BismilLaahir Rahmanir Rahiim
UJENZI WA MADRASA VIJIJINI
Asalaam aleykum warahmatullah wabarakatuh
Husika na Kichwa cha habari hapo juu,
Tunatarajia Kuanza Ujenzi wa Madrasa Mkoani Dodoma Wilaya ya Chemba katika Kijiji cha Kongogo.
Vijana na akina mama wanasoma chini ya mti na mvua zimeanza. Ustadh alitaka kufunga madrasa lakini tumeweka Niyah ya kujenga Madrasa Kubwa na Vyoo viwiili vyenye Thamani ya Shilingi 5,000,000/=(Milioni Tano)
Kiwanja tunacho na Mpaka sasa katika Kukusanya Michango yetu Tumepata Shilingi 1,500,000/= (Milioni Moja na Laki Tano) Na AlhamduliLaah tumepokea Mchango wa Mabati 20 kwa sasa.
Tunaomba Mchango wako wa Hali na Mali pia Tunapokea pesa Na Vifaa vya Ujenzi kama vile Matofali ,Mabati, Nondo, Mbao, Mchanga, cement na Nakadhalika .
Allaah (Subhanahu wa taala) anasema:-
مَن ذَا الَّذِي يُقْرِضُ اللَّهَ قَرْضًا حَسَنًا فَيُضَاعِفَهُ لَهُ وَلَهُ أَجْرٌ كَرِيمٌ
"Ni nani atakayemkopesha ALLAH mkopo mwema, ili Amrudishie maradufu, na apate malipo ya ukarimu" [Al-Hadiyd:11]
Na pia anasema:-
وَمَا تُنفِقُواْ مِنْ خَيْرٍ فَلأنفُسِكُمْ وَمَا تُنفِقُونَ إِلاَّ ابْتِغَاء وَجْهِ اللّهِ وَمَا تُنفِقُواْ مِنْ خَيْرٍ يُوَفَّ إِلَيْكُمْ وَأَنتُمْ لاَ تُظْلَمُونَ
Na kheri yoyote mnayotoa ni kwa nafsi zenu. Wala msitoe ila kwa kutafuta wajihi wa Allah. Na kheri yoyote mtakayotoa mtalipwa kwa ukamilifu, wala hamtadhulumiwa" [Al-Baqarah:272]
وَمَا أَنفَقْتُم مِّن شَيْءٍ فَهُوَ يُخْلِفُهُ ۖ وَهُوَ خَيْرُ الرَّازِقِينَ
سبأ (39) Saba
Na chochote mtakacho kitoa Yeye atakilipa. Naye ni Mbora wa wanao ruzuku.
Unaweza Kutuma mchango wako kwa namba zifuatazo
Tigo Pesa +255714974397
Airtel Money +255685779911
M-Pesa +255756403470
(Majina ni ARABI MANDOTA)
Kwa wale waliokuwa Nje ya Nchi unaweza Kutuma Mchango kwa njia ya Western Union au MoneyGram au ExpressMoney kwa ARABI SAID MANDOTA natumia Kitambulisho cha Mpiga Kura
Unaweza Kuleta Mchango wako moja kwa moja Mkoani Dodoma Wilaya ya Chemba Kijiji cha Kongogo,ukifika utapiga simu kwa namba hizo hapo juu.
Tunaomba Mchango Wako kwa Hali na Mali ili tufanikishe Jambo hili.
WabilLaah Tawfiq
from fisabilillaah.com https://ift.tt/2Q75uvW
via IFTTT
Translate
Jumamosi, 1 Desemba 2018
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah
إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! 20 - Isti’aadhah (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah ...
-
Dalili 18 zinazoashiria una ujauzito wa mtoto wa kiume Awali ya yote nitoe pongezi kwa mama K na Baba K wote popote walipo kwa kazi nzuri ...
-
SWALI: Assalaam alaykum Naomba maana ya majina yeyote tuwapao watoto wetu AU mnielekeze wapi naweza kupata labda katika kitabu cha fas...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni