
from FB-RSS feed for Islamkingdom - Swahili https://ift.tt/2Pwwdkl
via IFTTT
Wengi wanaaminu kuna nyoka mmoja tu aitwaye cobra, lakini ukweli ni kwamba kuna aina takriban 270 za viumbe za cobra. Hata hivyo, wataalamu wa elimu ya viumbe wanasema kuna wanaowaita kobra wa kweli 28 (true cobra), miongoni mwao ni huyo Indian cobra, Binosolate cobra, Cape cobra, Spitting cobra bila kumsahau mkubwa wao King cobra nk.
Indian cobra hapatikani katika maeneo yetu ya ukanda huu wa Afrika, bali wapo kwa wingi Asia ya Kusini katika nchi za l India, Pakistan, Bangladesh, Nepal na katika kisiwa cha Srilanka. Naye hutukuzwa sana katika imani na mila za kihindu na pia kule Srilanka katika dini ya Mabudha kiasi kwamba ni haramu kumuua katika sheria zao.
Sifa kubwa ya Indian cobra ni kutanuka shingoni na inatajwa kuwa ndiye nyoka pekee anayetanuka eneo hilo lakini kichwa kikabaki vilevile. Wengi wana urefu wa kati ya mita 1-mita 1.5 lakini wale wa Srilanka wapo mpaka kuanzia mita 2.1 hadi mita 2.2. Indian Cobra anaweza kuwa na rangi ya njano, kijivu, kahawia, nyekundu au nyeusi.
Uzazi
Indian cobra ni ‘oviparus’ yaani anataga mayai nje. Kipindi chao cha kutaga mayai ni mwezi wa Aprili hadi Julai. Nyoka hawa hutaga mayai kuanzia 10 hadi 30 katika mashimo ya panya au sungu sungu na baada ya siku 48 au 60 mayai yanaanguliwa.
Kama ilivyo kwa nyoka wengine, nyoka hawa pia hawana kawaida wala muda wa kulinda mayai yao. Ni King cobra pekee ndiye hulinda mayai yake. Pia, muda mfupi tu baada ya Indian cobra kutotoa mayai, vitoto vinavyozaliwa huanza kujitegemea.
Mambo 10 usiyoyajua kuhusu Indian cobra
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
1- Kauli ya Allaah (Ta´ala):
وَهُمْ يَكْفُرُونَ بِالرَّحْمَنِ
“… ilihali wao wanamkanusha Mwingi wa rehema.” (ar-Ra´d 13:30)
2- al-Bukhaariy amepokea katika “as-Swahiyh” yake kwamba ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Waelezeni watu kwa wanayoyajua. Je, mnataka akadhibishwe Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?”[1]
3- ´Abdur-Razzaaq amepokea kutoka kwa Ma´mar, kutoka kwa Ibn Twaawuus, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Ibn ´Abbaas ambaye alimuona mtu akisisimka wakati aliposikia Hadiyth kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) iliotaja sifa za Allaah akiwa ni mwenye kulipinga hilo ambapo akasema:
“Ni kitu gani kinachowatia woga watu hawa? Wanafanya woga kwa Aayah zilizo wazi ilihali wanaegemea Aayah sizizokuwa waz.”[2]
Pindi Quraysh walipomsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akitaja Mwingi wa rehema wakapinga hilo. Ndipo Allaah akateremsha juu yao:
وَهُمْ يَكْفُرُونَ بِالرَّحْمَنِ
“… ilihali wao wanamkanusha Mwingi wa rehema.”
MAELEZO
Mlango huu mwandishi ameutunga kwa ajili ya kubainisha uwajibu wa kuthibitisha majina na sifa za Allaah kwa njia inayolingana Naye (Subhaanahu wa Ta´ala) pasi na kupotosha, kukanusha, kuzifanyia namna, kuzifananisha wala kuzigeuza. Mtu hatakiwi kudhanganyika na maoni ya Mu´tazilah na watu wa batili wengine. Ni wajibu kwake kuchukua yale yaliyosemwa na Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah katika Maswahabah na wale waliofuata mwenendo wao. Hii ndio ´Aqiydah iliofikishwa na Mitume. Wote walikuwa ni wenye kuthibitisha majina na sifa za Allaah kwa njia inayolingana Naye. Maswahabah na wale wote waliowafuata kwa wema walizipitisha Aayah na Hadiyth zinazozungumzia sifa kama zilivyokuja na wakathibitisha zile dalili za majina na sifa. Yote hayo kwa ajili ya kutendea kazi maneno Yake Allaah:
قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ اللَّهُ الصَّمَدُ لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا أَحَدٌ
“Sema: “Yeye ni Allaah – Mmoja pekee, Allaah aliyekamilika, mkusudiwa wa haja zote. Hakuzaa na wala hakuzaliwa, na wala hakuna yeyote anayefanana na kulingana Naye.” (al-Ikhlaasw 112:01-04)
فَلَا تَضْرِبُوا لِلَّـهِ الْأَمْثَالَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ
”Basi msimpigie Allaah mifano! Hakika Allaah anajua nanyi hamjui.” (al-Israa´ 16:74)
لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ
“Hakuna chochote kinachofanana Naye – Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (ash-Shuuraa 42:11)
هَلْ تَعْلَمُ لَهُ سَمِيًّا
“Je, unamjua yeyote mwenye jina kama Lake?” (Maryam 19:65)
Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) hana Mwenye jina kama Lake wala anayelingana Naye.
Kuhusu Jahmiyyah wao wamekanusha majina na sifa za Allaah na wakayapindisha majina. Maoni yao yanapelekea kukanusha kabisa kabisa uwepo wa Allaah. Kwa ajili hiyo ndio maana Ahl-us-Sunnah wamewakufurisha. Ni wajibu kuwaua ikiwa hawakutubia. Wanatakiwa kuambiwa kutubia kwa sababu ya kupinga kwao yale yaliyotajwa katika Qur-aan na Sunnah na maafikiano. Mwandishi ametaja kichwa cha khabari kwa kutokufungamanisha pasi na kumhukumu yule mwenye kukanusha majina na sifa za Allaah. Hata hivyo hukumu yake ni kwamba ni kafiri.
1- Kauli ya Allaah (Ta´ala):
وَهُمْ يَكْفُرُونَ بِالرَّحْمَنِ
“… ilihali wao wanamkanusha Mwingi wa rehema.”
Allaah (Ta´ala) amebainisha kwamba Mwingi wa rehema ndio Mola na Mungu wetu na kwamba yule mwenye kumkufuru Mwingi wa rehema basi amemkufuru Allaah. Kwa hivyo ni wajibu kwa muumini kutahadhari na sifa za wapotevu hawa na afuate mwenendo wa wanachuoni na waumini. Allaah ameonelea kule kukanusha kwao sifa hii ni kumkufuru Mwingi wa huruma na ni dalili inayofahamisha kwamba mwenye kukanusha sifa amekufuru.
2- al-Bukhaariy amepokea katika “as-Swahiyh” yake kwamba ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Waelezeni watu kwa wanayoyajua. Je, mnataka akadhibishwe Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?”
Mtu ambaye anawawaidhi na kuwakumbusha wengine basi anatakiwa kutumia matamshi na usulubu wanaoutambua ili waweze kustafidi na kufaidika. Kila watu wana usulubu wao. Ukiwazungumzisha watu kwa njia wasiyoitambua basi kuna khatari wakaja kukufahamu vibaya. Haijalishi kitu maudhui yanahusiana na majina, sifa au hukumu za Allaah. Haijalishi kitu lugha unayozungumza ni kiarabu, kingereza, urdu au lugha nyingine. Hata waarabu wenyewe wanaelewa tofauti. Zungumza na watu wote kwa njia waliyozowea ili waweze kukifahamu kile unachokisema na ili wasije kumkadhibisha Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Wale wanaomkadhibisha Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika sifa za Allaah wako katika khatari kubwa. Kwa sababu wamezipindisha sifa za Allaah kinyume na tafsiri zake na wamezizungumzia kwa njia isiyostahiki mpaka mwishowe wakazikanusha. Wengi wao kuna uwezekano wakawa wamezifahamu kimakosa kwa sababu sio waarabu. Baadhi ya Salaf wamesema kuwa ´Amr bin ´Ubayd amesema kuwa watenda madhambi watadumishwa Motoni milele kwa sababu Allaah kawaahidi hilo. Ndipo Salaf wakamwambia kwamba Allaah anaweza kuvunja ahadi ya adhabu na hawezi kuvunja ahadi ya thawabu. Kuvunja ahadi ya adhabu ni utukufu na kuvunja ahadi ya thawabu ni kusemwa vibaya. Ndipo wakamwambia:
“Umetumbukia katika hayo kwa sababu sio mwarabu.”
Bi maana unadhani kuwa ni jambo baya kuvunja ahadi ya adhabu. Si kweli. Mshairi amesema:
Mimi nikiahidi kumuadhibu au kumlipa
nitaivunja ahadi yangu ya kumuadhibu na kutimiza ahadi yangu ya kumlipa
Hii ni sifa.
3- ´Abdur-Razzaaq amepokea kutoka kwa Ma´mar, kutoka kwa Ibn Twaawuus, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Ibn ´Abbaas ambaye alimuona mtu akisisimka wakati aliposikia Hadiyth kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) iliotaja sifa za Allaah akiwa ni mwenye kulipinga hilo ambapo akasema:
“Ni kitu gani kinachowatia woga watu hawa? Wanafanya woga kwa Aayah zilizo wazi ilihali wanaegemea Aayah sizizokuwa waz.”
Pindi Quraysh walipomsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akitaja Mwingi wa rehema wakapinga hilo. Ndipo Allaah akawateremshia juu yao:
وَهُمْ يَكْفُرُونَ بِالرَّحْمَنِ
“… ilihali wao wanamkanusha Mwingi wa rehema.”
Wakati wanaposikia Aayah za wazi na Hadiyth wanasikia woga na wanakuwa na unyenyekevu. Wanaposikia Aayah kuhusu sifa za Allaah zinawatatiza na wanaangamia kwa sababu ya kutatizika na kukanusha. Hii ni dalili inayoonyesha kuwa jambo hili ni la tokea hapo kale na kwamba kitu kama hicho kilikuwepo tokea hapo wakati wa Maswahabah. Wanaangamia kwa sababu ya Aayah za Qur-aan na Hadiyth ambazo wanaona kuwa haziko wazi na wanazitilia mashaka. Ni dalili inayofahamisha kwamba kupinga na kutilia mashaka yale Allaah aliyowabainishia waja Wake ni maangamivu.
Haki ni kuamini yale yote yaliyokhabarishwa na Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ukifahamu kilichosemwa, ni jambo zuri na himdi zote ni za Allaah, na kama bado hujafahamu, basi unachotakiwa kusema ni kwamba Allaah ndiye mjuzi zaidi na uwaulize wanachuoni. Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wanaamini yale yote yaliyotajwa katika Qur-aan na Sunnah. Wameridhishwa nayo na wanayatendea kazi. Pindi wanapokutana na kitu ambacho kimewatatiza basi wanakirudisha katika zile Aayah ambazo ziko wazi na bainifu na kwa njia hiyo wanakifahamu. Hawaifanyi Qur-aan wala Sunnah kuwa ni vyenye kugongana. Hawatilii mashaka. Wanatambua kuwa yale maandiko ambayo hayako wazi hayapingani na yale yaliyo wazi. Bali uhakika wa mambo yale maandiko yasiyokuwa wazi ni sehemu ya yale yaliyo wazi. Yale yote ambayo hawakuyafahamu wanamwacha Yeye ambaye anayajua yaliyofichikana ayashughulikie ambaye ni Allaah (Subhaanah). Kuhusu maana yake ni yenye kufahamika katika lugha ya kiarabu ambayo Allaah amewazungumzisha watu kwayo. Kwa ajili hiyo Imaam Maalik (Rahimahu Allaah) amesema wakati alipoulizwa swali kuhusu kulingana kwa Allaah:
“Kulingana kunatambulika. Namna haijulikani. Kuuliza juu ya hilo ni Bid´ah.”
Bi maana ni Bid´ah kuuliza kuhusu namna. Amebainisha (Rahimahu Allaah) kwamba kulingana kunatambulika na kwamba namna haitambuliki.
Faida:
Mwenye kusema kwamba Pepo na Moto vitatokomea/vitakwisha ni kafiri. Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amesema:
وَأَمَّا الَّذِينَ سُعِدُوا فَفِي الْجَنَّةِ خَالِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ إِلَّا مَا شَاءَ رَبُّكَ ۖ عَطَاءً غَيْرَ مَجْذُوذٍ
“Ama wale walio furahani, basi watakuwa katika mabustani, ni wenye kudumu ndani yake zitakavyodumu mbingu na ardhi isipokuwa atakavyo Mola wako – ni hiba isiyokatizwa.” (Huud 11:108)
لَا يَمَسُّهُمْ فِيهَا نَصَبٌ وَمَا هُم مِّنْهَا بِمُخْرَجِينَ
“Hautowapata ndani yake uchovu nao humo hawatotolewa.” (al-Hijr 15:48)
Kadhalika ni kosa kusema kwamba Moto utakwisha. Maoni sahihi walionayo Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ni kwamba Moto hautakwisha.
Faida:
Waislamu wamekubaliana juu ya kwamba ardhi imetulizana na jua ndio linalozunguka. Wale wanaosema kwamba ardhi ndio inayolizunguka jua wanachomaanisha ni kwamba ardhi ndio iliyotulizana, jambo ambalo ni kufuru:
وَالشَّمْسُ تَجْرِي لِمُسْتَقَرٍّ لَّهَا ۚذَٰلِكَ تَقْدِيرُ الْعَزِيزِ الْعَلِيمِ
“Na jua linatembea hadi matulio yake, hayo ni matengenezo ya Mwenye nguvu kabisa, mjuzi.” (Yaa Siyn 36:38)
[1] al-Bukhaariy (129).
[2] al-Muswannaf (20895). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwilaal-ul-Jannah” (485).
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
1- Allaah (Ta´ala) amesema:
أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ يَزْعُمُونَ أَنَّهُمْ آمَنُواْ بِمَا أُنزِلَ إِلَيْكَ وَمَا أُنزِلَ مِن قَبْلِكَ يُرِيدُونَ أَن يَتَحَاكَمُواْ إِلَى الطَّاغُوتِ وَقَدْ أُمِرُواْ أَن يَكْفُرُواْ بِهِ وَيُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُضِلَّهُمْ ضَلاَلاً بَعِيدًا
”Je, huoni wale ambao wanadai kwamba wao wameamini yaliyoteremshwa kwako na yale yaliyoteremshwa kabla yako, wanataka wahukumiane kwa Twaaghuut na hali wameamrishwa wakanushe hiyo, na shaytwaan anataka awapoteze upotofu wa mbali kabisa.” (an-Nisaa´ 04:60)
2-
وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ لاَ تُفْسِدُواْ فِي الأَرْضِ قَالُواْ إِنَّمَا نَحْنُ مُصْلِحُونَ
”Na wanapoambiwa: “Msifanye uharibifu katika ardhi.” Husema: “Hakika sisi ni watengenezaji.” (al-Baqarah 02:11)
3-
وَلاَ تُفْسِدُواْ فِي الأَرْضِ بَعْدَ إِصْلاَحِهَا
”Na wala msifanye ufisadi katika ardhi baada ya kutengenea kwake.” (al-A´raaf 07:56)
4-
أَفَحُكْمَ الْجَاهِلِيَّةِ يَبْغُونَ
”Je, wanataka [uwahukumu kwa] hukumu ya kipindi cha makafiri?” (al-Maaidah 05:50)
5- ´Abdullaah bin ´Amr (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hatoamini mmoja wenu mpaka matamanio yake yawe ni yenye kufuata yale niliyokuja nayo.”[1]
an-Nawawiy amesema:
“Hadiyth ni Swahiyh. Nimeipokea katika “Kitaab-ul-Hujjah” kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.
6- ash-Sha´biy amesema:
“Kulikuwa ugomvi baina ya mtu mmoja mnafiki na mwingine myahudi. Yule myahudi akasema: “Twende kwa Muhammad atuhukumu.” Mnafiki yule alijua kuwa hachukui rushwa. Mnafiki yule akasema: “Twende kwa mayahudi watuhukumu.” Kwa kujua kwake kuwa wao wanachukua rushwa. Hivyo wote wawili wakakubaliana kumwendea kuhani Juhaynah ili awahukumu. Ndipo kukateremka:
أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ يَزْعُمُونَ أَنَّهُمْ آمَنُواْ بِمَا أُنزِلَ إِلَيْكَ وَمَا أُنزِلَ مِن قَبْلِكَ يُرِيدُونَ أَن يَتَحَاكَمُواْ إِلَى الطَّاغُوتِ وَقَدْ أُمِرُواْ أَن يَكْفُرُواْ بِهِ وَيُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُضِلَّهُمْ ضَلاَلاً بَعِيدًا
”Je, huoni wale ambao wanadai kwamba wao wameamini yaliyoteremshwa kwako na yale yaliyoteremshwa kabla yako, wanataka wahukumiane kwa Twaaghuut na hali wameamrishwa wakanushe hiyo, na shaytwaan anataka awapoteze upotofu wa mbali kabisa.” (an-Nisaa´ 04:60)
Kuna maoni mengine yanayosema kwamba iliteremka juu ya watu wawili waliogombana ambapo mmoja wao akasema:
“Hebu tumpelekee kesi yetu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aihukumu.” Yule mwengine akasema: “Wacha tumpelekee Ka´b bin al-Ashraf.” Mwishowe wakampelekea nayo ´Umar mmoja wao akamueleza kisa kilivyokuwa. Akamuuliza yule ambaye hakuridhia ipelekwe kesi kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): “Mambo ni hivyo?” Mtu yule akasema: “Ndio.” ´Umar akampiga kwa upanga na akamuua.”
MAELEZO
1- Allaah (Ta´ala) amesema:
أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ يَزْعُمُونَ أَنَّهُمْ آمَنُواْ بِمَا أُنزِلَ إِلَيْكَ وَمَا أُنزِلَ مِن قَبْلِكَ يُرِيدُونَ أَن يَتَحَاكَمُواْ إِلَى الطَّاغُوتِ وَقَدْ أُمِرُواْ أَن يَكْفُرُواْ بِهِ وَيُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُضِلَّهُمْ ضَلاَلاً بَعِيدًا
”Je, huoni wale ambao wanadai kwamba wao wameamini yaliyoteremshwa kwako na yale yaliyoteremshwa kabla yako, wanataka wahukumiane kwa Twaaghuut na hali wameamrishwa wakanushe hiyo, na shaytwaan anataka awapoteze upotofu wa mbali kabisa.”
Anachotaka mwandishi ni kuwatahadharisha watu kuhukumiana kinyume na Shari´ah ya Allaah. Lililo la wajibu ni kuhukumian na Shari´ah ya Allaah katika mambo yote. Allaah (Ta´ala) amesema:
فَلَا وَرَبِّكَ لَا يُؤْمِنُونَ حَتَّىٰ يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيْنَهُمْ ثُمَّ لَا يَجِدُوا فِي أَنفُسِهِمْ حَرَجًا مِّمَّا قَضَيْتَ وَيُسَلِّمُوا تَسْلِيمًا
“Naapa kwa Mola wako! Hawatoamini mpaka wakufanye wewe ni hakimu katika yale wanayozozana kati yao kisha wasipate katika nyoyo zao uzito katika yale uliyohukumu na wajisalimishe kwa kujisalimisha” (an-Nisaa´ 04:65)
وَأَنِ احْكُم بَيْنَهُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ
“Wahukumu baina yao kwa yale aliyoyateremsha Allaah.” (al-Maaidah 05:49)
وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْكَافِرُونَ
“Yeyote asiyehukumu kwa yale aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio makafiri.” (al-Maaidah 05:44)
وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ
“Yeyote asiyehukumu kwa yale aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio madhalimu.” (al-Maaidah 05:45)
وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ
“Yeyote asiyehukumu kwa yale aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio mafasiki.” (al-Maaidah 05:47)
Haya yote yanafahamisha juu ya uwajibu wa kuhukumiana na Shari´ah ya Allaah na kwamba haijuzu kuhukumiana na kitu kingine. Huu ni msingi ambao kuna maafikiano juu yake.
Aayah inabainisha vilevile kwamba wapo watu wanaodai imani na Uislamu ilihali ukweli wa mambo sivo hivyo; bali ni wanafiki. Kunapotokea kitu basi wanataka wahukumiwe kinyume na Shari´ah ya Allaah na Twaaghuut. Twaaghuut ni kila chenye kuabudiwa badala ya Allaah na mwenye kuhukumu kinyume na Shari´ah ya Allaah kwa kukusudia na kwa matamanio. Wanafiki wanataka wahukumiwe na yule ambaye anaafikiana na matamanio yao na ambaye anapokea rushwa ili aweze kuwapatia haki wao. Hii ni dalili juu ya unafiki wao. Wanafiki kazi yao ni kuipa mgongo haki. Allaah (Ta´ala) amesema:
ذَا قِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا إِلَىٰ مَا أَنزَلَ اللَّـهُ وَإِلَى الرَّسُولِ رَأَيْتَ الْمُنَافِقِينَ يَصُدُّونَ عَنكَ صُدُودًا
“Wanapoambiwa: “Njooni kwenye yale aliyoyateremsha Allaah na kwa Mtume”, basi utawaona wanafiki wanakugeukilia mbali kwa mkengeuko.” (an-Nisaa´ 04:61)
Kwa hivyo ni wajibu kwa mtu kutahadhari nao na tabia zao mbaya.
2-
وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ لاَ تُفْسِدُواْ فِي الأَرْضِ قَالُواْ إِنَّمَا نَحْنُ مُصْلِحُونَ
”Na wanapoambiwa: “Msifanye uharibifu katika ardhi.” Husema: “Hakika sisi ni watengenezaji.”
Wanadai kwamba ni wenye kutengeneza, lakini uhakika wa mambo ni wenye kuharibu kwa sababu ya ujinga wao, upotevu wao na unafiki wao. Akili zao zimepinduliwa chini juu na ndio maana wakachukulia ufisadi kuwa ni matengenezo. Kwa ajili hii Allaah (Ta´ala) akasema:
أَلَا إِنَّهُمْ هُمُ الْمُفْسِدُونَ وَلَـٰكِن لَّا يَشْعُرُونَ
“Tanabahi! Hakika wao ndio mafisadi lakini hawahisi.” (al-Baqarah 02:12)
3-
وَلاَ تُفْسِدُواْ فِي الأَرْضِ بَعْدَ إِصْلاَحِهَا
”Na wala msifanye ufisadi katika ardhi baada ya kutengenea kwake.”
Kutengenea kwa ardhi kunakuwa kwa kufuata na kuhukumiana kwa Shari´ah. Inaharibiwa kwa kwenda kinyume na amri ya Allaah na kuhukumiana na sheria zengine.
4-
أَفَحُكْمَ الْجَاهِلِيَّةِ يَبْغُونَ
”Je, wanataka [uwahukumu kwa] hukumu ya kipindi cha makafiri?”
Watu hawa wanataka kuhukumiwa na mayahudi na Twaaghuut sampuli zengine kwa hukumu za kipindi cha kikafiri. Hivi kuna hukumu ilio bora kuliko hukumu ya Allaah? Yeye ndiye anajua bora manufaa ya waja Wake. Anajua namna mambo yatavyomalizika. Yeye ndiye mjuzi wa kila kitu.
5- ´Abdullaah bin ´Amr (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hatoamini mmoja wenu mpaka matamanio yake yawe ni yenye kufuata yale niliyokuja nayo.”
Bi maana hatoamini imani kamilifu na ya wajibu mpaka matamanio yake, utashi wake, makusudio yake na matakwa yake yawe ni yenye kufuata yale aliyokuja nayo yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ni wajibu makusudio ya muumini yawe ni yenye kujisalimisha na hukumu ya Allaah. Baadhi ya wanachuoni wamesema kuwa Hadiyth hii ni dhaifu, lakini hata hivyo maana yake ni sahihi.
