyowakuta nayo wazazi wetu.’ Je hata kama wazazi wao hawazingatii lolote wala hawakuongoka?” [Qur’an 2:170].

Kuomba ushauri na wasia

Katika maisha ya Salmaan tunajifunza pia umuhimu wa kuwaheshimu wanazuoni, kuwatumikia na kuomba ushauri katika masuala mbalimbali yakiwemo ya utekelezaji wa majukumu ya kidini kama alivyofanya swahaba huyu kila alipohisi mwalimu wake anakaribia kuondoka duniani.

Subira ndio ufunguo wa kheri

Mtu kamwe hawezi kuyafikia malengo kama vile kutafuta elimu, biashara nk, iwapo hatakuwa na subra na kuwa tayari kubeba mashaka ya safarini. Tumeona safari ya Salmaan ilivyomtoa Furs mpaka Sham, na kutoka Sham [Palestina] mpaka Iraq, na kutoka hapo mpaka Nasibiin, kisha mpaka Ammuuriya, na kutoka hapo mpaka Waadil-quraa [mji kati ya Madina na Sham] na mwisho akafika alipopakusudia, Madina.

Ilikuwa ni safari nzito iliyojaa mashaka ambayo ilikata maelfu ya kilomita kwa ajili ya kutafuta misk ya roho na utulivu wa nafsi.

Baada ya dhiki huwa faraja

Safari inapokuwa kwa ajili ya Allah, licha ya masumbufu yatakayomfika msafiri, mwisho huwa na kheri nyingi ambapo Allah hubadilisha dhiki mbele kuwa faraja.

Hili liko wazi katika safari ya Alfarisy [Allah amridhie]. Kwani hakuna faraja kubwa zaidi kuliko kukutana na Mtume na kuishi naye. Hapa tunajifunza pia kutokukata tamaa zinapotufika changamoto tunapokuwa katika shughuli zetu za kidaawa na za kimaisha kwa ujumla, madhalitunajua tupo katika yanayomridhisha Allah Aliyetukuka.

Allah Aliyetukuka awe radhi na Salmaan, Mwenda nyuma ya haki, na atunufaishe kwa historia na elimu yake, amiin.

 

MAISHA YA MASWAHABA: Salmaan al-Faarisy, Maisha yake baada ya kusilimu



from TIF https://ift.tt/2qkSYto
via IFTTT

New video by GROUP FAIDIKA NA MAWAIDHA on YouTube

*Tafsir Ya Qur-an๐Ÿ‘†* *๐Ÿ“– Surat Al Kahf 01-12* *๐Ÿ‘ค๐Ÿ‘คSh. Mishari Al Afasiy.* *Sh. Mahammad Sulayman.*
*Tafsir Ya Qur-an๐Ÿ‘†* *๐Ÿ“– Surat Al Kahf 01-12* *๐Ÿ‘ค๐Ÿ‘คSh. Mishari Al Afasiy.* *Sh. Mahammad Sulayman.*


View on YouTube

Ulimwengu Wa Wamasoni (2)

Imetafsiriwa na Naaswir Haamid


Bwana Rudyard Kippling ni Mmasoni mwengine ambaye ni mwandishi marufu wa riwaya ya "The Jungle Book", ameandika kitabu kinachoitwa "The Man Who Would One Day be King". Kitabu hichi badaye kikaingizwa katika bajeti kubwa ya Hollywood, wachezaji wakuu wakiwa ni Sean Connery, Michael Kane na Saeed Jaffery. Kitabu hicho ni hadithi ya askari wawili wanaofunga safari ya kwenda sehemu za mwisho za India. Nchi ambayo hapo kale ilikuwa ikisemwa mno kwa kuwa na matajiri wakubwa ambao walitokana na Mkuu Alexander. Walipofika nchi hiyo, askari wawili hawa wanakamatwa na wenyeji wanaotambulika kwa jina la Kafir walioitwa kutokana na nchi yao ya Kafiristan. Pale wanapokaribia watu wawili hao kuuawa, kidani kinaonekana shingoni mwa askari mmoja kikiwa na alama ya Jicho Moja La KimasoniKafir hao wanampa heshima ya mungu wao na kumsifia kwamba ni mwenye kuishi milele. Mtu mwenyewe hapo mwanzo alijisifia kwamba ni Mfalme na badaye anatambua nguvu mpya ndani yake binafsi inayomtambulisha kwamba ni mungu.

Kwa mujibu wa elimu ya Uislamu kama sio imani nyenginezo pia, mfano unaooneshwa kutokana na hadithi hiyo unastajabisha kweli kweli. Maandiko ya Kiislamu yanayoitwa Hadiyth yana simulizi nyingi za Utume wa Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Ndani ya Hadiyth hizi, zinaeleza kwamba kutatokea mtu miongoni mwa Kaffir ambalo ndani ya Uislamu lina maana ya wasiomuamini Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala), mtu huyu atatambulikana kwa Jicho lake Moja na atafanywa kuwa ni Kiongozi wa Dunia, mwanzo akidai kuwa ni Mfalme na baadaye kuwa ni mungu atakayeaminika kuishi milele hadi wakati wake aliowekewa (na Mola).

Katika mchezo mwengine, dhana ya kiongozi wa dunia na serikali moja pia inatiliwa mkazo mno katika hila za propaganda. Mnamo mwaka 1996, mchezo wa "Indepencence Day" ulivunja rikodi ya mauzo kwa kushikilia nafasi ya juu ya saba miongoni mwa michezo yote ya wakati wote. Mchezo huo unaoneshwa kwa dunia nzima ambao una hadithi ya kutunga kuhusu uvamizi wa kiumbe cha majabu ulimwenguni Alien. Hata hivyo, ndani kabisa ya mchezo huo kuna ujumbe uliojificha unaoweza kupatikana, unaoonesha kuwepo kwa Umasoni na agenda za Kimasoni. Ndani ya mchezo huo, kuna ngome ya kijeshi inayoitwa "Area 51" ni hapa ambapo mashambulizi yanaanza kufanywa na ni ngome hii ambayo dunia nzima na viumbe vyengine vyote inaitegemea. Mlango wake wa kuingilia umetengenezwa kwa aina ya pyramid (pembe tatu) na ambao umechongwa kwa alama ya Jicho Moja.
Mchezo huo unaonesha kwamba USA ndie mpiganaji mkuu dhidi ya uharamia huo unaohusisha mataifa mengine duniani. Uharamia ambao umevumbuliwa, kuongozwa na kuamrishwa na mtu mmoja – Kiongozi mkuu mmoja. Mchezo huo ni sehemu kuu ya upanuzi wa michezo na vipindi vya runinga katika mada za viumbe vya ajabu, UFO na uvamizi unaohatarisha maisha ya mwanaadamu ulimwenguni. Michezo kama hii inaitia hamasa jamii kufuatilia mada hizi. Hizi ni miongoni mwa njia nyingi zinazotumiwa na Wamasoni katika kutengeneza njia ya serikali moja. Wamasoni wanatumia aina nyingi za kuingiza khofu ndani ya mioyo ya watu, ikiwatia hamasa ya kuwa na haja ya ulinzi wa hali ya juu na hivyo kuwa na haja ya usalama wa ziada. Haja ya usalama na ulinzi zinaweza tu kutimizwa kwa kuwa na serikali moja ya Ulimwengu mzima ikilinda matakwa ya wanaadamu wote duniani. "Kwa hakika iwapo tutakutana na tishio la uvamizi wa kiumbe cha maajabu kutoka nje ya dunia, nafikiria kwamba ndivyo itatumiwa sababu hiyo kuzifuta kabisa tofauti zetu duniani kwa haraka, na bora nikuulize kwani bado hakuna nguvu za kiumbe wa maajabu miongoni mwetu?"

Njia nyengine wanazotumia Wamasoni ili kufanikisha serikali moja ya dunia nzima na haja ya kuwepo ulinzi wa dunia unaoongozwa na wao ni kuruhusu kuongezeka kwa makosa ya jinai hadi kufikia kiwango cha kutisha. Kwa kutumia njia hii, wanasababisha kuwepo kwa khofu ya kuhitaji usalama binafsi na wa taifa.

Uzalishaji wa madawa ya kulevya kwa mujibu wa maofisa unakadiriwa kwa mujibu wa makadirio ya fedha kuwa ni uzalishaji mkubwa kabisa duniani. Nchi tofauti hivi sasa zinajitahidi kusuluhisha tatizo hili katika ngazi za kitaifa na kimataifa. Kwa mfano USA ina tatizo baya kabisa na linaloongezeka pale unapozungumzia kuhusu madawa ya kulevya. Kinachoonekana ndani ya USA ni kwamba makosa ya jinai yanaongezeka katika kiwango cha juu kabisa. USA inasukumwa na malalamiko na madai ya wananchi kuitaka serikali kuchukuwa hatua kali, iwapo kwa kipigo cha dhahiri au siri kupambana na tatizo la madawa ya kulevya na kuridhisha maoni ya jamii. Hata hivyo, takwimu zinazoumiza kichwa kuhusiana na uzuiaji wa madawa ya kulevya nchini Marekani zinatia shaka kuhusiana na uwezo na msukumo wa serikali hiyo. Inaaminika kwamba mnamo miaka ya 1960, aliyekuwa mwenyekiti wa FBI Bwana J. Edgar Hoover, aliruhusu biashara ya madawa hayo kutumika ndani ya jamii ya Wamarekani Weusi (African American) katika jaribio lake la kudumaza harakati za watu weusi nchini Marekani.

Mnamo miaka ya 1980 pamoja na tishio la ukomunisti kuchukua hatamu Marekani ya Kati, pesa zilihitajiwa haraka kugharamia harakati za wanamgambo dhidi ya ukuaji wa ukomunisti. Na ili kufanikisha hili, CIA iliruhusu madawa ya kulevya kufanyiwa biashara ndani ya Marekani.  Hili linadhihirishwa kutoka kwa American Senator Bwana Jack Bloom ambaye alikuwa ni mjumbe wa kamati ya uchunguzi katika suala hilo.

Tokea hapo kale, Wamasoni wamekuwa wakitumia au wakibuni matatizo ndani ya jamii ili kugeuza na kuharibu matokeo kwa mujibu wa agenda zao. Ongezeko la tatizo la madawa ya kulevya nchini Marekani linawaridhia viongozi kutumia nguvu za aina zozote kwa wakati wanaotaka. Usafirishaji baina ya Atlantic American na Latin American tayari umeshawekwa chini ya uangalizi.

Haitochukuwa muda mrefu kabla ya kuwepo haja ya kutumia nguvu za pamoja ulimwenguni. Miongoni mwa mambo yanayoridhia lengo la kuwepo uendeshaji wa watu ni uharibifu wa habari za kweli na matumizi ya kutumia uzalishaji na takwimu za upande mmoja ambazo ni zana za serikali za Kimasoni za leo, kubuni haja ya uma katika ulinzi wa hali ya juu kitaifa na kimataifa, kuongeza idadi ya makosa ya jinai, madawa ya kulevya na kuongeza matendo ya ugaidi. Maendeleo katika teknolojia ndio inayowapatia uwepesi Wamasoni kufanya walitakalo, teknolojia hii inaruhusu matendo ya watu wote kuwepo chini ya uangalizi, kuchunguzwa na kuhifadhiwa.

Ufunguo wao ni kuwa na kila aina ya taarifa. Kila taarifa zinapoongezeka kuhusu watu ndipo wanapoweza kutabiri uhakika wa matendo yao na namna wanavyofikiri na inakuwa kwao rahisi kuwaongoza katika uharibifu na bila ya kujielewa. Wamasoni wanaziendesha jamii na mahitaji wanayoyahitaji, lakini kwa kutumia ulaghai wa teknolojia daima zipo kukuzuia yale unayoyataka na yale unayoyachagua, hakika ni ukweli wa uzalishaji wao na namna wanavyoharibu akili za watu. Njia ambazo zimetumiwa kuendesha upande unaoamuliwa kuuongoza watu na njia hizi ambazo zinadhibiti kila nyanja ya maisha ya mwanaadamu, na njia hiyo ndio maisha yako!!!

Vitendo vya kutisha kama vile vya ugaidi, ongezeko la makosa ya jinai, ongezeko la hujuma vyote hivi vina mzizi wake kutoka vyombo vya habari. Na kwa upande mwengine serikali nayo inatengeneza mazingira ambayo itaridhiwa kutumia mabavu, kuweka zana za kuchunguza mienendo ya watu. Teknolojia zaidi na zaidi zinavumbuliwa ili kuwachunguza watu, hali hii inaongezeka hadi kufikia kwamba ni serikali ya kibeberu tu ndio inafaidika na uchunguzi huu. Mawazo ya watu kwa mara nyengine yanageuzwa ili kuwapa Wamasoni ridhaa ya matendo yao na kuwarahisishia yale malengo yao. Hivi sasa tayari teknolojia ipo mbioni ya namna za kuchunguza watu na kuhifadhi maelezo binafsi ya watu ndani ya jamii kwenye sehemu ya kuhifadhia takwimu nyingi. Harakati zinavyozidi ndivyo inavyochukua nafasi ya kuhifadhi maelezo binafsi ya watu katika kifaa kidogo cha plastiki kama vile maelezo ya benki, leseni ya udereva na bima ya taifa. Inaonesha kwamba maelezo haya hivi sasa yanafanyiwa kazi ili kuyaunganisha pamoja katika kadi moja tu. Matokeo yake itakuwa ni kuchunguza hali zote za watu katika manunuzi na maelezo binafsi ya watu kwa kutumia kidole (on a click).

Mnamo mwaka 1992 Makamo Mwenyekiti wa Mahkama Kuu ya Uingereza Bwana Nicholas Brown Mulkinson alieleza kwamba iwapo polisi watapewa mamlaka ya kukusanya katika sehemu moja taarifa kuhusu kodi za ardhi, huduma za jamii na afya na huduma nyenginezo, basi uhuru wa mtu utakuwa hatarini. Watakuwa tayari wanaweza kutambua nani unazungumza naye kwenye simu, wapi unafanya kazi, wapi unafanya manunuzi yako, nini unakula, nini unavaa, unatumia gharama za aina gani, maingizo yako na orodha hii inakwenda mbele na mbele zaidi. Kadi moja tu inaweza kuruhusu uchunguzi wa karibu zaidi na kuwezesha kupatikana maelezo ya kina ya akili ya kila mtu katika jamii. Taarifa ambazo zinafanya wepesi kuagua udhibiti wa kuharibu matendo ya watu. Hata hivyo, kuna pengo ambalo Wamasoni wanahitaji kuliziba kwa kuondosha matumizi ya sarafu isiyotumia umeme (hard currency). Sarafu hizi ambazo zinatumiwa zaidi duniani, zinaweza kumfanya mtu kukimbia uchunguzi na kuhifadhiwa maelezo yake kwa njia ya teknolojia. Hili ni kwa sababu manunuzi ya sarafu hizi hayawezi kufuatiliwa kwa kina.

Kutokana na hili, harakati zinafanywa za kuondosha sarafu isiyotumia umeme kwa mtindo ambao zitakuwa zinategemea moja kwa moja katika kutumia umeme. Kwa maneno mengine, mfumo huu unaoetegemea moja kwa moja matumizi ya kadi, uchunguzi na udanganyifu umekamata alama za mwanzo katika harakati za kuanzisha kadi malumu na fedha za umeme nchi nzima ndani ya Uingereza. Mpango wa mondex ni wa mwanzo kutoka benki za magharibi na British telecom na ubunifu wa mwanzo wa kuanzisha kadi malumu. Ndani ya kadi hii kuna micro chip ambayo inaweka kumbukumbu ya kila manunuzi, sio tu ya pesa bali inahifadhi kila aina ya kitu kinachotumiwa. Inaweza kufanya kazi kama ni credit card, paspoti ya jamii, kadi ya maktaba, kadi ya kusafiria, kadi ya simu na bila ya shaka kadi ya utambulisho. Dhana ya kadi hii malumu imebuniwa kutoka Ufaransa ambayo ina mfumo wa kibabe katika kuhifadhi taarifa za watu.

Ingawa kadi ya utambulisho inaweza kufungua mlango wa maelezo mengi, hakika haitakuwa na uwezo wa kumuonesha wapi mtu alipo katika wakati fulani. Hili litahitaji kuwepo mfumo malumu wa kifaa cha kufuatilia mwenendo wa mtu ambacho kinaweza kuwekwa ndani ya kadi hiyo na kumfuatilia popote alipo duniani. Kifaa cha kufuatilia mwenendo wa mtu kinaweza kuwa ni kifaa kiduchu cha utambulisho au kifaa kinachotumia umeme ndani ya kadi. Vifaa kama hivi vinatumika kupasha habari ambazo zinachukuliwa na satellite kwenye low earth orbit ikimuonesha na kumtambua muhusika.

Ingawa kazi hii inaweza kuonekana kama ya uongo, hata hivyo inafanyiwa kazi hivi sasa kuwa ni ya kweli. Hivi sasa kuna takribani satallite 48 ulimwenguni ambazo zinatumika na Marekani na washirika wake. Satellite hizi zinaweza kupewa amri kwa kutumia alama (signals) na kusafirisha taarifa sahihi kutoka chanzo kinachohitajika. Kwa wakati wa sasa, chanzo cha signals hizi ni vifaa vilivyomo katika matanki, ndege na meli za vita au hata zana za mkononi kwa malengo ya kupata picha ya ramani iliyo sahihi kabisa. Hatua inayofuata itakuwa ni kuanzisha kifaa ambacho kitatoasignal asili kutoka kwa kila mtu.


Hivi sasa mfumo mmoja wa kifaa hicho ambacho kimevumbuliwa mahsusi kama nisignal asili kwa ajili ya satellite ni electronic tag. Huu ni mpango ambao unatumika Uingereza. Sababu ya kufanya hili ni kwamba inahitajika kwenda sambamba na ongezeko la idadi ya watu ndani ya jela zilizosheheni watu. Tag hii inavalishwa kwenye mkono wa wanaotiwa hatiani na wanaweza kufuatiliwa kuangalia iwapo watiwa hatiani hao wanakiuka amri za kuzima taa jioni (curfew).

Matumizi ya tag kwa marubani pia inafanyiwa kazi huko Manchester, Bark Shaw na Norfolk kwa mipango ya kutumika tag hii nchi nyenginezo huko mbele. Ndani ya makala katika gazeti la Daily Telegraph la tarehe 13/11/1997, Jack Straw aliyekuwa Waziri wa mambo ya ndani wa Uingereza amenukuliwa akisema kwamba electronic tag imetumika sana miaka iliyopita na matokeo yake watu wengi zaidi wanaridhika nacho. Hakuna mjadala kwamba kiini haswa cha mpango huu kwa maendeleo ya watu huko mbele imetumia jicho lao lililo makini na kwamba Wamasoni hivi sasa wanaweza kutia nguvu zaidi mipango yao ya kuiendesha dunia wakiiharibu kwa mujibu wa matakwa yao na uharibifu huu utafanikiwa kwa namna yoyote.

Wamasoni wanapanga mikakati madhubuti kuuendesha ulimwengu kwa kutumia serikali moja, na hivyo ni lazima watengeneze njia ya uchumi wa aina moja, utungaji wa sheria wa aina moja, siasa moja na jeshi la dunia nzima. Mnamo tarehe 25 ya Machi mwaka 1957, iliundwa Jumuiya ya Uchumi barani Ulaya European Economic Community EEC, hatua hiyo ni ya mwanzo katika kuanzisha serikali moja. Tokea hapo kale, EEC imekuwa ni uwanja wa majaribio kwa ajili ya mwenendo mpya duniani – new world order.


Kwa msingi wa kanuni za uhuru wa kutembea baina ya wajumbe wa nchi shirikishi, tayari wameanzisha bidhaa na watu ambao wanaweza kutembea huru kabisa ndani ya taifa hili kubwa. Mipango ipo mbioni kuanzisha mfumo mmoja wa uangalizi na harakati za kuanzisha serikali moja ya Ulaya zinapanda juu kila siku na hivyo kusafisha njia kwa ajili ya siasa moja na utungaji mmoja wa sheria. Yote haya yana maana kwamba hapo badaye ndani ya taifa hili kubwa la EEC kutakuwa na sarafu moja, uchumi mmoja na serikali moja na bila ya shaka serikali wenyewe ni lazima iwe ya Kimasoni.


Wachejaji watatu wakuu wa EEC ni Uingereza, Ufaransa na Ujerumani. Uingereza na Ufaransa tokea hapo zamani zimekuwa ni nchi zinazoongozwa na Umasoni. Wakati wa Vita vya Pili vya Dunia, Ujerumani ilishirikishwa moja kwa moja na Uingereza na Ufaransa pamoja na Marekani ambalo ni taifa jengine la Kimasoni na Umoja wa Kisovieti. Nyanja ambazo zilikuwa zikidhibitiwa na nchi tatu hizo zilizotajwa ni za Kimasoni, zilizotengeneza utambulisho mwengine wa kisiasa unaoitwa Ujerumani ya Magharibi na kutokana na kuporomoka kwake ukuta wa Berlin huko Magharibi ya Ujerumani imechukuliwa na Mashariki ya kale ya Ujerumani.

Ulaya haipo peke yake katika jitihada za kufanikisha hadhi ya mataifa yenye nguvu kubwa. Marekani na Mexico hivi sasa ndizo nchi mbili tu za Makubaliano ya Biashara Huru Marekani ya Kaskazini (NAPHTHA –North American Free Trade Agreement). Hata hivyo, mataifa ya Kusini yanaendelea kushajihishwa kujiunga na umoja huo. Kwa kuwepo mataifa makubwa ya Kimasoni ndani ya Ulaya na Marekani, umoja ulio imara utakuwa ndio dhana sahihi na maendeleo mepesi. Hata hivyo, kuna tatizo jengine ambalo Wamasoni wanahitaji kupambana nalo iwapo wanataka kuwa mabwana wa ulimwengu mmoja.

Ilipofika miaka ya 1970, ilikuwa inadhihirisha wazi kwamba idadi ya Wazungu na Wamarekani weupe inapunguwa kwa kasi. Hili liliwatia khofu na juhudi zilihitajika kulitafutia ufumbuzi, kwani kuachiwa kuendelea kuna maana ya kwamba idadi kubwa ya watu katika mataifa ya ulimwengu wa tatu yatahatarisha usalama wa kitaifa wa nchi zinazodhibitiwa na Wamasoni. Manunuzi ya Magharibi na uzalishaji wake yatapunguwa na matokeo yake mataifa haya yatakuwa yanategemea moja kwa moja kwa watu wa ulimwengu wa tatu. Kwa upande mwengine, pengo baina ya watu wa Magharibi na idadi ya watu wa dunia ya tatu lilihitajika kujazwa ili kurudisha hadhi ya juu ya Magharibi au kwa lugha sahihi hadhi ya Kimasoni ulimwenguni.

Mnamo miaka ya 1970, raisi Jimmy Carter aliunda kamisheni ya dira ya ulimwengu wa 2000, ripoti hiyo ililaumu matatizo yote kuwa yanatokana na ukuaji wa idadi ya watu wasio kuwa weupe. Ripoti hiyo ilikwenda mbali hadi kushauri udhibiti wa idadi ya watu angalau bilioni mbili ndani ya mataifa ya ulimwengu wa tatu hadi kufikia mwaka 2000. Hili lilishauriwa ili kurudisha hadhi ya juu ya Magharibi. Maajabu kwamba pia ndani ya miaka ya 1970, janga la UKIMWI likaripuka na kuchukuwa idadi kubwa kabisa ya maisha ndani ya mataifa ya ulimwengu wa tatu na halikadhalika ndani ya watu weusi na Wahispania kutoka Marekani.


Ilisemwa kwamba kirusi cha UKIMWI kilitokana na kima wa rangi ya kijani ndani ya Afrika na badaye kilisambazwa kwa wenyeji iwapo ni kwa matendo ya kinyama au matumizi ya chakula.

Hata hivyo, simulizi hiyo ilikuwa ni ndogo kinyume na ukweli wenyewe.Mnamo tarehe 2 ya Juni mwaka 1988, gazeti la Los Angeles Times lilichapisha makala iliyokataa maelezo ya kwamba kirusi cha mwanaadamu cha UKIMWI kimetokana na kima wa rangi ya kijani. Makala hiyo ilifichua ushahidi kwamba DNA kutoka kwenye virusi haishabihiani hata kidogo na kima hao. Bila ya shaka itatambulika kwamba virusi vya UKIMWI haviwezi kuonekana sehemu yoyote ya asili na vinaweza tu kuishi ndani ya mfumo wa kutengenezwa wa kuhifadhi baiolojia wa mwanaadamu – human biological system.

Iwapo kirusi hicho hakikuibuka kutokana na viumbe, suala linakuja wapi kiliibuka na ni wapi hakika kirusi hichi kilitoka mzizi wake? Mnamo tarehe 4 ya Julai mwaka 1984, gazeti la New Delhi nchini India linaloitwa Patriot lilichapisha makala inayoonesha kwa mara ya kwanza kwamba madai ya UKIMWI yanapingana na baiolojia. Mtaalamu wa utabibu wa wanyama kutoka Marekani ambaye hakudhihirisha jina lake, ameyanukuu madai ya UKIMWI kuwa yametengenzwa kitaalamu kutoka maabara ya kijeshi ya Marekani huko Ford Detrick karibu na Frederick. Baadaye mnamo tarehe 30 ya Oktoba mwaka 1985, gazeti la Kisovieti la Liternia Gazetta lilirudia madai yaliyochapishwa na gazeti la Kihindi na kusababisha mgogoro wa kimataifa. Hata hivyo, zogo lote hili la chanzo cha kirusi cha UKIMWI liliondoshwa na Wamasoni wa Kimagharibi kama lilivyoondoshwa taifa babe la Kikomunisti.

Mnamo tarehe 26 ya Oktoba mwaka 1986, gazeti la Sunday Express lilikuwa ni gazeti la mwanzo la Kimagharibi kuweka habari kwenye ukurasa wake wa mwanzo kuthibitisha hitimisho walilokuja nalo magazeti ya Kihindi na Kisovieti walilolipa jina la "UKIMWI umetengenezwa ndani ya maabara".Ndani ya makala hii, kwa wakati na nafasi tofauti Dr. John Seal na Prof. Jacob Seagall ambaye ni mkurugenzi mstaafu wa idara ya baiolojia katika Chuo Kikuu cha Berlin, walimaliza na maelezo kwamba kirusi cha UKIMWI ni cha kutengenezwa na mwanaadamu.

Uripukaji wa UKIMWI umeunganishwa na mipango ya kutoa chanjo ulimwenguni.Gazeti linaloheshimika kimataifa la London Times lilichapisha makala ukurasa wa kwanza mnamo tarehe 11 ya Mei mwaka 1987 yenye kichwa cha habari "Chanjo ya Suruwa Yagundulika kuwa na UKIMWI". Makala hiyo inaunganisha baina ya chanjo ya suruwa iliyofanywa na Jumuiya ya Afya Duniani kwa takribani watu milioni 50 – 70 ndani ya nchi tofauti Afrika ya kati na kule kuibuka kwake UKIMWI ndani ya maeneo hayo. Jumuiya ya Afya Duniani ni tawi la kiafya la Umoja wa Mataifa.

Ushahidi huo unaonesha kwamba UKIMWI ni virusi vilivyoenezwa kupitia zoezi la kufanya chanjo ndani ya ulimwengu wa nchi za tatu. Ni kirusi kibaya dhidi ya watu wasio na hatia na wanyonge kwa lengo la kudhibiti idadi ya watu duniani.

UKIMWI si chochote zaidi ya suluhisho la kisasa na yote haya yanafanywa kwa lengo la kupenyeza sera ya kiuchumi ambayo itaruhusu utegemezi wa ulimwengu mzima kwa Wamasoni wa Magharibi. Hata hivyo kuhodhi uchumi kwa Wamasoni peke yake halitoshelezi. Ili kuwezesha serikali ya Kimasoni kutimiza malengo yao ambayo itakuwa ndio jumuiya ya ulimwengu mzima chini ya udhibiti wa Kimasoni na uchumi mmoja wanahitaji kuwa na jeshi moja, na hakuna shaka yoyote kwamba umoja huo ni wa Umoja wa Mataifa - UN.

Ufaransa na Marekani tayari zina nafasi ya juu ndani ya mataifa makuu ya Baraza la Usalama na wengine wakiwa ni Urusi na Uchina. Hili lina maana kwamba wana nguvu tosha kuruhusu tendo lolote linalohitaji kupitishwa - VITO. Mnamo Disemba ya mwaka 1992, raisi wa Baraza Kuu alitangaza kwamba UN ni lazima iwe na bunge lake la dunia nzima na aliendelea kusema kwamba UN ni lazima iwekewe huduma zake malumu za kiusalama.

Hata hivyo, UN hivi sasa imeshakuwa na nguvu za kijeshi. Inafanya kazi kama ni jeshi. Jeshi ambalo lilikaa nyuma wakati maelfu ya Waislamu walipouliwa na Waserbia huko Bosnia na badala yake wakacheza mchezo wa kuzuia silaha ambao uliwaacha Waislamu kutokuwa na himaya yoyote. Majeshi ya UN yaliwahi kupelekwa kupigana vita dhidi ya Kamanda Muhammad Farah Idiid kipindi cha baina ya miezi Juni na Oktoba mwaka 1993. Na matokeo yake ni kwamba helikopta za Kimarekani zilishambulia hospitali, nyumba na makundi ya watu. Yakiuwa mamia ya watu wasio kuwa na silaha waliovamiwa na ambapo watu 71 waliuawa. Juu ya yote mkuu wa kitengo cha malengo ya UN bwana Admiral Jonathan Howard alisema: "Tulitambua nini tunapiga, tulipanga vizuri."

Tendo hili hakika lilikuwa ni kinyume na makubaliano yaliyofanyika Geneva – Geneva Convention. Lakini pale alipoendewa mwanasheria wa jeshi la Marekani kuhusiana na dondoo hizi, jibu lake lilikuwa kwamba makubaliano ya Geneva hayafanyi kazi kwa majeshi ya UN. Utetezi wake kwa njia ya kijanja ni kwamba UN sio mtiaji saini wa makubaliano hayo.

Kwa maneno mengine ni kwamba majeshi ya UN yalikuwa huru kutenda jinai za vita (war crimes) au kuuwa namna wanavyopenda na walikuwa juu ya sheria. Ukweli ni kwamba UN, mbali na kuleta (msaada wa) vyakula kama wanavyodai, wametandaza ubadhirifu ardhini wakiacha athari ya vifo na maangamizi popote inapokwenda. Zimeondoka siku za vita baridi ambapo Umoja wa Kisovieti ulikuwepo kila mahala na ambapo fikra za Kimasoni za serikali moja zilichukuwa muda kufanikiwa. Sasa kwa vile Ukomunisti umemalizwa, inaonesha kuwa Wamasoni angalau wanaweza kuwatumia UN kufanikisha malengo yao ya serikali moja ulimwenguni.

Kutokana na kuihodhi dunia nzima ndani ya mikono yao na akiwa hayupo wa kuzuia wanapotaka kwenda, hivi sasa Dunia inatoa kilio kwa sababu ya ubadhirifu na unyama waliyoyatandaza ardhini kupitia karne zao za kutisha za kuuhodhi ulimwengu. Ingawa wanaona kwamba hakuna wa kupingana nao, lakini Dunia inashuhudia kuja tena majeshi yaliyopo huko kabla. Sasa hivi Wamasoni wana adui mwengine wa kupambana naye, adui ambaye hapo kabla walidhani kwamba wameshammaliza. Adui ambaye daima hatasalimu amri dhidi ya ubadhirifu na mipango ya kinyama ya Kimasoni. Adui huyo ni Uislamu na dhidi yake wametangaza vita.

Inaendelea in Shaa Allaah...


from Muislamu https://ift.tt/2qoa7Cz
via IFTTT

42. Mlango kuhusu maneno Yake (Ta´ala) “Hivyo basi msimfanyie Allaah washirika, na hali ya kuwa nyinyi mnajua.”

Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:

1- Allaah (Ta´ala) amesema:

ุงู„َّุฐِูŠ ุฌَุนَู„َ ู„َูƒُู…ُ ุงู„ْุฃَุฑْุถَ ูِุฑَุงุดًุง ูˆَุงู„ุณَّู…َุงุกَ ุจِู†َุงุกً ูˆَุฃَู†ุฒَู„َ ู…ِู†َ ุงู„ุณَّู…َุงุกِ ู…َุงุกً ูَุฃَุฎْุฑَุฌَ ุจِู‡ِ ู…ِู†َ ุงู„ุซَّู…َุฑَุงุชِ ุฑِุฒْู‚ًุง ู„َّูƒُู…ْ ูۖَู„َุง ุชَุฌْุนَู„ُูˆุง ู„ِู„َّู€ู‡ِ ุฃَู†ุฏَุงุฏًุง ูˆَุฃَู†ุชُู…ْ ุชَุนْู„َู…ُูˆู†َ

“Ambaye amewafanyieni ardhi kuwa kama tandiko na mbingu kuwa kama paa na akateremsha kutoka mbinguni maji akawatolea kwayo matunda kuwa ni riziki kwenu. Hivyo basi msimfanyie Allaah washirika, na hali ya kuwa nyinyi mnajua.” (al-Baqarah 02:22)

2- Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:

“Washirika ni shirki ambayo imejificha zaidi kuliko mdudu mchungu apitae juu ya jiwe jeusi katika usiku wenye giza. Nako ni kusema: “Naapa kwa jina la Allaah na kwa uhai wako fulani na uhai wangu”, “Lau ama si kijibwa hiki mwizi angelituingilia”, “Lau kama si bata ya nyumbani wezi wangelituingilia” na mtu kumwambia mwenzake: “Akitaka Allaah na wewe” na mtu kusema pia: “Lau kama si Allaah na fulani”. Usimchanganye Allaah na mwingine yeyote. Yote haya ni kumshirikisha Allaah.

Ameipokea Ibn Abiy Haaatim.

3- ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mwenye kuapa kwa asiyekuwa Allaah amekufuru au ameshirikisha.”[1]

Ameipokea at-Tirmidhiy ambaye ameisahihisha na al-Haakim pia ameisahihisha.

4- Ibn Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

“Kuapa kwa Allaah hali ya kuwa ni mwenye kusema uongo inapendeza zaidi kwangu kuliko kuapa kwa asiyekuwa Allaah hali ya kuwa ni mwenye kusema ukweli.”

5- Hudhayfah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Msisemi “Akitaka Allaah na fulani”. Lakini semeni: “Akitaka Allaah kisha akataka fulani”.”[2]

Ameipokea Abu Daawuud kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.

6- Imekuja kutoka kwa Ibraahiym an-Nakha-iy ya kwamba alikuwa akichukia mtu kusema: “Najilinda kwa Allaah na kwako”, lakini alikuwa anajuzisha kusema: “Najilinda kwa Allaah kisha kwako”. Pia akijuzisha mtu kusema: “Lau kama si kwa ajili ya Allaah kisha fulani” na wala usisemi: “Lau kama si kwa ajili ya Allaah na fulani”.

MAELEZO

1- Allaah (Ta´ala) amesema:

ุงู„َّุฐِูŠ ุฌَุนَู„َ ู„َูƒُู…ُ ุงู„ْุฃَุฑْุถَ ูِุฑَุงุดًุง ูˆَุงู„ุณَّู…َุงุกَ ุจِู†َุงุกً ูˆَุฃَู†ุฒَู„َ ู…ِู†َ ุงู„ุณَّู…َุงุกِ ู…َุงุกً ูَุฃَุฎْุฑَุฌَ ุจِู‡ِ ู…ِู†َ ุงู„ุซَّู…َุฑَุงุชِ ุฑِุฒْู‚ًุง ู„َّูƒُู…ْ ูۖَู„َุง ุชَุฌْุนَู„ُูˆุง ู„ِู„َّู€ู‡ِ ุฃَู†ุฏَุงุฏًุง ูˆَุฃَู†ุชُู…ْ ุชَุนْู„َู…ُูˆู†َ

“Ambaye amewafanyieni ardhi kuwa kama tandiko na mbingu kuwa kama paa na akateremsha kutoka mbinguni maji akawatolea kwayo matunda kuwa ni riziki kwenu. Hivyo basi msimfanyie Allaah washirika, na hali ya kuwa nyinyi mnajua.”

Katika mlango huu mtunzi wa kitabu anachotaka ni kuwatahadharisha watu kumfanyia Allaah washirika. Washirika ni wingi wa mshirika na walinganizi. Allaah amewaita waungu kama makaburi, miti na sayari kuwa ni “washirika” kwa sababu watu wanawaabudu pamoja na Allaah. Kama mtu anakiomba kitu, anakiomba uokozi, anakiomba mambo mengine na anaamini kuwa kinanufaisha na kudhuru kinaitwa “mshirika”. Allaah (Ta´ala) amesema:

ูˆَุฃَู†ุชُู…ْ ุชَุนْู„َู…ُูˆู†َ

“… na hali ya kuwa nyinyi mnajua.”

Bi maana na nyinyi mnatambua kuwa Yeye ndiye Muumbaji, Mruzukaji na Mungu wa haki (Subhaanahu wa Ta´ala). Amesema wakati alipokuwa akiwasema vibaya baadhi ya watu:

ูˆَู…ِู†َ ุงู„ู†َّุงุณِ ู…َู† ูŠَุชَّุฎِุฐُ ู…ِู† ุฏُูˆู†ِ ุงู„ู„َّู€ู‡ِ ุฃَู†ุฏَุงุฏًุง ูŠُุญِุจُّูˆู†َู‡ُู…ْ ูƒَุญُุจِّ ุงู„ู„َّู€ู‡ِ

“Miongoni mwa watu wako wenye kuchukua asiyekuwa Allaah kuwa ni mungu mshirika ambapo wanawapenda kama mapenzi wanavyompenda Allaah… “ (al-Baqarah 02:165)

Lengo kwa haya ni kuwaita watu kumtakasia ´ibaadah Allaah (Ta´ala) pekee. Yeye ndiye awe Mungu wa haki wa kuabudiwa pekee. Amesema (Ta´ala):

ูˆَุฅِู„َู€ٰู‡ُูƒُู…ْ ุฅِู„َู€ٰู‡ٌ ูˆَุงุญِุฏٌ ۖ ู„َّุง ุฅِู„َู€ٰู‡َ ุฅِู„َّุง ู‡ُูˆَ ุงู„ุฑَّุญْู…َู€ٰู†ُ ุงู„ุฑَّุญِูŠู…ُ

“Mungu wenu ni Mungu mmoja pekee; hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Yeye, Mwingi wa huruma, Mwenye kurehemu.” (al-Baqarah 02:163)

ูˆَู…َู† ูŠَุฏْุนُ ู…َุนَ ุงู„ู„َّู€ู‡ِ ุฅِู„َู€ٰู‡ًุง ุขุฎَุฑَ ู„َุง ุจُุฑْู‡َุงู†َ ู„َู‡ُ ุจِู‡ِ ูَุฅِู†َّู…َุง ุญِุณَุงุจُู‡ُ ุนِู†ุฏَ ุฑَุจِّู‡ِ ۚ ุฅِู†َّู‡ُ ู„َุง ูŠُูْู„ِุญُ ุงู„ْูƒَุงูِุฑُูˆู†َ

“Yeyote yule anayeomba pamoja na Allaah mungu mwengine – hana ushahidi wa wazi juu ya hilo – basi hakika hesabu yake iko kwa Mola wake. Hakika hawafaulu makafiri.” (al-Mu´minuun 23:117)

2- Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:

“Washirika ni shirki ambayo imejificha zaidi kuliko mdudu mchungu apitae juu ya jiwe jeusi katika usiku wenye giza. Nako ni kusema: “Naapa kwa jina la Allaah na kwa uhai wako fulani na uhai wangu”, “Lau ama si kijibwa hiki mwizi angelituingilia”, “Lau kama si bata ya nyumbani wezi wangelituingilia” na mtu kumwambia mwenzake: “Akitaka Allaah na wewe” na mtu kusema pia: “Lau kama si Allaah na fulani”. Usimchanganye Allaah na mwingine yeyote. Yote haya ni kumshirikisha Allaah.

Ameipokea Ibn Abiy Haaatim.

Ibn ´Abbaas ameyafasiri yote hayo kuwa ni shirki. Anamaanisha kuwa ni shirki ndogo iliyofichikana. Kwa sababu shirki ndogo ndani yake kunaingia kufanya washirika. Lakini baya na khatari zaidi ni kuyaomba masanamu na mawe. Hii ni shirki kubwa. Mtu anatakiwa kutia akilini kwamba shirki iliyofichikana (yaani shirki ndogo) inapelekea katika shirki kubwa. Kwa ajili hiyo ndio maana akazindua juu ya hilo ili watu waweze kujitenga mbali na yote mawili. Wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipoambiwa “Akitaka Allaah na wewe” akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Je, umenifanya kuwa mshirika wa Allaah? Sema: “Akitaka Allaah pekee.”[3]

Hivyo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaonelea kusema “Akitaka Allaah na wewe” ni katika kumfanyia Allaah washirika. Kwa ajili hiyo ndio maana inatakiwa kwa mtu kujiepusha na mambo kama hayo na misemo kama hiyo, kwa sababu “wa” inafahamisha ushirikiano na usawazishaji. Kadhalika inahusiana na msemo “Lau kama si bata au mbwa nyumbani basi watu wa nyumbani wasingeliwatambua wageni”. Ni kosa. Badala yake unatakiwa kusema “Lau kama si Allaah kisha bata”. Allaah ndiye Mwenye kusababisha sababu. Mtu hatakiwi kutegemea sababu; anatakiwa amtegemee Allaah pekee. Kwa ajili hiyo zile sababu hazitakiwi kutajwa peke yake au kuambatanishwa pamoja na “na”, isipokuwa ziambatanishwe na “kisha/halafu”. Mfano wa usemi mwingine ni “Lau kama si mtu yule basi alikuwa azame.” Ni kosa. Bali inatakiwa kusemwa “Lau kama si Allaah kisha fulani basi angelizama”.

 3- ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mwenye kuapa kwa asiyekuwa Allaah amekufuru au ameshirikisha.”[4]

Ameipokea at-Tirmidhiy ambaye ameisahihisha na al-Haakim pia ameisahihisha.

Ukweli wa mambo ni kwamba Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ndiye kasimulia haya. Mashaka katika Hadiyth inawezekana yanatokamana na Ibn ´Umar au mpokezi mwingine. Lakini maana yake ni moja. Kuapa kwa jina la mwingine asiyekuwa Allaah ni kumuadhimisha na kuona kuwa mtu/kitu hicho ni chenye kustahiki kiapo hicho. Kwa ajili hiyo inatakiwa kuapa kwa jina la Allaah pekee kwa sababu Yeye ndiye Mwenye kujua siri na mambo yaliyofichikana.

Hapo kabla waarabu walikuwa wakiapa kwa baba zao na kwa watu wakuu. Ni jambo lililokuwa linafaa mwanzoni mwa Uislamu. Kisha baadaye Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akalikataza na kulitahadharisha. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Msiape kwa baba zenu, mama zenu wala washirika.”[5]

Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mwenye kutaka kuapa basi aape kwa Allaah au anyamaze.”[6]

Imaam Ahmad amepokea kupitia kwa ´Umar kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mwenye kutaka kuapa basi aape kwa Allaah au anyamaze. Mwenye kuapa kwa kitu kingine badala ya Allaah ameshirikisha.”

Haya ni matamshi ya ´Umar kama tulivosema.

Kitendo hichi ni shirki ndogo. Kuna uwezekano vilevile ikawa ni shirki kubwa ikiwa yule muapaji anaonelea kuwa mtu huyo anayemuapia ana hadhi, anaendesha ulimwengu au anastahiki kuabudiwa badala ya Allaah. Vinginevyo ni shirki ndogo. Kwa ajili hiyo imepokelewa kwamba Salaf walikuwa wakiapa kwa baba zao mwanzoni mwa Uislamu. Lakini kwa ajili ya kukamilisha Tawhiyd, kumuadhimisha Allaah na kufunga njia zote zinazopelekea katika shirki wakayakataza hayo.

4- Ibn Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

“Kuapa kwa Allaah hali ya kuwa ni mwenye kusema uongo inapendeza zaidi kwangu kuliko kuapa kwa asiyekuwa Allaah hali ya kuwa ni mwenye kusema ukweli.”

Kwa sababu kuapa kwa asiyekuwa Allaah ni shirki na kuapa kwa kuapa kwa Allaah kwa kusema uongo ni dhambi. Shirki ni jambo la khatari kuliko dhambi. Sampuli ya shirki ni khatari kuliko sampuli ya maasi. Pamoja na hivyo uongo pia ni haramu.

5- Hudhayfah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Msisemi “Akitaka Allaah na fulani”. Lakini semeni: “Akitaka Allaah kisha akataka fulani”.”[7]

Ameipokea Abu Daawuud kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.

Kwa sababu “na” inafahamisha ushirika na usawazishaji. Kwa ajili hiyo haijuzu kusema hivo. Hata hivyo inafaa kusema “kisha/halafu” kwa sababu inaonyesha tofauti. Hata hivyo bora zaidi ni kusema “Lau kama si Allaah pekee.”

6- Imekuja kutoka kwa Ibraahiym an-Nakha-iy ya kwamba alikuwa akichukia mtu kusema: “Najilinda kwa Allaah na kwako”, lakini alikuwa anajuzisha kusema: “Najilinda kwa Allaah kisha kwako”. Pia akijuzisha mtu kusema: “Lau kama si kwa ajili ya Allaah kisha fulani” na wala usisemi: “Lau kama si kwa ajili ya Allaah na fulani”.

Haijuzu kusema “Najilida kwa fulani na fulani” au “Najilinda kwa Allaah na fulani na fulani”. Badala yake sema “Najilinda kwa Allaah”. Huu ndio ukamilifu wa Tawhiyd. Ni wajibu kwa muislamu kutilia bidii juu ya ukamilifu wa Tawhiyd na imani na kujiepusha na aina zote za shirki. Ni wajibu vilevile kujiepusha na sampuli zote za maasi kwa sababu ni mambo yanaipunguza Tawhiyd, imani na yakini.

Faida:

Hadiyth inayosema “Naapa kwa baba yangu atafaulu”[8] ni jambo lilitokea mwanzoni mwa Uislamu na kabla ya kukatazwa kusema hivo.

Haijuzu kusema “Lau kama si Allaah kisha Mtume wake basi tusingeongoka.”

Hadiyth inayosema “Hamwogopi isipokuwa Allaah na mbwa mwitu”[9] ni jambo haliingii katika maudhui haya. Inajuzu.

Haijuzu kusema “Nakuuliza kwa dhimma yako” au “Nakuuliza kwa amana” ikiwa mtu amekusudia kuapa kwa vitu hivyo. Vinginevyo inajuzu.

Inajuzu kusema “Naomba ulinzi kwa Allaah kutokamana na wewe”. Pindi mwanamke alipomwambia hivo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwambia mwanamke yule:

“Umeomba ulinzi kwa aliye Mtukufu.”[10]

Baada ya hapo akamwacha.

Mtu akitendewa wema na mwengine na akamwambia kwamba yeye ni mwokozi mkubwa, yote haya yanategemea nia. Bora ni kusema “Lau kama isingelikuwa Allaah kisha wewe”. Kusema “Wewe ni mwokozi mkubwa” ni jambo linaweza kuleta mashaka.

[1] Abu Daawuud (3251), at-Tirmidhiy (1535) na Ahmad (6072). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”al-Irwaa’” (2561).

[2] Abu Daawuud (4980), Ahmad (23313) na Ibn Abiy Shaybah (2669). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”as-Silsilah as-Swahiyhah” (137).

[3] Ahmad (1839), al-Bukhaariy katika ”al-Adab al-Mufrad” (783) na at-Twabaraaniy (13005). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”as-Silsilah as-Swahiyhah” (139).

[4] Abu Daawuud (3251), at-Tirmidhiy (1535) na Ahmad (6072). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”al-Irwaa’” (2561).

[5] Abรป Daawuud (3248) na an-Nasaa’iy (3769). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh-ul-Jaami´” (7249).

[6] al-Bukhaariy (2679) na Muslim (1646).

[7] Abu Daawuud (4980), Ahmad (23313) na Ibn Abiy Shaybah (2669). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”as-Silsilah as-Swahiyhah” (137).

[8] Muslim (11).

[9] al-Bukhaariy (3852).

[10] al-Bukhaariy (5254).



from Firqatu Nnajia https://ift.tt/2CSHftu
via IFTTT

41. Mlango kuhusu maneno Yake (Ta´ala) “Wanazielewa vyema neema za Allaah, kisha wanazikanusha – na wengi wao ni makafiri”

Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:

1- Allaah (Ta´ala) amesema:

ูŠَุนْุฑِูُูˆู†َ ู†ِุนْู…َุชَ ุงู„ู„ّู‡ِ ุซُู…َّ ูŠُู†ูƒِุฑُูˆู†َู‡َุง ูˆَุฃَูƒْุซَุฑُู‡ُู…ُ ุงู„ْูƒَุงูِุฑُูˆู†َ

”Wanazielewa vyema neema za Allaah, kisha wanazikanusha – na wengi wao ni makafiri.” (an-Nahl 16:83)

2- Mujaahid amesema kuhusu maana yake:

“Ni mtu kusema: “Hii ni mali yangu. Nimeirithi kutoka kwa mababu zangu.”

3- ´Awn bin ´Abdillaah amesema:

Wanasema:  “Lau  kama si fulani nisingelikuwa hivi na hivi.”

4- Ibn Qutaybah amesema:

“Wanasema: “Haya ni kutokana na uombezi wa waungu wetu.”

5- Abul-´Abbaas amesema baada ya Hadiyth ya Zayd bin al-Haarith:

“Katika asubuhi hii kuna baadhi ya waja Wangu wamepambaukia wakiwa ni wenye kuniamini na wengine wamekufuru. Ama yule aliyesema kwamba: “Tumenyeshewa mvua kwa fadhila na rehema ya Allaah”, basi huyo ndiye aliyeniamini Mimi na amekufuru sayari. Ama yule aliyesema ya kwamba tumenyeshewa mvua kutokana na sayari fulani na fulani, basi huyo amenikufuru Mimi na ameamini sayari.”

“Haya yamekuja sehemu nyingi katika Qur-aan na Sunnah; Allaah (Subhaanah) anawasema vibaya wale ambao wanazinasibisha neema Zake kwa asiyekuwa Yeye na wanamshirikisha.”

6- Baadhi ya Salaf wamesema:

“Aayah inawazungumzia wale wenye kusema: “Upepo ulikuwa mzuri na baharia huyu alikuwa hodari” na mfano wa maneno kama hayo ambayo hupitika katika ndimi za watu wengi.”

MAELEZO

1- Allaah (Ta´ala) amesema:

ูŠَุนْุฑِูُูˆู†َ ู†ِุนْู…َุชَ ุงู„ู„ّู‡ِ ุซُู…َّ ูŠُู†ูƒِุฑُูˆู†َู‡َุง ูˆَุฃَูƒْุซَุฑُู‡ُู…ُ ุงู„ْูƒَุงูِุฑُูˆู†َ

”Wanazielewa vyema neema za Allaah, kisha wanazikanusha – na wengi wao ni makafiri.”

Mwandishi amechokusudia ni watu wazitambue neema za Allaah (Subhaanah) na wamshukuru Yeye kwa ajili yazo kwa sababu watu wengi wanaghafilika juu ya hilo. Wanastareheka na neema za Allaah lakini pamoja na hivyo hawamshukuru. Bali wanazinasibisha neema hizo kwa sababu yazo na kwa nguvu zao wenyewe na matendo yao na wakati huohuo wanaghafilika Naye ambaye kihakika ndiye kawatunukia neema hizi. Lau Allaah angelitaka basi angelitokomeza sababu na nguvu ya neema hizo. Allaah ndiye ambaye kamtunukia mtu huyo usikizi, uoni, akili, werevu na mengineyo. Hii ni moja katika tabia za makafiri ambao husema kuwa wamepata mali kwa sababu ya mirathi na mengineyo. Allaah (Ta´ala) amesema:

 ุซُู…َّ ูŠُู†ูƒِุฑُูˆู†َู‡َุง

“… kisha wanazikanusha… “

Wanastareheka nazo na wanazitambua vyema, halafu pamoja na yote haya wanazinasibisha kwa waungu na masanamu yao. Hawataki kuzikiri.

 2- Mujaahid amesema kuhusu maana yake:

“Ni mtu kusema: “Hii ni mali yangu. Nimeirithi kutoka kwa mababu zangu.”

Anasema hivo kwa kujisifu na kujiona juu ya jambo hili pasi na kuzikiri neema za Allaah na anaghafilika na hilo. Hasemi hivo kwa njia ya kuelezea, bali anasema hivo kwa kughafilika na kusahau kwamba ni Allaah kweli ndiye kamtunukia neema hiyo. Hata hivyo ni jambo linalofaa mtu akaelezea sababu ya neema fulani.

3- ´Awn bin ´Abdillaah amesema:

Wanasema:  “Lau  kama si fulani nisingelikuwa hivi na hivi.”

Hili pia ni kosa. Mtu anatakiwa kusema:

“Lau kama si Allaah kisha hivi na hivi… “

Neema inatakiwa kunasibishwa kwa Alallah. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) ndiye mwenye kutoa na kutunuku.

4- Ibn Qutaybah amesema:

“Wanasema: “Haya ni kutokana na uombezi wa waungu wetu.”

Haya ni maneno ya makafiri. Ni wajibu kwa muislamu kujitofautisha nao na kuzinasibiha neema kwa Allaah. Allaah ndiye Mwenye kusababisha sababu. Kwa ajili hiyo ni wajibu kwa muislamu kumshukuru Allaah na kuyatendea kazi maamrisho Yake. Allaah (Ta´ala) amesema:

ูˆَู…َุง ุจِูƒُู… ู…ِّู† ู†ِّุนْู…َุฉٍ ูَู…ِู†َ ุงู„ู„َّู€ู‡ِ ۖ ุซُู…َّ ุฅِุฐَุง ู…َุณَّูƒُู…ُ ุงู„ุถُّุฑُّ ูَุฅِู„َูŠْู‡ِ ุชَุฌْุฃَุฑُูˆู†َ

“Neema yoyote mliyo nayo, basi ni kutoka kwa Allaah. Kisha inapokuguseni dhara Kwake mnamlilia msaada.”[1]

5- Abul-´Abbaas amesema baada ya Hadiyth ya Zayd bin al-Haarith:

“Katika asubuhi hii kuna baadhi ya waja Wangu wamepambaukia wakiwa ni wenye kuniamini na wengine wamekufuru. Ama yule aliyesema kwamba: “Tumenyeshewa mvua kwa fadhila na rehema ya Allaah”, basi huyo ndiye aliyeniamini Mimi na amekufuru sayari. Ama yule aliyesema ya kwamba tumenyeshewa mvua kutokana na sayari fulani na fulani, basi huyo amenikufuru Mimi na ameamini sayari.”

“Haya yamekuja sehemu nyingi katika Qur-aan na Sunnah; Allaah (Subhaanah) anawasema vibaya wale ambao wanazinasibisha neema Zake kwa asiyekuwa Yeye na wanamshirikisha.”

 Wanasema hivo kwa kujisifu na kujitapa mbele za wengine.

6- Baadhi ya Salaf wamesema:

“Aayah inawazungumzia wale wenye kusema: “Upepo ulikuwa mzuri na baharia huyu alikuwa hodari” na mfano wa maneno kama hayo ambayo hupitika katika ndimi za watu wengi.”

Wanasema hivo pindi safina inaporudi salama salimina. Wanamsahau Allaah kwamba ndiye ambaye aliwapa upepo huo na ndiye ambaye kamfunza baharia huyo. Kwa hivo ni wajibu kuzinasibisha neema kwa Allaah (Ta´ala) pamoja na kuzitambua sababu kama vile kusema kwamba Allaah katusahalishia upepo mzuri. Hili linafaa. Hii ni dalili inayoonyesha namna ambavo Salaf walikuwa wakitilia bidii na kupupia juu ya kumshukuru Allaah na kuzitambua neema Zake (Subhaanahu wa Ta´ala).

[1] 16:53



from Firqatu Nnajia https://ift.tt/2Q9qUnW
via IFTTT

Adhkaar Zenye Thawabu Maradufu

MAWAIDHA : Sheikh Nuruddin Kishki - Mwanamke alieolewa na Mahari yake ni Uislamu [Listen/Download]

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

  ุฅِู†َّ ุงู„ุดِّุฑْูƒَ ู„َุธُู„ْู…ٌ ุนَุธِูŠู…   Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!   20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah   ...