6- ash-Sha´biy amesema:
“Kulikuwa ugomvi baina ya mtu mmoja mnafiki na mwingine myahudi. Yule myahudi akasema: “Twende kwa Muhammad atuhukumu.” Mnafiki yule alijua kuwa hachukui rushwa. Mnafiki yule akasema: “Twende kwa mayahudi watuhukumu.” Kwa kujua kwake kuwa wao wanachukua rushwa. Hivyo wote wawili wakakubaliana kumwendea kuhani Juhaynah ili awahukumu. Ndipo kukateremka:
أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ يَزْعُمُونَ أَنَّهُمْ آمَنُواْ بِمَا أُنزِلَ إِلَيْكَ وَمَا أُنزِلَ مِن قَبْلِكَ يُرِيدُونَ أَن يَتَحَاكَمُواْ إِلَى الطَّاغُوتِ وَقَدْ أُمِرُواْ أَن يَكْفُرُواْ بِهِ وَيُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُضِلَّهُمْ ضَلاَلاً بَعِيدًا
”Je, huoni wale ambao wanadai kwamba wao wameamini yaliyoteremshwa kwako na yale yaliyoteremshwa kabla yako, wanataka wahukumiane kwa Twaaghuut na hali wameamrishwa wakanushe hiyo, na shaytwaan anataka awapoteze upotofu wa mbali kabisa.”
Hii ni dalili inayoonyesha kuwa mnafiki ana shari zaidi kuliko myahudi. Kwa sababu wanawababaisha watu na kusababisha upotevu. Kwa ajili hio ndio maana wakawa katika tabala ya chini kabisa Motoni.
Ni wajibu kuhukumiana na Shari´ah ya Allaah na kutoridhia nyengine. Kisa cha ´Umar kinathibitisha kwamba kuhukumu kinyume na Shari´ah ni kufuru na kuritadi. Vilevile yule mwenye kuchukia hukumu ya Allaah ni kafiri. Usahihi wa visa vyote viwili unahitajia kutazamwa vizuri, lakini maana zake ni sahihi.
ash-Sha´biy ni ´Aamir bin Sharaahil.
Faida:
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah amemuumba Aadam kwa sura Yake.”[2]
Ina maana kwamba Allaah alimuumba Aadam kwa usikizi, uoni, akizungumza, uso, mikono, nyayo na mengineyo. Allaah anasikia na Aadam pia alikuwa akisikia. Allaah anazungumza na Aadam pia alikuwa akizungumza na kadhalika. Lakini hafanani na Allaah inapokuja katika dhati na sifa za Allaah:
لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ
“Hakuna chochote kinachofanana Naye – Naye ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (ash-Shuuraa 42:11)
Kuhusiana na ambaye amesema kuwa dhamiri inarudi kwa Aadam, ni kosa. Aliyesema hivo lengo lake ilikuwa kukimbia kufananisha.
[1] Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwilaal-ul-Jannah” (15)na ”Mishkaat-ul-Maswaabîh” (167).
[2] al-Bukhaariy (6227) na Muslim (2841).
Swali: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mimi nimejiweka mbali na kila muislamu anayeishi kati ya washirikina.”[1]
Je, ni dalili yenye kuthibitisha kwamba dhambi hii ni kubwa?
Jibu: Ndio. Kuishi kati ya washirikina, kutulizana kati yao na mtu akaacha kuhajiri katika miji ya waislamu anaguswa na matishio haya.
[1] Abu Daawuud (2647) na at-Tirmidhiy (1604) som sade att al-Bukhârî menade att hadîthens berättarkedja saknar en följeslagare. Detsamma sade Abû Hâtim ar-Râzî och ad-Dâraqutnî. Se ”al-Badr al-Munîr” (9/163). Autentisk enligt al-Albânî i ”Sahîh Sunan Abî Dâwûd” (2420).
Swali 24: Ni ipi hukumu ya kikao cha mapumziko (جلسة الاستراحة)?
Jibu: Kimependekezwa. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikikaa. Baadhi ya wanachuoni wengine wanasema kuwa hakikupendekezwa kwa sababu huenda (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alifanya hivo kwa sababu ya uzito wake au kwa sababu ya kuchoka. Lakini maoni yaliyo na nguvu ni kwamba kimependekezwa.
إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! 20 - Isti’aadhah (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah ...